Salama Na OMMY DIMPOZ SE6 EP31 | ELEGANT PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460
Ойын-сауық
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Kama kukiwa kuna mkutano wa Chama cha Watanashati hapa Africa na pengine Duniani basi Ommy Dimpoz anaweza kuwa mmoja wa viongozi wa juu kabisa wa Chama hiko na pengine anaweza kuwa hata Mwenyekiti. Hakuna swali juu ya utanashati wake kuanzia vivazi hadi nywele na hata kuongea. Anakumbuka utanashati wake ulianza toka alipokua mdogo sana, na wakati anakua si kama kila kitu alichokua anakitaka alikua anakipata ila alihakikisha vile vile vichache alivyokua navyo alihakikisha vinakua visaaafi na vinamkaa kweli kweli. Na tabia hiyo ya kujipenda na kuvaa vizuri ndo inamtambulisha Ommy Dimpoz kuwa ni mmoja wa wasanii wanaovaa vizuri zaidi hapa barani Afrika.
Omary amekua analelewa na Bibi yake baada ya Mama yake kufariki akiwa mdogo. Anakumbuka mapenzi ambayo amekua akimuonyesha toka zamani, ni kweli kama mtoto lazima utakua unamkumbuka Mama yako, ila Bibi yake alihakikisha anapata vile vyote ambavyo mtoto anakua anahitaji.
Mimi na Omary ni mtu na Rafiki yake kwahiyo mazungumzo haya zaidi yalikua ni kwaajili yako, uweze kumuelewa na kuifahamu milima na mabonde ambayo ameyapitia mpaka leo hii unamuona kasimama imara.
Kama mtoto siku zote unakua unataka kumjua Baba yako na haikua tofauti kwa Ommy pia. Shuleni watoto huitwa na wazazi wao, ukiwaona wenzako wanawaleta Baba zao na wewe hujawahi kumuona au pengine ni kwa nadra sana lazima likutie unyonge. Anakumbuka Mama yake alivyofariki na jinsi ambavyo Mzee wake alikata mawasiliano ki lazima kabisa, anakumbuka kwamba Mzee wake tayari alikua na familia nyengine lakini kama mtoto anaamini na yeye pia alikua na haki ya kupata mapenzi hata kidogo tu kutoka kwake.
Miaka ya hivi karibuni Mzee wake ameonekana kuutaka ukaribu nae kwa kasi kubwa sana ila kwa Omary huo umekua kama mtihani hivi, ana kinyongo nae bado na anaamini kwamba Mzee wake anataka kuwa karibu na yeye kwasababu tu ameona mwanae amekua maarufu na pengine anaonekana mambo yake mazuri. Hapo ndo panapo mtatiza yeye maana anaamini huo si upendo wa dhati, na hiyo ni sababu ya yeye kuendelea na maisha yake bila ya Baba yake. Pengine kuna siku itafika wawili hawa wataacha tofauti zao zipite na pengine watafahamiana vizuri na kuyafanya mahusiano kama Baba na mwana yastawi.
Pia tunafahamu kwamba miaka miwili na nusu au mitatu iliyopita Ommy aliumwa sana, na baadhi ya watu walithubutu kusema pengine hata kuimba inaweza isiwezekane tena ila kwa Rehma za Mwenyezi Mungu alimponya na kazi yake ya muziki anaendelea kuifanya kama kawaida. Nimekua nikispend nae muda mwingi kipindi ambacho tumekua tukifanya Bongo Star Search msimu wa kumi na mbili mimi na yeye, na kwasababu tumekua tukifahamiana kwa muda nimemuona kabisa hayuko 100% ila mimi na yeye tunamshkuru Mungu kwa hali alonayo sasa maana mitihani aliyopitia ni mingi sana. Haya maisha ambayo anaishi sasa ni zawadi kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na hatuna budi kumshukuru yeye kwa kumpa watu kwenye maisha yake ambao walihakikisha anapata matibabu yote ya hali ya juu ili maisha yake yaweze kurudi kama zamani.
Huku hilo hatukulizungumzia sana maana limeshaongelewa sana, ila tume ongea suala la ukuaji wake na mahusioano yake na familia. Urafiki wake na TID na jinsi walivyokutana. Urafiki wake na Ally Kiba, maisha yake ya shuleni na jinsi alivyokua. Urafiki wake na Diamond Platnumz na nini kilitokea kati yao. Muziki wa kizazi kipya na faida ambazo watu wana pata sasa na mahusiano yake na Chriatine ‘Seven’ Mosha na nini ambacho kimemfanya yeye afanye nae kazi. Pia tumezungumzia kutofahamiana kwake na meneja wa Diamond Platnumz Bwana Sallam Sharaff na Ommy emetuambia pia wawili hao maneno hasa yalianza kutoka wapi.
Yangu matumaini uta enjoy maongezi haya na utaokota mawili matatu pia ambayo yatakusaidia kwenye maisha yako ili mambo yazidi kuwa mswano.
Tafadhali Enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Пікірлер: 67
Siku moja na mimi nitakaa kwenye hicho kiti nikihojiwa💪🏾 Amen
@pamanyango8917
Жыл бұрын
Mungu ampe maisha marefu salama, lnshallah Siku yako itafikaa,
Nimemuelewa sana Ommy..,hatakama ni mimi watu wanisaidie hivyo kwenye ugonjwa ningewaoshaga na miguu nakuwalamba miguu mbele ya tv. Ndio waja waseme najipendekeza vizuri.
Bonge moja ya interview 😅😅 kuna nilipolia na kucheka sana. All the best Ommy. Salama Shikana pia arudiwe 😅
Much love from Kenya 🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪 ommy dimples napenda sannaaa, interview zako, sababu unajuakujieleza sanaa
Last part ya joho imenitoa machozi we people need hugs
Aisee Ommy mpumbavu sanaa😂😂😂😂😂😂😂 eti ngaaa my son
Umejua kunichekesha Ommy hahaha et my Son
Hongera sana Ommy Dimpoz,endelea kupiga kazi,na Mungu akuzidishie Zaidi..💥🔥🔥
ngaaaa my son 🤣🤣🤣🤣🤣
inapendeza saana aise
Namuomba Mungu sana usiku na mchana tena sana ili Mwanangu niwe nae karibu kwani kiukwel sijalelewa na wazazi hivyo najua chuki nilizokuwa nazo juu yao na naelewa maisha ni kama mate kuyatema juu hivyo nisipokuwa nae karibu lazima atanichukia tuu
Joho came at the right time to help this guy…only God know y joho and why Omy kwenye maisha hutokea mambo kama haya ,,,when you least espect if you truly beleive in God and you are a good person…it comes back!! PeriodT
Nimekuelewa sana Ommy, Sasa hapa Babako ndio chawa😅😀😀, Mungu hawasamehe mababa wote wapumbavu,Akiwemo mzazi mwenzangu.
@vivianjonathan1783
Жыл бұрын
🤣🤣🤣🤣🤣🤣
@vivianjonathan1783
Жыл бұрын
Kam wangu piah
Interview yangu pendwa nimeludia tena kuisikiliza mwka huu ilo life uliloisha ndio langu alafu wala sijali hata kama ajanitafuta ishi maisha yako ommy
My soooooon ! Mamae walah
Nganganga my soooon yuhuuuu
Hongera sana sister. Sema ushauri wangu naomba kama kuna session ya mashabiki wa hao unao wahoji kuuliza maswali kwao ingekuwa poa, kuna vitu tunajifunza sana na kupenda kujua vingne pia. Ahsante sana
hapo wenye my son hahahahhahaha🤣🤣🤣🤣
Kuna yakujifunza umu🙌✊
Big up home boy before nilikuwa nakuchukilia bishoo.frani.hivi lakini sasa nimekuelewa unajitambua sana (jiongeze kielimu u very wise, ,one love nigga
Hahaha nimecheka sana hapo kwenye myson 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Was nice interview 👌
Mm naona hii time ni ndogo sana
Ommy samehe na usahau mzee ni mzee tuu
🤣 Kwenye Story ya Mchuwa umenichekesha Wewe Ommy 😂, wawe wetu waki swahili ndo Walivyo.
@salomewandya7257
Жыл бұрын
Ata mimi nimecheka saana🤣🤣🤣
Sad that most parents neglect their kids, and then when they make it in life , they want to come back n force themselves into their lives as if nothing happened in the name of "mzazi ni mzazi" if u cant support ,love or acknowledge your kid whn young don't come pretend to be supporting him whn he's made in life that is just greed
hiyo story ya Baba jamani imenigusa basi tu
Ommy🥰🥰
Sulut sana
Interviews ni biashara unavyo mzungumzia msanii kwa mafumbo unakosea
😂😂😂😂😂my son
Hiyo nyimbo ya kipindi chako naikubali sana alafu siijui jina wala msanii
@edwinmbugua7738
Жыл бұрын
Yeah by Marco Chali
Haya mazinhira wengi tumepitia na nimependa hilo suala la bond ni kweli hadi unajikuta hata mkikaa saa nzima hamna cha kuzungumza kama mzazi na mtoto.
Salama hivyo viti vya kurithi vinaonekana toka enzi za mababu😂
Mbona swali umeuliza kinafki eti msanii anae tushika mkono uku unacheka
👋
Hayo mambo ya Joho sasa sahau.
Kwanini ukumuliza kusu urafiki wake na diamond
Wa kwanz
Sawa kama unapato nyengine so bora music acha maana Alhamdulilah mngu anakupa riziki yako, u concentrate na mambo mengine ambayo yatam furahisha mngu wako
Salama 🤩🤩🤩🤩
Umetunyima bana. Nilitegemea vi comedi vya bwana dimpoz😂 but sio mbaya ameweka sawa kwenye vile anapatia wapi mtonyo. Na AM SURE wasanii wataaamka ili kujiwekeza sehem kujiingizia kipato zaidi.
@wanzakleruu8648
Жыл бұрын
Vyote hivyo kajibu bro. Kumbuka this is #Salamana en not others 🚮 f*ckn blaa blaa interviews🥴
Bonge ya interview 🙌
Deo non iposiku Salam utanihoj naamin kabsa kam ipo ipo 2
@deogratiusdaudi4975
Жыл бұрын
Amin mungu yup kabsa
Mswahil sio wa kumsikiliza hata kidogo
Hapo kwenye mama Ila acha nikae kimya nipate baraka 😢
Mbna ajaalizwa kuhus stev nyerere
@johnmwandu2116
Жыл бұрын
Salama siyo mtu wa udaku
Mbon hii intv imekimbizwa hivi jmniii
😢😂😂
Dada salama ivo viti jaman angalau uweke kamto kidogo wageni wasiumie makalio na uvipake rangi mbona vimeisha sana
Wanasema pia anapumuliwa
Ommy anachosema nimeelewa kuwa Hana mapenzi makubwa na babake Kwa sababu ya mazingira ya kukaa mbali mbali,na nijambo la kawaida hata Mimi na wewe Kuna vitu unatakiwa umfanyie Mtoto ili baadae usipate tabu kumwaminisha kuwa Mimi ndio babako.
@terrychaupole9473
Жыл бұрын
Sawa kigwegwe
@BIGBOSS-hl3bu
Жыл бұрын
Terry wangu🤓🤓🤓🤓🤓🤓 ♥️♥️♥️♥️♥️🙏🙏🙏🙏🙏🙏 nakupenda sana
Huyo mondi anatushika mkono? Hivi we salama wajuwa kama diamond ni mwizi wa views na subscribers feki? 😩 yeye mondi anajibostia views wamilioni 50,000000 wasanii wake anawabostia 20,000000 karibu kila video na ni times ya kuongea hizi issues za kuiba views maana zinakandamiza music wa tanzania.
@fathiafathia6324
Жыл бұрын
mavi wewe nawe si ufake stupid
@mwikamwika4851
Жыл бұрын
Sasa kama mondo anaiba na anafanikiwa kwanini wewe usiibe ufanikiwe? ACHA ujinga wewe. Roho mbaya Yako ni shida Kwa Maisha Yako.
@user-sp3gg7id8q
Жыл бұрын
@@mwikamwika4851 mwenye roho mbaya sio mimi wala wewe ni huyo diamond platnumz anaeichiti system na kupokonya opportunity wasanii wa kitanzania, halafu nyinyi munaosema nunueni nanyie ! Are you serious? mimi, wewe na kila mtu including huyo mondi tunajua wasanii wetu ni maskini wengine hata pesa za kushoot video ni tabu alafu umwambie atoe pesa nyengine ya kuboost views ili nyimbo na video yake iyonekane imeenda mjini? Diamond ni disgraceful kwenye mziki wa tanzania hana hata huruma yeye anatoa nyimbo iwe nzuri or mbaya or kaimba kawaida yeye hajali yeye anchokijuwa ni kutoa tu video na kuboost views 50,000000 + then anakuja kutwambia imehit huko nje ! Nje ipi? Mbona kwenye shows anazoandaa mwenyewe mondi huko London na marekani anaparfome kwenye kitchen party kama harmonize?
@vincentmushi1247
Жыл бұрын
Hapo unapokazia pa kununua views Muulize yule mla panya ,alievunja rekodi ya dunia wakati...anafahamika zaidi mtwara...ndio utajua maana ya kununua views...naoana mafanikio ya simba yanakupa malaria plus plus...na bado ndege inakuja