Dizasta Vina - Kesho
Музыка
Official Music Audio of the record Kesho
Written and Performed by Dizasta Vina
Music by Ringle Beatz
Produced by Ringle Beatz
Audiomack - audiomack.com/dizastavina/son...
Boomplay - www.boomplay.com/songs/635549...
Mdundo - mdundo.com/song/2081302
Spotify - open.spotify.com/track/60dmJt...
lyrics - genius.com/Dizasta-vina-kesho...
Other Musical contents
Audiomack - audiomack.com/dizastavina
KZread - / dizastavina
Deezer - www.deezer.com/artist/67967532
Apple music - artists.apple.com/a/profile
Mdundo - mdundo.com/a/2263
Genius - genius.com/DizastaVina
Boom play - www.boomplay.com/artists/3288... - artists.spotify.com/c/artist/...
Connect with Dizasta Vina on social medias
Instagram - / dizastavina
Twitter - / dizastavina
Facebook - / theblackmaradona
Business: Pan.authentik@yahoo.com
Website - bio.link/dizastavina
Lyrics
Okay
Wanasema tomorrow is the mystery
Wanasema tomorrow...
Leo zawadi ikumbatie, jana ni History
Ya jana hayawezi yakafana kwenye script hii
Wanasema tomorrow is the mystery
Wanasema tomorrow...
Leo zawadi ikumbatie, jana ni History
Ya jana hayawezi yaka....
ah Kesho nafasi ya kuanza upya
Kumaliza kuishi nafasi ya kuanza kufa
Kuivunja sheria nafasi ya kufata ruksa
Kuikumbuka jana au kuanza kuifuata FUTURE
FUTURE ni leo siku ambayo miti hukimbia
Jua hushuka upendo wa marafiki HUFIFIA
HUFIFIA wimbi la wanafiki huingia
Kesho ya TUMAINI hubakia
TUMAINI shika walau shika walau
Na ujifunza kuziba kombe pindi anapopita nyang'au
Akishapita tenda wema alafu kisha sahau
Na uchunge unaponena watakuzika WADAU
WADAU walikuwa uchi ukawavika mavazi
Nyumba yako ikavunjika wakakunyima hifadhi
Je utasamehe utasahu kulipa kisasi?
Au kesho itakukuta umeshika RISASI?
RISASI nawaza wapi itakukutisa kesho
Utatoroka kambi ama utavungia Ghetto
Tusipofikia lengo utahama ukoo kwa kitu kidogo
Au utaiitumikia NEMBO?
NEMBO ya mjeshi ninayekaza mwendo kishujaa
Kama unavyoza nyonga kwenye tendo la zinaa
Napiga goti nashukuru uwepo wa sanaa
Kihisia nawapeleka kesho MAJAMAA
MAJAMAA walikuwa wavivu hawakukazana
Waliishia kuamini kuwa kuna wingu la laana
Wali-set mipango ila siku hazikufanana
Huwezi kuikabili kesho kwa mbinu za jana ah!
Wanasema tomorrow is the mystery
Wanasema tomorrow
Leo zawadi ikumbatie, jana ni History
Ya jana hayawezi yakafana kwenye script hii
Wanasema tomorrow is the mystery
Wanasema tomorrow...
Leo zawadi ikumbatie, jana ni History
Ya jana hayawezi yakafana kwenye script hii
Nakuwekea Logic penye Faith
Nakutazama ukishahama nakuwekea topic kai-debate
Ninakunyima msosi kwenye Plate
Njaa ya kesho ikufunze kuheshimu pochi yenye PAY
PAY huna unatia neno kwenye bao
Ukirudi unalalama kuhusu kesho ya wanao
Myahudi ukisujudu kwenye uwepo wa Farao kwa wayahudi
Utaishia kwenye Tempo ya KARAO
KARAO kazikwa kama Historia ilivyozikwa na jana
Kesho ni siku ya kujitwika lawama
Kesho ni mbali natumai nitafika salama
Najipa moyo kisha ninaibusu picha ya MAMA
MAMA sishiki simu wakati na-drive sitii vocha
Na mafuta full tank kwa gari sisikii uwoga
Big G za kutosha, Chupa za maji na Diclopa
Na Cd za muziki wa Papii KOCHA
KOCHA kasema Kesho inataka bidii tosha
Nawaeleza watu wangu na bado hawasikii hoja
Wamesahau kesho ni nini, Niliwaamini leo najuta
ila kesho sirudii KOSA
KOSA ni kuchoka maana akili haifikiri
Taswira ya kesho naiona na mboni hazihimili
Kelele zimeshamiri masikio yameshagota na
Na mdomo unaropoka, Dunia haina SIRI
SIRI ikasambaa viganja vikanakiri
Miguu ikalemaa ila ubongo ulikariri
Tumbo halikujaa na mwili haukunawiei
Kesho ifike mapema inikute nipo Kamili
Wanasema tomorrow is the mystery
Wanasema tomorrow
Leo zawadi ikumbatie, jana ni History
Ya jana hayawezi yakafana kwenye script hii
Пікірлер: 227
The Great Dizasta Vina 🔥🔥🔥
Uwepo wa haya madini ,inabidi ujulikane kote, kuna wa2 wanaretire hip hop, wengine wanakufa. Wanakosa basic needs za kufeed brain zetu kama hizi✊️
Huwez kuikabiri kesho Kwa mbinu za Jana✌️✌️🎧
Mwenye connection na huyuu jamaa dizasta naombeniii
KESHO NAFASI YA KUANZA UPYA gonga like kama umeenda hii
BIG NACOMMENT LEO ILA KESHO NIPE NGOMA MPYAAA🙌🙌😂😂😂😂
Asante kwa ku pay homage kwa ushairi wa kimapokeo; mistari umeipanga minne minne (tarbia) kama beti, halafu umetengeneza "mkufu" kwa kurudia neno la mwisho la ubeti kwenye ubeti unafuata mtindo wa aina ya mashairi ya Pindu! We ni noma!
Huyu mwamba ni wachache wanamuelewa halaf hana pupa na upepo wa mziki wa bongo ila anaamin kwakila anachosema kuwa ni sahihi so ipo sku ataeleweka kwa umma i do appreciate you Vinna
huwezi kuikabili kesho kwa mbinu za jana
Dizastavina akili kubwa kwenye uandishi🫡🫡🫡
Upendo wa marafiki hufifia ( nan mwingine kaona pic ya rapcha kwa mbaliiii)
Kuifwata ruksa - mwinyi Upendo wa marafiki hufifia -rapcha Je utasamehe utasahau kulipa kisasi ? -Lisu Utahama ukoo -lowasa 😂 Huwezi kuikabili kesho kwa mbinu za jana -Chadema Myahudi kwenyew tempo ya falao -baba levo Kalao kazikwa kama historia - Mengi Dmt the best artists we will ever see 🙌🫡🇹🇿
@eaglemaris327
Жыл бұрын
Good
@PhilimonAmbilikile-ri1iz
10 ай бұрын
Nimekuelewa
@mikewmtui2727
Ай бұрын
Khaa 🔥
Huwezi kuikabili kesho kw Mbinu za Janaaa
Huwezi kuukomoa mmea Kwa kuumwagilia maji machafu harakati zangu za ujamaa kama kama mision ya siafu!Kesho imenigusa sana kama unaona kilichonikuta days ago nimefanya kazi kubwa sana kweny taasisi flan halaf nimeliwa kichwa Kwa unafiki ila kesho inanipa nguvu ya kuipigania nembo ya mjeshi
Kesho ni mbali sjui kama ntaifika salama.. Najipamoyo kisha naibusu picha ya mama.❤❤ Umenikumbusha my late mama.
Hii ni chakula tosha ya ubongo..🔥🔥
Tisha san, huyu jamaa ana Kill mastanza namkubal san
Wanao fanya hip-hop isishike namba moja ni madj siku nzima nyimbo zinazopigwa radio tv ni kinabonge la nyau na
Mawe juu ya mawe
Dizasta Ni Akili Kubwa🔥🔥🔥
Muundo wa Pindu... Neno la mwisho, linaanzisha Beti mpya... Utunzi wa akili nyingi sana
Oooy huyu mtu ni kisanga
Kazi Kali sana ,. Fundi sna vina ,,
Dizastar ni mmoja tu wengine ni paka-paka pusi-pus,, oya kama haujasuscribe fanya usubscribe hiki kichwa sio cha kukosa nyimbo zake Jah bless vina keep up💪💪💪
black maradona 💥💥 midundo ieendlee mwafrica
Wa kwanza ktk uwanja wa comment, Disasta Vina you're always the real and Best rapper alive, Mungu ndo Kila kitu ipo siku wataelewa tu, one love from Zanzibar.
Hyo background ndo inaleta majibu ya hii mistari, wewe ni 🔥🔥🔥
Uyu jamaa
Wadau walikuwa uchi ukawavika nguo
Dom city tunaku appreciate sana broo
HipHop Legend of All the Time,On Top fvr Bro
kazi nzuri brother dizasta hii nchi umebaki peke yako wa madini kama haya
Noma sana
Kichwa kilicho jaa madini🙌🙌
Uwezi kuikabili kesho kwa mbinu za jana✍️📌💥💥▶️🎶🎶🫡
Ni noma kt og
Huwezi kuikabili kesho kwa mbinu za jana💥💥💥DIZASTA "hakuna rapper atakaye survive bongo akikutana na MAJANGA
Nakubal broo
Madj maboya kweli eti wanapanga top ten tena za hip hop vina hayumo harafu ngoma ya kwanza dunga mawe
Nakubar xanaa we ni mtu na nusu kwenye vina unatisha kila ngoma ni kari hujaway tuangusha mashabiki zako
Ooh men 🎉🎉🎉🎉🎉🎉🎉🎉
Mbeya City boy
Nimegundua kuna mtu atageuzwa sajna kabisaaaa
Kesho ndio siku ya kuanza upya ... let's do it...tuifanye kesho hii ngoma iwe kwenye mainstream ....🇹🇿🇹🇿
Noma
Kumaliza kuishi nafasi ya kuanza kufa😅
Dizasta ni zaidi ya jini
Yan ww hakuna kama ww bro 🔥🔥🔥🔥👑👑🤴🤴
Kwahyo tumekubaliana BIFU na COSMAS imeisha ....?😂😂Sema nlitaman iendelee maana MIMI sku zote DIZASTA N BEST RAPPER OF TZ Comments zngne bak nazo nyinyi😊
kesho ndio starter yetu💪
Huwez kuikabil kesho kwa mbinu za jana
Asante kwa chakula cha ubongo@dizastavina
Mmmh nabiih wa kweliih ajitangazi vina vina kweli tungo wanaelewa wenye uelewa🔥🔥🔥
Vile ulikua una tease hii Ngoma insta nilitafuta sana sikujua kama ilikua haijatoka Leo ipo naikumbatia kama zawadi kesho ni mystery VINA VIPO MAHALA PAKE....ELIMU KUBWA KWENYE UANDISHI HII NGOMA.... SALUTE D..🎉❤❤❤❤
kaka Best rap of All Time. Ila mimi sijapenda tuu hiyo sura ina Waka Waka na rangi za upinde
Hataree 🔥💯🥵
Noumaaaaaaa
Huwezi kuikabili kesho kwa mbinu za jana...@Vina
Leo zawadi ikumbatie ya Jana NI history.
Dammn,,, the guy is killin. This guy is a master of hip hop,, I compare him with none of them rappers in a game
Brilliant.. Hip Hop is on safe hands 🔥 support from+254🇰🇪
❤❤❤ iko juu Sana pamoja Sana Real nigga tokea huku Kenya
Shikamoo kaka Dizasta
Vina the Brainer✊🏿✊🏿✊🏿✊🏿
My Best rapper in est afrka heshima kwako bro Dizasta vina🤜
Mwamba hajawahi niangusha mi ni fans wako toka kipindi chá goma la kanisa 💯💯💦🔥🔥
💥💥💥💥💥💥💥💥dizasta moto
Ukisikilizwa hautochukuliwa poa hata siku moja... chap chap naaccept wee ni fire bro
One love
Panorama my big brother ww upo peke ako na kitaa tunajua thaman yako let's keep it up ❤❤❤🎉
Vina
Kz pw
the best
kesho
The first one to comment.... Kesho the verteller.... My best song
For generation ya 2090 nilipata bahati ya kusikiliza hip hop Kali from big brain dizasta vina 2023..
Alafu kama umegundua hii nyimbo dizasta anajaribu kuwasaidia kufumbua mafumbo yake kwa kutumia picha zinazopita nyuma ya hii video this guy is so fucking talented no matter what 😂❤🐐
@kilimapozimuvinajr.
Жыл бұрын
Huwez kuikabili kesho qwa mbinu za Jana nikaona picha ya nembo ya chadema. Ahsant broo umenisanua.
@rahimmlanzi185
Жыл бұрын
Jee utasamehe au utalipa kisasi,,, Tundu lissu kadislay background daah...Asante bro nami nimesanuka...
@OptatusHaule-hk2zg
Жыл бұрын
Kweli kabisa ... Jamaa hii ngoma Ni ya siasa 😂😂
@japharysety6890
Жыл бұрын
Laivu umenisanua mwamba alipo sema utahama ukoo kwa kitu kidogo nmeiona picha ya lowasa
@hassanmakweto6299
Жыл бұрын
Oya brother umetisha sana izi picha zinazopita kwenye hii video nimegundua wote ni wanaharakati💪💪huyu jamaa sio wa sayar yetu kabisa
Kesho nafasi ya kuanza upya. Kumaliza kuishi nafasi ya kuanza kufa. KWENYE HIP HOP UPO PEKE YKO "DZVN"
😮 daah bro nikipata pesa nakuja mbeya town center apo najenga sanamu yako Dizasta
This man ni Best rapper of all time respect sana my G🔥
Big up Sana broo 🎤🎶🎹
NOMA
D teacher🙌🙏
Wooo
💪💪💪💪
🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
🔥🔥🔥🔥🔥
🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥 atariiiii snaaaaa
arts 🎉
My brother🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
uandishi✊🏿
🌍
King is back
More love bro
Huwezi kuishinda kesho kwa mbinu za jana...Vina Dizasta.🙌🔥
VINA Mwenyewe, you got this man💪 love from 🇧🇮Burundi! napenda nyimbo zako, let the following be a storytelling😊💪
Dizasta hujawahi kuniangusha 🔥🔥🔥
📌
Kaka uliweka tu basi lazima niwe wakwanza kusikiliza maboya hawatupati
Dizasta Is Not Pregnant But Always Deliver Good Stuff🔥🔥🔥