Salama Na SAMATTA SE6 EP49 | HEADMASTER PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Ойын-сауық

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Kila kijana wa ki Tanzania ambae anaupenda na kuuthamini mpira wa miguu na ambaye angependa ndo iwe kazi ya maisha yake basi Mbwana Ally Samatta ndiye role model wake, hakuna doubt kwamba watakua na mapenzi na Cristiano Ronaldo au Leo Messi au Kylian Mbappe au Marcus Rashford ila yule ambaye amewaaminisha kwamba INAWEZEKANA ukacheza POPOTE hapa duniani na hasa kwenye ligi yetu pendwa ya Uingereza ni Samatta. Rafiki tu kutoka Mbagala rangi tatu ambaye kashacheza saaana ndondo na makombe ya mbuzi wakati anakua na mwisho wa siku akaenda kucheza kwa wazungu na bado anaendelea kutafuta rizki yake huko, hata kama sio ligi ile ambayo hata yeye mwenyewe angependa awepo ila BADO ni MWAMBA wetu. Samatta huyu huyu ndo ambaye alijitwika mpira kichwani na kuitika nyavuni mbele ya beki ambae anaaminika kuwa BORA kwa misimu hii miwili mitatu ndani ya Virgil van Dijk. Hata wakati naandika hii bado mwili unanisisimka kwa wazo tu kwamba nililishuhudia lile, pata picha kwa mtoto ambaye ana ndoto hizo. Lile goli lilimfanyia NINI kwenye ndoto zake. KRC Genk walipoteza mchezo ule wa ugenini wa kombe la mabingwa wa Ulaya kwa magoli 2-1 ila kwenye mitaa yote ya mikoa ya Tanzania ile mechi ilikua ya USHINDI.
Mbwana ametokea kwenye familia ya kawaida sana sana, wazazi wake wote kama kumbukumbu yangu itakua 100 basi walikua polisi, najua kwa hakika Baba yake alikua Polisi kwa asilimia 100. Kwa marehemu Bi Mkubwa wake ndo sina hakika sana ila kwa hakika jibu limo kwenye haya maongezi yetu. Anakumbuka jinsi ambavyo Mzee wake alikua anasisitiza kwenye suala la elimu na heshima, kama mtoto wa mwisho kwenye familia hiyo, Mbwana aliupenda sana mpira, zile za kujiiba na kwenda kucheza mechi za mbali alishafanya sana na matunda ndo haya ya leo. Nadhani ilifika kipindi Mzee mwenyewe aliona basi sawa, twende huko utakako. Familia yao yote ni wapenzi wa mpira na Kaka yake Mouhamed bado anacheza hapa hapa Tanzania. Sasa akiwa kama kioo kikubwa sana kwenye jamii hii Samatta anazungumzia presha ambayo hupewa hasa pale anapoitwa kwenye timu ya Taifa, jinsi maneno mengi ya kashfa yanaporushwa kwake kutoka kwa wananchi na anakumbuka pia wakati bado anacheza T.P Mazembe kuna kipindi kocha aliacha kumuita yeye na Rafiki yake Thomas Ulimwenguna ilisemekana kama pengine hakuna na interest na team au hakua anatoa 100. Pengine kipindi hicho aliumia zaidi maana hiyo haikua jambo zuri kwake.
Mbwana anazungumza na mimi kuhusu urafiki wake na Ulimwengu na maisha ambayo walikua wanaishi pamoja wakati wako DRC, anakumbuka jinsi walivyokua wanapanga kufanikiwa pamoja na mipango yao endelevu kwenye career yao. Ulimwengu nae ana siku yake kwenye kiti chetu In Shaa Allah maana nae ana mengi ya kutuelezea. Majeraha ya mara kwa mara bila ya shaka yalisababisha kwa kiasi kikubwa ndoto zake za kucheza Ulaya kutochukua hatua ya juu kama ambavyo angependa, ila mimi naamini hayo yote maisha tu, kila kitu kilikua tayari kimesha andikwa.
Samatta ni Baba ambaye watoto wake wanasoma hapa hapa nyumbani, nilimuuliza kama watoto wake wanajua yeye ni nani na akanipa story ndogo ya yeye kung’amua kama wanafahamu fika Baba yao ni nani.
Mwenzangu humu kuna mengi sana ambayo yatakufaa na kwa nafasi ya kipekee ningependa kumshukuru Captain wa Taifa kwa kuchukua time kwenye ratiba yake ambayo ilikua imebana kweli kweli ili tu aje kutubarikia meza yetu kwa uwepo wake.
Yangu matumaini uta enjoy sana.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Пікірлер: 134

  • @mbwanamtessa8607
    @mbwanamtessa8607 Жыл бұрын

    Kama bado unamkubali huyu jamaa gonga like twenzetu

  • @Jibambeshow254k
    @Jibambeshow254k5 ай бұрын

    Santa very humble and peaceful guy naona ananyayo kama za Ali hana mbwembwe and that's why he's unique ❤hii sampuli ndio kio cha jamii

  • @samniza1763
    @samniza1763 Жыл бұрын

    The first ever sensible young Tanzanian born and raised in Tanzania. Proud of who you have become.

  • @JJ-sx7ne

    @JJ-sx7ne

    Жыл бұрын

    Labda wewe kingereza hakipo kabisa! 98% kaongea kiswahili..

  • @chiconinde8135
    @chiconinde8135 Жыл бұрын

    Baada ile ya Jakaya....Hii tena umefanya kubwa Salama🙌⚽️💪

  • @rashidchimwenda
    @rashidchimwenda Жыл бұрын

    Big up kwa Salama kuweza kutuletea Samatta. Anaongea mambo mengi mazuri ya mfano kwa vijana wetu kwa soka letu. Ila suala la maadili sikubaliani naye aliposema ni yeye mwenyewe. Bila shaka maadili yake mazuri yamejengwa ktk familia yao (baba na mama) na hususan kwakuwa ni familia ya kipolisi, timu alizopitia hapa bongo na tamaduni zetu za kitanzania. Sisi watanzania tupo vizuri kimaadili kuliko baadhi ya watu wa mataifa mengi. Kila la heri kwake na Salama.

  • @sawaabyahya584
    @sawaabyahya584 Жыл бұрын

    Huyu mwanamme mbona best baba! Ni kioo cha jamii..... Vijana wajifunze kupitia tabia yake.... Ahsante Salama kumtafuta...

  • @stevewanga957
    @stevewanga957 Жыл бұрын

    Hes very humble like Ali Kiba...much love from🇶🇦🇶🇦

  • @mnasicafe1319

    @mnasicafe1319

    Жыл бұрын

    Yeah

  • @GodfreyPaul

    @GodfreyPaul

    Жыл бұрын

    Much appreciation for your popa🔥🔥🔥

  • @arafajabir3194
    @arafajabir3194 Жыл бұрын

    Mungu amempa uwezo ila hapendi show off anaishi kama Ali kiba good bless you

  • @nellymatalanga5033

    @nellymatalanga5033

    Жыл бұрын

    You are ths two people wamebarikiwa but wako humble na down to earth

  • @mzirairebeca9996

    @mzirairebeca9996

    Жыл бұрын

    Nature ya kazi yake pia

  • @mzirairebeca9996

    @mzirairebeca9996

    Жыл бұрын

    Ukiwa msanii makelele hayakwepeki

  • @silvanusremmy9575

    @silvanusremmy9575

    Жыл бұрын

    Sasa Alikiba ametokea wapi. Acha makasiliko 😀

  • @mussachabonga9595
    @mussachabonga9595 Жыл бұрын

    Fantastic interview big up sister Salama 2023

  • @hanssenbensonmturi2435
    @hanssenbensonmturi2435 Жыл бұрын

    Ulivofanya interview na Idris, nilitamani ufanye na Samatta as well. Nilivyoona hii leo, ilinikosha sana kwani Samatta ni nguli na role model to a lot of us young footballers. I am currently playing my football in The Thailand 3rd division and I dream one day not only to replicate the legend’s work but also I dream of being part of this show. Thank you Salama and Samatta for this wonderful interview

  • @Chemba67

    @Chemba67

    Жыл бұрын

    Keep it up Hanssen Benson.......your name sound Danish.......

  • @allahisone6386

    @allahisone6386

    Жыл бұрын

    @Hanssen God bless you ❤️🙏❤️

  • @shwaibukhatibu2838
    @shwaibukhatibu2838 Жыл бұрын

    SAMATA NA KING KIBA ALLAH BLESS YOU OTHER CELEBRITIES THEY HAVE TO COPE FROM YOU

  • @com5766
    @com5766 Жыл бұрын

    The best interview Hey kenyans give likes for it

  • @tatutumbi4640
    @tatutumbi4640 Жыл бұрын

    Salama Hongera Sana. Nafatilia Sana Vipindi Vyako. Navipenda. 👍

  • @majomamajoma8776
    @majomamajoma8776 Жыл бұрын

    Nina mwanangu anakupenda na anacheza mpila hatari Huwa anajiita samata, sapoti wanetu vijijin kaka nao watimize ndoto zao Allah akufanyie wepesi uzidi kung'ara

  • @SaidiHassan-pq3zf
    @SaidiHassan-pq3zf3 ай бұрын

    Bless captain Diego

  • @RehemaChap3
    @RehemaChap34 ай бұрын

    Samanta MUNGU akubariki sana una busara sana

  • @albogastmselejr4583
    @albogastmselejr4583 Жыл бұрын

    Aiseh! Jamaa Mbona Haongei Kingereza Kama Mimi Wakati Mimi Nimekaa Week Tu Nime Sahau Kiswahili 😁😁

  • @jackbujimu3220

    @jackbujimu3220

    Жыл бұрын

    🤣🤣🤣🤣 mie nimesoma tu English medium primary Ila mpka Sasa ninachanganya ngeli Kama nimeish mambele

  • @maishakisunzu391
    @maishakisunzu391 Жыл бұрын

    Kama umegundua lafudhi ya samatta ishabadilika automatically kuwa ya kiingereza gonga like hapa😝

  • @navigatorelias9794

    @navigatorelias9794

    5 ай бұрын

    Wewe acha zako babu, Asa si lazima hiyo hata wwe ukitoka kwenu huko dongo kusimamia ukija mjini lazima kiswahili chako kibadilike, so sielewi unataka kumaanisha nn

  • @rosemofuga8101
    @rosemofuga8101 Жыл бұрын

    Waoooooo fantastic mr Samatta

  • @deospackle2158
    @deospackle2158 Жыл бұрын

    Samatta anasound humble sana🔥🔥🔥

  • @luciasteven3314
    @luciasteven33145 ай бұрын

    Nimechelewa sn kumjua samatta❤

  • @nomamatata754
    @nomamatata754 Жыл бұрын

    I keep saying salama you got best questions for your guests.....you keep asking my questions every time i get time to see your sessions.....be blessed girl

  • @homan_nkwama
    @homan_nkwama Жыл бұрын

    kama baadhi ya majibu yanatakiwa Sana ili kutimiza mahojiano ni sawa ila kama sivyo, naomba salama punguza kujenga MASWALI yanayo mlazimu mtu ajibu katika mtazamo fulani.....awe huru tusitarajie atajibu nini I LOVE YOU SALAMA

  • @peterkichochi7510
    @peterkichochi7510 Жыл бұрын

    This Guy is very humble and smart, he knows how to communicate

  • @ahmedjaffari9375

    @ahmedjaffari9375

    Жыл бұрын

    Exactly… he is truly a professional footballer, may Almighty Allah bless him abundantly 🙏🏿

  • @mofungoya9729
    @mofungoya9729 Жыл бұрын

    Best player ever ♥️🇹🇿

  • @erickchitumbi1308
    @erickchitumbi1308 Жыл бұрын

    Mbwana unayo hekima na busara sana.safi sana.

  • @mountaincoffee7
    @mountaincoffee7 Жыл бұрын

    Noma sana

  • @ayubuakko9495
    @ayubuakko9495 Жыл бұрын

    Salama jabir Ur on 🔥🔥

  • @dseven7094
    @dseven7094 Жыл бұрын

    mbagala boy

  • @jojigeorige1056
    @jojigeorige1056 Жыл бұрын

    He's well programmed aisee

  • @januarysungura8119
    @januarysungura8119 Жыл бұрын

    Your the best not just of luck but you deserve it keep up samatta

  • @mweusiasili8345
    @mweusiasili8345 Жыл бұрын

    Capten Diego

  • @user-xu2vg2ge2q
    @user-xu2vg2ge2q11 ай бұрын

    Uyu yomuli Dar Es Salaam Tz 🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿

  • @nadildylan6124
    @nadildylan6124 Жыл бұрын

    Legend Bro

  • @furahambwembwe6935
    @furahambwembwe6935 Жыл бұрын

    Humble man...

  • @marwajuma7493
    @marwajuma7493 Жыл бұрын

    Nilisubili Sanaa asante sanaa

  • @andrewjulius2306
    @andrewjulius2306 Жыл бұрын

    Sam ✊🔨 keep it up bro unjua

  • @safiyatheonlything7848
    @safiyatheonlything7848 Жыл бұрын

    leo salama na samata

  • @nadildylan6124
    @nadildylan6124 Жыл бұрын

    Huna Baya bro

  • @mrlabay9871
    @mrlabay9871 Жыл бұрын

    🔥🔥🔥🔥

  • @bish_daddiyao
    @bish_daddiyao Жыл бұрын

    Mimi mkenya Ila Huyu Jamaa namkubali🙌🏾⚽♥️⚽

  • @ramadhanmaisa788

    @ramadhanmaisa788

    Жыл бұрын

    Hakun ulazim wa kusema ww n mkenya

  • @moganfred6473
    @moganfred6473 Жыл бұрын

    Nakkubali sana

  • @daggerslick
    @daggerslick Жыл бұрын

    Woyoooo mbwana samatta😜😜😜

  • @flavianchuwa4370
    @flavianchuwa4370 Жыл бұрын

    Waaaaoooh Asante kwa hii Salama

  • @robinhomesuza8906
    @robinhomesuza8906 Жыл бұрын

    Naskia sauti ya ommy dimpoz zinafanana

  • @Revo_silayo
    @Revo_silayo Жыл бұрын

    Hyo ni nature ya intruvant peoples Huwa wanakuwa na rafiki wachche lkn wanapendwa na wengi na Huwa wanajifanyia maamuzi wenyewe na pia wapo focused na hutoboaa sanaaa.

  • @nadildylan6124
    @nadildylan6124 Жыл бұрын

    Salama tunaomba ufanye interview na nadir haruob canavaro

  • @brunofernandez6608
    @brunofernandez6608 Жыл бұрын

    Samagoal Mbagala Boy

  • @mr.graphics3213
    @mr.graphics3213 Жыл бұрын

    Tz oneeee🔥🔥🔥🔥

  • @ibraimoissiaca6058
    @ibraimoissiaca6058 Жыл бұрын

    Popa

  • @googleus4903
    @googleus4903 Жыл бұрын

    MWAKINYO ANGEPATA NIDHAMU NA HESHIMA KAMA YA NDUGU NYETU SAMATTA ANGEFIKA ZAIDI YA ALIPO LEO.

  • @tztanzania2262

    @tztanzania2262

    Жыл бұрын

    Mbona na mwakinyo yupo fresh tu!

  • @barbarasara4033

    @barbarasara4033

    Жыл бұрын

    @@tztanzania2262 dharau nyingi

  • @mickidadybakari9974

    @mickidadybakari9974

    Жыл бұрын

    Mwakinyo mtu poa saaana kama utam chukulia poa ila kama ukiwa mduanzi utam hulia mbona ila ni mshikaji saaana tena zaid ya saaana

  • @hansigajijime4108
    @hansigajijime4108 Жыл бұрын

    Mwamba kabsa

  • @dmikepresenter
    @dmikepresenter Жыл бұрын

    Samatta Goal 🇹🇿🇹🇿🇹🇿

  • @aishaomarry6996
    @aishaomarry6996 Жыл бұрын

    Huyu ni mimi kabisa hua naamua mwenyewe mambo yangu.

  • @tztanzania2262

    @tztanzania2262

    Жыл бұрын

    Usifanye hivyo mara zote jtahd baadhi ya mambo kuomba ushaur

  • @dullayomwinyi3359
    @dullayomwinyi33595 ай бұрын

    Mwamba huyu ni hatari sana

  • @hassanikipusa8328
    @hassanikipusa8328 Жыл бұрын

    Champion Boy 🇹🇿

  • @donnietommie8444
    @donnietommie8444 Жыл бұрын

    #SalamaNaDrLeaky

  • @mwasagamwambuli3513
    @mwasagamwambuli3513 Жыл бұрын

    Mbwana you are what your father and mother groomed you to be what you are. Be appreciative of your parents

  • @mashamassingisa8738

    @mashamassingisa8738

    Жыл бұрын

    True

  • @FranklinMtei

    @FranklinMtei

    Жыл бұрын

    Was looking for this. Kajikuza mwenyewe? Heshima kwa wazazi

  • @abuujuhayfa4321
    @abuujuhayfa4321 Жыл бұрын

    SAMATTA 🔥🔥🔥 gonga like kwa mwamba

  • @xnobmedia1
    @xnobmedia1 Жыл бұрын

    Dah Salama kwa kumleta salama umenitouch saaaana yan. Hebu pokea 10k la soda hapooo.

  • @thefeyotz
    @thefeyotz Жыл бұрын

    Aliifunga Liverpool 😁😁

  • @edwardfaraji1133
    @edwardfaraji1133 Жыл бұрын

    Sama goal Sama Sama goal....

  • @kabirigisaidi8253
    @kabirigisaidi8253 Жыл бұрын

    Sama goal Sama goal. You de best bro

  • @MariamHamad-lr3xc
    @MariamHamad-lr3xc5 ай бұрын

    Kipendacho moyo dawa

  • @dreamfootballclip1096
    @dreamfootballclip1096 Жыл бұрын

    Home boi

  • @FireHouse123
    @FireHouse123 Жыл бұрын

    Samatta mkali sana namkubali

  • @samludo5435
    @samludo5435 Жыл бұрын

    Mlete mandonga salama

  • @henrymassawe699

    @henrymassawe699

    Жыл бұрын

    😁🤣🤣🤣🤣😁😁😁😁 hatavuruga interview aiseee!!!🤣🤣

  • @anumario7footballlife936
    @anumario7footballlife936 Жыл бұрын

    Kaka yangu

  • @pheninhojr5875
    @pheninhojr5875 Жыл бұрын

    Samagoal #hainakufel

  • @jamaalsaleem2926
    @jamaalsaleem2926 Жыл бұрын

    WA kwanza leoooooo

  • @kanyika14kanyika16
    @kanyika14kanyika16 Жыл бұрын

    SAMATTA anatabia kama zangu😁😁

  • @kulwamwakagali24
    @kulwamwakagali24 Жыл бұрын

    Champs Boy

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan2499 Жыл бұрын

    Laana ya wazazi ndio hiyo mitihani.

  • @gasorekassim5499
    @gasorekassim5499 Жыл бұрын

    Kizaz san

  • @MariamHamad-lr3xc
    @MariamHamad-lr3xc5 ай бұрын

    Wanasema pesa ni sabuni ya roho

  • @nahyialetomia9284
    @nahyialetomia9284 Жыл бұрын

    Nafurahia wewe kujenga msikiti

  • @mdalamgir-gu9hu
    @mdalamgir-gu9hu Жыл бұрын

    Yan pia salama leo ujui umulize nn..

  • @rehemambilinyi9452
    @rehemambilinyi9452 Жыл бұрын

    Tuletee na pastor Tony kapola,

  • @cvanoedward3093
    @cvanoedward3093 Жыл бұрын

    Salama mbona watukatisha?

  • @abdallahmanula1627
    @abdallahmanula1627 Жыл бұрын

    Apo salama umenichanganya kabla amjaaanza nyuma muanze mbele mimi cjakuelewa kabisa

  • @walafredchikawe4113

    @walafredchikawe4113

    Жыл бұрын

    😂😂😂😂

  • @kostasagelidis5326
    @kostasagelidis53264 ай бұрын

    ωχχ ο σαματαςς χαχα

  • @albertbayona8441
    @albertbayona8441 Жыл бұрын

    Kwan jaman ilo neno shock mbona watu ulitumia vibaya

  • @Oldskulgemini9991

    @Oldskulgemini9991

    Жыл бұрын

    SEMA hata wazungu hutumia Hilo neno mara nyingi Sana so Wala sio ajabu SEMA labda kwakuwa umeona wabongo pekee😅

  • @ahz6907

    @ahz6907

    Жыл бұрын

    Linatakiwa litumikaje?

  • @kamanziian1073

    @kamanziian1073

    Жыл бұрын

    Wewe ndo hulielewi

  • @Bam268
    @Bam268 Жыл бұрын

    Apo mnatuchanganya Birmingham ipi sasa ya gwajima au?

  • @eddiearts3713

    @eddiearts3713

    Жыл бұрын

    birmingham ni mjini ndani ndio kuna club ya aston villa

  • @barbarasara4033

    @barbarasara4033

    Жыл бұрын

    Nakojoa. ..... Kwa kucheka

  • @mdalamgir-gu9hu

    @mdalamgir-gu9hu

    Жыл бұрын

    Tatzo utembei nawala ulizi pia mitandao uoni

  • @denisruvugo1764

    @denisruvugo1764

    Жыл бұрын

    Hahahahahahahahahahahahahahaha

  • @adamsengo1869
    @adamsengo1869 Жыл бұрын

    Wape points zao wazazi maana wao ndio source ya tabia yako

  • @mashamassingisa8738

    @mashamassingisa8738

    Жыл бұрын

    Masikito kua cjasikia hili kutoka kwake

  • @adamsengo1869

    @adamsengo1869

    Жыл бұрын

    @@mashamassingisa8738 eti ni yeye tu amejikuta yupo ivo yani kama vile alijikuza mwenyewe, naona kama vile kwa mbali ana katabia cha kujimwambafai flani hivi

  • @mashamassingisa8738

    @mashamassingisa8738

    Жыл бұрын

    Masikitiko makubwa kk

  • @izzi198

    @izzi198

    Жыл бұрын

    angevuta bangi na kuwa teja mngewapa point wazaz wake? Acheni kushinikiza ujinga

  • @mashamassingisa8738

    @mashamassingisa8738

    Жыл бұрын

    @izzi haya kk uko vyema sana

  • @msuyatztv5201
    @msuyatztv5201 Жыл бұрын

    kzread.info/dash/bejne/lIN3k7CLct3OgaQ.html Ujumbe wa wafanyakazi Kwa Mama samia

  • @nadildylan6124
    @nadildylan6124 Жыл бұрын

    Bro umetupa funzo kubwa cc vijana, wewe nd mchezaji usie kuwa na wajivuno na nadir haruob Kwa maono yangu

  • @ibrahimshilinde6129
    @ibrahimshilinde6129 Жыл бұрын

    Kwani wewe Salam,Nani huaga anakushauri kuwakandia vijana wenye talent za mziki?

  • @tutumarzouk9803
    @tutumarzouk9803 Жыл бұрын

    mbona sama goal anajifanya kama hajui kiswahil vzr, yan kama ameish eurupe since he was childhood

  • @mdalamgir-gu9hu

    @mdalamgir-gu9hu

    Жыл бұрын

    Kizungu gan kazumgumza apo izo actualy nyingi..

  • @bryanlimbi326

    @bryanlimbi326

    Жыл бұрын

    Sasa he was childhood ndo nini ..!? , Jifunze grammar mbwa wewe

  • @timmahbee

    @timmahbee

    Жыл бұрын

    @@bryanlimbi326 ilikua na ulazima wa kumtukana????

  • @noelsanga6853

    @noelsanga6853

    Жыл бұрын

    @@timmahbee wivuuu tu unawasumbua

  • @anoldjefsta177

    @anoldjefsta177

    Жыл бұрын

    @@bryanlimbi326 na aanze kubweka saivi

  • @jilalajr_official
    @jilalajr_official Жыл бұрын

    @samagoal77 #diego

  • @baritone_online_tv2565
    @baritone_online_tv2565 Жыл бұрын

    Noma sana

Келесі