Mkenda awakumbusha wananchi Rombo kuwaepuka wachonganishi

Rombo. Mbunge wa Rombo ambaye pia ni Waziri wa Elimu, Profesa Adolf Mkenda amewataka wananchi wilayani humo kutokufanya makosa kwenye chaguzi zijazo kwa kusikiliza maneno ya porojo ambayo yanawachonganisha viongozi na wananchi.
Amesema wananchi wanapaswa kuelewa kuwa siasa siyo porojo bali ni maendeleo, hivyo akawataka kuendelea kuwaamini viongozi wao kwa kuwa ndiyo waliowapa dhamana ya kuwaongoza na kuwaletea maendeleo.
Mkenda ameyasema hayo leo Julai 5, 2024, wakati akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara ambao uliofanyika katika Kata ya Mengeni, wilayani humo, Mkoa wa Kilimanjaro.
Na Janeth Joseph

Пікірлер