KIPINDI MAALUM CHA RAIS DKT.JOHN MAGUFULI ALIPOZUNGUMZA NA VIONGOZI WAKUU WASTAAFU

Hii ni mara ya kwanza kwa Mhe. Rais kukutana na viongozi hao wakuu wastaafu na kupokea ushauri na maoni yao juu ya uendeshaji wa Serikali na mustakabali wa Taifa.
Katika mkutano huo viongozi hao wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuwaita kwa lengo la kusikiliza ushauri na maoni yao, na wamempongeza kwa kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kipindi kifupi cha miaka miwili na nusu tangu ilipoingia madarakani.
Viongozi hao wamemshauri Mhe. Rais Magufuli kuimarisha na kujenga taasisi zinazosimamia uendelevu wa kazi nzuri zinazoendelea kufanywa na Serikali ya Awamu ya Tano zikiwemo utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo kama vile ujenzi wa reli, mapambano dhidi ya rushwa, kuimarisha nidhamu kazini, kutilia mkazo watu kuchapa kazi, kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Serikali na utoaji wa huduma za jamii.
Viongozi hao wamesisitiza umuhimu wa kudumisha amani kwa kuhakikisha haki inatendeka, kutathmini matatizo ya wananchi na kubuni mbinu za kuyatatua, kusimamia kwa ukaribu shughuli za kilimo na ufugaji ambazo zinaajiri Watanzania wengi na ni muhimu kwa maendeleo ya viwanda na kuboresha kiwango cha elimu.
Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amewashukuru viongozi hao kwa maoni na ushauri waliompa na amewahakikishia kuwa ataufanyia kazi.
Mhe. Rais Magufuli amewaeleza viongozi hao juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali hivi sasa ikiwemo kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Serikali ambao umeongezeka kutoka Shilingi Bilioni 800 hadi kufikia Shilingi Trilioni 1.3 kwa mwezi, ujenzi wa reli ya kisasa kuanzia Dar es Salaam hadi Dodoma utakaogharimu Shilingi Trilioni 7.26, kujenga mradi wa umeme katika mto Rufiji (Stieglers’ Gorge) utakaozalisha Megawati 2,100 za umeme, kutoa elimu ya msingi na sekondari bila malipo na kuongeza mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.
Mhe. Rais Magufuli amewahakikishia kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea vizuri na kwamba itaendelea kutatua changamoto ambazo bado zipo kwa juhudi kubwa ili Tanzania iwe nchi nzuri kwa Watanzania wote.

Пікірлер: 54

  • @Epicmarkmedia
    @Epicmarkmedia6 жыл бұрын

    Ninafurahi sana kwa hili mheshimiwa Rais. Hongera. Pia pongezi kwa wastaafu kukubali kutete na rais.

  • @nyanda427
    @nyanda4276 жыл бұрын

    Well done wazee wetu, Mungu awabariki sana

  • @peterlibota1052
    @peterlibota10526 жыл бұрын

    Ni heshima kubwa sana aliyoitoa Rais JPJ Magufuli kwa kutambua uwepo wa hao waliomtangulia katika kuijenga Nchi hii.Mungu Ibariki Tanzania,Mungu wabariki Viongozi wetu wote kila mmoja na sehemu yake ya Utendaji.Amina.

  • @jameslikata1581
    @jameslikata15818 ай бұрын

    Mungu aiweke roho yake pema.

  • @kilimanjaroICE
    @kilimanjaroICE6 жыл бұрын

    Wooooow!!! That was so deep and amazing at same time. Magufuli is probably the best President in the Continent right now and the history will prove that. Tanzania Kwanza.

  • @dmstephano8643
    @dmstephano86436 жыл бұрын

    Nimefurahi sana kuwaona viongozi wetu wakiwa pamoja 🙏🙏🙏god bless my Tanzania

  • @mukhtaribura6159
    @mukhtaribura61594 ай бұрын

    M,mungu awake roho yake peponi ameen

  • @alexfrance5486
    @alexfrance54866 жыл бұрын

    I always appreciate my President for the great job

  • @bonifacegamba495
    @bonifacegamba4956 жыл бұрын

    Mungu ibariki Tanzania Mungu mbariki Rais wetu

  • @edwardedward2520
    @edwardedward25206 жыл бұрын

    Hongera sana Mh. Rais wetu mpendwa Mungu aendelee kukulinda kukupigania.... Si kazi nyepesi MTU lelemama asingeiweza.

  • @amabilis-mariesangu9500
    @amabilis-mariesangu95006 жыл бұрын

    This is absolutely beautiful to see. Precedence is the way to go..Mungu Ibariki Afrika Mungu Tubariki watanzania

  • @deusgabri
    @deusgabri6 жыл бұрын

    Mhe. Benjamini kaongea mstari mnyoofu.......

  • @greensky9607
    @greensky96076 жыл бұрын

    Hongera sana Mh. Rais wangu kwa uamuzi wako wa kuwakutanisha wastaafu wa ngazi za juu kabisa katika nchi yetu na kuchota baraka zao. Ninakuamini katika kusikiliza na kutenda, kwa jitihada zako Tanzania ya mfano inakuja kwa kasi ya ajabu, ni lazima sasa kila mtu atambue ama afahamu kuwa kuna SERIKALI, na ni lazima iheshimiwe. Umeweza kwa muda mfupi kulirudisha Taifa la uchapa kazi, japo bado wachache hawajaweza kukuelewa, WATAKUELEWA TU. TANZANIA TUTAIJENGA WENYEWE, AMANI, UPENDO NA UTULIVU TULIONAO TUTALINDA KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE. VIVA JPM, ASANTE MAWASILIANO IKULU.

  • @agneomasonda2462
    @agneomasonda24626 жыл бұрын

    Hongera sana Mheshimiwa Rais Magufuli

  • @abeidmayanga809
    @abeidmayanga8096 жыл бұрын

    our greatest president in Africa ubarikiwe

  • @yahayaseif5175
    @yahayaseif51756 жыл бұрын

    Tunaiomba ikulu ikitoa habari wakalimani wawepo kutafsiri kwa lugha ya alama. Viziwi wa tanzania nao pia wanadai haki yao kupata habari bila kubanwa uhuru wao wa kupata habari. Yahya al sawafi. DEAF PERSON. chake chake Pemba

  • @sk-wj9or
    @sk-wj9or6 жыл бұрын

    Umeshinda Magufuli good way ahead. Well done.

  • @yusuphshabani7285
    @yusuphshabani72856 жыл бұрын

    mungu akujaalie maisha marefu kiongozi wetu kwasbbu yeye ndie aliekuchagua mtetezi wawanyonge.

  • @prospermakundi2787
    @prospermakundi27876 жыл бұрын

    Safi sana raisi wetu Mungu azidi kukuongoza

  • @khamismallya7588
    @khamismallya75886 жыл бұрын

    Ziundwe taasisi zitakazosimamia serikali ili tusije rudi nyuma tena ushauri si wakuacha huu

  • @athumanomary1438
    @athumanomary14386 жыл бұрын

    Mwenyez MUNGU tunazidi kukuomba enderea kumuongoz raisi wetu

  • @ValEmaChannel
    @ValEmaChannel6 жыл бұрын

    And that's all God bless the retired and Our currently President and God bless Tanzania. Fulfill #GreatTanzanianDreams

  • @shukuruexperius5035
    @shukuruexperius50353 жыл бұрын

    Mzalendo wa kweli hongera sana Jpm haijawahi kutokea wewe ndio wa kwanza

  • @ambelecheyo5667
    @ambelecheyo56676 жыл бұрын

    Nakupenda buree rais wangu.

  • @dickaugustino2214
    @dickaugustino22146 жыл бұрын

    Good Mr president j.p.m, sisi wanyonge tupo na tunakutazama, tukisubiri useme kitu ktk hizi taasisi za mifuko ya bima,pesa kutoka isiwe mpaka MTU afikishe miaka amsini na za zaidi,bora kuwe na utaratibu kwamba MTU akichukua pesa zake, aende akafanye masuara ya msingi.kuepusha utegemezi baadae.

  • @yusufurahabiamu6052
    @yusufurahabiamu60526 жыл бұрын

    Mungu akuongezee hekima na busara zaidi amen

  • @NyakiMollel
    @NyakiMollel5 ай бұрын

    Kuna mzee kaongea kitu cha ajabu cjui alitawalaje hii nchi

  • @emmanuellyatuu4103
    @emmanuellyatuu41036 жыл бұрын

    Great indeed Mr President...nimekuelewa sana

  • @omaryyusuph3251
    @omaryyusuph32516 жыл бұрын

    Ahsante warioba na malecela

  • @dickaugustino2214
    @dickaugustino22146 жыл бұрын

    Better be so, its bitter but sweet!?

  • @hassansamata3666
    @hassansamata36666 жыл бұрын

    Mzee mwinnyi umeongea vizuri

  • @kalundemedia242
    @kalundemedia2426 жыл бұрын

    Ninafikiri sana namna ya kuwashawishi watanzania wote wakubaliane nami kuuondoa utaratibu wa "Periodic Election" kwa kiti cha Urais, ili Rais DKT JOHN POMBE MAGUGULI ubaki madarakani mpaka utakapoona kuwa kuna haja ya kustaafu mwenyewe; maana ktk Afrika na duniani kote sjaona Rais Mzalendo kama wewe. Tanzania ilikokuwa imefikishwa ni kubaya hakuna mfano, lakini leo ni miaka miwili na nusu tu ya utawala wako mambo yamegeuka na kuwa mazuri kiasi hiki. Nakuombea kwa Mungu akujalie Afya njema, ili utufikishe salama ulipopalenga.

  • @edwardedward2520
    @edwardedward25206 жыл бұрын

    Indeed it is very clear..

  • @abellabv
    @abellabv6 жыл бұрын

    Mstarini: (Wimbo wa Taifa - kwa sauti Kuu) "...Heekima, Umooojaaa, na Amaaaniiii: hiiiziii ni ngao zeetuuu,..." Darasani: (Salaam - kwa sauti Kuu) "Ili tuendelee twahitaji vitu vinne: Watu, Ardhi, Siasa Safi, na Uongozi Bora. SHIKAAAMOOO MWAAALIM."

  • @sumaiyaturky7023
    @sumaiyaturky70236 жыл бұрын

    Fantastic speech. Kweli ni mtu wa Mungu. Hats off for my President.

  • @greensky9607
    @greensky96076 жыл бұрын

    The Making of Tanzania to be Great Again

  • @athumanomary1438
    @athumanomary14386 жыл бұрын

    Ewe mwenyez MUNGU ewe mwenyez MUNGU ewe mwenyez MUNGU tunazidi kukuomba enderea kumuongoza kumsimamia kumrinda kumuipushia kira yario mabaya na zidi kuimarisha afya yake raisi wetu ewe mwenyez MUNGU mkuu

  • @ValEmaChannel

    @ValEmaChannel

    6 жыл бұрын

    Athuman Omary Amen. Mungu asikie kuomba kwetu

  • @abellabv

    @abellabv

    6 жыл бұрын

    Isaac Valema. AMEN, AMEN, AMEN.

  • @ahmed59122
    @ahmed591226 жыл бұрын

    IS GOOD MAN

  • @mosesmkopi4786
    @mosesmkopi47864 жыл бұрын

    Nimerud kusikiliza hekima za Muheshimiwa Dr Benjamin william mkapa may his soul rest in peace

  • @allyfutto8763
    @allyfutto87636 жыл бұрын

    Hakika ni Faraja kubwa sana kuwaona wazazi Viongozi waliotutowa huko tulikotoka mpaka hapa tulipo wapo salama na wanayo Amani mimi binafsi hili ni tukio kubwa sanakabisa maana Dunia ya sasa hakuna Nchi ya mfano huu ulimwengumzima. watanzania wamefarijika sana na mtindo huu Bora, Tanzania JUU!!! Juu!!! Juu!!! JuuZaidi!!!!!!!

  • @seifhabibu9890
    @seifhabibu98906 жыл бұрын

    Sasa naino tanzania inavuka maana imepata mtu wa kuivusha, miaka 15 ijayo wakenya watakua nyuma yetu

  • @japhetdaud3889
    @japhetdaud38896 жыл бұрын

    Ama kweli MUNGU awafungue macho watu yawezakuwa hawaoni yale anayotenda mh. Magufuli hajawahi tokea Rais kama huyu :Labda kama msemo usemao watakuwa ma macho hawataona ,masikio wanayo hawasikii, akili wanayo hawaitumii - hivyo Mungu awasaidie watanzania wanaobeza

  • @ibraobed8273
    @ibraobed82735 жыл бұрын

    Kikwete vp mbona ajatimba hapo.

  • @HakunaMatata_2024
    @HakunaMatata_20246 жыл бұрын

    safi

  • @Weplanetitsolutions

    @Weplanetitsolutions

    6 жыл бұрын

    That is great things our president did it should be a continously

  • @omariwazirikibao1932

    @omariwazirikibao1932

    4 жыл бұрын

    Wataona tu hawana nafasi nchi hii

  • @agrikolaleo677
    @agrikolaleo6776 жыл бұрын

    JAMAA HAJAACHATU ZIARA?

  • @nyanyimarwa2637

    @nyanyimarwa2637

    6 жыл бұрын

    agrikola leo Anapenda sana ziara jamaa yetu

  • @omariwazirikibao1932

    @omariwazirikibao1932

    4 жыл бұрын

    Aaaa hajamumunya mzee mkapa

  • @omariwazirikibao1932

    @omariwazirikibao1932

    4 жыл бұрын

    Mzee mbele tuu hakuna kurudi nyuma hicho kiti watakiona hivyohivyo tuu

Келесі