Dizasta Vina - Siku Mbaya
Музыка
Stream And download SIKU MBAYA
Audiomack - audiomack.com/song/dizasta-vi...
Mdundo - mdundo.com/a/2263
Boomplay - www.boomplay.com/songs/646553...
Apple Music - music.apple.com/us/album/siku...
Spotify - open.spotify.com/track/65361i...
Follow Dizasta Vina on socials
FACEBOOK - / dizastavina07
TWITTER - / dizastavina
INSTAGRAM - / dizastavina
Music video by Dizasta Vina performing SIKU MBAYA. (C) 2018
PanoramaAuthentik
Lyrics
[Yeah!
Black market!
Ringle Beatz!
Nakurupuka kitandani baada ya ndoto za kutisha
Moyo unadunda sana na jasho linanitiririka
Macho nafikicha, taswira, naona kiza
Kwa muda nasizi kimya na dakika zinapita
Zikijirudia ndoto hatari naona woga
Nakosa hoja napotafakari nilichoota
Namwamsha wife aniwekee maji ya kuoga
Ananijibu anahisi homa na mwili mzima umechoka
Nampa pole, Staki kuanzisha zogo wala nini
Maana hata sura inaonesha ana kinyongo na mimi
Ni muda sasa napokua nae hajiamini
Nacheki saa nagundua nimechelewa kazini
Napiga zangu maji mwilini
And just for the record, Mimi ndo mtunza funguo za ofisini
Nakuta wafanyakazi na bosi wapo getini
Kwa ghadhabu kila mmoja akinitazama mimi
Kabla sijameza mate wala sijabuni sala
Naambiwa walikuja wazabuni kwa biashara
Na kwakua nilichelewa kufungua ofisi
Mchongo ukafa, nimeingizia kampuni hasara
Baada ya masaa kibao ya kufikiri
Ofisi ikaweka kikao kunijadili
Waliniona driver nimeangusha basi
Wakafikia mwafaka wakunifukuza kazi
Nikatahamaki, sikujua lakufanya
Pale kwenye kamati hakuna wa kumtazama
Nikahisi ni mipango ya kikuda imefanywa
Sio gari tu, maana hata nyumba nilinyang'anywa
Nikajiuliza huruma imekwenda wapi?
Kila mtu alijua kua nilipenda kazi
Niliheshimu kama navyoheshimu ndoa ama mzazi
Ama muumba, leo nimepata doa kwenye shati
Acha familia, vipi deni la ofisi
Wamenipa mwezi, nikifeli watanifilisi
Mtoto shule, pia bunju nina shamba la kukopa
Sijalipa na kijiji nina ndugu wa kutosha
Nguvu zilimalizika, nikatoka kwa adabu
Licha ya ghadhabu kunishika
Nikajipa moyo kua nna mikono pia na miguu
Vyote vyangu sina sababu ya kushindwa
Nilikosa wa kunishika wa kumweleza
Mshahara ulikua mdogo nilishindwa kuwekeza
Nikapiga moyo konde mimi mwanaume nita-fight
Nikpanda gari nikampe taarifa wife
Nikiwa ndani ya dimbwi la mawazo
Nikitafakari hivi vitimbi na vikwazo
Mbele yangu akakatiza mpita njia
Kwakua sikua makini na gari nikamvamiA
Dakika mbili, wananchi wakalizunguka gari
Wakinishutumu sana sababu ya mwendo mkali
Nikaitikia wito nikitegemea thawabu
Nikampeleka mgonjwa na akaanza matibabu
Narudi zangu home, misemo ya kishenzi nikitema
Chumbani nasikia mihemo ya mapenzi
Bila hodi, mlango nikaufungua kwa ghadhabu
Nikamkuta house-boy juu ya kifua cha mke wangu!
Nikabaki kama zuzu
Yule wa kunifariji ndio ameniletea uchungu
Nilitaka nilianzishe sikua na nguvu
Huku nafsi inanishauri kwamba nimwachie Mungu
Swalini kwamba sina moyo mkunjufu?
Au kwakua muda sijaenda kuabudu?
Au tuseme mja nina gundu?
Au kwakua nilijenga nyumba na sikuwajulisha ndugu?
Sijaona faida ya pato langu
Wazazi walikufa bila kula jasho langu
Mawazo kwenye kichwa yamezidi
Dunia ina watu wengi na sioni wa kunifariji
Naitazama ardhi, naitazama mbingu
Sioni nuru nachoona ni maumivu
Maswali mengi, bila majibu
Ila Swali kubwa ni vipi mimi nitaimaliza siku?
Jua linazama bado sijiamini
Naona nadondoka ila sioni nikifika chini
Saa tano na dakika hamsini
Bado dakika kumi siku iishe na sijui kinafata nini
Oh my God!
Пікірлер: 114
Thank you for watching, Pakua audio hapa www.audiomack.com/artist/dizasta-vina
@davidlendoro4819
5 жыл бұрын
Much respect.... Getting you from +254
@gun_vina7283
4 жыл бұрын
U are ze best rapper and my roll modal
@khalidyndi
4 жыл бұрын
2020 weka vitu master
@mussamasanja5842
3 жыл бұрын
uko saw jietekeze
Afadhali nimekutana na ngoma kali nilikuwa nazitafuta kila siku. Ahsante sana brother Dizasta
Hakuna story Kali kama siku mbaya aisee anayebisha atoe ngoma tuiskize
Duuh unaweza kulia aisee hii movie hatarii...!!(kumbe nyimbo) unajua kilichoongelewa chote kinakuja Kama picha kichwani.🙌🏼🙌🏼
@stanleydancertz4099
3 жыл бұрын
Point bonge bonge#🙏
unatumia lugha ya kiswahili kwa ufasaha, pongezi sana kwako. ni vema wasanii mufahamu zaidi namna ya kuwa na mtiririko mzuri wa lugha, mfano MSTARI MMOJA NI VEMA UKAWA NA LUGHA MOJA HATA KAMA WIMBO UMEIMBWA KWA LUGHA ZAIDI YA MOJA. sio mambo ya "yoooh! nilimove fasta na binti nikamkonyezaa, she was pretty haswaa mwenye macho ya kulegeza....nk" hiyo inakuwa sio sanaa bali kinyaa. BIG UP sana #Dizastavina
@yaedlifemedia3203
4 жыл бұрын
Uyu mchiz fundi
Thank you for watching, subscribe
@PaWahMusic
3 жыл бұрын
Maaad bars. KE follwing
@dennishullu870
3 жыл бұрын
Daaam
Nikiona wanavyo pewa promo mabwege nahisi kulia kiukweli😭😭 Pia mimi nina kipaji ila cha kwako ni moto kaka🔥🔥🔥🔥💯💪💪🇰🇪
@yaedlifemedia3203
4 жыл бұрын
Yah kwel kabisa
2023 tujuane hapa👇👇👇👇
Tunaosikiliza 2023 tujuane
This channel diserve my Subscription.🔥
Dizasta broh ubongo wako una kitu kukuubwa sana hii ni moja ya ngoma nnayoikubali sn toka kwako..Endlea kushusha zana mwana.
@enockmelita34
6 жыл бұрын
Jamaa ana chora sana. Kazi safi'
2023🔥🔥🔥
Daiiim ..! Yo day was fuckd up foreal
Uko vzur sana Braza kazi nzur sana hii hongera
The verteller again the verteller bro u got huge gift from God
All the way from kenya...uyu mnigga ni hatari
😭😭😭😭nikisikiliza ngoma zako uwa nalia kaka
proffesa wa tungo dizasta vina.
Nakubali uwezo wako dah nooooma Sana
Unawez❤
Salute homie
I wish ningekuwa presenter wa radio au Tv ningekuwa na bonge la show kwa hizi ngoma mtaani.... tungefunika show zao zotee mbovu za mchana...
oya d ww unafanya real hip hop wasikubadilishe mwana stay kwenye njia yako boy u made it.nitafute muhim sana D
Salutiii zebabaaa 💪
dizasta ngoma zako ziko powa sana my Brother Big up
Da hip hop inatuweka sehemu yaani.niivyooo sisi hatuharibu umeme kwa wabana pua.no ngumu na kweliiii tuuuu.hiphophiphop.
We jamaa hufai🤣🔥
Nyumba ndogo.kanisa.no body safe.du hii ni kweli dizasta.Ila ni dizasta kwa fake rappers
Story teller mnoma sana Dizasta
fund mkal dizasta Ngoma Bado ya moto
Brother, unajua mpaka unawakera wanaaaaaa,😂😂😂😂😂❤❤❤❤
Naelewa xana uandishi wako kaka noma xana
daah asee apart from otherswe want these kind of artists too
Duh! Mwana unaandika vtu almasi.
jamaa anajua mpaka unaboa
Kila nikiskiliza ngoma zako najifunza kitu
Shidaaa sana
ONE LOVE FROM KENYA DOGO LANDU
Daaah Hawa watoto wasijaribu kumpima Dizasta miaka 100
🔥🔥🔥🔥🔥🔥😅😅😅daaah nakosa la kusema
safi sana mwanangu... kuna kimdundo fulani kama cha Jayz FT Alicia keys NEW YORK
motoooo huo
Bongo bahati mbaya
Nakusikiliza sana vina we ni mtu hatari
Naelewa mziki wako upo kihalisia isee we jamaa ni hataree
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks, please share
Tishaaaa SaNa ma boi Wewe ndie mC pekee tz
So sensitive...
Maandishi makubwa sana mzeee unachora kwa bikari nini....hahaaaaaa Rap
Vinaaa
disaster nakuelewa xana bro
Vip xx kuhusu video
informative content, big tune +254 love
Yani dizasta ulijua nilichokua naitaji dahh
Great
Yeyeeee
My favorite song
Uko vizur broo
2023 twende bado tunasikiliza
NC one
Bigap kaka❤🎉
ur lyrics Live homie,big up
bad day...... shsss, this is fire Man.... one for the record.
Sana iko poa
🔥🔥🔥🔥🎤🎤🎤 much love from kampala Uganda
iko pw san
OH MY GOD
ila sio mbaya ukapiga double double hizi za kwetu na mainstream pia tunahitaji kuona unafanikiwa kupitia kipaji chako
Dizasta vina ni achecheee achecheaaaa noma
Vina vimekaaa
Hii ni movie
Daaaaah mwanangu husikate tamaa kuandika hizi lyrics za kibabe
Bro.... Nakukubali sana
Oyoo 2019 twende sawa
ebwana blessed sana d vina
💯💯
The verteller
extra odinary!
komaaa kk
Still watching
🎉🎉
Respect bro
😮
Skills💪
Nc
Life time Experience in a Day. Too deep mzee
@zittotv9972
5 жыл бұрын
austin komb
Nomaaa
wejamaa noma
good idea bro
Fundi
🔥🔥
Dizasta
Anzia leo nipo kwenye boat yako
@dizastavina
3 жыл бұрын
Karibu
ziggy hendrix signed
Bro siongei sana ila una akili kubwa
mzee mbona nyimbo zako ni nzuri ila zote hazina chorus
@dizastavina
6 жыл бұрын
mrmanjale jr napenda zikiwa hazina chorus
@manjalejuniorlg7024
6 жыл бұрын
POA POA MZEE BABA NYIMBO ZAKO CONTENT IKO POA SANA NIKUOMBEE KILALAHERI KTK SAFARI YAKO YA MUZIKI UTAFIKA MBALI KIKUBWA NI KUKAZA TU
Maandishi makubwa sana mzeee unachora kwa bikari nini....hahaaaaaa Rap
motoooo huo