Profesa Issa Shivji: Tusikubali Kuwa Nchi ya Kufanyiwa Majaribio, Ni Juu ya Dira ya Taifa 2050
Profesa Shivji: Dira ya Taifa Haina Muda Maalum.Tusikubali Kufanyiwa Majaribio
Akizungumza leo Juni 08,2024, katika kongamano la kwanza la kitaifa la maandalizi ya dira ya taifa ya maendeleo lililofanyika katika ukumbi wa Nkurumah, Profesa Issa Shivji ameeleza kuwa dira ya taifa ni tofauti na mipango ya maendeleo yenye muda maalum.
"Dira haina maana ya mpango wa maendeleo, mpango wa maendeleo unakuwa wa muda maalum. Kwa maoni yangu dira haina muda maalum," ameeleza Profesa Shivji.
Profesa Shivji alifafanua Zaidi kuwa moja ya mfano wa dira ya taifa ni Azimio la Arusha. Akijibu hoja hii Waziri wa OR Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo alieleza kuwa wameyapokea maoni hayo.
Katika wasilisho lake hilo Shivji ameasa juu ya taifa kuepuka kufanyiwa majaribio katika utengenezaji wa dira yake.
"Tusikubali kufanyiwa majaribio, majaribio yaliyofanyika miaka ya 1960 yanatosha. Tuwashirikishe wananchi kikamilifu popote pale walipo tupate maoni yao kuhusu nchi wanayotaka, Tanzania wanayoitamani, matamanio yao yapewe kipaumbele.Hii haiwezekani bila kuwa na mjadala wa kitaifa," alieleza Profesa Shivji.
Alifafanua Zaidi: "Tusifanye ile tuliyozoea wananchi wanatoa maoni, halafu wataalamu ndio wanachambua maoni haya. Popote pale walipo wananchi; vijijini, viwandani, mashuleni na kadhalika ili kujenga muafaka wa nchi tunayoitaka. Na mengine ya kupanga mpango wa muda mrefu wa muda mfupi itafuata."
Пікірлер: 16
Nimekubali lecturing ya professor Issa shivji, you will be my teacher forever. Your professionalism will remain in the heart of Tanzanian forever.
Maoni mazuri ya Prof Shivji. Wkt wanachi wakishirikishwa kikamilifu kutoa maoni ya DIRA ya Taifa, Serikali kwanza iwaelimishe wananchi aina na kiasi pia matumizi ya Raslimali zote muhimu zilizomo Nchini.
Kweli kabisa tufanye mijadala kama hii mingi kabla ya kuwapa wataalamu kututengenezea mipango ya kinadharia isiyotekelezeka. Asante profesa.
Asante sana mzee professor kwa darasa huru yaaani unaongelea mambo kwa kuunganisha dot kama slow poison 😊😊
Tunachangamoto kubwa ya wanasayansi katika kila nyanja muhimu nadhani ingefanyika tathmini kwanza ya uwezo wa kuandaa DIRA kisayansi ili tusije kuingia kwenye mtego ule ule wa Miaka 60 iliyopota. Given mazingira ya Dunia inahitaji zaidi ya Ujanja (smartness) kuweza kukwepa mitego ya Mataifa makubwa Duniani ambayo yanafaidika na hali tuliyonayo. Safari ni ngumu na ndefu lakini hatuna budi kuianza. Mungu ibariki Afrika , Mungu ibariki Tanzania.
Hawa ndo think-tank wanaotakiwa. Na siyo chawa- watengeneza dira.
Akili kubwa
Serikali imeshindwa kusimamia kampuni za Kitanzania kuendesha BRT. Anapewa mwarabu. Atakusanya fedha atazipeleka kwao. Ataondoa fedha nchi na kuzipeleka nje.
Hakika kama watanzania hatujutii wew kusomeshwa na rasilimali ya wazazi wako na ya Tanzania, wew ni mtanzania mkweli.
Mzee saivi watu Ni machawa tu😅
Je,vijana. Wananchi, wattaalam,hasa wanauchumi, wanasheria wanao uwezo wa kuona mbele, wanao uzalendo, wako huru, tunaelewa mambo muhimu kwenye Dirac? Na je, wale wananchi wachache waliozoea kupanga Dirac ya taufa kwa maslahi yao wamelala?
@oscarsagara8813
28 күн бұрын
Na aidha hata hawaelewi kabisa kilichosemwa na proff hapa...,amewachanganya kabisa.
Kwani hawa wanathaminiwa??? Kulliko wasaniiii!!!
Sasa wewe jifanye huelewi kana kwamba wenye dhamana hawaelewi.