Dizasta Vina - Hatia IV
Музыка
Category: Music
Song: Hatia IV
Artist: Dizasta Vina
Music: Ringle Beatz
KZread: / jwa21m5eyl
Mdundo: mdundo.com/song/1670618
Audiomack: audiomack.com/dizastavina/son...
Soundcloud: / hatiaiv
Lyrics: genius.com/Dizasta-vina-hatia...
Other Musical contents
Audiomack - audiomack.com/dizastavina
KZread - / dizastavina
Deezer - www.deezer.com/artist/67967532
Apple music - artists.apple.com/a/profile
Mdundo - mdundo.com/a/2263
Genius - genius.com/DizastaVina
Boom play - www.boomplay.com/artists/3288... - artists.spotify.com/c/artist/...
Connect with Dizasta Vina on social medias
Instagram - / dizastavina
Twitter - / dizastavina
Facebook - / dizastavina07
sw.wikipedia.org/wiki/Dizasta...
Business: Pan.authentik@yahoo.com
Website - bio.link/dizastavina
Lyrics
“JASIRI JOHN….. ALIYAANGALIA MAISHA YAKE
HAKUONA JINSI ANGEWEZA KUISHI BILA JANE
MSICHANA ANAYEMPENDA
LICHA YA KUZONGWA NA UMASIKINI
ALIJITAHIDI KUMPA JANE MAHITAJI MADOGOMADOGO KADRI ALIVYOWEZA
LAKINI ALIFAHAMU SHUBIRI YA KUSUBIRI KUPENDWA HUKU ANAFAHAMU KUSUBIRI KUPENDWA NI
MATUMAINI YANAYOUMIZA. KAMA WANAVYOSEMA, MTAFUTAJI HACHOKI AKICHOKA KASHAPATA…
.ALIENDELEA KUNGOJA”
Ah! Sikuwa na zali sikuziamini ndumba
Sikuwa na mali za kufuja
Nilijitahidi kuuza mitumba kufuga mipunga
Ili siku nimpe gari nimpe nyumba. Nilishindwa…
Niliishia kumpa chai, ‘chipsi’ mayai na ‘vocha’
Nywele za kimasai na mkoba
Pesa za magauni, majuba na viatu vya kuzuga
Nilimpa muda ila bado haikutosha, kwani…
Nilipomwambia nampenda hakujibu
Akaweka moyo wangu maumivu
Na mtima wangu akauweka ‘solemba’
Nikaapia kuwa sitakuja kupenda ‘forever’
Ah! Nilimpa upendo nilimpa sifa
Niliweka mitego ya faida, haikuwa shwari
Nikabadili mwenendo wa maisha
Niliweka malengo sikutimiza, hakunikubali
Alikuwa na ndoto kubwa kushinda mimi
Alikuwa na misimamo kuipita dini
Aliniambia ameomba nije kuokota utajiri
Amengoja sana na sasa amechoka kusubiri
Ah! Sikuwa na hali ya kuikosha roho yake
Nilimwacha aende aufate moyo wake
Alipata bwana wa kizungu magharibi
Alimwahidi kuishi maisha ya ndoto zake
Nilipata uchungu niliishia kuhamaki nilitaka nijiue
Nilitaka nimzuie abaki nikakumbuka
Ukipenda ua haulikati unaliacha likue
Duka langu nilifunga biashara niliacha zote
Uchumi uliyumba kwa maana nilianza pombe
Niliumwa bado kidogo moyo uzime
Nilimfanya ndoto kumbe naye ana ndoto nyingine
Alisema anakwenda jiji la Miami
Hakuna alichowaza zaidi ya kuishi kifahari
Kamtumia picha na ‘mchizi’ kazikubali
Na yupo tayari kumlipia gharama za safari
Aliondoka na kipande kimoja cha mwili
Nilikonda nilipata ugonjwa wa akili
Haikuwahi kupita hata sekunde nisilie
Nilitamani mpaka ardhi ipasuke niingie
Ah! Muda ukaenda nitapata ‘Mwanamwali’
Nikamwomba awe mwenza wa maisha akakubali
Nikamvisha pete nikalipia mahari
Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali
Aliuliza kama nampenda, nilimjibu
Sikutaka kuweka moyo wake maumivu
Sikutaka kuuweka Mtima wake solemba
Kiasi aseme hatakuja kupenda ‘‘forever’’
Ah alinikumbatia nikamfunga kwa ishara
Akanikabidhi tunda nikala
Akaniamini tukajuana nikapanga kumwoa
Akaidhisha na tukaanza na mipango ya ndoa
“Habari naamini u bukheri wa afya
Unaendeleaje maisha na huyo mpenzi wa sasa
.nashukuru nahema ughaibuni si kwema
Nakiona cha mtema mpaka naona ni heri nikafa…
Ah! Maisha niliyowaza yote ni uongo
Nauzishwa madawa nalazimishwa ngono
Nafungiwa ndani kama mtumwa ufungwani
Roho yangu rehani kiasi sasa naitamani Bongo
Ukubwa umekuja kunisafisha jicho
Ndoto imeisha na taswira imenionyesha sivyo, ah
Naomba unifate uniondoshe kwenye hichi kifo
Na hii namba ya msamaria atakueleza nilipo”
Sherehe ilikuwa na mipango madhubuti
Kabla mimi kuichukua michango ya Harusi
Nikatoroka ughaibuni kufuata hisia zangu
Kwenda kumfata njiwa wangu mahususi
Nilivuka majangwa na majabali
Sehemu ya safari anga sehemu nyingine bahari
Niliacha kila kitu nyuma upendo na huruma vilinijaa
Penzi likanipeleka mbali
Nikakutana na bopa la kizungu
Lenye sura ya kuichachisha mboga kwenye chungu
Kiko kwenye mdomo,Tatuu kila kona na wapambe
Pamoja na vishoka wenye mtutu
Sio siri alizungukwa na wasichana wengi
Sikujua umri walikuwa wadogo ka’ “madent”
Baadhi walikuwa uchi wanahesabia “chenchi”
Wengine masaji huku wengine wanamchezea nyeti
Hata nilipomuuliza kama ananipenda hakujibu
Akaweka moyo wangu maumivu
Nilijua hawezi kufa kwa sababu hakunipenda
Na ni rasmi nikapoteza shilingi kwenye msitu
Nilikiambia kifo kama unakuja njoo
Maana sikuwa mtu ilishakufa roho
Sikuumia kama alivyoniumiza yeye
Kwahiyo sikujali jinsi nilivyoteswa na wale mbwa no
Aliambiwa ambusu bosi hakubisha
Alipewa bunduki hakusita
Aliishika risasi akaiingiza
Akaambiwa anipige kwenye kichwa
Пікірлер: 641
"Nilimfanya ndoto, kumbe naye ana ndoto nyingine"
“JASIRI JOHN….. ALIYAANGALIA MAISHA YAKE HAKUONA JINSI ANGEWEZA KUISHI BILA JANE MSICHANA ANAYEMPENDA LICHA YA KUZONGWA NA UMASIKINI ALIJITAHIDI KUMPA JANE MAHITAJI MADOGOMADOGO KADRI ALIVYOWEZA LAKINI ALIFAHAMU SHUBIRI YA KUSUBIRI KUPENDWA HUKU ANAFAHAMU KUSUBIRI KUPENDWA NI MATUMAINI YANAYOUMIZA. KAMA WANAVYOSEMA, MTAFUTAJI HACHOKI AKICHOKA KASHAPATA… .ALIENDELEA KUNGOJA” Ah! Sikuwa na zali sikuziamini ndumba Sikuwa na mali za kufuja Nilijitahidi kuuza mitumba kufuga mipunga Ili siku nimpe gari nimpe nyumba. Nilishindwa… Niliishia kumpa chai, ‘chipsi’ mayai na ‘vocha’ Nywele za kimasai na mkoba Pesa za magauni, majuba na viatu vya kuzuga Nilimpa muda ila bado haikutosha, kwani… Nilipomwambia nampenda hakujibu Akaweka moyo wangu maumivu Na mtima wangu akauweka ‘solemba’ Nikaapia kuwa sitakuja kupenda ‘forever’ Ah! Nilimpa upendo nilimpa sifa Niliweka mitego ya faida, haikuwa shwari Nikabadili mwenendo wa maisha Niliweka malengo sikutimiza, hakunikubali Alikuwa na ndoto kubwa kushinda mimi Alikuwa na misimamo kuipita dini Aliniambia ameomba nije kuokota utajiri Amengoja sana na sasa amechoka kusubiri “JOHN ALIFAHAMU HALI YA JANE, KUWA JANE ALIZALIWA KWENYE FAMILIA MASIKINI, NA ALIUCHUKIA MNO UMASIKINI. ALIFAHAMU UMASIKINI ULIVYOCHUKUA UHAI WA MAMA YAKE KIPENZI, ALIYEFARIKI KWA KUKOSA MATIBABU. ALIIFAHAMAU NADHIRI ALIYOIWEKA JANE YA KWAMBA HATOKUBALI TENA KUISHI KWENYE MAISHA YA KIMASIKINI, NADHIRI ILIYO MWEKA JOHN NJIAPANDA” Ah! Sikuwa na hali ya kuikosha roho yake Nilimwacha aende aufate moyo wake Alipata bwana wa kizungu magharibi Alimwahidi kuishi maisha ya ndoto zake Nilipata uchungu niliishia kuhamaki nilitaka nijiue Nilitaka nimzuie abaki nikakumbuka Ukipenda ua haulikati unaliacha likue Duka langu nilifunga biashara niliacha zote Uchumi uliyumba kwa maana nilianza pombe Niliumwa bado kidogo moyo uzime Nilimfanya ndoto kumbe naye ana ndoto nyingine Alisema anakwenda jiji la Miami Hakuna alichowaza zaidi ya kuishi kifahari Kamtumia picha na ‘mchizi’ kazikubali Na yupo tayari kumlipia gharama za safari Aliondoka na kipande kimoja cha mwili Nilikonda nilipata ugonjwa wa akili Haikuwahi kupita hata sekunde nisilie Nilitamani mpaka ardhi ipasuke niingie “JANE ALIPOONDOKA ALIMWACHIA JOHN KIDONDA KILICHOCHELEWA SANA KUPONA NA YEYE AKAWEKA NADHIRI YA KUTOJIHUSISHA NA MAPENZI TENA MAISHANI MWAKE. ALIKAA KWA MUDA MREFU BILA MAHUSIANO. LAKINI… HAKUNA DAKTARI MZURI KAMA MUDA, JOHN ALIPONA MAUMIVU NA ALIIRUDIA HALI YAKE YA KAWAIDA” Ah! Muda ukaenda nitapata ‘Mwanamwali’ Nikamwomba awe mwenza wa maisha akakubali Nikamvisha pete nikalipia mahari Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali Aliuliza kama nampenda, nilimjibu Sikutaka kuweka moyo wake maumivu Sikutaka kuuweka Mtima wake solemba Kiasi aseme hatakuja kupenda ‘‘forever’’ Ah alinikumbatia nikamfunga kwa ishara Akanikabidhi tunda nikala Akaniamini tukajuana nikapanga kumwoa Akaidhisha na tukaanza na mipango ya ndoa “WAKATI KARNE YA 21 INAINGIA, JOHN ALIKUWA NI MIONGONI MWA VIJANA WALIOKUWA ‘FASCINATED’ NA UKUAJI WA TEKNOLOJIA YA MITANDAO YA KIJAMII. ALIJIUNGA NA DUNIA HII MPYA, MARA KADHAA ALIKAA KWENYE UBARAZA, AKIANGAZA SIMU YAKE. AKIPAPASA KILA KITUFE, NDIPO SIKU MOJA AKAPATA UJUMBE KUTOKA KWA JANE” “Habari naamini u bukheri wa afya Unaendeleaje maisha na huyo mpenzi wa sasa .nashukuru nahema ughaibuni si kwema Nakiona cha mtema mpaka naona ni heri nikafa… Ah! Maisha niliyowaza yote ni uongo Nauzishwa madawa nalazimishwa ngono Nafungiwa ndani kama mtumwa ufungwani Roho yangu rehani kiasi sasa naitamani Bongo Ukubwa umekuja kunisafisha jicho Ndoto imeisha na taswira imenionyesha sivyo, ah Naomba unifate uniondoshe kwenye hichi kifo Na hii namba ya msamaria atakueleza nilipo” Sherehe ilikuwa na mipango madhubuti Kabla mimi kuichukua michango ya Harusi Nikatoroka ughaibuni kufuata hisia zangu Kwenda kumfata njiwa wangu mahususi Nilivuka majangwa na majabali Sehemu ya safari anga sehemu nyingine bahari Niliacha kila kitu nyuma upendo na huruma vilinijaa Penzi likanipeleka mbali “JOHN ALIFIKA UGHAIBUNI, AKAMTAFUTA MSAMARIA ALIYETAMBULISHWA NA UJUMBE, MSAMARIA AKAMWELEKEZA NJIWA WAKE ALIPO, NA NIKWELI… HAPAKUWA PEMA” Nikakutana na bopa la kizungu Lenye sura ya kuichachisha mboga kwenye chungu Kiko kwenye mdomo,Tatuu kila kona na wapambe Pamoja na vishoka wenye mtutu Sio siri alizungukwa na wasichana wengi Sikujua umri walikuwa wadogo ka’ “madent” Baadhi walikuwa uchi wanahesabia “chenchi” Wengine masaji huku wengine wanamchezea nyeti “MASIKINI JOHN, ALIDANGANYA KWA KUJITAMBULISHA KAMA KAKA KWA JANE, AKIMSIHI YULE MAFIA AMRUHUSU AONDOKE NA JANE WAKAANZE MAISHA MAPYA, LAKINI… PALIPOSHINDWA SHOKA WEMBE HAUWEZI TAMBA. KWA KUZIDIWA NA UOGA WA KUUAWA… JANE ALIMKANA JOHN KWA KUSEMA HAMJUI…” Hata nilipomuuliza kama ananipenda hakujibu Akaweka moyo wangu maumivu Nilijua hawezi kufa kwa sababu hakunipenda Na ni rasmi nikapoteza shilingi kwenye msitu Nilikiambia kifo kama unakuja njoo Maana sikuwa mtu ilishakufa roho Sikuumia kama alivyoniumiza yeye Kwahiyo sikujali jinsi nilivyoteswa na wale mbwa no Aliambiwa ambusu bosi hakubisha Alipewa bunduki hakusita Aliishika risasi akaiingiza Akaambiwa anipige kwenye kichwa JOHN ALIKUWA NI JINA JIPYA LA WAHANGA WA UPENDO WA DHATI, VIPOFU WA MAPENZI, WAJINGA WA MAHABA... JOHN ALIKUWA ROMEO KWENYE ROMEO AND JULIETH, ALIKUWA SAMSON KWA DELILAH KWENYE WAHUKUMU WA AGANO LA KALE, ALIKUWA JACK KWENYE TITANIC, FRED WEASLEY KWENYE HARRY POTTER.. JOHN ALITUKUMBUSHA KUWA UPENDO NI SADAKA, SADAKA YA MUDA NA PESA, ALITUKUMBUSHA UPENDO NI SADAKA YA DAMU JOHN, ALIPOTEZA UHAI AKIWA KWENYE SAFARI YA KUTAFUTA UPENDO WA MTU ALIYEMHUSUDU NA JANE ALIPOTEZA AMANI NA THAMANI YAKE KAMA MTU AKIWA KWENYE SAFARI YA KUTAFUTA UTAJIRI ALIOUHUSUDU Hatia iko wapi?
@challymchaff374
3 жыл бұрын
Daaah dizasta wewe ni vina hivi naanzaje kuchoka kusikiliza nyimbo zako
@wilsontonga3728
3 жыл бұрын
🤝🏾
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Naskiza ngoma mpaka moyo unataka kupasuka. Dizasta vina, MC Mahiri, Mc Katiri. Yaan hauishi kbs katika dunia tunayoishi sisi! Huku kwetu kitaa kizima wanajua n kiasi gani Mwamba unawika, wameacha kuniita jina langu, sikuhizi wananiita Dizasta Vina. Ngoma zako ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri na hana hatia. Ngoma zako zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zako zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu! Dizasta vina, katika ulimwengu wa Hip Hop zaidi yako wewe bado sijamuona mwingine. Hata Fareed Qubanda umemtupa kule, kabakia jina tu! Hebu pitia hii ili uone uzao wa tungo zako broo kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
@castorymwaipopo290
3 жыл бұрын
Nakukubali sana bro 💪
@sautidawa2222
3 жыл бұрын
Real talent
Dizasta vina bro we ni mkaliii Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali Kama tupo pamoja tia like 25-12-2020
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks.. Please share. Usisahau kuorder my new album
@emilysaimon481
3 жыл бұрын
@@dizastavina pamoja bro nigei no yako
@dizastavina
3 жыл бұрын
@@emilysaimon481 pre order kupitia tigo pesa 0655696811 au Mpesa 0762158871
Hii True story nimesikiza ×10....song imenipeleka mpaka gaibuni ....utahisi mkono wa mungu umeandika Hii✔✔#KingOfRap
dizasta unao uwezo mkubwa sana wenye nguvu kama meli ya mizigo aiseee
Duuhh nlichelewa😪😪😪 Dizzasta's fan number one from +257🇧🇮🇧🇮🇧🇮
Huu mziki wako ni dawa ya ubongo asee Viva dizasta vina 💪💪💪👊👊💥💥💥
... nilipo mwambia nampenda hakujibu... 2024
This dude is a script writer, story teller inshort ni Verteller,,, he can compose a movies of 2 hrs in 7 mins,, daaaamn🔥🔥🔥🔥
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks, please share
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
@mussabutanwa8693
3 жыл бұрын
@@dullywamashairi121 yes he's a genius we should support him lol!!!
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
@@mussabutanwa8693 dats true my blood Dizasta vina: The man one army 💪💪
@mussabutanwa8693
3 жыл бұрын
@@dullywamashairi121 yes for really man
Hii ni movie kabisa bro one day andaa scripts then simama as diirector naamini itakuwa kazi kubwa BIG UP DIZASTA VINA
@dizastavina
3 жыл бұрын
Hopefully one day
Wasanii kama hawa Bongo ni wachache Sana... Big up bro....
Wimbo wangu wa mwaka kbsa Asante dizasta 2020
@dizastavina
3 жыл бұрын
Apreciate, umeshaweka order ya album
Daaaa bro unajua mpaka unaboa.. masikio yetu hayalali njaa kila unaposhika kipaza!!
Dizasta hii nyimbo ni funzo tosha yani ww ndo mwalimu wangu najifunza vitu vingi nkasikiliza nyimbo zako$
Nilikwambia unajua na ctoacha kukwambia unajua💪💪
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks kev
You are so Genius, asante kwa uwezo wako wa kunifanya niamini kuwa wewe ndie Rapper Bora
Dizasta vina ni akina Joh 70. Mtiririko mzuri ,kazi nzuri. Big up brother.
🎶🎶🎶🎶Dizasta nadownlod nyimbo zako zote
Wewe wewe weeeeeewe🥺🥺🥺ulishushwa ututeke🇹🇿❤️
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
Aisee hii ni ya moto kushinda jua🔥🔥🔥🔥
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
Hii ngoma ni zaidi ya albamu nzima ya Weusi, Prof Tungo we ni 🔥🔥🔥🔥🔥
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
@shabannyamsalika8959
3 жыл бұрын
@@dullywamashairi121 Hip hop inahitaj wenye uwezo mkubwa wa kufkr, pole sana kwako mwny uwezo mdogo nkushauri kasikilize waaah!!!
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
@@shabannyamsalika8959 inaelekea wewe ndo hujanielewa Mimi. Wewe bado mbana pua. Wagumu wakipita wataelewa nimemaanisha nini. Umekurupuka mzee, maana kitaani wamenibatiza jina wananiita Dizasta vina!!💪💪💪
@shabannyamsalika8959
3 жыл бұрын
@@dullywamashairi121 We ndo umekurupuka kusema huu wimbo ni wawagumu, hii ngoma anasikiliza mtu yeyote na anaelewa. Tuondoe mawazo finyu ya kudhania kuwa hip hop inasikilizwa na watu wagumu, cjui makatiri km wewe ulivyosema mwanzo...
@obeidjoseph3610
3 жыл бұрын
@@dullywamashairi121 mwanangu ww bado Sana na hilo jina la dizasta mwalichafua kitaan kwenu
Duuuhhh.... hii inabeba sababu muhimu ya muziki kwenye maisha....
Dizasta..... you're very UNIQUE broo...Mungu akuzidishe maarifa na afya tele just because unajua kutupa Raha mashabiki zako..GOD BLESS TOUR TALENT
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks bro
Wewe mwamba ni mwehu sema tuu unafikiri sana Yaani movie moja classic
@dizastavina
3 жыл бұрын
😂 😂 😂
Ahsante sana Dizasta Vina Kwa Muziki Mzuri unaoacha/utakaoacha Alama ya Milele
Dah dizasta umezigusa hisia umenifanya nijione mwenye hatia
@erastompongo8400
3 жыл бұрын
Dah Kama umeniimba mimi vile Haso za mapenzi duniani zinaumiza wengi
Sauti yako tu mi hoiiiii🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🌹🥰❤️
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thank you........
Daaa hiingom Kali
Wa KUMI kutazama 🙌
@dizastavina
3 жыл бұрын
👏🏾 👏🏾 👏🏾 👏🏾
Master vina fan toka 🇰🇪🔥✅ tumengoja sana umewakilisha kama kawaida
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks, please share
kazi nzuri bro,,,, nakubali kazi zakoo
Brother unawezaaaaah na xo unaweza 2 we ni MWALIMU
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks bro
Waaaaaah... Dizasta vina..tisha sana.. Kenya tunakuaminia.
This is the kind of music I expect to listen to in heaven.
Dizasta vina noma sana
Muda utafika Inshaallah dizasta utakua jina kubwa na ramani ya maarifa kwa kizazi kijacho
@dizastavina
3 жыл бұрын
Hopefully
Brazaaa umegusa maisha ye2 kwa hii ngoma
Mistar unachora Broo!!! Ni nomah ,we mkali aise,big up
Aisee dizastar noma Sana mshkaji wangu darasa Hilo namimi napenda Nije nipate mautundu ya asali ya hip-hop
Naenda kama sina hatia II always!! Thanks Dizasta kwa kuendelea kutujenga.
Najivunia kua shabiki ako bro...hujawahi kuniangusha🙏🙏🙏🙏🔥🔥🔥🔥
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
Yule dogo raptcha akae mbali....ajifunze kuchana, sio fujo nyingi ....dizasta ni disaster balaa🔥
The best hiphop rapper kwa sasa nchini, hakuna wa kumzidi Dizasta vina kwa sasa
@boniphacelutusyo9110
2 жыл бұрын
Hip hop 👍👍👍
Kaka hii ngoma naomba niifanyie cover yn nmeikubal Kias kwmb mpk nawaboa watu Everyday nackiliza
Verteller ...Dah huwezi amini nimeiona movie yote kichwani mwangu the way Mwamba unavoflow... nilichofeli ni kuipata sura ya Jane.
Aliondoka na kiungo cha mwili 😃🔥🔥
Umetisha sana mzee baba bonge moja la ngoma
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
Asie elewa kazi ya hiki kichwa aisee hatokuja kuelewa milele @dizasta vina ndio nembo ya hip hop isio vunja nguzo ata moja ya hip hop brother umetisha sana
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks, please share
The pure art of storytelling! I love it man. Great job
naikubali kinoma hingoma bigp bro
Si Movie kabisa hili la masaa2 kwenye dk7 mzee wangu 💥💥💥 Dizasta eeee We ni Mnooo Aseee
What a lesson..daaaaaah We jamaa ni zaidi ya hip hop bro.
Nomaa sanaa
Dizasta vina saiv umesha convert akili yangu kwenye hiphop naenjoy sana napo usikia mziki wako nakuwa makini ili nielew unachokimaanisha nanukuu kwenye hatia 2 ulisema wanaume wote mbwa ila cjui sasa wewe ni kubwa la ma mbwa mana sioni wa kucompare na mziki unaoimba
@dizastavina
3 жыл бұрын
Shukrani sana ndugu, please share na marafiki
Dah Dizasta ...salute
THE VERTELLER!! Wachache watakuelewa na kukusifia!!
Daaah black maradona.. home boy unajua
Kumamakeeeeee
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha💪💪 kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
Vina vingi sana humu👑
Nomaa Mzee...nasubir confessions za hiz HATIA
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Ngoma zake zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zake zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu! Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
Incredible punch lines. What a song keep it up brother!!
Extra oldinary Nakubali kaka
Disasta bro 💪 hiphop ngumu ya kiakil na yenye uelewa wa kwel💥💥
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks man
Ukipenda ua haulikati unaliacha likue 🎶
I'm Doing Music Because Of You That's It, You Are Extraordinary Man
@dizastavina
3 жыл бұрын
Appreciate the love brother
@alextanzania
3 жыл бұрын
Angusha ngoma Trickson ,tutakusupport tu
Dah! Hatimae mzigo umeachiwa. Hatia IV ni moto
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Ngoma zake zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zake zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu! Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
Emotional 🔥🔥🔥🙌🙌
Jamaa unaimba sana aiseh🔥🔥🔥🔥
Daaah!! Ama kweli wewe ni THE VERTELLER bro,. 👏👏👏👏🙌🙌
REST IN PEACE MAGUFULI ULIPAMBANA SANA NA HIYO VITA! MUNGU AKUPUNGUZIE ADHABU YA KABURI NASI SOTE TWAJA! Ameen
daah..💯💯 shukrani sana
My all time Banger..!! ❤
Ningekua baraza la sanaa ngomaa zako kaka zingetumika kujibia mitihan kaka...yan wanafunz ningewataka waskize kisha wachambue kila kipengele cha fasihiiiiiii
dizasta vina ni kina joh 70 // sio wakazi kadhaa wa kitongoji mkija njoo makini
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha 💪💪 kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
My best movie ever @dizasta🙌🧠🧠🧠
Nimerudi hapa baada ya mistari mingi kunigusa na kuendana na ninachikipitia kwenye maisha ya mahusiano
Ahsaante tena kwa 💣💣💣 bomu la kufungia mwaka 2020..
Unyama sana broo
Umeshushwa.brooo...yan.unajuaa.brooo
Aseee wewe ni mtu hatari kwelikweli big up kka
@dizastavina
3 жыл бұрын
Shukrani sana ndugu, please share
Mungu ametupaga disaster vina
Daaah jiji lina habar kamil mzee,🙌🙌🙌
Nyimbo nzur sana
Imenitoa machoz hii ngoma mapenz yanauma sana
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
@ramadhanally138
3 жыл бұрын
My broo really umenitoa mazur kweli VINA NI HAFAHI KABISA
Unatishaaa yaaaani hiii ngoma mengne live
We dizasta fundi ni kweli nikitaka mziki mzuri nimtafute dizasta
New fan from +254 hapa.... Huyu kaka balaa sanaa dah
So much blessings....vina for real..
Dizasta vina ujawai kosea big ✊✊
Makini sana mzee
Umeuaaaa🔥🔥🔥🔥
Dah Dizasta, uko hatua ambayo mimi naiota kufikia.
@dizastavina
3 жыл бұрын
Patience and practice
Dizasta vina unastahili kuwa mtu Wang wa kalibu Ila sio mbaya hata hap nakupata
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thank you
Professor Tungo🔥👊🎼🐐
Wejamaaa weeeeee!!!! Ninomaaaaa
Dizasta vina ✍️💯
@dullywamashairi121
3 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Ngoma zake zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zake zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu! Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti kzread.info/dash/bejne/kap715alYbDVfdo.html
Duuh..! sijui nikupe jina gani broh... una hatari kubwa sana. 🙌🙌🙌
@dizastavina
3 жыл бұрын
👏🏼👏🏼
Big up bro Dizasta,you know wat you're doing,mm ni shabiki yako no 1
@dizastavina
3 жыл бұрын
Asante sana. The Verteller ALBUM is out. Check me 0762158871 /0655696811
Hii ni zaidi ya nyoko.Hainaga kufeli🔥🔥🔥
We jamaa nomaa