Priva wa Yanga atoa ombi kwa Jokate, amtaja Chama

Meneja wa Kitengo cha 'Digital' wa Klabu ya Yanga, Priva Abiudi 'Privaldinho' ametoa ombi kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Jokate Mwegelo la kuboreshwa kwa viwanja ili viweze kuwa na hadhi ya kimataifa akitamba viweze kuendana na hadhi ya wachezaji wa timu yake, Clatous Chama na Pacome Zouzoua.
Meneja huyo amesema hayo aliposhiriki hafla ya kutoa hamasa kwa vijana kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na vijiji na vitongoji 2024 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa leo Jumamosi Julai 6, 2024.
Aidha, ameongeza kuwa kama Mwalimu Julius Nyerere aliweza kuvijenga viwanja vyote hivyo, anatumaini Rais Samia Suluhu Hassan ataweza kuvitunza viwe viwanja bora kwa manufaa ya vijana.

Пікірлер

    Келесі