Salama Na SAMATTA SE6 EP49 | HEADMASTER PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460
Ойын-сауық
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Kila kijana wa ki Tanzania ambae anaupenda na kuuthamini mpira wa miguu na ambaye angependa ndo iwe kazi ya maisha yake basi Mbwana Ally Samatta ndiye role model wake, hakuna doubt kwamba watakua na mapenzi na Cristiano Ronaldo au Leo Messi au Kylian Mbappe au Marcus Rashford ila yule ambaye amewaaminisha kwamba INAWEZEKANA ukacheza POPOTE hapa duniani na hasa kwenye ligi yetu pendwa ya Uingereza ni Samatta. Rafiki tu kutoka Mbagala rangi tatu ambaye kashacheza saaana ndondo na makombe ya mbuzi wakati anakua na mwisho wa siku akaenda kucheza kwa wazungu na bado anaendelea kutafuta rizki yake huko, hata kama sio ligi ile ambayo hata yeye mwenyewe angependa awepo ila BADO ni MWAMBA wetu. Samatta huyu huyu ndo ambaye alijitwika mpira kichwani na kuitika nyavuni mbele ya beki ambae anaaminika kuwa BORA kwa misimu hii miwili mitatu ndani ya Virgil van Dijk. Hata wakati naandika hii bado mwili unanisisimka kwa wazo tu kwamba nililishuhudia lile, pata picha kwa mtoto ambaye ana ndoto hizo. Lile goli lilimfanyia NINI kwenye ndoto zake. KRC Genk walipoteza mchezo ule wa ugenini wa kombe la mabingwa wa Ulaya kwa magoli 2-1 ila kwenye mitaa yote ya mikoa ya Tanzania ile mechi ilikua ya USHINDI.
Mbwana ametokea kwenye familia ya kawaida sana sana, wazazi wake wote kama kumbukumbu yangu itakua 100 basi walikua polisi, najua kwa hakika Baba yake alikua Polisi kwa asilimia 100. Kwa marehemu Bi Mkubwa wake ndo sina hakika sana ila kwa hakika jibu limo kwenye haya maongezi yetu. Anakumbuka jinsi ambavyo Mzee wake alikua anasisitiza kwenye suala la elimu na heshima, kama mtoto wa mwisho kwenye familia hiyo, Mbwana aliupenda sana mpira, zile za kujiiba na kwenda kucheza mechi za mbali alishafanya sana na matunda ndo haya ya leo. Nadhani ilifika kipindi Mzee mwenyewe aliona basi sawa, twende huko utakako. Familia yao yote ni wapenzi wa mpira na Kaka yake Mouhamed bado anacheza hapa hapa Tanzania. Sasa akiwa kama kioo kikubwa sana kwenye jamii hii Samatta anazungumzia presha ambayo hupewa hasa pale anapoitwa kwenye timu ya Taifa, jinsi maneno mengi ya kashfa yanaporushwa kwake kutoka kwa wananchi na anakumbuka pia wakati bado anacheza T.P Mazembe kuna kipindi kocha aliacha kumuita yeye na Rafiki yake Thomas Ulimwenguna ilisemekana kama pengine hakuna na interest na team au hakua anatoa 100. Pengine kipindi hicho aliumia zaidi maana hiyo haikua jambo zuri kwake.
Mbwana anazungumza na mimi kuhusu urafiki wake na Ulimwengu na maisha ambayo walikua wanaishi pamoja wakati wako DRC, anakumbuka jinsi walivyokua wanapanga kufanikiwa pamoja na mipango yao endelevu kwenye career yao. Ulimwengu nae ana siku yake kwenye kiti chetu In Shaa Allah maana nae ana mengi ya kutuelezea. Majeraha ya mara kwa mara bila ya shaka yalisababisha kwa kiasi kikubwa ndoto zake za kucheza Ulaya kutochukua hatua ya juu kama ambavyo angependa, ila mimi naamini hayo yote maisha tu, kila kitu kilikua tayari kimesha andikwa.
Samatta ni Baba ambaye watoto wake wanasoma hapa hapa nyumbani, nilimuuliza kama watoto wake wanajua yeye ni nani na akanipa story ndogo ya yeye kung’amua kama wanafahamu fika Baba yao ni nani.
Mwenzangu humu kuna mengi sana ambayo yatakufaa na kwa nafasi ya kipekee ningependa kumshukuru Captain wa Taifa kwa kuchukua time kwenye ratiba yake ambayo ilikua imebana kweli kweli ili tu aje kutubarikia meza yetu kwa uwepo wake.
Yangu matumaini uta enjoy sana.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Пікірлер: 81
Kiukweli Salama huchoshi Pia watu unaowahoji ni moja Kati ya watu wenye madini sanjari na Hilo Mbwana ni moja Kati ya watu uliowahoji vyema na wenye Radha ya namna yake Alhamdulillah mungu akuongoze na akurahisishie katika kila mahojiano yako INSHA'ALLAH.
Natamani siku moja nichangie hichi kipindi eeehh mola nisaidie na mie ridhki ikue nimkumbuke sister salama in shaa Allah
Leo nimegundua Samatta anastahili kufika zaidi ya alipofika
@allahisone6386
Жыл бұрын
More more ❤️🙏❤️
Aunty Salama siku tunamuhitaji Mgunda
Salama ww hodari hasaaa
Tangu nchi yetu imepata uhuru mbwana samata ndio mchezaji wangu ninae mkubali kuliko mchezaji yeyote alie wahi kutokea tanzania hii nakukubali sana mbwana samata wewe ni fundi wa mpira mimi huwa nagombana na watu kuhusu mbwana kwenye timu ya taifa ya tanzania hatuna viungo bora kama viungo anaochezanao mbwana kwenye kwenye vilabu va ulaya mbwana huyo aludi kukabapia akafunge goli
Miongoni mwa interview bora zaidi ,hakika Salama na Samatta mmeonesha utofauti mkubwa sana na mafunzo mazuri kwa watu wa kada mbalimbali
@shakilakhamis2109
Жыл бұрын
Kbc
Sauti yake Kama omy dimple,,, humble
Nakubaliana naye sana kuhusu wazo la timu ya Taifa. Kudos sana.
Napenda sana ayo maisha mimi pia mpaka nalaumiwa na marafiki wakisema ndo maisha yote aya shekh
As A fan of soccer Am proud of him nice interview 🙌🏾❤️
Samagoal much appreciation for you 🤝🤝
Asante Sana Dada. Sama upo vizuri Sana Mungu akulinde utafika mbali Sana.
Yuko makin sana kaka
Wakwanza kukoment
Real guy never live with showoff ,, congratulations samatta
Jamaa ana displini sana uyu anajielewa ndo mana taifa linamuangalia yeye
Bravo Samatta
Very humble guy...I like it
Samatta mbona unamadini kiasi icho ndugu yangu upo vizuri na Allah akupe kila zuri unalostahili BLESS
This guy is very humble and matured.
Yuko humble sana sammata
Naipenda tabia ya aina hii best fan of him
Sounds like Ommy Dimpoz (sauti)❤
@roots_tz7403
Жыл бұрын
exactly
@josephk90
Жыл бұрын
Sure, umetisha sana.
@furahambwembwe6935
Жыл бұрын
Exactly
I appreciate what you are doing skipper
Swali la mwisho,muhimu sana
Nimependa sana haya maojiano💪
Captain Diego #Haina kufel 🇹🇿
Hujamaa ndio sampuli y Alkiba hongera bb endelea kua kimya hivyo itaepusha husda pia
Salama mkorofi et rangi ya maiki iko vizuri
Uyooo anaitwaa samaaaaaaa bichwaaaaaaaa kambaaaaa
jamaa yupo vizuri🔥🔥🔥
Siku hizi Salama hakuna mambo ya Misosi na majuice
jamaaa nom san anajua nini vha kusem nin chakuachaa sem for me his my rollmodle
SAMATA ANAONGEA KAMA OMMY DIMPOZ.
@shadyahamad3724
Жыл бұрын
Unaye umegunduwa km mimi😀
@geofreymhando8674
Жыл бұрын
@@shadyahamad3724 Yes Mamy
Kila la kheri champion 🏆
Mbona Samata haujamletea msosi jaman super star wetu kaondoka na njaa na kama hamujui uyo mwamba ndio ninajivunia nae huku Bagdad 🇮🇶 Wakiniuliza TANZANIA mnawachezaji wanaocheza nje ya bara la Africa naingia google nawaonesha mgoli aliowafunga Liverpool haraf ndo nafata kina Cram afif na kina porsen💪
@ahmedjaffari9375
Жыл бұрын
Kipindi kilirekodiwa asubuhi ndio maana mezani kuna chai/kahawa pamoja na keki. Endapo wangerekodi mchana au jioni basi msosi ungehusika 😃
Ufikirie episode moja umlete koyoko Ramadhani...nisikie refa wetu anavyoongea mawazo yake
🏃🏽10
Tunaomba huo mziki uondolewe tafadhali tunataka kufaidi au kusikia mahojiano vizuri
@mjinjatv8120
Жыл бұрын
Huo mziki ndo unatambulisha kipindi.
@Josh_1194
Жыл бұрын
Mbona wanasikika fresh
@Josh_1194
Жыл бұрын
Huyu jamaa ni very humble
@dianerditto
Жыл бұрын
Yaan ninavyofucos kwenye interviews za salama huo mziki siusikiagi kabisa
@fahadfahmy
Жыл бұрын
@@dianerditto hata nami namfatilia Salama tokea ana kipindi chake cha Mkasi ila huu mziki unazingua
Anasauti kama Ommy Nyembo
@CertifiedStoic
Жыл бұрын
Nilikuwa nawaza kitu hiki hiki.
Karibu Tena unyamanii Simba SC
Ungemuulizaa kuhusu goli alilowafunga Liverpool kwenye champions league alijisikiaje ??lile goli ndo goli bora kuwa kutokea kutoka kwa samatha ,,maana match lilikataliwa ila mechi ya marudiano akalifunga vile vile ,,so ilikuwa kubwa maana watanzania alitueshimisha sana na kwa mda ule tulifurahi sana ,,any way its ,,but samatha is a heaven sent ,,ana stahili Urais kama etoo
Samagooool
@emmyandrew8670
Жыл бұрын
Samata na mm mtoto wangu ana miaka 9 anataka kuwa km ww
@charliestyles5535
Жыл бұрын
@@emmyandrew8670 kwa iyo 😒
Woyoooo💣😜😜
Bro muna mawazo mazuri hila mchango wenu kwa taifa ni jambo njema hapa usa kunakuwa game roldinho na Carlos hivyo nawapongeza na mchango wangu hupo ni capital lansing michigan usa
Mbona manjare hujampa au Jessica amezingua
Umesema Kutumia Kichwa Gani Hapo
Mbona hamjampa samata chakula
Nilichokigundua huyu jamaa nimuoga sanaaa
NIA YA SAMATA YA KUWA KIONGOZI WA TFF BAADA YA KUSTAAFU SOKA NI WAZO ZURI.LAKINI DUINIA YA SOKA IMEJAA FITINA ZA KIPUUZI SANA..HUWEZI AMINI KAMA DROGBA ALIENGULIWA KTK UCHAGUZI WA CHAMA CHA SOKA IVORY COAST KWA KIGEZO ETI HANA UZOEFU,,,UPUUZI MTUPU
@allahisone6386
Жыл бұрын
WATU WA IVORY COAST WANAMBEZA SAAAAAAAN HASA FIFA FOOTBALL YAO KUA NI MGUM MGUMU SN TOFAUTI NA SAMUEL ETO'O
Ila huyu jamaa ilibidi ahojiwe na muandishi wa Mambo ya soka mfano maulid kitenge.yusuph mkule. Shafii dauda . Edo kumwembe. Nk tungefaidi madini Mengi Sana Salama kajitahidi Ila Kwa Upande Wangu Maswali Yake Hayajakata Kiu Yangu
@makayabanzi2929
Жыл бұрын
Ni sahihi kabisa kaka
@makayabanzi2929
Жыл бұрын
Sema wanawake wanapenda sana kujua personality ya mtu hasa kuhusiana na mahusiano au kipato nk
@emmamatemu8225
Жыл бұрын
Salama na sio channel ya mpira, comment hii peleka kulee
KUNA KAKA YANGU MMOJA ANA TABIA ZA SAMATA INSHORT SIPENDAGI NAONA ANAKUWAGA KINYUME KINYUME HARUSI ANAONA ANASA SHEREHE KULA BATA YAANI ANAONGEAGA SIO ISSUE YAANI ANAISHI KAMA Okonkwo. Kuwa kinyume na kila kitu sio issue
@choggysly3541
Жыл бұрын
Hahahaha eti okonkwo umenifanya niitafute things fall apart nimsome now wakati nipo timamu
@nkamangi4707
Жыл бұрын
@@choggysly3541 kila kitu anajifanya mimi oh hivi vile yaani anawezakuwa mtemi huyu jamani umbea huu
@bernaberna4159
Жыл бұрын
😂😂😂
@kadirdhulfiqaar7820
Жыл бұрын
🤣🤣🤣🤣🤣🤣👋👋👋
Utuitie MAYELE
Salama hujamuuliza kama alikuwa anatuona kwenye comment za astonvilla tulikuwa hatulali jamani bila kupita kwenye ile page yq Instagram