RAIS DKT. MAGUFULI ATOA MSIMAMO WA SERIKALI KUHUSU BEI YA KOROSHO NCHINI 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 28 Oktoba, 2018 amekutana na wanunuzi wa zao la korosho na kutoa msimamo wa Serikali kuhusu bei ya zao la korosho kufuatia kuwepo kwa mvutano wa bei ya zao hilo kati ya wanunuzi na wakulima.
Mhe. Rais Magufuli amekutana na wanunuzi hao katika mkutano wa majadiliano uliokuwa ukiendelea kati ya wanunuzi wa korosho na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Katika msimamo huo Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali inaungana na msimamo wa wakulima kukataa bei zilizotolewa na wanunuzi katika mnada uliofanyika hivi karibuni ambapo kampuni za ununuzi wa korosho zilitangaza kununua korosho kwa bei ya kati ya shilingi 2,717/= na shilingi 1,900/= kwa kilo ikiwa imeshuka kutoka zaidi ya shilingi 3,600 ya msimu uliopita.
Mhe. Rais Magufuli amesema endapo wanunuzi hao hawatakuwa tayari kununua korosho kwa bei isiyopungua shilingi 3,000/= kwa kilo, Serikali ipo tayari kununua korosho kwa bei yenye maslahi kwa wakulima na kutafuta masoko yenye bei nzuri.
“Kama hamtanunua korosho kwa bei yenye maslahi kwa wakulima, Serikali itanunua korosho kwa bei nzuri kwa wakulima na tutaihifadhi, nipo tayari hata kutumia majeshi yetu kununua korosho na tutatafuta masoko ya uhakika ili tuuze kwa bei nzuri” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
Wakizungumza katika mkutano huo, wanunuzi wa korosho wamekubali kununua korosho kwa bei isiyopungua shilingi 3,000 kama ilivyoelekezwa na Serikali na wameomba baadhi ya tozo zinazosababisha kupungua kwa bei ya zoa hilo kwa mkulima ziondolewe pamoja na kuruhusiwa kusafirisha korosho kupitia bandari ya Dar es Salaam ambako wanaweza kupata meli zinazotoza gharama nafuu za usafirishaji wa korosho kwenda kwenye masoko ya nje ya nchi.
Mhe. Rais Magufuli amekubali kuondolewa kwa utozaji ushuru wa mara ya pili wa ushuru wa halmashauri uliokuwa ukifanywa baada ya korosho kufikishwa Mtwara, kupunguza ushuru wa Bodi ya Korosho kutoka shilingi 17/- hadi shilingi 10/- kwa kilo na ameruhusu wafanyabiashara kununua magunia yao wenyewe kwa ajili ya korosho badala ya kuuziwa na vyama vya ushirika kwa bei kubwa.
Kuhusu bandari ya kusafirishia korosho Mhe. Rais Magufuli amekubaliana na maombi ya wanunuzi kutaka kusafirisha korosho kwa kutumia bandari ya Dar es Salaam ambapo kilo moja inasafirishwa kwa shilingi 47/- kwa kutumia meli ambazo zimeleta mizigo mingine ikilinganishwa na bandari ya Mtwara ambako kilo moja inasafirishwa kwa shilingi 203/- kwa kutumia meli zinazokodiwa kwa ajili ya kubeba korosho tu.
“Bandari ya Mtwara na bandari ya Dar es Salaam zote ni bandari za Serikali, mimi sina tatizo na kusafirisha korosho kupitia bandari ya Dar es Salaam lakini na nyinyi muwe tayari kutozidisha uzito kwenye magari mnaposafirisha kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam, kutotorosha korosho na pia kutimiza masharti ya usafirishaji” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
Ameagiza Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na vyombo vya dola kuweka utaratibu mzuri utakaowezesha usafirishaji wa korosho hizo kupitia bandari ya Dar es Salaam kama ambavyo wanunuzi hao wameomba.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewataka wanunuzi hao kuwekeza viwanda vya kubangua korosho ama kuwahamisisha washirika wao kuja kuwekeza katika viwanda hivyo na kwamba Serikali itaunga mkono juhudi hizo ikiwa ni pamoja na kuweka vivutio vya kikodi.

Пікірлер: 123

  • @mohamedkassimu8789
    @mohamedkassimu87895 жыл бұрын

    Mh.Rais,simamia maslahi ya wanyonge, hata mimi niliamini lazima utaliingilia Kati TU, wewe ni Rais wa mfano duniani sio tu Tanzania .mungu akulinde Sana na akupe maisha marefu.amin.

  • @lameckbalekele2901
    @lameckbalekele29015 жыл бұрын

    Rais 2020 usihangaike kuzunguka tena kupigakampeni tunakupakula mpaka washangae

  • @wasshaincmwanza4374
    @wasshaincmwanza43745 жыл бұрын

    This man is a true and patriotic leader and above all he is absolutely genius

  • @shabanmlekwa9513

    @shabanmlekwa9513

    5 жыл бұрын

    Definitely, you are really true

  • @josephsospeter8304
    @josephsospeter83045 жыл бұрын

    Hiki kichwa nihatari kinajua mambo mengi sana

  • @mohammedjuma6736
    @mohammedjuma67365 жыл бұрын

    Raisi wangu, Mungu akulinde na akupe umri mrefu utuongoze miaka mingi, aaaaamin, asante baba

  • @kiyabonjemu9885

    @kiyabonjemu9885

    5 жыл бұрын

    Hbdy to you Mr presidaaaa

  • @kingmayatz9999
    @kingmayatz99995 жыл бұрын

    Sikukupigia kula ila hakika unanidai kula yangu 2020 nakpenda huna mpinzan

  • @mazeramatimo1110
    @mazeramatimo11105 жыл бұрын

    Nimeiona hasira yako Mh. Rais ukiona wananchi wako wanataka kuonewa Mungu akubariki. Nikutakie tu heri ya siku ya kuzaliwa Mungu akupe maisha, siku moja nitakuwa kiongozi na nitakuwa na nitaongoza kwa mfano wako na Nyerere,

  • @mwinukafundibombanjombe
    @mwinukafundibombanjombe Жыл бұрын

    😭Kwenye direcrion ya Mzee Ukilaza unaondoka.

  • @rosenamilia4140
    @rosenamilia41405 жыл бұрын

    Mh Rais wetu JPM wewe ndie Rais muwazi,mkweli mchapa kazi, mtetezi wa wanyonge na unaetoa mwelekeo sasa wananchi wako.Mungu akupe maisha marefu Mh JPM. HAPPY BIRTHDAY RAIS WETU.

  • @kingmayatz9999

    @kingmayatz9999

    5 жыл бұрын

    Nilikuwa mpinzani sana ila wewe ni rais unaejielewa sana nakupenda sana

  • @greensky9607
    @greensky96075 жыл бұрын

    Daah! Mheshimiwa Rais sina cha kuongezea, Mungu akubariki sana

  • @salumkseleman1470
    @salumkseleman14705 жыл бұрын

    Baba umenifurahisha sana asante sana mzee baba😂😂😂wanakuletea ujanja hapa wakat zao hili lina kazi c ya kitoto..... Hao wahindi wanajifanya wajanja wakat wao wenyewe ni middlemen pumbavu zao Asante magu baba Korosho yetu itanunuliwa tu alhamdulilah 👏👏👏👏👏👏👏

  • @yugakiyumbi9909
    @yugakiyumbi99095 жыл бұрын

    Mungu atupe nini, this is the best president ever. Endelea kutawala hadi uchoke mwenyewe,hakuna shida,tunahitaji Maendeleo na wewe unatuletea maendeleo na pili ww n mtetezi wa WANYONGE. Nani kama Magufuli ,We love you our President, you're doing what every well minded Tanzanian needs. Rule even 40 years,we still need you. Chapa kazi ,HAPA KAZI TU.

  • @neemamasangula7404

    @neemamasangula7404

    5 жыл бұрын

    Enzi Za Mwl. JK. Nyerere tulisema UHURU NA KAZI sasa tunasema HAPA KAZI TU BIG UP MY PRESIDENT

  • @rtvmediare805

    @rtvmediare805

    5 жыл бұрын

    Ongela

  • @agneomasonda2462
    @agneomasonda24625 жыл бұрын

    Mheshimiwa Rais nakuombea mema asante sana Mungu akupe maisha

  • @acrestv8636
    @acrestv86365 жыл бұрын

    Asante rais wetu kwa kuwapigania wakulima ..... Mwenyezi Mungu azidi kukuongoza

  • @talenterick4209

    @talenterick4209

    5 жыл бұрын

    Siku zote haki ikisimama malaghai wengi huumia sana wakati mwingi wanatafuta sehem wakosoe na si kutoa ushirikiano kwa yanayotendeka mh jpm pambana zid ya wanyonge usiwasikilize watakao kukatisha tamaa pambana zaid ya hapa ulipo yupo atakaye kulipa nayeye ni mwenyez mungu si mwanadam Mungu akujalie miaka mingi ili uitetee tanzania na fahari zake

  • @acrestv8636
    @acrestv86365 жыл бұрын

    Asante sana kwa yote unayoifanyia nchi yetu ..... Kipekee kabisa napenda nkushukuru kwa ujenzi wa barabara ya Mpemba kwenda Ileje unaoendelea .... Asante sana mh rais

  • @derickgambi8627

    @derickgambi8627

    5 жыл бұрын

    Hakika MUNGU alikuleta kwa kusudi maalum ubarikiwe sana

  • @allymichael7310
    @allymichael73105 жыл бұрын

    Sina cha kuongeza muheshimiwa Rais wangu..mwili unasisimka kila ninapokusikiliza , unayawakilisha mawazo yangu. Mungu akulinde na kila wabaya na aina ya ubaya! Pamoja tutaijenga Tanzania.

  • @kaizamulinda633
    @kaizamulinda6335 жыл бұрын

    Ila kumbe kuwa Rais si masihara. Nikisikiliza namna JPM anavyoongea kwa details na uelewa mkubwa wa mambo, najiuliza haya alijifunza lini. Anaongea vitu very technical kwa kweli.

  • @siwonikewilliam8832
    @siwonikewilliam88325 жыл бұрын

    Happy birthday Mr.President

  • @davidandrew9575
    @davidandrew95755 жыл бұрын

    Mnaenda kununua au hamuendi

  • @prospermakundi2787
    @prospermakundi27875 жыл бұрын

    Raisi wangu umenifurahisha sana,hakika unafanya kazi ya kutetea wakulima tz.

  • @paulchugu9198
    @paulchugu91985 жыл бұрын

    Nyerere II in the house.

  • @iamjoseph795
    @iamjoseph79510 ай бұрын

    I miss you Mangufuli. Rest in peace ✌️ byou are my hero up to now from Kenya 🇰🇪

  • @angelanather9640
    @angelanather96405 жыл бұрын

    Yaani nikimsikia Rais wetu mpendwa John Pombe Magufuli natokwa na machozi kwa furaha. Kweli ni zawadi toka kwa Mungu.

  • @samiahazali2027
    @samiahazali20275 жыл бұрын

    Mweshimiwa rais alipo xema tuzae alikuwa anamanisha angalia nchi zote zilioendelea zina watu wengi xana angalia apo wahindi wengi na angalia kwetu kira sehemu kuna duka la muyindi mweshimiwa anaona mbali xana mungu amuongoze katika majukumu yake 👍👍👍👍

  • @danielmmbaga976
    @danielmmbaga9765 жыл бұрын

    Hakika huyu ni raisi mtetezi wa wanyonge mungu azidi kukulinda mkuu.

  • @siwonikewilliam8832
    @siwonikewilliam88325 жыл бұрын

    Happy birthday Mr.president

  • @melickzedeckmunuo190
    @melickzedeckmunuo1905 жыл бұрын

    Mungu akubariki kwa kuwa mzalendo wa Taifa letu tunakuombea sana wana nchi wamenyonywa sana

  • @samwelmalwa9814
    @samwelmalwa98145 жыл бұрын

    Wanaompinga Mh, JPM watapata tabu sana maana utendaji kazi wake umetukuka sana. Hongera sana JPM, juhudi zako tunaziona,tunakuunga mkono na tunakuombea Mungu akubaliki.

  • @shukurumwangosi1537
    @shukurumwangosi15375 жыл бұрын

    Rais wangu nchi yangu. Haya tunayoyaandika tunatamani uwe unasoma mwenyewe ha ha ha Kiukweli Raisi wangu unawapigania wakulima wanyonge kwa kiwango kikubwa sana Tatizo watu wako (watendaji)wanakuangusha. Haya mambo sasa ulitakiwa baada ya wewe kulipigia kelele mwaka Jana ilitakiwa sasa upumzike .wanakutesa sana sana. Lakin tutafika tuu. Good job JPM

  • @japhetmombia
    @japhetmombia5 жыл бұрын

    Mungu akulinde Mh.Rais

  • @milimomashini9432
    @milimomashini94325 жыл бұрын

    Nakupata vzur MH.Rais kutoka masharik ya kati kimsing hao wengi madalali huwa wanataka supernormal profit hayo matatzo mengi yako hata kwenye zao la ufuta na mazao mengine ya biashara

  • @paulshamba1746
    @paulshamba17465 жыл бұрын

    Mungu akulinde maana wewe ni mtetezi wa kweli

  • @yusuphluwali5514
    @yusuphluwali55145 жыл бұрын

    Huyu ndie aliekapaswa akabidhiwe nchi km alivyokabidhiwa rais wa China mpk afe

  • @robertthomas7709

    @robertthomas7709

    5 жыл бұрын

    mahindi nayo vipi ndo basi tena mweshimiwa

  • @susangibai2691
    @susangibai26915 жыл бұрын

    Hahahaaaaaa, jkt. Mtabangua korosho kwa mdomo Kweli, chezea jembe we! Hakika Mh. Rais. Unakonga mioyo ya wakulima Mungu akuongoze baba.

  • @mwamengele
    @mwamengele5 жыл бұрын

    Nimejialika,..! Hehee umetisha mzazi

  • @user-pn9ii9iz8f
    @user-pn9ii9iz8f5 жыл бұрын

    The best leader in Africa

  • @jenyyusuph4973
    @jenyyusuph49735 жыл бұрын

    Kwaajili ya maendeleo yanchi yetu huyu baba alizaliwa mungu ulitupa Bure zawad ya jpm mlinde muongezee muda waungozi siku kwasikuamina

  • @allyabbas4793
    @allyabbas47935 жыл бұрын

    Rais wa wanyonge

  • @makumbele
    @makumbele5 жыл бұрын

    Ukisikia Raisi basi ndio huyu.

  • @isackjuma7973
    @isackjuma79735 жыл бұрын

    VIVA magufuli VIVA

  • @hyeragerald4442
    @hyeragerald44425 жыл бұрын

    Nawaza cha kufanya ili kukuongezea muda wa uongozi. Hakuna namna

  • @khadijaabdalla1011
    @khadijaabdalla10115 жыл бұрын

    This is my president. ..

  • @raphaelpaschal7892
    @raphaelpaschal78925 жыл бұрын

    mzee hongera sana jitahidi ufike maswa wananchi tunatahabika maji ayatoki wilaya nzima wiki ya tatu sasa fatilia mzee maji ni uhai

  • @petercosmas4376

    @petercosmas4376

    5 жыл бұрын

    Ni kweli kabisa nmetka juzi huko tabu tupu

  • @mswadikubushumbilo7170
    @mswadikubushumbilo71705 жыл бұрын

    mzee umenifurahisha speech yako yale,

  • @edwinmalale1513
    @edwinmalale15135 жыл бұрын

    ohooo hii ya kubangua kwa mdomo tusiende kichwakichwa asije akaangiza watanzania wote wabangue kwa mdomo

  • @geraldlazaro4523
    @geraldlazaro452310 ай бұрын

    Yessssssssssssssss assessed tanzaniaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

  • @jacksonrwebangira9446
    @jacksonrwebangira94465 жыл бұрын

    What a great president!

  • @oscarmisiru9725
    @oscarmisiru9725 Жыл бұрын

    This is the Man of Yes and No, no mbambamba

  • @BennyChristian
    @BennyChristian5 жыл бұрын

    Kweli kabisa wakilaza = kilaza, fukuza tu, hata hii bodi jipu tu, watu wanunue tu hata wauza dagaa wanaweza jalibisha biashara ikiwashinda watavulia samaki

  • @jerichoseth4188
    @jerichoseth41885 жыл бұрын

    haki ya Mungu ingekuwa ni amri yangu huyu Rais angeendelea angalu hata miaka ishirini maana kumpata kama huyu tena ni mtihani japo nina amini wapo ila kumpata ni shughuli kubwa.

  • @samwelhechei8537
    @samwelhechei85375 жыл бұрын

    Hongera sana mkuu,

  • @alvangidion9366
    @alvangidion93665 жыл бұрын

    Mr president anaijua korosho

  • @salumkseleman1470
    @salumkseleman14705 жыл бұрын

    Asante baba jkt na majesh yetu yote hata kwa mdomo👏👏👏👏😂😂😂😂

  • @mussambilu229
    @mussambilu2295 жыл бұрын

    safisana

  • @ezekielnjau8830
    @ezekielnjau88305 жыл бұрын

    Huyo ndio mh. JPM, my favourite president

  • @sabatojoshwa6684
    @sabatojoshwa66845 жыл бұрын

    Hadi Bodyguard ametabasamu!!! Heshima yako mzee Magufuli

  • @boniphaceelphace1693
    @boniphaceelphace16935 жыл бұрын

    Bravo JPM

  • @kareembesta1057
    @kareembesta10575 жыл бұрын

    Good Mr president"

  • @jilugalamarco9308
    @jilugalamarco93085 жыл бұрын

    good president

  • @tajinehemia3961
    @tajinehemia39615 жыл бұрын

    Mungu Akuzidishie Hekima Na Maarifa Raisi Wetu

  • @furahamwajeka3708
    @furahamwajeka37085 жыл бұрын

    nakuelewa sana baba magu thanx maana kuongoza ni kazi sana baba piga kaziiii

  • @musamakuka8319
    @musamakuka83195 жыл бұрын

    Ibadilishwe tu katiba ya Tanzania uwendelee mbaka kuzeeka kwako ayupo mwingine wa kuvaa viatu vyako

  • @jamesngundateresia2600
    @jamesngundateresia26005 жыл бұрын

    BABA DUNIA ZIMA INAKUTAMANI UJUE UNA MADINI YASIYOISHA ALIKUZAAA ANASTAILI SIFA ZOTE DUU HATUWEZI PATA TENA MTU HUYU MIMI NASEMA HATA AKIPATIKANA ATAFIA TUU JANGWANI MAANA NCHI WATU KARIBIA WOTE NI WATUMWA WA WA WATU WEUPE TUU

  • @mswadikubushumbilo7170
    @mswadikubushumbilo71705 жыл бұрын

    mzee tunakukubali,we ni Rais wa wanyonge,asiekubali akafie mbali,

  • @mwalamimtupa4728
    @mwalamimtupa47285 жыл бұрын

    Jpm ever domination...we love u mo

  • @athumanomary1438
    @athumanomary14385 жыл бұрын

    Mwenyez MUNGU yupo pamoja nawe raisi wetu

  • @hilalihashimu5693
    @hilalihashimu56935 жыл бұрын

    Mr Prisedent anglia uwezekano wa shirika la Tanganyika perkas yale maeneo ni muhimu sana kwani yamesahaulika kwa muda mrefu sana

  • @alvangidion9366
    @alvangidion93665 жыл бұрын

    My President big up

  • @newtonmunenekaibiria6623
    @newtonmunenekaibiria66235 жыл бұрын

    Hakika huyu ni mtetezi Wa wanyonge. Kongole Rais.

  • @abdoullahioumari7442

    @abdoullahioumari7442

    5 жыл бұрын

    Hongera waelemishe

  • @pascalgwandu1657
    @pascalgwandu16575 жыл бұрын

    mungu akulinde siku zote!

  • @athumanomary1438
    @athumanomary14385 жыл бұрын

    Ewe mwenyez MUNGU tunazidi kukuomba enderea kuyapa nguvu majeshi yetu yote ewe mwenyez MUNGU mkuu

  • @jumaulamba25
    @jumaulamba255 жыл бұрын

    Hongera mtetezi wa wanyonge

  • @salimamri9488
    @salimamri94885 жыл бұрын

    🔥🔥🔥🔥

  • @singinowelnel4656
    @singinowelnel46565 жыл бұрын

    Pongezi ziende kwa John

  • @michaelmrosso2106
    @michaelmrosso21065 жыл бұрын

    😂😂 hata kwa meno jesh litabenguaa korosho..

  • @suleimanbakar1271
    @suleimanbakar12715 жыл бұрын

    baada yale kuongelea issue anazunguka kross

  • @fbr5113
    @fbr51135 жыл бұрын

    Nawapongeza sana Ikuilu mawasiliano pia kwa kuanzisha vyombo vyenu vya habaria na kwenda na wakati kama hivi mana hao waandishi wa TZ wengi tumeshawashtukia washanunuliwa na magaidi wa mabepari, wanakimbilia kutangaza habari za kuvuruga nchi zaidi kuliko habari za kuikomboa nchi. Watu wa hivyo wote wachunguzwe na wanyang'anywe uraia, tunataka watanzania wanaoitetea nchii kama Rr. Magufuli sio kuteketeza nchi na Wananchi.

  • @shifumponda666
    @shifumponda666 Жыл бұрын

    Kweli ulisema tutakukumbuka kweli nakukumbuka sasa

  • @charlesmakuri792
    @charlesmakuri7925 жыл бұрын

    Wale wanao jiita wapinza huwa hawakosi kukosoa watatia ujuaji wao et wao ndio wanajua ,upinzani huu ni chuki matusi na lawama ,zito atakosoa tu

  • @fraviansweetberty8819
    @fraviansweetberty88193 жыл бұрын

    Leo ih atupo nawewe Jpm pumzika kwa Amani

  • @petercosmas4376
    @petercosmas43765 жыл бұрын

    Nmeona mzee mmja kama haelewi kabisa,hahaaaa

  • @isayaupson7712
    @isayaupson77125 жыл бұрын

    Mheshimiwa tunaomba tuangalie upande wa mbaazi hali ni mbaya kilo mia mbili 200 mkoa wa manyara

  • @yakoboisack9054
    @yakoboisack90545 жыл бұрын

    jamani acheni siasa tunataka ela hadi mwezi wa kumi na mbili hatujapata ela kama hela haipo wapeni wahindi wanunue

  • @mbwanaomary7537
    @mbwanaomary75375 жыл бұрын

    Raisi bora wa muda wote

  • @maxmilliankibura1047
    @maxmilliankibura10475 жыл бұрын

    Mbele itabaki kuwa mbele tu speed hainashida nakuunga mkono raisi wangu hata kama tunaspeed ndogo naamini mbele tutafika tu HAPA KAZI TU

  • @mochings8012
    @mochings80125 жыл бұрын

    43:50 😅😅

  • @Michael-dl1lu
    @Michael-dl1lu28 күн бұрын

    ❤❤❤❤❤❤❤❤❤🎉🎉🎉🎉🎉

  • @ramadhanimgaya8287
    @ramadhanimgaya82875 жыл бұрын

    Piga kazi Mr President, Watanzania tupo pamoja nawe

  • @mongliclassic5642
    @mongliclassic56425 жыл бұрын

    Ndomaana 2nakunda Rais. Jpm

  • @japhetmwamlenga7078
    @japhetmwamlenga70785 жыл бұрын

    ndo uzuri wa kuchagua rais msomi huwezi kumdanganya.

  • @nyakytito4954
    @nyakytito49545 жыл бұрын

    nitaasisi maandamano ya kupinga kuondoka madaraka kwa anco magu bado tunakuhitaj

  • @fbr5113
    @fbr51135 жыл бұрын

    Tawala miaka yote Magufuli, hadi hao majambazi wa mabepari wakimbie nchi, kwanza wote wale sio Watanzani wanatumwa kuivuruga nchi. Kwa mwendo huu uwezo wa kuiendesha nchi unao hata bila msaada wa wanyonyaji wa nje, sisi hata njaa tutalala mradi ututoe utumwani, kunyonywa Tanzania ibaki kuwa historia, unaonesha njia ambayo wengi walishindwa kwasababu walikwamishwa na kuwaogopa hao wahalifu wa mabepari. Magufuli oyeee

  • @suleimanbakar1271
    @suleimanbakar12715 жыл бұрын

    kigeugeu

  • @geraldlazaro4523
    @geraldlazaro452310 ай бұрын

    Mangu baba says

  • @avax5717
    @avax57175 жыл бұрын

    Natamani nione jinsi jeshi linavyobangua korosho kwa meno.. Lol

  • @dickngimba4333
    @dickngimba43334 жыл бұрын

    Kwanini mzee usiongeze mika 30 mzeee

  • @najimcompanyltd2096
    @najimcompanyltd20965 жыл бұрын

    kama nikijana alafu huumpend magufuli inabidi ukapimwe akilii

  • @salumkseleman1470
    @salumkseleman14705 жыл бұрын

    👏👏👏👏😂😂😂😂😂👏👏👏👏

  • @athumanomary1438
    @athumanomary14385 жыл бұрын

    Ewe mwenyez MUNGU tunazidi kukuomba enderea kumuongoz kumsimamia kumrindi na kuzidi kuimalisha afya yake raisi wetu ewe mwenyez MUNGU pia enderea kuwaongoza vyema viyongoz wete wanaomsaidia raisi wetu turiongoza taifa retu

  • @titoluchagula4957

    @titoluchagula4957

    5 жыл бұрын

    Uko vizur baba piga kazi

  • @onesmombilinyi8386

    @onesmombilinyi8386

    5 жыл бұрын

    Hicho kichwa kaa nacho mbali

  • @onesmombilinyi8386

    @onesmombilinyi8386

    5 жыл бұрын

    Happy birthday mzee wa kaz

  • @wilsonbrownkajiba650

    @wilsonbrownkajiba650

    5 жыл бұрын

    😀😀😀

  • @stephenshio588
    @stephenshio5885 жыл бұрын

    Hongera President hili ndo tulikuwa tunalitaka kwa wananchi fukara

Келесі