Salama Na OMMY DIMPOZ SE6 EP31 | ELEGANT PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Ойын-сауық

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Kama kukiwa kuna mkutano wa Chama cha Watanashati hapa Africa na pengine Duniani basi Ommy Dimpoz anaweza kuwa mmoja wa viongozi wa juu kabisa wa Chama hiko na pengine anaweza kuwa hata Mwenyekiti. Hakuna swali juu ya utanashati wake kuanzia vivazi hadi nywele na hata kuongea. Anakumbuka utanashati wake ulianza toka alipokua mdogo sana, na wakati anakua si kama kila kitu alichokua anakitaka alikua anakipata ila alihakikisha vile vile vichache alivyokua navyo alihakikisha vinakua visaaafi na vinamkaa kweli kweli. Na tabia hiyo ya kujipenda na kuvaa vizuri ndo inamtambulisha Ommy Dimpoz kuwa ni mmoja wa wasanii wanaovaa vizuri zaidi hapa barani Afrika.
Omary amekua analelewa na Bibi yake baada ya Mama yake kufariki akiwa mdogo. Anakumbuka mapenzi ambayo amekua akimuonyesha toka zamani, ni kweli kama mtoto lazima utakua unamkumbuka Mama yako, ila Bibi yake alihakikisha anapata vile vyote ambavyo mtoto anakua anahitaji.
Mimi na Omary ni mtu na Rafiki yake kwahiyo mazungumzo haya zaidi yalikua ni kwaajili yako, uweze kumuelewa na kuifahamu milima na mabonde ambayo ameyapitia mpaka leo hii unamuona kasimama imara.
Kama mtoto siku zote unakua unataka kumjua Baba yako na haikua tofauti kwa Ommy pia. Shuleni watoto huitwa na wazazi wao, ukiwaona wenzako wanawaleta Baba zao na wewe hujawahi kumuona au pengine ni kwa nadra sana lazima likutie unyonge. Anakumbuka Mama yake alivyofariki na jinsi ambavyo Mzee wake alikata mawasiliano ki lazima kabisa, anakumbuka kwamba Mzee wake tayari alikua na familia nyengine lakini kama mtoto anaamini na yeye pia alikua na haki ya kupata mapenzi hata kidogo tu kutoka kwake.
Miaka ya hivi karibuni Mzee wake ameonekana kuutaka ukaribu nae kwa kasi kubwa sana ila kwa Omary huo umekua kama mtihani hivi, ana kinyongo nae bado na anaamini kwamba Mzee wake anataka kuwa karibu na yeye kwasababu tu ameona mwanae amekua maarufu na pengine anaonekana mambo yake mazuri. Hapo ndo panapo mtatiza yeye maana anaamini huo si upendo wa dhati, na hiyo ni sababu ya yeye kuendelea na maisha yake bila ya Baba yake. Pengine kuna siku itafika wawili hawa wataacha tofauti zao zipite na pengine watafahamiana vizuri na kuyafanya mahusiano kama Baba na mwana yastawi.
Pia tunafahamu kwamba miaka miwili na nusu au mitatu iliyopita Ommy aliumwa sana, na baadhi ya watu walithubutu kusema pengine hata kuimba inaweza isiwezekane tena ila kwa Rehma za Mwenyezi Mungu alimponya na kazi yake ya muziki anaendelea kuifanya kama kawaida. Nimekua nikispend nae muda mwingi kipindi ambacho tumekua tukifanya Bongo Star Search msimu wa kumi na mbili mimi na yeye, na kwasababu tumekua tukifahamiana kwa muda nimemuona kabisa hayuko 100% ila mimi na yeye tunamshkuru Mungu kwa hali alonayo sasa maana mitihani aliyopitia ni mingi sana. Haya maisha ambayo anaishi sasa ni zawadi kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na hatuna budi kumshukuru yeye kwa kumpa watu kwenye maisha yake ambao walihakikisha anapata matibabu yote ya hali ya juu ili maisha yake yaweze kurudi kama zamani.
Huku hilo hatukulizungumzia sana maana limeshaongelewa sana, ila tume ongea suala la ukuaji wake na mahusioano yake na familia. Urafiki wake na TID na jinsi walivyokutana. Urafiki wake na Ally Kiba, maisha yake ya shuleni na jinsi alivyokua. Urafiki wake na Diamond Platnumz na nini kilitokea kati yao. Muziki wa kizazi kipya na faida ambazo watu wana pata sasa na mahusiano yake na Chriatine ‘Seven’ Mosha na nini ambacho kimemfanya yeye afanye nae kazi. Pia tumezungumzia kutofahamiana kwake na meneja wa Diamond Platnumz Bwana Sallam Sharaff na Ommy emetuambia pia wawili hao maneno hasa yalianza kutoka wapi.
Yangu matumaini uta enjoy maongezi haya na utaokota mawili matatu pia ambayo yatakusaidia kwenye maisha yako ili mambo yazidi kuwa mswano.
Tafadhali Enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Пікірлер: 67

  • @yusuphpilion2465
    @yusuphpilion2465 Жыл бұрын

    Siku moja na mimi nitakaa kwenye hicho kiti nikihojiwa💪🏾 Amen

  • @pamanyango8917

    @pamanyango8917

    Жыл бұрын

    Mungu ampe maisha marefu salama, lnshallah Siku yako itafikaa,

  • @damariszuckschwert9489
    @damariszuckschwert9489 Жыл бұрын

    Nimemuelewa sana Ommy..,hatakama ni mimi watu wanisaidie hivyo kwenye ugonjwa ningewaoshaga na miguu nakuwalamba miguu mbele ya tv. Ndio waja waseme najipendekeza vizuri.

  • @amytullah2175
    @amytullah2175 Жыл бұрын

    Bonge moja ya interview 😅😅 kuna nilipolia na kucheka sana. All the best Ommy. Salama Shikana pia arudiwe 😅

  • @pamanyango8917
    @pamanyango8917 Жыл бұрын

    Much love from Kenya 🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪 ommy dimples napenda sannaaa, interview zako, sababu unajuakujieleza sanaa

  • @fatmakiraga4016
    @fatmakiraga4016 Жыл бұрын

    Last part ya joho imenitoa machozi we people need hugs

  • @hamadisalehe4566
    @hamadisalehe4566 Жыл бұрын

    Aisee Ommy mpumbavu sanaa😂😂😂😂😂😂😂 eti ngaaa my son

  • @leaherasto929
    @leaherasto929 Жыл бұрын

    Umejua kunichekesha Ommy hahaha et my Son

  • @manyangumashala466
    @manyangumashala466 Жыл бұрын

    Hongera sana Ommy Dimpoz,endelea kupiga kazi,na Mungu akuzidishie Zaidi..💥🔥🔥

  • @fortunatanasuwa6789
    @fortunatanasuwa6789 Жыл бұрын

    ngaaaa my son 🤣🤣🤣🤣🤣

  • @dejavevents
    @dejavevents Жыл бұрын

    inapendeza saana aise

  • @bakariomary5781
    @bakariomary5781 Жыл бұрын

    Namuomba Mungu sana usiku na mchana tena sana ili Mwanangu niwe nae karibu kwani kiukwel sijalelewa na wazazi hivyo najua chuki nilizokuwa nazo juu yao na naelewa maisha ni kama mate kuyatema juu hivyo nisipokuwa nae karibu lazima atanichukia tuu

  • @xasaxuma9835
    @xasaxuma9835 Жыл бұрын

    Joho came at the right time to help this guy…only God know y joho and why Omy kwenye maisha hutokea mambo kama haya ,,,when you least espect if you truly beleive in God and you are a good person…it comes back!! PeriodT

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan2499 Жыл бұрын

    Nimekuelewa sana Ommy, Sasa hapa Babako ndio chawa😅😀😀, Mungu hawasamehe mababa wote wapumbavu,Akiwemo mzazi mwenzangu.

  • @vivianjonathan1783

    @vivianjonathan1783

    Жыл бұрын

    🤣🤣🤣🤣🤣🤣

  • @vivianjonathan1783

    @vivianjonathan1783

    Жыл бұрын

    Kam wangu piah

  • @ukhutfatumah1154
    @ukhutfatumah11547 ай бұрын

    Interview yangu pendwa nimeludia tena kuisikiliza mwka huu ilo life uliloisha ndio langu alafu wala sijali hata kama ajanitafuta ishi maisha yako ommy

  • @gracegeorge4848
    @gracegeorge4848 Жыл бұрын

    My soooooon ! Mamae walah

  • @bakariomary5781
    @bakariomary5781 Жыл бұрын

    Nganganga my soooon yuhuuuu

  • @denisbruno9898
    @denisbruno9898 Жыл бұрын

    Hongera sana sister. Sema ushauri wangu naomba kama kuna session ya mashabiki wa hao unao wahoji kuuliza maswali kwao ingekuwa poa, kuna vitu tunajifunza sana na kupenda kujua vingne pia. Ahsante sana

  • @ednamushi601
    @ednamushi601 Жыл бұрын

    hapo wenye my son hahahahhahaha🤣🤣🤣🤣

  • @egnokapinga16
    @egnokapinga16 Жыл бұрын

    Kuna yakujifunza umu🙌✊

  • @kidevusitu3817
    @kidevusitu3817 Жыл бұрын

    Big up home boy before nilikuwa nakuchukilia bishoo.frani.hivi lakini sasa nimekuelewa unajitambua sana (jiongeze kielimu u very wise, ,one love nigga

  • @salomewandya7257
    @salomewandya7257 Жыл бұрын

    Hahaha nimecheka sana hapo kwenye myson 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣

  • @ibrahimkibira9943
    @ibrahimkibira9943 Жыл бұрын

    Was nice interview 👌

  • @stevewanga957
    @stevewanga957 Жыл бұрын

    Mm naona hii time ni ndogo sana

  • @albusayyd3020
    @albusayyd3020 Жыл бұрын

    Ommy samehe na usahau mzee ni mzee tuu

  • @itNeza
    @itNeza Жыл бұрын

    🤣 Kwenye Story ya Mchuwa umenichekesha Wewe Ommy 😂, wawe wetu waki swahili ndo Walivyo.

  • @salomewandya7257

    @salomewandya7257

    Жыл бұрын

    Ata mimi nimecheka saana🤣🤣🤣

  • @nellymatalanga5033
    @nellymatalanga5033 Жыл бұрын

    Sad that most parents neglect their kids, and then when they make it in life , they want to come back n force themselves into their lives as if nothing happened in the name of "mzazi ni mzazi" if u cant support ,love or acknowledge your kid whn young don't come pretend to be supporting him whn he's made in life that is just greed

  • @mashakashobo2529
    @mashakashobo2529 Жыл бұрын

    hiyo story ya Baba jamani imenigusa basi tu

  • @jahadi5062
    @jahadi5062 Жыл бұрын

    Ommy🥰🥰

  • @sambasamlay
    @sambasamlay Жыл бұрын

    Sulut sana

  • @alikobrand
    @alikobrand Жыл бұрын

    Interviews ni biashara unavyo mzungumzia msanii kwa mafumbo unakosea

  • @witnessnyavili4788
    @witnessnyavili4788 Жыл бұрын

    😂😂😂😂😂my son

  • @isackmagita7938
    @isackmagita7938 Жыл бұрын

    Hiyo nyimbo ya kipindi chako naikubali sana alafu siijui jina wala msanii

  • @edwinmbugua7738

    @edwinmbugua7738

    Жыл бұрын

    Yeah by Marco Chali

  • @khadijamasoud7261
    @khadijamasoud7261 Жыл бұрын

    Haya mazinhira wengi tumepitia na nimependa hilo suala la bond ni kweli hadi unajikuta hata mkikaa saa nzima hamna cha kuzungumza kama mzazi na mtoto.

  • @fatmaabdallah7709
    @fatmaabdallah7709 Жыл бұрын

    Salama hivyo viti vya kurithi vinaonekana toka enzi za mababu😂

  • @elizabethandrew8533
    @elizabethandrew8533 Жыл бұрын

    Mbona swali umeuliza kinafki eti msanii anae tushika mkono uku unacheka

  • @asmassan
    @asmassan Жыл бұрын

    👋

  • @oyay2821
    @oyay2821 Жыл бұрын

    Hayo mambo ya Joho sasa sahau.

  • @ibrawalas834
    @ibrawalas834 Жыл бұрын

    Kwanini ukumuliza kusu urafiki wake na diamond

  • @abdulraufmohammedsalum6806
    @abdulraufmohammedsalum6806 Жыл бұрын

    Wa kwanz

  • @nooromar6233
    @nooromar6233 Жыл бұрын

    Sawa kama unapato nyengine so bora music acha maana Alhamdulilah mngu anakupa riziki yako, u concentrate na mambo mengine ambayo yatam furahisha mngu wako

  • @OnlyRuky
    @OnlyRuky Жыл бұрын

    Salama 🤩🤩🤩🤩

  • @kitonekantasha1687
    @kitonekantasha1687 Жыл бұрын

    Umetunyima bana. Nilitegemea vi comedi vya bwana dimpoz😂 but sio mbaya ameweka sawa kwenye vile anapatia wapi mtonyo. Na AM SURE wasanii wataaamka ili kujiwekeza sehem kujiingizia kipato zaidi.

  • @wanzakleruu8648

    @wanzakleruu8648

    Жыл бұрын

    Vyote hivyo kajibu bro. Kumbuka this is #Salamana en not others 🚮 f*ckn blaa blaa interviews🥴

  • @MamaLorenzo
    @MamaLorenzo Жыл бұрын

    Bonge ya interview 🙌

  • @deogratiusdaudi4975
    @deogratiusdaudi4975 Жыл бұрын

    Deo non iposiku Salam utanihoj naamin kabsa kam ipo ipo 2

  • @deogratiusdaudi4975

    @deogratiusdaudi4975

    Жыл бұрын

    Amin mungu yup kabsa

  • @masawemalick3964
    @masawemalick3964 Жыл бұрын

    Mswahil sio wa kumsikiliza hata kidogo

  • @mwanaidimuhindi6671
    @mwanaidimuhindi6671 Жыл бұрын

    Hapo kwenye mama Ila acha nikae kimya nipate baraka 😢

  • @directorimmah_vfx3043
    @directorimmah_vfx3043 Жыл бұрын

    Mbna ajaalizwa kuhus stev nyerere

  • @johnmwandu2116

    @johnmwandu2116

    Жыл бұрын

    Salama siyo mtu wa udaku

  • @julianamushi3392
    @julianamushi3392 Жыл бұрын

    Mbon hii intv imekimbizwa hivi jmniii

  • @kelvinjackson6667
    @kelvinjackson6667 Жыл бұрын

    😢😂😂

  • @getrudanorbert8738
    @getrudanorbert8738 Жыл бұрын

    Dada salama ivo viti jaman angalau uweke kamto kidogo wageni wasiumie makalio na uvipake rangi mbona vimeisha sana

  • @shakilaburhan9552
    @shakilaburhan9552 Жыл бұрын

    Wanasema pia anapumuliwa

  • @BIGBOSS-hl3bu
    @BIGBOSS-hl3bu Жыл бұрын

    Ommy anachosema nimeelewa kuwa Hana mapenzi makubwa na babake Kwa sababu ya mazingira ya kukaa mbali mbali,na nijambo la kawaida hata Mimi na wewe Kuna vitu unatakiwa umfanyie Mtoto ili baadae usipate tabu kumwaminisha kuwa Mimi ndio babako.

  • @terrychaupole9473

    @terrychaupole9473

    Жыл бұрын

    Sawa kigwegwe

  • @BIGBOSS-hl3bu

    @BIGBOSS-hl3bu

    Жыл бұрын

    Terry wangu🤓🤓🤓🤓🤓🤓 ♥️♥️♥️♥️♥️🙏🙏🙏🙏🙏🙏 nakupenda sana

  • @user-sp3gg7id8q
    @user-sp3gg7id8q Жыл бұрын

    Huyo mondi anatushika mkono? Hivi we salama wajuwa kama diamond ni mwizi wa views na subscribers feki? 😩 yeye mondi anajibostia views wamilioni 50,000000 wasanii wake anawabostia 20,000000 karibu kila video na ni times ya kuongea hizi issues za kuiba views maana zinakandamiza music wa tanzania.

  • @fathiafathia6324

    @fathiafathia6324

    Жыл бұрын

    mavi wewe nawe si ufake stupid

  • @mwikamwika4851

    @mwikamwika4851

    Жыл бұрын

    Sasa kama mondo anaiba na anafanikiwa kwanini wewe usiibe ufanikiwe? ACHA ujinga wewe. Roho mbaya Yako ni shida Kwa Maisha Yako.

  • @user-sp3gg7id8q

    @user-sp3gg7id8q

    Жыл бұрын

    @@mwikamwika4851 mwenye roho mbaya sio mimi wala wewe ni huyo diamond platnumz anaeichiti system na kupokonya opportunity wasanii wa kitanzania, halafu nyinyi munaosema nunueni nanyie ! Are you serious? mimi, wewe na kila mtu including huyo mondi tunajua wasanii wetu ni maskini wengine hata pesa za kushoot video ni tabu alafu umwambie atoe pesa nyengine ya kuboost views ili nyimbo na video yake iyonekane imeenda mjini? Diamond ni disgraceful kwenye mziki wa tanzania hana hata huruma yeye anatoa nyimbo iwe nzuri or mbaya or kaimba kawaida yeye hajali yeye anchokijuwa ni kutoa tu video na kuboost views 50,000000 + then anakuja kutwambia imehit huko nje ! Nje ipi? Mbona kwenye shows anazoandaa mwenyewe mondi huko London na marekani anaparfome kwenye kitchen party kama harmonize?

  • @vincentmushi1247

    @vincentmushi1247

    Жыл бұрын

    Hapo unapokazia pa kununua views Muulize yule mla panya ,alievunja rekodi ya dunia wakati...anafahamika zaidi mtwara...ndio utajua maana ya kununua views...naoana mafanikio ya simba yanakupa malaria plus plus...na bado ndege inakuja

Келесі