Dizasta Vina - Mwanajua ft Dash
Музыка
Category: Music
Song: Mwanajua
Artist: Dizasta Vina/Dash
Music: Ringle Beatz
Soundcluoud - / mwanajua-ft-dash
Mdundo - mdundo.com/song/1674042
Audiomack - audiomack.com/dizastavina/son...
Lyrics - genius.com/Dizasta-vina-mwana...
Other Musical contents
Audiomack - audiomack.com/dizastavina
KZread - / dizastavina
Deezer - www.deezer.com/artist/67967532
Apple music - artists.apple.com/a/profile
Mdundo - mdundo.com/a/2263
Genius - genius.com/DizastaVina
Boom play - www.boomplay.com/artists/3288... - artists.spotify.com/c/artist/...
Connect with Dizasta Vina on social medias
Instagram - / dizastavina
Twitter - / dizastavina
Facebook - / dizastavina07
sw.wikipedia.org/wiki/Dizasta...
Business: Pan.authentik@yahoo.com
Website - bio.link/dizastavina
Lyrics
Alizaliwa mashariki alifahamika mahali pote
Alikuwa malaika wa ndoto zetu wote
Walimwita Mwanajua kwa maana alijua vyote
Alitamalaki nuru ilitua mahali kote
Na kila mahala alipita watu walimuheshimu
Hakwenda shule ila aliheshimika ka' mwalimu
Alikuwa mzuri kweli lakini shobo hana
Hakuna aliyemgusa kwani alikuwa wa moto sana
Urembo ulimuweka juu hakushuka anga zetu
Alikuwa maarufu kushinda hata bwana Yesu
Hata watoto walimpenda walifanya sherehe
Tuliobalehe alipopita tulimwaga mbegu
Ilipofika asubuhi tulimuwaza yeye kwanza
Ilikuwa ni kama desturi kumfata
Tulikuwa hatuli tukasaza
Tuliwaonea wivu rafiki zake Mekuli na Veneranda
Walikuja madogo wajanja na mapesa
Wakauliza mama ukivaaje unapendeza
Wakamuahidi ndizi, mawaridi na hariri
Lakini jasiri rangi yake ya asili ilitesa
Warembo wa dunia na vivazi vyao
Waliwaza kumfikia na ilibaki njozi kwao
Wazungu walikuja na pozi kibao
Walimkaribia mwisho walibabuka Ngozi zao
Mwanajua... amepotea kama hakuwepo
Mwanajua... ameondoka kama hakuja
Mwanajua anatukumbusha kuwa kilichopo
Kitakuwepo tu kwa muda
Mwanajua... Mwanajua... Mwanajua...
Tulijaribu kutumia chambo
Apite anase ili tuweze kutupia mambo
Mitego iliwekwa aje atumbukie hapo
Tuliishia kumwona mbali na mwisho kuumia macho
Haki ya nani, kuna walo'diri kumwita Mungu
Walitukuza walisadiki na kuabudu
Na sisi alitupa nguvu
Tuweze kupambana kutafuta pesa ili tu tuweze kummudu
Manyoka waliyavua magamba yao
Wapendeze ili waje waweze kupata fao
Walitanguliza vyeti na madaraka yao
Waliisha kufa tukawazika na haraka zao
Licha ya utofauti wake
Alikuwa mkimya hakuna aliyeisikia sauti yake
Wenye wivu walichoshwa na mizingu
Maana alingáa sana kiasi alizificha nyota kama wingu
Naziwaza features zote complete
Nilitazama sikuona diva wa ku-compete
Bila ina ala make-up za kisasa
Aliwaka sana. mtoto Fulani konki
Mwanajua... amepotea kama hakuwepo
Mwanajua... ameondoka kama hakuja
Mwanajua anatukumbusha kuwa kilichopo
Kitakuwepo tu kwa muda
Mwanajua... Mwanajua... Mwanajua...
Yeah!
Iwapi barabara isiyo na kona?
Simulizi isiyo na mwisho?
Makala zimeandikwa tupo na nakala tunasoma
Imeandikwa upasuka inapovuma sana ngoma
Vile alikuwa amesukwa ni kwere
Alipofika ilikuwa ka' umeshushwa umeme
Kwa uzuri utadhani amejiumba mwenyewe
Tulihisi hatashuka milele
Tulikosea kwani... zile sifa hazivai tena
Imefika jioni na yeye hang'ai tena
Ndege hawaimbi nyimbo, misa zimefungwa
Wamwaga mbegu wote tumebaki dilemma
Najiuliza, alifichwa na ndugu kwenye kaya?
Au alinenepa kutoka aliona haya?
Hakujua, tulishindwa kutafakari chanzo
Maana alizima na hakuwa wa moto kama mwanzo
Anatukumbushwa kuwa tayari inapofika zama
Hatamu yake imefika, zamu yake imekwisha
Hajaacha hata alama ya damu yake
Amekufa na utamu wake Yarabi nasikitika sana
Namkumbuka sababu hakudanganyika
Nuru yake pahala pote ilitawanyika
Toka mzizima pwani kote alipagawisha
Aliondoka na mwisho alionekana ziwa Tanganyika
Dhahania zimeandikwa alichoka pengine
Aliondoka ili wang'ae nyota wengine
Itakufa damu, itakufa nyama
Nenda mwanajua nenda tutakumbuka sana
Mwanajua... amepotea kama hakuwepo
Mwanajua... ameondoka kama hakuja
Mwanajua anatukumbusha kuwa kilichopo
Kitakuwepo tu kwa muda
Mwanajua... Mwanajua... Mwanajua..
Пікірлер: 351
It's rare to find poetic minds like this, with a deep meaning within the verses✊
@dizastavina
3 жыл бұрын
It in deed is
@GibiGene
3 жыл бұрын
Sure
Tunawo amini mwana jua ni upendo wa dhati tujuane hapa 2024
"MWANAJUA" , kwa kufanya stori ndefu kuwa fupi ni KILA KITU KINA MWANZO NA MWISHO, CHUNGA SANA MWENDENDO WAKO.
MWANAJUA NI NYIMBO NGUMU SANA LKN KWA MAONO YANGU HAPA DIZASTA ULITAKA KUPOTRAY ISHU YA SIASA YA BONGO, HASWA RAISI WETU HAYATI MAGUFULI
Mbona kama Jamaa ana Madini ya Kutosha kuliko kikosi flani hivi... Jamaa ni jeshi la mutu Mmoja aisee
Respect sana vina mungu akupe maisha marefu ngoma zako zidumu
Kwamba tuliobalehe “tulimwaga mbegu” 🙌🏾🙌🏾 Let’s support Dizasta kwa kununua nakala halisi kutoka kwake.
@stevenmpeka9536
3 жыл бұрын
Mzigo tunapataje
Walimwita mwanajua maana alijua vyote...safi sana dizasta vina
Sanaa iliyotumika ktk uandishi na picha mtembeo imejenga upekee ktk ufikishaji wa kazi hii Verse 01-Kwny Background JUA LINACHOMOZA Verse 02-Jua LIMETULIA KTK NAFASI YAKE Verse 03-Jua LINAANZA KUZAMA TARATIBU Daaamn,and DASH inabd azingatiwe sn kwa CHORUS kalii
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks man
We m2 au jini""co kwa uandishi huo,salute mzee wa kumwaga vina
@tofatofali9803
3 жыл бұрын
Definition of story telling ni dizasta
LYRICS VERSE 1 Alizaliwa mashariki alifahamika mahali pote Alikuwa malaika wa ndoto zetu wote Walimwita Mwanajua kwa maana alijua vyote Alitamalaki nuru ilitua mahali kote Na kila mahala alipita watu walimuheshimu Hakwenda shule ila aliheshimika ka’ mwalimu Alikuwa mzuri kweli lakini shobo hana Hakuna aliyemgusa kwani alikuwa wa moto sana Urembo ulimuweka juu hakushuka anga zetu Alikuwa maarufu kushinda hata bwana Yesu Hata watoto walimpenda walifanya sherehe Tuliobalehe alipopita tulimwaga mbegu Ilipofika asubuhi tulimuwaza yeye kwanza Ilikuwa ni kama desturi kumfata Tulikuwa hatuli tukasaza Tuliwaonea wivu rafiki zake Mekuli na Veneranda Walikuja madogo wajanja na mapesa Wakauliza mama ukivaaje unapendeza Wakamuahidi ndizi, mawaridi na hariri Lakini jasiri rangi yake ya asili ilitesa Warembo wa dunia na vivazi vyao Waliwaza kumfikia na ilibaki njozi kwao Wazungu walikuja na pozi kibao Walimkaribia mwisho walibabuka Ngozi zao CHORUS Mwanajua ..amepotea kama hakuwepo Mwanajua..ameondoka kama hakuja Mwanajua anatukumbusha kuwa kilichopo Kitakuwepo tu kwa muda Mwanajua…Mwanajua…Mwanajua… VERSE 2 Tulijaribu kutumia chambo Apite anase ili tuweze kutupia mambo Mitego iliwekwa aje atumbukie hapo Tuliishia kumwona mbali na mwisho kuumia macho Haki ya nani, kuna walo’diri kumwita Mungu Walitukuza walisadiki na kuabudu Na sisi alitupa nguvu Tuweze kupambana kutafuta pesa ili tu tuweze kummudu Manyoka waliyavua magamba yao Wapendeze ili waje waweze kupata fao Walitanguliza vyeti na madaraka yao Waliisha kufa tukawazika na haraka zao Licha ya utofauti wake Alikuwa mkimya hakuna aliyeisikia sauti yake Wenye wivu walichoshwa na mizingu Maana alingáa sana kiasi alizificha nyota kama wingu Naziwaza features zote complete Nilitazama sikuona diva wa ku-compete Bila ina ala make-up za kisasa Aliwaka sana.. mtoto Fulani konki CHORUS Mwanajua ..amepotea kama hakuwepo Mwanajua..ameondoka kama hakuja Mwanajua anatukumbusha kuwa kilichopo Kitakuwepo tu kwa muda Mwanajua…Mwanajua…Mwanajua… VERSE 3 Yeah! Iwapi barabara isiyo na kona? Simulizi isiyo na mwisho? Makala zimeandikwa tupo na nakala tunasoma Imeandikwa upasuka inapovuma sana ngoma Vile alikuwa amesukwa ni kwere Alipofika ilikuwa ka’ umeshushwa umeme Kwa uzuri utadhani amejiumba mwenyewe Tulihisi hatashuka milele Tulikosea kwani…zile sifa hazivai tena Imefika jioni na yeye hang’ai tena Ndege hawaimbi nyimbo, misa zimefungwa Wamwaga mbegu wote tumebaki dilemma Najiuliza, alifichwa na ndugu kwenye kaya? Au alinenepa kutoka aliona haya? Hakujua, tulishindwa kutafakari chanzo Maana alizima na hakuwa wa moto kama mwanzo Anatukumbushwa kuwa tayari inapofika zama Hatamu yake imefika, zamu yake imekwisha Hajaacha hata alama ya damu yake Amekufa na utamu wake Yarabi nasikitika sana Namkumbuka sababu hakudanganyika Nuru yake pahala pote ilitawanyika Toka mzizima pwani kote alipagawisha Aliondoka na mwisho alionekana ziwa Tanganyika Dhahania zimeandikwa alichoka pengine Aliondoka ili wang’ae nyota wengine Itakufa damu, itakufa nyama Nenda mwanajua nenda tutakumbuka sana CHORUS Mwanajua ..amepotea kama hakuwepo Mwanajua..ameondoka kama hakuja Mwanajua anatukumbusha kuwa kilichopo Kitakuwepo tu kwa muda Mwanajua…Mwanajua…Mwanajua…
@africanicodemus6037
3 жыл бұрын
Oyaa mwanajua ni Nani?
@emistoramisto3234
3 жыл бұрын
Nahisi mwanajua atakua #Pesa😊
@BongoCryptos
3 жыл бұрын
Mkuu Lyrics uwe unaweka kwenye description pia (mara baada ya links) kwaajili ya SEO.
@saidsaid-dg3yq
3 жыл бұрын
kal mnoooo respect broooo
@mathayojohn5440
3 жыл бұрын
Hii ngoma ni tata Sana! Kuna Mambo matano Kati ya haya nayawaza ndio maan ya huu wimbo 1. Wakati 2. Kifo 3. Tanzania 4. Afrika 5. Nyerere. Km si ivyo bhc wew ni zaidi ya mrisho mpoto.
Tanzania and whole world is sleeping on dizasta..i have all his music on my phone, laptop,BT device...God bless you sir, keep going.. much love and blessings from KENYA 💯
@dizastavina
3 жыл бұрын
appreciate, Buy my new album now. call/text +255 655 696 811/+255 762 158 871
@ramadhanally138
3 жыл бұрын
@@dizastavina how much my brother nakuelewa sana
@ilomogold1715
3 жыл бұрын
Kuna ile ngoma kaimba dizasta inamuhusu mama inaitwaje boss naomba nisaidie jina lake
@ziggyhendrixx7445
2 жыл бұрын
Bruh He is so underated!!! Tatizo Tz wapenda taarabu wengi!!! "Hip hop haikubaliki tz angekua kenya jamaa angekua top sahii
@willinjowritter206
2 жыл бұрын
@@ziggyhendrixx7445 East Africans we have this culture of not supporting our own till one dies,apo ndio utaskia "alikua mkali,alikua legend"....till then brother our artists will continue battling depressions and mental health.
dizasta is the best hiphop
Mtaalamu dizasta vina,,, ukiwaka unaeza mgeuza fid akawa sajna
Moja Kati ya Tungo zilosheheni Mnururisho Murua katika Lugha ghafi na Ngeni kiasi..#👏🏿
Dah nsha comment sana sina cha ku comment. Eh Mungu tutunzie Mr. Tungo, Amin 🤲🏽
Wanangu mi sjaelewa.. kanichanganya sana aiseee... hii fasihi nomaaa💥💥
@msimika_III
2 жыл бұрын
Kama mm😂😂🤣
Nakbl dizasta vina hiphop ngmu ndo fundisho kwa makinda kwamba unaweza
Diza ee kaza ivo ivo wapo wenye mapenzi ya dhati na really HIP HOP unajua usibadilike nakikubali
Hahaah crazy D vina mwanzo kt & mwisho.
D again, ebwana kuna joto ila Dizasta wamoto kushinda jua na mwanae (mwanajua) ,, Bro u'r just out of this world ; Peter Drury anisaidie kuieleza Dunia the genius mind of you broh
@dizastavina
3 жыл бұрын
😂 😂 😂 Thanks man
Wewe jamaaa ni balaaa sijaona kama wewe jah bless u brother😊😊😊
Since nimeiskia ngoma yake ya SISTER aisee nikazikubal sana na zile HATIA nikihisi jamaa anakisia but nimekuja kujua mm ndo nilikua nakisia kuhisi jamaa hajui@@Kilichobaki kwangu nikununua albamu ya the VERTELLER
This is lit..bro..hii ni zaid ya zawadi ..msimu huu wa sikukuu
Best story teller in Tanzania hakuna kama ww professor 🙌🙌
"Maana aling'aa sana kiasi alizificha nyota kama wingu". 🔥🔥🔥🙌🙌
We Jamaa Nakuheshimu Sana. Thanks For creating this music Bro..
Di zasta Anajua Sana...nice story Vichwa kama hivi vipo vichache ktk Game
That's why u are real dizasta vina....professa Tungo ✅
Muda huongea kwa sauti ndogo yenye kelele kubwa hilo mwanajua hakujua...wish one day tupige story
Dizasta mtu mbad, unatisha faza. Big up
Fanya kazi kila mtu anaugenius wake kwa hip hop unaweza ntapataje albam
@dizastavina
3 жыл бұрын
PLEASE CALL/TEXT 0655696811/0762158871
Vina kwe mdundo namkubal. Tuliobaree alipopita tulimwaga mbegu
kal sanaa broo sema ile verteller nimeilewaaa sanaaa
Yes
Mwanajua alikua maaruf saan kulko hata bwana yesu hhhhh umetsha saan #dizasta vina"TT empire"
Thank you for watching!!
@hoodinparadisetv8664
3 жыл бұрын
nashukuru kwa Album bro nimekutumia hela umenitumia Album..Mpaka sasa hivi Ngoma ya *Wimbo usio bora* unaongoza 3-1
@respectmorigha5279
3 жыл бұрын
Album yako ina nyimbo ngapi dizasta?
@oswardnelson4205
3 жыл бұрын
Bro ngoma zako kali kinoma sa nauliza namna ya kupata albam zako Kama uko mbali yaan haupo tz.
@dizastavina
3 жыл бұрын
@@respectmorigha5279 20
@dizastavina
3 жыл бұрын
@@oswardnelson4205 unatumiwa kwa whatsApp au Email. Lipia 0762158871 MPESA au 0655696811 TIGO PESA nikutumie
This links deep about African History..."great thinker" respect creative author. Mistari konki'
Dizasta sijui unawazaga saa ngapi ila hongera una zaidi ya kipaji broo 🙏🙏🙏🙏
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks man
Nakukubali bro na mm sitochoka kusikiliza nyimbo zako,, unaimba kwa hisia Sana na mungu azidi kuwa na ww
@dizastavina
3 жыл бұрын
Amina... Nunua album ya THE VERTELLER sasa kwa shilingi 10,000 tu kupitia hizi namba 0655696811 na 0762158871
@oswardnelson4205
3 жыл бұрын
@@dizastavina poa bro lakn Kama uko mbali zinaweza kufikia vp sasa maan nahitaji Sana hiyo album
@dizastavina
3 жыл бұрын
@@oswardnelson4205 unatumiwa kwa email au WhatsApp baada ya kukamilisha muamala kwa shilingi 10000 tu kwa namba hizi 0762158871 au 0655696811.
@oswardnelson4205
3 жыл бұрын
@@dizastavina tatzo siku hizi wezi ni wengi naweza jua ni dizasta kumbe ni mtu tu mwingne
Tungo juu ya tungo. Unaweza usielewe chochote kama unasikiliza KWA masikio 😄✊😃🤣👏
@abdusephania2497
3 жыл бұрын
Huu ndo mziki man lzm uwe na akir ndo uelewe
@jimmymgata7555
3 жыл бұрын
Mimi nimesikiliza ila sijajua kamaanisha nini
Unaweza Dizasta
Imeandikwa hupasuka inapovuma sana ngoma,!!! %usiache KUTABASAMU%
@dommie444
3 жыл бұрын
Nimefurah kuona wajina anaependa hip hop km mim
Kali sn bro
"Ambae ajaelewa hii ngoma aniulize mm"
@msimika_III
2 жыл бұрын
nielezee Mzee😂
@raynoldyraymix7971
Жыл бұрын
Ujaelewa wapi
@briandelight6776
Жыл бұрын
@@raynoldyraymix7971 fanya long story short
Hakika hisia zangu ziko kwenye mikono salama HIP-HOP is my first choice music
Oya vina.....sikupingi....tupo underground mitutu inapofichwaaa.....💯👊
Nani kaona kuchomoza na kuzama kwa JUA
MI MARA ZAIDI YA 70 NAISIKILIZA HII TRACK, BUT MPAKA SASAHIVI SIJAELEWA KIPI KINAZUNGUMZIWA 🙌🙌 HII NDO MAANA HALISI YA HIP HOP BROO, UMETISHA SANA HILI FUMBO NI💥💥
@lucasthomas188
Жыл бұрын
Ina maanisha nini hata na hivyo,hadi sasa sijaambulia chochote
@uducadabla7223
10 ай бұрын
Hapo Anaongelewa IRENE UWOYA kwamujibu wamistari ya dizasta alipo sema "Alizaliwa mashariki" nahapa inaonesha anaezungunziwa anatokea wapi nahapoa nadhani ni Africa mashariki "Walikuja madogo wajanja na mapesa Wakauliza mama ukivaaje unapendeza" moja kwa moja apo anazungumziwa dogo janja kutokana na line ya mwisho ilivyo sema ukivaaje unapendeza hiyo ni nyimbo ya dogo janja kumbuka dogo janja pia alisha wahii kuwa mume wa uwoya "Wakamuahidi ndizi, mawaridi na hariri" navosema waka muahidi ndizi dogo janja pia ananyimbo inaitwa banana Soma moja kwa moja mistari ina mlenga Uwoya kutokana na sifa Alizopewa kwenye shairi ila code inafunguliwa na dogo janja baada ya kuhusishwa nae NB:uandishi umetumia sana code language na code nyingi huwezi kuelewa mpka ufatilie unaweza kushanga una crack code hapo maana inabadilika tena mafano anaposema "Toka mzizima pwani kote alipagawisha Aliondoka na mwisho alionekana ziwa Tanganyika" apo kuna kitu mwandishi anatumbia saa hizo line sijajua kama zina match na uwoya tena hapo that why yabidi uwe mfatiliaji hasa
@emmanueljudas4522
8 ай бұрын
wangapi wanajua hii ngoma inamuhusu Magufuli.. mambo ya fasihi haya.
@binahmedjuma8681
3 ай бұрын
@@emmanueljudas4522 Haiwezi kuwa amemwongelea Magufuli, nyimbo imetoka 2020 na Magufuli amefariki 2021 🤷🏾♂️🤷🏾♂️🤷🏾♂️
Hii itaftie muendelezo au background Kaka... Tunaitaman Sana kitaa as if Kama tunamjua mwanajua😄✌️
Damn😂😂😂😂,,I want to meet this man, mwambaa anajua mpaka najiuliza hivi inawezekenaje mtu kama huyu tupo nae zama zetu😂🙌🙌
Tununue album kwa fujo wanasta tumpe support The Verteller 👊
@muberluck9120
3 жыл бұрын
Eti wanasta?😂😂
MY TOP 5 TRACKS FROM "THE VERTELLER" ALBUM 1. Muscular Feminist 2. A confession Of A Mad Man 3. A confession Of A Mad Philosopher 4. Money 5. Tatuu Ya Asili Album imeshiba madini 🔥🔥 Big up sana #TheVerteller #DizastaVina
HII NGOMA NI FUMBO SAANA TUNAOMBA UFAFANUZI D MASTER D ZASTA. JESUSTER
Walikuja madogo wajanja na mapesa wakauliza "mama ukivaaje unapendeza?"
@fixmor7003
3 жыл бұрын
Dah nmeuelewa huo mstari ,kinoma
Dizasta ni tatizo. We ni best mc wa TZ, hakika
Unapata maarifa na burudani at the same time uksikiliza velteller Prof wa tungo uko vizuri kuliko wanawaita wazurri
yaani hii nyimbo nasikiliza sitaman iishe dizasta ni mtalam wa vina misemo na misamiat flan ivi fasaha
Big thinker. best story teller in AFRICA. DIZASTA VINA
@abdusephania2497
3 жыл бұрын
Yaa
Unaweza sana bro 💥💥
Salute bro,kweli hakuna mchawi wala mwanga atakaewanga hiki kichwa.....The verteller inanipa kiu yakusikiza madongo unayoturushia...
Daaah leo nimetoka kapa cjaelewa licha ya kusikiliza mara nyingi🤔
@bukuruhenry8787
3 жыл бұрын
Aise kama mimi tuu, jamaa ni fundi wa encryption
@fanleck2922
3 жыл бұрын
Dah.. hii noma. Inakuja inakataa
Ila jamaa huyu wakuitwa rigle beat mashine sana
Wengine walimwita mungu ni jua tu ila limefichwa kiaina ukweli anaujua yeye ila kama nimelosea anielekeza bro ni wazo tu
nakubali kaka mauwezo unayo one day nita ku gongea mdundo uni bless kaka naelewa sana
Ama kwel we ni dizasta wa vina kwa huo uandishi am i salute u for this y're so creative and talented
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks man
@hassanamimu1892
3 жыл бұрын
Thankx too
DIZASTA HUFAI KABISA 😎
@dizastavina
3 жыл бұрын
Thanks brother...
ni moto huuuu🔥🔥🔥🔥
You never dissapoint Mr verteller Sjutii kuwa shabiki yako Your number one fan
Asee ni zaidi ya movie. Jamaa una kipaji Sana✊✊
Vina ndio future yako nijogoo ulomkwepa kitaani lkn ukamkuta kwako
Funguaa shule ya muziki kaka me nitakuwa mwanafunzi wa kwanza
@dizastavina
3 жыл бұрын
Karibu, ada ni laki 3 kwa mwezi. Uandishi, midondoko, delivery, perfoming
Disasta vina you never disappoint man! Every song is a banger, every line a punchline! Madini mwanzo mwisho.
The verteller.. Ile intro imenipa madini ambayo nki speak mbele ya waelewa wananielewa. #Street_knowledge.
Real lyrist in Tanzania 👊🏾❤️💪🏾🔥🔥Dizasta
Kwangu mimi tafsiri ya hii ngoma ni clouds fm, jinsi mwanzo ilivyokuwa inasifika, jinsi kila msanii alivyokuwa anatamani kupata nafas ya kusikika pale, lakin leo hii ni kama haipo jinsi ilivyopotea
Natabari mwanajua ni africaa
Yes mwambaaa
🔥🔥🔥, always ni noma
Wanajua umetisha Sana mzazi
Daah Braza 👐 am yo fan since SITAKI GAME hadi Leo...nawaonea huruma wasiokusikia
Dizasta vina nakukubali
MWANAJUA Nimeisikiliza hii nyimbo ni miongoni mwa nyimbo zinazotoa ujumbe kwa njia ambayo sio rahisi kueleweka, mwandishi kaweza kuelezea mambo mawili kwa wakati mmoja na kuacha swali kwa hadhira Mwanajua ni msichana aliepewa sifa za jua au ni jua limepewa sifa za mwanake ?. Hii ndio maana ya sanaa Dizasta Vina #JAH BLESS YA
@fanleck2922
3 жыл бұрын
Au ni media imepewa jina la jua na sifa za kike.🤔
@calvinsabuni9277
2 жыл бұрын
Wewe pekee ako ndonaona unawezo Unaweza ku reveal the meaning brother kwa direct ni jua kwangu mara mwanamke wengine magufuli
@michaelramadhan9466
Жыл бұрын
ni magufuli😢sikiliza tena
@petercharles8572
7 ай бұрын
@@michaelramadhan9466Nyimbo ilitoka kabla ya kifo cha Magufuli... still ujumbe kila chenye mwanzo kina mwisho
Nakubali..... 🦁🦁
Ujawai kosea big ✊✊
Mmmmh vina, mwanajua ni afrika nn? Ngoma iko pw kinoma. Appreciate Sana Mungu wa rap!.
Dizasta: ni balaaa sana nakubali mzeee💯💯💯 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
Nakukubali sana kaka
Old School is Gold..... 🔥
hakuna wakuweza kumfunika huyu aliye kipendwa chamoyo wangu mwenye saut ilito pendwa maskion kwang
@dizastavina
3 жыл бұрын
Appreciate brother
Noma Sana home boy
Wamwaga mbegu wote tumebaki dialema...vinaaa...🤒🤒
Dizar tusaidie tujue maana yake
Alizaliwa mashariki then mda wa jion halina ata moto maana yake likizama mchana likiwaka linazuia nyota zote zisionekane jion Galina hata moto,
Dizasta vina hajawahi kufeli...
kubali sana dizastavina... respect kamandaaa....
Work of art toka kwa dizasta much respect big brain
...nimekuwa addicted na mziki wako bro,,,tanzu za kufikilika na zenye tija 🔥🔥 the one and only dizasta vina...
izi ni tungo za kichawi mpaka ufike miaka 50 ndo utaelew😢
🧠💥💯