Dizasta Vina - A confession of a Mad Philosopher
Музыка
Official Music Audio of the record A confession of a Mad Philosopher
Written and Performed by Dizasta Vina
Music by Ringle Beatz
Produced by Ringle Beatz
Audiomack - audiomack.com/dizastavina/son...
Boomplay - www.boomplay.com/songs/635535...
Mdundo - mdundo.com/song/2081293
Spotify - open.spotify.com/track/3831rX...
lyrics - genius.com/Dizasta-vina-a-con...
Other Musical contents
Audiomack - audiomack.com/dizastavina
KZread - / dizastavina
Deezer - www.deezer.com/artist/67967532
Apple music - artists.apple.com/a/profile
Mdundo - mdundo.com/a/2263
Genius - genius.com/DizastaVina
Boom play - www.boomplay.com/artists/3288... - artists.spotify.com/c/artist/...
Connect with Dizasta Vina on social medias
Instagram - / dizastavina
Twitter - / dizastavina
Facebook - / theblackmaradona
Business: Pan.authentik@yahoo.com
Website - bio.link/dizastavina
Lyrics
Maana ya uhuru huisha baada ya utambuzi
Baada ya kutambua kwamba uhuru si maamuzi
Maana Kifungo na mipaka vinafanana
Aliyekuambia kuna uhuru utaupata kakudanganya
Ipo asili inayofanya mwili wako mashine
Kufanya Ugonjwa uwe jela alafu afya ni jela nyingine
Mjamaa amemwaga damu tayari
Awe huru ili akawe mtumwa kwa mabepari
Chagua kufa ukiona waja hawalipi wema
Kufa wokovu kilichokufa hakifi tena
Kufa ni uhuru kamili tabu ni nini
Haupo huru sasa uhuru wa kweli ni kaburini
Unakumbatia uhuru wa kuambiwa
Wakati unaishi na haukuchagua kuzaliwa
Uhuru hautafutwi msafiri pumzika kubali chai
Hauwezi kuwa huru ungali hai
Uhuru si halisi jamaa badili umbo
Uhuru sio jibu hata usikariri fumbo
Uhuru ni falsafa ya vitabu iliandikwa na mababu
Tutaisoma na mwisho itabaki huko
Anayehitaji uhuru aelewe
Kuogopa kufa ni utumwa kwa maana kufa ndio uhuru wenyewe
Hata uwe mfalme ambaye anatoa idhini
Huwei kuwa huru uhuru wa kweli ni kaburini
Freedom freedom
Freedom freedom
Freedom freedom
Freedom freedom
Ukikumbatia mwanga jua utaificha nuru
Uhuru si kwa mwafrika kumkimbiza mkabulu
Kuutaka uhuru sana jamaa si dalili njema
Kama upo hai na unahisi uko huru fikiri tena
Cheo huleta nuru pahala nuru haifiki
Na pesa ndio njia ya uhuru ukiimiliki
Pesa na cheo upita kule hakuingiliki
Alisema mlevi mmoja ambaye pombe tu imemdhibiti
Mwathirika ambaye dawa za kulevya zimefunga
Na anahisi yuko huru mara baada tu ya kuvuta
Labda si kweli haupo huru ukijiongeza
Maana ukishaujua uhuru tayari ushaupoteza
Je utaniona chizi au mwivi
Au pumbavu au mshenzi ninayeongea vituko
Au utaamua ukae chini utafakari
kisha ukakubali ndoa ajira navyo pia vifungo
Aliye huru ni nani nieleze mtoto anayeenda kwa viboko
Au mlokole mtenda mema baada ya kutishiwa moto
Au msomi elimu mpaka chuo kihakiki
I swera kama uhuru ndio huo siuafiki
Anayehisi yuko huru pita mbele
Piga kelele maana hata Mungu wako hayuko huru
Hawezi kubadili mipango hawezi kumuumba
Mungu mwingine mkubwa kupita yeye
Unaetafuta uhuru wa kweli utateseka
Utapoteza damu utatoa machozi na utakesha
Hauwezi kuupata maana hakuna ulipouweka
Uhuru haupatikani kwa fedha
Uhuru is priceless kwakuwa si bidhaa halisi
Wenye chapaa walihakiki
Utaniangusha sana ukishindwa kuamini
Upo uhuru ila uhuru wa kweli ni kaburini
You've got no freedom
You've got no freedom
You've got no freedom
You've got no freedom
Freedom freedom
Freedom freedom
Freedom freedom
Freedom freedom
Пікірлер: 324
🎶🎶🎶 Maandishi ya Dizasta sometimes I wish Kama yeye ndo angeitwa "Darasa" 😅😅😅 unajifunza, unaburudika na unatafakari HapaHapa kwenye wimbo mmoja
@husseinmtima6106
7 ай бұрын
Hiii kichwa ni curriculum kaka Kwa wenye akili sio kusifu nyuchi tuu
Lyrics Maana ya uhuru huisha baada ya utambuzi Baada ya kutambua kwamba uhuru si maamuzi Maana Kifungo na mipaka vinafanana Aliyekuambia kuna uhuru utaupata kakudanganya Ipo asili inayofanya mwili wako mashine Kufanya Ugonjwa uwe jela alafu afya ni jela nyingine Mjamaa amemwaga damu tayari Awe huru ili akawe mtumwa kwa mabepari Chagua kufa ukiona waja hawalipi wema Kufa wokovu kilichokufa hakifi tena Kufa ni uhuru kamili tabu ni nini Haupo huru sasa uhuru wa kweli ni kaburini Unakumbatia uhuru wa kuambiwa Wakati unaishi na haukuchagua kuzaliwa Uhuru hautafutwi msafiri pumzika kubali chai Hauwezi kuwa huru ungali hai Uhuru si halisi jamaa badili umbo Uhuru sio jibu hata usikariri fumbo Uhuru ni falsafa ya vitabu iliandikwa na mababu Tutaisoma na mwisho itabaki huko Anayehitaji uhuru aelewe Kuogopa kufa ni utumwa kwa maana kufa ndio uhuru wenyewe Hata uwe mfalme ambaye anatoa idhini Huwei kuwa huru uhuru wa kweli ni kaburini Freedom freedom Freedom freedom Freedom freedom Freedom freedom Ukikumbatia mwanga jua utaificha nuru Uhuru si kwa mwafrika kumkimbiza mkabulu Kuutaka uhuru sana jamaa si dalili njema Kama upo hai na unahisi uko huru fikiri tena Cheo huleta nuru pahala nuru haifiki Na pesa ndio njia ya uhuru ukiimiliki Pesa na cheo upita kule hakuingiliki Alisema mlevi mmoja ambaye pombe tu imemdhibiti Mwathirika ambaye dawa za kulevya zimefunga Na anahisi yuko huru mara baada tu ya kuvuta Labda si kweli haupo huru ukijiongeza Maana ukishaujua uhuru tayari ushaupoteza Je utaniona chizi au mwivi Au pumbavu au mshenzi ninayeongea vituko Au utaamua ukae chini utafakari kisha ukakubali ndoa ajira navyo pia vifungo Aliye huru ni nani nieleze mtoto anayeenda kwa viboko Au mlokole mtenda mema baada ya kutishiwa moto Au msomi elimu mpaka chuo kihakiki I swera kama uhuru ndio huo siuafiki Anayehisi yuko huru pita mbele Piga kelele maana hata Mungu wako hayuko huru Hawezi kubadili mipango hawezi kumuumba Mungu mwingine mkubwa kupita yeye Unaetafuta uhuru wa kweli utateseka Utapoteza damu utatoa machozi na utakesha Hauwezi kuupata maana hakuna ulipouweka Uhuru haupatikani kwa fedha Uhuru is priceless kwakuwa si bidhaa halisi Wenye chapaa walihakiki Utaniangusha sana ukishindwa kuamini Upo uhuru ila uhuru wa kweli ni kaburini You've got no freedom You've got no freedom You've got no freedom You've got no freedom Freedom freedom Freedom freedom Freedom freedom Freedom freedom
@kingdeukoo2361
Жыл бұрын
Huwa unawazaje aisee ebu nipe siri ya mafanikio 🔓🔓
@alphanlukombe3774
Жыл бұрын
Mm ni mpenzi wa mziki wa hip hop tangu zaman lkn sijaona mtu ambaye anaweza akafata nyayo zako kaka ww ni sawa na passed like a shadow
@landiismollel4075
Жыл бұрын
Huyu Jamaa Taifa limuangalie sana maana ni Genius
@Boazi_B4
Жыл бұрын
Dizasta vina🔥🔥✍️
@florianmasawe9520
Жыл бұрын
Big up sna kamanda 🫡🫡🔥
nakuja tena hapa kusema "you are the greatest of all time"
GONGA LIKE APA KWAAJILI D_VINA👍
Waaaah Moto sana
HIP HOP USKIVUU Uelewi Fatiliaaa Sebene🤗🤗🤗🤗😁
KENYANS 🇰🇪 🇰🇪 kunjeni hapa mnipee like juu nimeskia sauti ya PLO LUMUMBA hapo mwanza kwa into
Yes.. hip pot inaniacha nitafakal maisha sio muziki ya wachumba na wabembeleza mapenz... GOOD SING MA -BRO VINA
Uhuru wa kweli ni kabulini
uhuru wa kweli ni kaburini.
Uyu jamaa noma sanaa
Nimekuw fan baada ya bigu la rapcha
🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
Siku ukijikuta umeteuliw huongoz wa juu usishangae bro maaana hata taifa linaelewa unajua✊✊✊
Ok dizaina wangu
Dizasta we ni mwandishi mkuu
Dah mashahir kam Okot Pbitek
Nakuelewa sana
Vinna
Noma Sana
Unaetafuta uhuru wa kweli utateseka
Aliyekwambia kuna Uhuru utaupata kakudanganya.
Vina vingi kama mchanga wa bahari
Au mlokole mtenda wema baada ya kitishiwa MOTO.... Boooooom. D ALMANDO FUNDI WA MISTARI..
Darasa lisilo na shaka ndani ya bongo na fleva zenye funzo ndio naokota humu..kama chuo hapa ni zaidi ya Harvard let's support the energy and talent🤘🤘🤘🤘
I said it am a say it again ke or ug or Tz hands down he is the pure of definition of lyrisism last of a dying breed goat 🐐
daah ee bwana ee salute sana kaka
My top 5 bestest lapper in Tz.🇹🇿.. First is -Dizasta Vina Second is- Dizasta Vina Third is -Dizasta Vina Forth is ......am just thinking who is either came near to this lap killer Fifth is...... still ristening their songs while doesn't sound good to me. Yo nigga,,, I real appreciate your songs man,I even never exprain my feelings while ristenig your songs.... salute brother🏆🏆🏆🎖🥇🥈🥉🎧🎤
vinaaaaa
Unajua sana kaka you are really philosopher
Dizasta haya madini unayoyatoaga unaoteshagwa au vipi 🔥🔥
Naisikia sauti ya dash kwa mbali
Hakika
Umetisha Mkali
mwimbaji anasema "UKISHAUJUA UHURU TYR UMESHAUPOTEZA" .....noma sanaa📌📌
That's very sure; Dizasta Vina ni wamoto kushinda jua.
UHURU WA KWELI NI KABURINI!!
Kitoko makasi D.vina
Unyama mwingi
Ii ni kichwa ingine wazee uyu jamaa ni hatari na nusu
Vinaaa
Lini ataanza kuwalipa maproduza
IT IS GOAT THING KUCHANA KAMA HIVI
DIZASTA DIZASTA DIZASTER🎉✌✌✌✌🤙🐆
Falsafa za huu wimbo katika uhuru zinaendana na zile za Socrates...hii nyimbo inanishawishi kuanza kumfatikia dizasta❤
Hongera Vina ...inafikirisha kwakweli ni njema kipata msanii aliyemua kwenda kiasili na kuwekeza kwenye elimu...Mkuu Vina nataka nitoe ushauri kwako ukae mbali na wa Industry wenu watakupoteza na watakualbukiza ujinga natamani muda mwingi uutumiye kusoma kujitenga na kutafakari namuona Frederick Nietzche ndani ...kaza buti bro
👊👊👊👊
perfect Bro hatupo huru
Hip hop tz imebaki kwako tu wengine wote amapiano
Kilicho kufa hakifi tena ,kuogopa kufa fuu mwamba uko juu sana kwenye ngoma zako Respec and be respected
Rapcha anatakiwa ajue pale alipo hana UHURU. Uhuru wa kweli ataupata Kaburini.
@brianedward9705
Жыл бұрын
uhuru utampata kenya
✍️..... freedom
Nyieeee hao marapper waje wote mi nakuja na huyu mwamba na wanakaa duuh DIZASTA NI NOMA
Mtu anaweza kukuelewa wewe Brother 😇 ni extraordinary mind 🙌
Haters are going to hate. Fans, let's gather here and show some love to this exceptional talent.
Vinna🙌
Tatizo midia wanazingua hawapigi hip hop mwambani rapcha awe huru mwamba hana mpinzani
A petition for it to be played at John Wick's Funeral.
@fadhilmwami1478
Жыл бұрын
💥💥Where do we sign?
Ubora katika fani🔥🔥
Aye!!!! Baaaad news to those who fear the truth.
Ngoma kali sana ujawai kutuangusha mashabik zako bigaup san vina rapa bora🇹🇿
Dizasta vina bratha ujawai kukosea mwamba...!
Nionyeshen EmCee anaechora kumzid Vinna mamaee 😂🙌 jamaa litengweeee
Meeleza bitu uhalisia sana ukifikilia do iko hivyo good🤫🤫🤫🤫
Huu wimbo ilinifanya nibadili imani, nikajikuta nakubaliana na DIZASTA kwamba hakuna uhuru wa kweli zaidi ya kupumzika kaburini😁 In short DIZASTA Ulitulia sana kuandikia hii mada mana ulienda deep sana mpaka inaleta hamu kuendelea kusikiliza.. That's a mad philosopher really 😁🙌
Uhuru aupatikani kwa pesa..🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
uhuru wa kweli ndio huu..wazungu walitudanganya baada ya kufa kuna moto/pepo kitu ambacho ni uongo mtupu😅😅😅
Hatariii varteller
Ur the best
Vinaaaaa
freedom ni state ya mind, hutaipata bunge, walai
Noma sana,bonge la song MTU wangu
Dizasta unaweza xnaaaaaaaaaa,kwel unasukuma ling kisomi,,,,,kutoka pandorama,,,🇹🇿🇹🇿🇹🇿
Hakika wewe ni mwandishi bora wa mda wote tangu game ya hiphop ianze nchii wewe ni mnomaaa nasemajeee we jamaa unaandika🙌🙌🙌🙌
Free dome
Kama uko huru na uko hai, fikiri tena😅 Hatuko huru wanangu😂❤
Vina hujawai kukosea mwamba wewe ni masta maind
MAD MAN
Waulize mtaani wanaomfaham vina... Nikitaka kumbato mtu lazima nimtaje jina... 🫡🫡🫡
Daah hii nyimbo Ina ujumbe sijui huwa unawazaga Nini wakati unatunga nyimbo mistari Yako haifanani na mtu yeyete yule duniani
Vina
Wewe ni mwamba kakaa....hiphop to another level
Akili kubwa sana D.VINA💯💯
Mtaalam
Akilinyingi Sana yani da mi ni mswahili lakini umakini mwingi Sana we kweli mwana fasihi
mana ukisha ujua uhuru ushaupotezaa🙌🙌
Dizasta vina 🗽🗽🗽🗽🗽🚀🚀🚀🚀🚀
nakubali kaka unatuelimisha sana ngoma zako zote nidarasa tosha
Muuwaji katika matukio ya kufikirika na kweli. Kongole kwa uwandishi bora ndugu msanii wa hip hop.
Kweli Bado sipo huru duh much respect broh
Philozofa ubongo. Mr Ubongo Genius. You are like octopizzo in critical thinking . Munaongeleya kufikiriya kutumiya ubongo ili kutatuwa maswala yetu .most of our intellectuals are corrupt they are not good critical thinkers they have limit but you you speak what black people are afraid to talk about about god Allah or others subject man salute and longlife we need more more thinkers who don't have limit in thinking who use critical thinking and reason in all situation problem in our black community. Dizasta respect heshima .
asee saluti sana imeningia iyo
Uhuru wa kweli ni kaburini
Uhuru ni semi tu za Wana philosopher
Rapcha usikudie tena kufata hizi njia ngumu sana …. Oya mwanangu Dzasta we ni konyo
Genius
Nimekua shabiki ya dizasta vina toka nipo shule mpk sasa na kazi,i appreciate this man,Niliwahi taka kupoteza kazi kisa nasikiliza ngoma za dizasta ♥️♥️
Hyo verse ya Mungu inataka moyo sana duuh
@kiluaidd5427
4 ай бұрын
Sio poa
🔥🔥🔥🦁🔨✌️
We jamaa dah!! Dah!!🙏🙏🙌🙌🙌 🔥🔥🔥🔥