Dizasta Vina - Hatia II
Музыка
Category - music
song - Hatia
writer - Dizasta Vina
Music composer - Dizasta Vina
Stream & Download Hatia II
Mdundo - mdundo.com/song/1013476
Boomplay - www.boomplay.com/songs/646553...
Spotify - open.spotify.com/track/3g7QrL...
Audiomack - audiomack.com/dizastavina/son...
Other Musical contents
Audiomack - audiomack.com/dizastavina
KZread - / dizastavina
Deezer - www.deezer.com/artist/67967532
Apple music - artists.apple.com/a/profile
Mdundo - mdundo.com/a/2263
Genius - genius.com/DizastaVina
Boom play - www.boomplay.com/artists/3288... - artists.spotify.com/c/artist/...
Connect with Dizasta Vina on social medias
Instagram - / dizastavina
Twitter - / dizastavina
Facebook - / dizastavina07
sw.wikipedia.org/wiki/Dizasta...
Business: Pan.authentik@yahoo.com
Website - bio.link/dizastavina
Lyrics
Ah!
Nilipaa sasa natua Kwenye,
kwenye Siri ya moyo Na siri ya moyo Anayeijua mwenye
Mwenye ujasiri wa Kutunza nafanya Ninachodhani ni Sahihi kitachotokea
Nitajua mbele
Wanasema mwanaharamu Haijui laana,
kashalaanika Nasikitika kuwa haujui Kama
naonekana ka' Kondoo kwa mchungaji
Lakini... lakini kwa ndani
Mi' ni chui mama
Kwa mfano nakuita mpenzi
Na tabasamu zuri wakati
Najua kuwa sikupendi
Kuitoa hii siri ndo' siwezi
Kwahiyo nitakudanganya
Mpaka ifike siku niutimize
Ushenzi
Huwa nawaza nikuweke
Ufahamu,mtambue
Kuwa mpo wengi
Na lengo niwateke
Ili mpeleke salamu
Masikini mrembo
Nashangaa jinsi unavo'ngoja
Pete kwa hamu
Vile hunioni kwenye
Makundi ya baa
Na bahati nzuri haujawahi
Kusikia nikizushiwa uzushi
Kumbe unampigia mbuzi gitaa
Sometimes unanisongea nguna
Au wali ukidhani mi' najali ilihali
Sina habari, sina hisia siwazi
Hata kukuonea huruma
Na sibadili dhambi hata
Mbingu ikisogea nyuma
Ah!
Nashiriki nawe nyakati
Twitter mpaka instagram
Picha unani-hashtag drunk in love
Nanunua brand za gharama za
Simu ya ghali breakfast
Zanzibar
Haimaanishi kuwa
Tunaianza safari
Nataka nikuandalie maumivu
Ili kila unachokiona
Kiwe kinafanya unikumbuke
Ni hatari
Inaitwa zuia nanga kabla
Bado haijang'oa
Maana haujaheshimu
Mvua kama bado hujaloa
Kwa huu mchango ninaotoa
Ndo' unafanya unazama
Zaidi kiasi unaiwaza mipango
Ya ndoa
Jicho la tatu hauna
Fungua jicho lako la pili
Utagundua kila ninachofanya
Ndo' maana haujaona bado
Wala haupo kwenye
Mpango wa pili
Ah!!
Unaniletea zawadi toka
Nilishawaacha
Na walinichora tattoo
Mi sio tunda mama
Mama mi' kidonda
Utachelewa kusonga
Ka' bado unaingoja nafuu
Sherehe ya birthday yako
Kwenye 'temple' ya anasa
Umekuwa 'mental' kwa
Huu mwendo ndo'
Umenasa
Kiasi unahisi huu ni upendo
Tukishiriki tendo tu nakuacha
Kichwa changu hichi, kichwa
Nitalala na wewe na
Wewe na haifiki jumapili
Nitakuwa nimeshakuacha
Ah! utanitafuta
Kwenye simu ambayo
Namba nitakuwa nishaibadili
Utanitafuta mara mbili
Mara tatu kisha nne
Utagundua kurudi
Itang'ata moyo wako
Watu maumivu
Hukujiandaa kuyakabili
Utanipamba majina ya
Nitakuwa mbali nishasafiri
Nishasahau utatunga nahau
Wakati haukuwahi kuutabiri
Ila upo
Utaumia utashindwa kusimulia
Utaniulizia kwa wanaonijua
Hauna tena chako
Okota vipande vya moyo wako
Nenda zako kaandike
Tanzia
Kisha watajua wenzio
Wanafiki watacheka
Wanaokujali wataangua kilio
Watakusindikiza kulia
Watakupa pole wengine watasema
Wanaume wote mbwa
Taswira itazongwa
Na wingu
Picha utazichoma
Kwa kisu
Utanitukana mara mwana
Haramu mara malaya
Rafiki zako wakuu watakuwa
Filamu na riwaya
Wimbo niliokuimbia
Kamwe hautokukonga
Utachoma mkuki moyoni
Kisha kunyonga
Utaendelea kungoja
Utagundua mvumilivu
Hali mbivu hiyo
Methali iliongopa
Utagundua ilikuwa
Ni soga
Hii itafanya ukonde
Na kuanza
Kutumia pombe na ganja
Nayajua haya yote
Kwa maana ndo nilikotoka
Utasimama kijasiri
Na mwisho utadondoka
'Sikiliza'
Wataleta daktari
Akuulize nini shida
Hawatapata
Jawabu kabisa
Wataleta sheikh
Wataleta mchungaji
Wa kanisa
Watasahau kwamba
Moyo uliovunjika
Hauna tiba
Natamani nikuambie kuwa nimekuteka makusudi
Maana unasikia na hujifunzi
Nikuumize kama mke wangu mpuuzi
Aliyekimbia na rafiki yangu siku moja baada ya harusi
Nilishaambiwa na
Mama nikapuuzia
Kuwa haujawahi
Kupenda kama
Haujawahi kulia
Kuna muda mtu mbaya
Hutengwa na hatia
Maana kafiri hazaliwi
Utengenezwa na dunia
Ukijiua sitakuona
Mzembe amini
Nitakuvalisha pete
Ruksa uipeleke baharini
Najua tiba ya
Upweke amini
Mwisho wako ni
Kuwa kicheche kama
Mimi
Hapo utajua kunihukumu
Sio haki
Mwanamke kama
Wewe ndio amenifanya
Niwe muasi
Bila hofu wala
Kiwewe
Nitaendelea kuzunguka
Kutafuta wasichana
Vipofu kama wewe
Sina hati
Пікірлер: 165
Listening from Kenya.Stellar and classic music indeed.
Kazi nzuri Dizasta....mwanzo nilihofia kua hii haitaweza kua kali kama HATIA I...daaah lakn sasa nimeshindwa kujua ipi kali kati ile part 1 au part 2....yan zote kali
HAtiA! | & || Nahc ni goma bora sana maishan mwangu! Big thumb Dizasta! Binafs Hujawah kuniangusha !
sishangai kukuta huu wimbo iko hivi ,nimechoka kusifia......ur le best broo....
Dizasta Vina my all time rhymer, heshima yako bro sijawahi chukia kusikiliza nyimbo zako ( nyumba ndogo, siku mbaya, hatia, siku nikifa, no body is safe, the lost one,kanisa na nyingine nyingi), we ni kioo cha jamii kila mmoja ruksa kutumia!
zuia nanga kabla haija2a huto heshimu mvua kma bdo haujarowa. kwa mchango ninaotoa ndo unokufanya unawaza mipango ya ndoa 100%
Dahhh 🔥 🔥, hatari sana broo vitu vyako huwa vimetulia sana namtuu awezi ielewa story mpaka afike mwishoo
mtu mbaya Dizasta vina nakubali kaka kazi kazi kafiri hazaliwi hutengenezwa na dunia daah mamae we ni sumu isiyotibika na maziwa
"inaitwa zuia nanga kabla haijang'oa/ maana haujaheshimu mvua kama bado hujaloa/ Dizasta uko makini katika uandishi na ndio fasihi hizi, vizuri kaka unatufunza wengi.
namuelewa sana huyu jamaa,kila mtu nnayemsikilizisha basi jua atanisumbua nimtafutie nyimbo za jamaa,anajua kichz.....na kila siku anazidi kuwa mbaya,nomaaaaaaas
hii kweli hatia ii..... dis z panorama.... we kiboko...
🙌🙌🙌🙌🙌 Kweli na mm Sina Hatia kukuubaliii hii ngoma
Dizasta vina your a pure MC broo respect mno arifuuuu
Officially Dizasta ndio emcee bora contentwise,fid Q anaeza akawa mzuri kwa rhymes na flows kuliko Zasta,Mbishi anaweza akawa mbunifu lyrically lakini kwa kuzingatia uwezo wa kuform combination ya content nzuri na better lyrics,Zasta is the best,ts sad kwamba anaweza asifike ambapo wamefika watu wa mainstream hiphop lakini akipata management nzuri bado hiphop kama hii ikiwekewa beat LA mainstream itafanya vizuri sokoni,kina Eminem,kendrick na Jigga wanaandika mistari mizuri kwenye beat nzuri ndomana wanatawala mpk ma chart regardless kuwa na vielement baadhi vya old school,Zasta yupo kama JCole ivi,beat kwake haina maana,cha muhimh sana n content na flows.keep the good music alive brother
@dizastavina
5 жыл бұрын
prosper deogratius I'm grateful!!! Thank you
@phillimonambilikile2846
3 жыл бұрын
Hakika anaweza
@ziroke
Жыл бұрын
I'm a kenyan but Dizasta is the best Emcee in Africa despite doing Swahili only.
Wimbo niliokuimbia kamwe hauta kukonga/ Utachoma mkuki moyon kisha kunyonga/ Dizasta vina we mkali sana yan unajua had bac respect kwako braza
Today KZread algorithm recommended this gem 💎 and now am locked ...kazi safi aise one love from H Town
Man katika ma lyricist bongo hapa, you run this category. Nimefuatilia ma emcees kibao, but you're the illiest!
Nahisi hii ni zaidi ya uandishi..sitaki kukulinganisha ila naona unaandika vitu kuntu sana.umeandika maana halisi ya wimbo wa fasihi haswa.tamathali za lugha umezitendea haki..dizasta wewe ni mshairi mzuri sana
from kenya....bro uko juu tu sana. well done dizasta vina..
Daaaah broooo! Naomba nisiseme kitu nitatukana bure kuna wasenge wengi Sana wanapewa heshima Tanzania na hawajafika hata robo ya uwezo wako .. nadhani muda wakwenda mainstream umefika brother tunatamani kuona umefanikiwa kupitia kipaji chako mzee bless up 🙌🙌
@isayaanyisile4115
6 жыл бұрын
daaaaaa mbeya we dizaxta ni janga sana mbeya city we ndo king
@hamzasylvain8503
5 жыл бұрын
Rajab Seif u're alright bro anakipaji huu msera watu
@official_bk_melodytz2802
3 жыл бұрын
sahihi
@goodluckkankara9088
2 жыл бұрын
🖐️🖐️🖐️🖐️🖐️
haipiti siku.bila yakumskiliza dizasta......... kunanyimbo sikuikifa. ninyimbo inayo fundisha san
Braza we ni nyoko
da! kwel we ni dizasta huna deni na ilo Jina kabisa 💪💪👏
Mmh mzee hatia 2 n noma nmeelewa dizasta vina#
I'm here 2022, tz government should consider about your lyrics students can learn something if this could be one of the subject in classes.
brother we ni balaa, m nmpenz sana wa tamaduni lakni kwasasa naona umebaki wewe, tu unae imba real hip hop keep it bro
dizasta na songa ndio waliobaki kutufahamisha nguzo za hip hop Tanzania
Heshima 🔥🔥🔥🔥🔥
Dizasta ww fundi wa mistari tanzania nzima
Daaaah nimeamin bongo magumashii aiseeeee yan dizasta wew ni zaidi ya MC cha ajabu show anapata whozuu duuuuunh
Gonga like tazama kama la 10 maana haishi utam #dizasta mi sikupingi mzee
Kali sana mwanangu very discriptive
So talented, upo vizuri sana Man, isingekua promo zao tz hizi za kujuana duuh!
Dizasta unajua sana mwanang Dah 🙏🙏🙏🙏
Nomaaa sana
haimaanishi kuwa tunaianza safari nataka nikuandalie maumivu makalii,,, ni hatari
Dondoko LA Hatari.... Mtiririko akisi!!! Dizasta unajua!!!
dah! tabia yangu hii kabisa
Dah!! nice broo❤❤
duuuh jamaa balaaa mjinii.
Kichwa changu ich , kichwa changu kishahadili kuwa ntalala na ww na haifiki......
Dazasta we ni profesa wa hiphop...hcho kichwa ni madini
Dooh Greeny city stand up. ..broh yah the illest lyrist to happen in Bongo. .. cool beat blended with emotive lyrics and rappin style demonstrate your music excellency. ...I love the track in its totality. .amount up brah
Kijogoo nakubali boy uko njema
Good bro nazipenda kazi zako dizasta
nakubali sana mzee wa vina, hii kali sana
Kazi nzuri sana dizasta vina
kichwa kimejadiliii...... ntalala na ww kabla ya jumapilii
Blessed broo
Dizasta beet original mashail mazur na Tena yanaendana na uhalisia
Duuh😲😲 ukweli kam huu machiz tunasemaga wachache
Kuna Akina koba na wapenzi wao mdaa huuu af Kuna sisi kina tekash na ngoma za dizasta HII NI VIOLENCE KABISA
bongeee mojaa la ngoma dizasta umeua kazi nzuriii sanaa $unaweza
Mashairi mazuri
Welldone! Jamaa unaandika kilichobora zaidi.
Kwel dah some times wanawake wenyew wanatuwek lweny #hatia
Kichwa changu ichi kichwa changu kishajadili kwamba ntalala na ww na aifiki jumapili ntakuwa nimeshakuacha.......
nakukubali sna mzee
Respect to your brother ✋
unajuwa jamaa
Dah! Nimekosa chakusema. Hongera bro kazi nzur.
Dzasta broo ww noma ani dah🔥🔥
Dizasta vina Naheshimu uwezo wako sina wasiwasi na kila ngoma yako Kali hii bro
tisha san broo
Respect kwako unajua sana Dizasta Vina
Kazi Kali.... MTU anaejua mziki mzuri lazima akucklze
dizasta umenichanganya sana br nimeludia zaid ya mala5 nimejikuta chozi linatoka
Sibadili dhambi hata mbingu ikisogea nyumaaaaa(unaweza usimwelewe mjuba kamaanisha sana let music make sence vina ushakuwa dizasta maisha marefu sana kaka mkubwa
You on yur Zone Broddah.
my favourite song..🔥🔥🔥
Brother your writing is very eloquent....shkamoo kaka ...i salute you
@dizastavina
3 жыл бұрын
Appreciate the love , please share
Dizasta vina,,,,, we ni mkali balaaaaa
safi jamaaa
damn!! vina we ni hatari
mvumilivu hali mbivu iyo mezali iliondoka
Nakubali
Conscious
Tunaomba hatia 4
Bongo nzima hakuna MC mwenye mistarii kama yako mzee daaaaaah unajua sana mzazii
#moyo ulio vunjika hauna tiba.
Mwamba Sana,
brother, nakubali sana.
viewer wapili kabisa nlkua naisubiri sana hii.heshima kwako dizasta
Nakubali distasta vinaaa
Piga mawe ya shingo D nigaa
Nashukuru dizasta
@dizastavina
5 жыл бұрын
Welcome
Hivi Dizasta Vina anaishi kwenye hii sayari au yupo nje ta sayari? ... anyway my Favourite artist always ✊
dizasta a hiphop story teller.
🔥🔥🔥🔥
Bro we ni shida
Amani Ndugu #DizastaVinA
Respect💪
duuuu we mkali mzee
this guy is underrated for real
@omogacharles7361
3 жыл бұрын
Very underrated
they need rapper like you in tz
Dizasta 🔥 🔥 🔥
Digg down tena
Motoooooooooooooooooooooo
Genius
hatuwez kujutia kaz kutoka kwa wenye vipaji miaka miaaa mzeee