Salama Na Master Jay SE6 EP21 | NDUGU MHANDISI PART 1| SendTip MPESA LIPA NO 5578460
Ойын-сауық
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
NDUGU MHANDISI
Joachim Msafiri Kimaryo ni Kaka yangu na rafiki yangu wa kweli kabisa, mimi na yeye tukiwa pamoja vicheko huwa haviakauki maana tumekutana sote tunapenda sana kucheka na tunapenda utani. Humtania sana kuhusu karibia kila kitu, kampani yake ni moja ya kampani ambazo nazipenda sana. Tunaongelea kuhusu kila kitu mimi na yeye, iwe kuhusu binti yake Nuru kukua na kuwa na boyfriend, au kipaji na muonekano wa baadhi ya wana muziki wa hapa nyumbani, iwe kuhusu Zanzibar na jinsi anavyopata mafua akiwa kule au jokes za ndani kati yetu ambazo mara nyingi zinakua na lugha za kikubwa, yote hayo huongea nae na hucheka sana.
Si mtu ambaye tunakutana kila siku au tunaongea kila siku Ila pale tunapoongea huongea na tunapokutana basi ndo tumekutana. Nna heshima nyingi sana kwake, kwa jinsi ambavyo ameweza ku maintain status yake ila kubwa zaidi ni jinsi ambavyo aliweza kumzidi Marehemu Mzee wake maarifa ki aina na akaweza kufuata roho yake ilichokua inataka na akafanya mziki. Mziki ambao hapa wewe unavyosoma unajua umesaidia kutoa ajira na kubadilisha maisha ya watu wangapi. Na unajua kama Joachim Marunda Msafiri Kimaryo ni mmoja wa waasisi hao. Baba yake alilipia ada ya mwanaye kwenda kusoma nchini Uingereza ili aje apate kazi Tanesco ambapo yeye alikua akifanya kazi, ndo maana alimchagulia mpaka cha kusoma, ila Jay alipifika Uingereza gea ilibadilikia hewani INGAWA alimaliza kwa uzuri tu ile elimu ambayo Mzee wake alikua anataka aipate.
Baada ya kurudi nyumbani sasa, instead ya kwenda kuanza kazi Tanesco ambako nafasi yake ilikua tayari, Jay alitaka kuwa producer na aliweza kufanya hivyo ingawa Marehemu Mzee wake hakupenda, hili ni moja ya maswali nilimuuliza Kaka yangu, kama Mzee wake alishawahi kuyaona hata kidogo mafanikio yake au alishawahi kuskiliza kazi ambazo ni nzuri kijana wake alishawahi kufanya na ambazo zinaishi mpaka leo hii.
Master ametoka kwenye familia za kishua tu, Mama yake Scholastica Sylvan Kimaryo ni mmoja kati ya Ma Coach wazuri tu wa masuala ya kibinadamu na jamii, ashawahi kufanya kazi kwenye mashirika makubwa tu ya Kimataifa na mpaka leo mchango wake bado unatumika kwenye taasisi mbalimbali ili kuweza kuwaendeleza vijana katika nyanja mbalimbali za uongozi na maadili bora. Na Dadake yake Catherine naye pia yuko vizuri tu kwenye masuala ya u coach kama ambavyo Mama yake naye anafanya. So familia iko vyema na mambo yanaenda vizuri tu.
Master ni shule inayotembea, anajua vitu vingi kuhusu karibia kila kitu, ni rafiki mzuri na mtu ambaye mziki huu wa kwetu ameupigania tu sana na pengine wakati wa kujilipa au kulipwa ndo huu umefika. Kwenye maongezi yetu haya tuliongelea kuhusu maisha yake binafsi kama ilivyo ada, kuhusu familia yake na watoto wake lakini pia kuhusu Marehemu Mzee wake na Mama yake na studio yake, miaka ya nyuma wakati wanaanza na mahusiano yake na maproducer wa zamani haswa P-Funk ambaye pia alikua BEST MAN kwenye harusi yake.
Master pia nimeongea naye kuhusu mustakabali wa Bongo Flava, hapa tulipo na huko tuendako, na majibu yake ni kitu ambacho ungependa kuskiliza sana.
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Пікірлер: 90
Nimeisubiri sana hii...MastaJay ana story nyingi sana za zamani. Likes zangu kama commentator wa kwanza😎😎🍹
Tanzania raha sana mzanzibar mchaga wanacheka na kufurahi kama wamezaliwa pamoja
Watu wa wili napenda kuskiliza tanzania wanao towaga maoni ya akili bila kumficha mtu kwa lengo yakumbadilisha awe bora. Big up Salam and Master j
Dread locks ni fashion Rasta ndio dini...not the other way round sir.
hapo patamu na ukimleta na chid benz itakuwa mpango mzima
Yaaniii Bora kwasasa kusikiliza wakenya na bongo Flava ya zamani
Mungu ndio mtoaji kuhusu watoto nakubali mtoto wakike
Hii kazi ya kupanda Gari la njano ilinishinda😭
Hakuna kitu kigumu kama iyo issue ya watoto baada ya kutengana 😔🤦🏽♂️
Am ur big fun salama frm Nairobi.......salama na Otile Brown ikam thru itakua 🔥🔥
Salama yuko mrembo san🎉❤
BEST OF THE BEST !! MASTER MASTER TU.✊
Kipindi kizuri sana.turetey na harmonize
Ningependa kiswahili kingetumika kwa ability kubwa
@kareemmohammed1521
6 ай бұрын
We mwenyw umetumia ngeli 😂😂
Bongo Flava ivi wasani wanaimba matusi na Kiki uchawa ukahaba yaanii industry ya bongo entertainment iko vibaya. Amna wa producer wasomi wala wa director wasomi. Akuna wa sound engineer.
yani salama nakupenda sana mdogo wangu natamani sikumoja nikuone
Salama Boss Lady💪
jamani salama,,,,,uwe unawazuia kiingereza
Mzee Kijana...Maneno kintu Sana🔥🙏🏾🤞🏾❤️🇰🇪❤️.
@julianakimaro5474
2 жыл бұрын
Nimewapendaaa dah eti the eyeeess
straight from the 254 with mob love mnakaa biee
Swala la muda tuu
Salama naomba utuletee KALA JEREMIAH
Nakukubali sana Master J
Duuuh master J 🙌🙌🙌 napenda SN interview zako nikiona tuuu interview yko nafungua kaka
True master jay….joliee dada mkali yulee sema showw show za wasanii weng zimemuweka pemben
Kweli kbs watoto wakike wanapenda sana baba zao
Nasaubiri SALAMA NA MCHOMVU, SALAMA NA MILLARD AYO na SALAMA NA MWIJAKU
Master 💃Jay🤸♂️🤸♀️🤸♂️ 💛
Master J u said it all....big mind
Haya majama mi nayapendaga sana!
Tuletee Fatma Abdulhabib Fereji
Hio ni kweli wanaume tunakufa kwa kuficha mengi moyoni
Nilikua Na Isubiri sana salama na jay
24:00 🔥
Kiingereza kingi sana
Sasa si muongee kiswahili jamani
Great interview salama from zanzibar
Shabiki wa salama nampenda look yak
🔥🔥
Lete master J hio list ninaisubiri kwa hamu
🔥🔥🔥💯💟❤️
Kingerez kingi
Ukweli mchungu sana huu kauongea
Very honest
Good
Salamaaaaa
Machale wawili wamekutana pia ila akili mingi hao 😂
@evelinemsaki2057
2 жыл бұрын
Sanaa salama amembadikisha master si amekubali kuwa yeye siyo mangi tena
M nikimuonaga tu master nafungua link madini mengi sana huyujamaa
Master Jay
Asante Sana master j wanajifanya muziki unawapa maisha kumbe malaya
❤️❤️❤️❤️
ndo maana munauwana sana kwa tabia hii wachaga mn munaficha mingi at the end munauwa wazee au familia na watu wa karibu kwa vile munabeba mizigo moyoni
👍
tuleteee na watu wa futbal
Master kama ulikua kwenye mawazo ya fikra zangu, wahuni wengi wana tupotosha sana hata show moja mwaka mzima hana alafu anabang nakujitamba mziki umempa
Master umependeza saaana bonge la dress code
Salama tuleteeni na madebe lidai
BADO WEMA 😥NA NASB
Kama kizungu kinazidi tuwekeeni subtites
Salama Leo umeamua kutuonesha hayo mapaja ya kuku😊
@evelinemsaki2057
2 жыл бұрын
Salama was kishua wewee
Nahisi itakua kwa wanaume umemzungumzie ommy dimpoz kua mwenzetu sio riziki 😂😂😂
@khadijahali4837
Жыл бұрын
🤣🤣km kwl
Br ni mkweli kabisa
look like he was high
Salama mlete Mume wako hapo.
Salama Y black every day
@officialmimi269
2 жыл бұрын
I think it looks good on her😊
Unifungua master j, these guys are kidding me
🇹🇿🇹🇿🇹🇿✌
tunapenda kujua na kujifunza lakni kiingereza kingi ananikera aisee
@rommelmauma5872
2 жыл бұрын
Kiswahili, Kiswahili; itapendeza!
@ebenezerkaaya7345
2 жыл бұрын
Acha kukerwa na maisha ya watu aloo, jifunze na ww
Naomba mjomba aletwe kwenye kipindi,kwasababu mrisho mpoto anamambo mengi sana yakuongeya alafu muhimu kwelikweli,toka nimeanza kufuatiliya interview za mjomba hajawahi kupewa nafasi ya kutowa aliyo nayo moyoni nahiyo ni hasara !,kwamimi kama kio chajamii basi mjomba ni zaidi ya kio . Nadhani ombi langu litafanyiwa kazi.
Jamaniii Kiswahili hii kitu hatuelewo
Wachaga tunalilia hela tu mekuuu
@evelinemsaki2057
2 жыл бұрын
Sasa huo ni ujinga mnakufa na majanga moyoni
Sasa salama kila kipindi unavaa nguo nyeusi hauna nguo nyengine
@evelinemsaki2057
2 жыл бұрын
Wewe salama analipua mavazi hatar huyo ni tajiri na msomi ety usimchukulie was kawaida tajiri huyo
BROO YOU LIKE ME SORRY BROO.
Dred na rasta Tofauti ni lugha au ni aina?
@khadijahali4837
Жыл бұрын
Dredi ni zauzi na rasta hz km nywele
@emmamatemu8225
Жыл бұрын
@@khadijahali4837 na zile wanazosuka akina dada zinaitwaje
@khadijahali4837
Жыл бұрын
@@emmamatemu8225 zote ndo hz hz
WachGue moja nigg