Salama Na Master Jay SE6 EP21 | NDUGU MHANDISI PART 1| SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Ойын-сауық

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
NDUGU MHANDISI
Joachim Msafiri Kimaryo ni Kaka yangu na rafiki yangu wa kweli kabisa, mimi na yeye tukiwa pamoja vicheko huwa haviakauki maana tumekutana sote tunapenda sana kucheka na tunapenda utani. Humtania sana kuhusu karibia kila kitu, kampani yake ni moja ya kampani ambazo nazipenda sana. Tunaongelea kuhusu kila kitu mimi na yeye, iwe kuhusu binti yake Nuru kukua na kuwa na boyfriend, au kipaji na muonekano wa baadhi ya wana muziki wa hapa nyumbani, iwe kuhusu Zanzibar na jinsi anavyopata mafua akiwa kule au jokes za ndani kati yetu ambazo mara nyingi zinakua na lugha za kikubwa, yote hayo huongea nae na hucheka sana.
Si mtu ambaye tunakutana kila siku au tunaongea kila siku Ila pale tunapoongea huongea na tunapokutana basi ndo tumekutana. Nna heshima nyingi sana kwake, kwa jinsi ambavyo ameweza ku maintain status yake ila kubwa zaidi ni jinsi ambavyo aliweza kumzidi Marehemu Mzee wake maarifa ki aina na akaweza kufuata roho yake ilichokua inataka na akafanya mziki. Mziki ambao hapa wewe unavyosoma unajua umesaidia kutoa ajira na kubadilisha maisha ya watu wangapi. Na unajua kama Joachim Marunda Msafiri Kimaryo ni mmoja wa waasisi hao. Baba yake alilipia ada ya mwanaye kwenda kusoma nchini Uingereza ili aje apate kazi Tanesco ambapo yeye alikua akifanya kazi, ndo maana alimchagulia mpaka cha kusoma, ila Jay alipifika Uingereza gea ilibadilikia hewani INGAWA alimaliza kwa uzuri tu ile elimu ambayo Mzee wake alikua anataka aipate.
Baada ya kurudi nyumbani sasa, instead ya kwenda kuanza kazi Tanesco ambako nafasi yake ilikua tayari, Jay alitaka kuwa producer na aliweza kufanya hivyo ingawa Marehemu Mzee wake hakupenda, hili ni moja ya maswali nilimuuliza Kaka yangu, kama Mzee wake alishawahi kuyaona hata kidogo mafanikio yake au alishawahi kuskiliza kazi ambazo ni nzuri kijana wake alishawahi kufanya na ambazo zinaishi mpaka leo hii.
Master ametoka kwenye familia za kishua tu, Mama yake Scholastica Sylvan Kimaryo ni mmoja kati ya Ma Coach wazuri tu wa masuala ya kibinadamu na jamii, ashawahi kufanya kazi kwenye mashirika makubwa tu ya Kimataifa na mpaka leo mchango wake bado unatumika kwenye taasisi mbalimbali ili kuweza kuwaendeleza vijana katika nyanja mbalimbali za uongozi na maadili bora. Na Dadake yake Catherine naye pia yuko vizuri tu kwenye masuala ya u coach kama ambavyo Mama yake naye anafanya. So familia iko vyema na mambo yanaenda vizuri tu.
Master ni shule inayotembea, anajua vitu vingi kuhusu karibia kila kitu, ni rafiki mzuri na mtu ambaye mziki huu wa kwetu ameupigania tu sana na pengine wakati wa kujilipa au kulipwa ndo huu umefika. Kwenye maongezi yetu haya tuliongelea kuhusu maisha yake binafsi kama ilivyo ada, kuhusu familia yake na watoto wake lakini pia kuhusu Marehemu Mzee wake na Mama yake na studio yake, miaka ya nyuma wakati wanaanza na mahusiano yake na maproducer wa zamani haswa P-Funk ambaye pia alikua BEST MAN kwenye harusi yake.
Master pia nimeongea naye kuhusu mustakabali wa Bongo Flava, hapa tulipo na huko tuendako, na majibu yake ni kitu ambacho ungependa kuskiliza sana.
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Пікірлер: 90

  • @CoachHafidh
    @CoachHafidh2 жыл бұрын

    Nimeisubiri sana hii...MastaJay ana story nyingi sana za zamani. Likes zangu kama commentator wa kwanza😎😎🍹

  • @franklinassey6600
    @franklinassey66002 жыл бұрын

    Tanzania raha sana mzanzibar mchaga wanacheka na kufurahi kama wamezaliwa pamoja

  • @soumayarubuka6900
    @soumayarubuka69002 жыл бұрын

    Watu wa wili napenda kuskiliza tanzania wanao towaga maoni ya akili bila kumficha mtu kwa lengo yakumbadilisha awe bora. Big up Salam and Master j

  • @millymack1370
    @millymack13702 жыл бұрын

    Dread locks ni fashion Rasta ndio dini...not the other way round sir.

  • @mbarakasaidi8243
    @mbarakasaidi82432 жыл бұрын

    hapo patamu na ukimleta na chid benz itakuwa mpango mzima

  • @maishaforreal7798
    @maishaforreal77982 жыл бұрын

    Yaaniii Bora kwasasa kusikiliza wakenya na bongo Flava ya zamani

  • @suleimansaid2633
    @suleimansaid26332 жыл бұрын

    Mungu ndio mtoaji kuhusu watoto nakubali mtoto wakike

  • @jasmineedamu6089
    @jasmineedamu60892 жыл бұрын

    Hii kazi ya kupanda Gari la njano ilinishinda😭

  • @chrisbonfils4024
    @chrisbonfils40242 жыл бұрын

    Hakuna kitu kigumu kama iyo issue ya watoto baada ya kutengana 😔🤦🏽‍♂️

  • @isaacmweni164
    @isaacmweni1642 жыл бұрын

    Am ur big fun salama frm Nairobi.......salama na Otile Brown ikam thru itakua 🔥🔥

  • @BerthaModest
    @BerthaModest5 ай бұрын

    Salama yuko mrembo san🎉❤

  • @Djso26
    @Djso262 жыл бұрын

    BEST OF THE BEST !! MASTER MASTER TU.✊

  • @danielnderagakura8174
    @danielnderagakura81742 жыл бұрын

    Kipindi kizuri sana.turetey na harmonize

  • @georgechande8140
    @georgechande81402 жыл бұрын

    Ningependa kiswahili kingetumika kwa ability kubwa

  • @kareemmohammed1521

    @kareemmohammed1521

    6 ай бұрын

    We mwenyw umetumia ngeli 😂😂

  • @maishaforreal7798
    @maishaforreal77982 жыл бұрын

    Bongo Flava ivi wasani wanaimba matusi na Kiki uchawa ukahaba yaanii industry ya bongo entertainment iko vibaya. Amna wa producer wasomi wala wa director wasomi. Akuna wa sound engineer.

  • @mariamkitwana6148
    @mariamkitwana61482 жыл бұрын

    yani salama nakupenda sana mdogo wangu natamani sikumoja nikuone

  • @chikotosammy3891
    @chikotosammy38912 жыл бұрын

    Salama Boss Lady💪

  • @danieljoseph4725
    @danieljoseph47252 жыл бұрын

    jamani salama,,,,,uwe unawazuia kiingereza

  • @bish_daddiyao
    @bish_daddiyao2 жыл бұрын

    Mzee Kijana...Maneno kintu Sana🔥🙏🏾🤞🏾❤️🇰🇪❤️.

  • @julianakimaro5474

    @julianakimaro5474

    2 жыл бұрын

    Nimewapendaaa dah eti the eyeeess

  • @mosesmuithi5693
    @mosesmuithi56932 жыл бұрын

    straight from the 254 with mob love mnakaa biee

  • @Boaz22
    @Boaz22 Жыл бұрын

    Swala la muda tuu

  • @Epicmarkmedia
    @Epicmarkmedia2 жыл бұрын

    Salama naomba utuletee KALA JEREMIAH

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan24992 жыл бұрын

    Nakukubali sana Master J

  • @faustinombilinyi9809
    @faustinombilinyi98092 жыл бұрын

    Duuuh master J 🙌🙌🙌 napenda SN interview zako nikiona tuuu interview yko nafungua kaka

  • @kisamokachema3064
    @kisamokachema30642 жыл бұрын

    True master jay….joliee dada mkali yulee sema showw show za wasanii weng zimemuweka pemben

  • @siasia5469
    @siasia54692 жыл бұрын

    Kweli kbs watoto wakike wanapenda sana baba zao

  • @mrfashion1687
    @mrfashion16872 жыл бұрын

    Nasaubiri SALAMA NA MCHOMVU, SALAMA NA MILLARD AYO na SALAMA NA MWIJAKU

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum72792 жыл бұрын

    Master 💃Jay🤸‍♂️🤸‍♀️🤸‍♂️ 💛

  • @joshuamacha8751
    @joshuamacha87515 ай бұрын

    Master J u said it all....big mind

  • @drtobias_
    @drtobias_2 жыл бұрын

    Haya majama mi nayapendaga sana!

  • @mkuuhapingwi
    @mkuuhapingwi5 ай бұрын

    Tuletee Fatma Abdulhabib Fereji

  • @franklinassey6600
    @franklinassey66002 жыл бұрын

    Hio ni kweli wanaume tunakufa kwa kuficha mengi moyoni

  • @kapona927
    @kapona9272 жыл бұрын

    Nilikua Na Isubiri sana salama na jay

  • @user-xf1xq3ky2w
    @user-xf1xq3ky2w5 ай бұрын

    24:00 🔥

  • @GodfreyWilliam-pb3wh
    @GodfreyWilliam-pb3wh Жыл бұрын

    Kiingereza kingi sana

  • @AmCool_
    @AmCool_2 жыл бұрын

    Sasa si muongee kiswahili jamani

  • @Hassanchora
    @Hassanchora Жыл бұрын

    Great interview salama from zanzibar

  • @fernandokezumukama1537
    @fernandokezumukama15372 жыл бұрын

    Shabiki wa salama nampenda look yak

  • @khadijahali4837
    @khadijahali4837 Жыл бұрын

    🔥🔥

  • @thatkidluffy6390
    @thatkidluffy63902 жыл бұрын

    Lete master J hio list ninaisubiri kwa hamu

  • @lufundishajigoro4323
    @lufundishajigoro43232 жыл бұрын

    🔥🔥🔥💯💟❤️

  • @hassanhajj6804
    @hassanhajj6804 Жыл бұрын

    Kingerez kingi

  • @athmanjuma3768
    @athmanjuma37682 жыл бұрын

    Ukweli mchungu sana huu kauongea

  • @salimdibundile4872
    @salimdibundile4872 Жыл бұрын

    Very honest

  • @honestgroup2116
    @honestgroup21162 жыл бұрын

    Good

  • @kazkaz1943
    @kazkaz19432 жыл бұрын

    Salamaaaaa

  • @sumayasumaya6455
    @sumayasumaya64552 жыл бұрын

    Machale wawili wamekutana pia ila akili mingi hao 😂

  • @evelinemsaki2057

    @evelinemsaki2057

    2 жыл бұрын

    Sanaa salama amembadikisha master si amekubali kuwa yeye siyo mangi tena

  • @wedream7506
    @wedream75062 жыл бұрын

    M nikimuonaga tu master nafungua link madini mengi sana huyujamaa

  • @israelmkaka2807
    @israelmkaka28072 жыл бұрын

    Master Jay

  • @evelinemsaki2057
    @evelinemsaki20572 жыл бұрын

    Asante Sana master j wanajifanya muziki unawapa maisha kumbe malaya

  • @naomiprincess4169
    @naomiprincess41692 жыл бұрын

    ❤️❤️❤️❤️

  • @zuleikhakhamis3303
    @zuleikhakhamis33032 жыл бұрын

    ndo maana munauwana sana kwa tabia hii wachaga mn munaficha mingi at the end munauwa wazee au familia na watu wa karibu kwa vile munabeba mizigo moyoni

  • @rockyvlogs2214
    @rockyvlogs22142 жыл бұрын

    👍

  • @meky9404
    @meky94042 жыл бұрын

    tuleteee na watu wa futbal

  • @mathewdyzymaleyafrica9128
    @mathewdyzymaleyafrica91282 жыл бұрын

    Master kama ulikua kwenye mawazo ya fikra zangu, wahuni wengi wana tupotosha sana hata show moja mwaka mzima hana alafu anabang nakujitamba mziki umempa

  • @lufundishajigoro4323
    @lufundishajigoro43232 жыл бұрын

    Master umependeza saaana bonge la dress code

  • @mikhitaryankombo9604
    @mikhitaryankombo96042 жыл бұрын

    Salama tuleteeni na madebe lidai

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum72792 жыл бұрын

    BADO WEMA 😥NA NASB

  • @mtukwaomedia
    @mtukwaomedia Жыл бұрын

    Kama kizungu kinazidi tuwekeeni subtites

  • @jasmineedamu6089
    @jasmineedamu60892 жыл бұрын

    Salama Leo umeamua kutuonesha hayo mapaja ya kuku😊

  • @evelinemsaki2057

    @evelinemsaki2057

    2 жыл бұрын

    Salama was kishua wewee

  • @Masaki_001
    @Masaki_0012 жыл бұрын

    Nahisi itakua kwa wanaume umemzungumzie ommy dimpoz kua mwenzetu sio riziki 😂😂😂

  • @khadijahali4837

    @khadijahali4837

    Жыл бұрын

    🤣🤣km kwl

  • @juvenalxavier6477
    @juvenalxavier64772 жыл бұрын

    Br ni mkweli kabisa

  • @farajilalah8379
    @farajilalah83792 жыл бұрын

    look like he was high

  • @noelbernard6390
    @noelbernard63902 жыл бұрын

    Salama mlete Mume wako hapo.

  • @wariobavedastus3157
    @wariobavedastus31572 жыл бұрын

    Salama Y black every day

  • @officialmimi269

    @officialmimi269

    2 жыл бұрын

    I think it looks good on her😊

  • @erastomwakalukwa3946
    @erastomwakalukwa3946 Жыл бұрын

    Unifungua master j, these guys are kidding me

  • @King_Of_Everything
    @King_Of_Everything2 жыл бұрын

    🇹🇿🇹🇿🇹🇿✌

  • @danieljoseph4725
    @danieljoseph47252 жыл бұрын

    tunapenda kujua na kujifunza lakni kiingereza kingi ananikera aisee

  • @rommelmauma5872

    @rommelmauma5872

    2 жыл бұрын

    Kiswahili, Kiswahili; itapendeza!

  • @ebenezerkaaya7345

    @ebenezerkaaya7345

    2 жыл бұрын

    Acha kukerwa na maisha ya watu aloo, jifunze na ww

  • @bitegemurisho54
    @bitegemurisho542 жыл бұрын

    Naomba mjomba aletwe kwenye kipindi,kwasababu mrisho mpoto anamambo mengi sana yakuongeya alafu muhimu kwelikweli,toka nimeanza kufuatiliya interview za mjomba hajawahi kupewa nafasi ya kutowa aliyo nayo moyoni nahiyo ni hasara !,kwamimi kama kio chajamii basi mjomba ni zaidi ya kio . Nadhani ombi langu litafanyiwa kazi.

  • @sabraridhwan2858
    @sabraridhwan28582 жыл бұрын

    Jamaniii Kiswahili hii kitu hatuelewo

  • @kilimonachangamotozake6652
    @kilimonachangamotozake66522 жыл бұрын

    Wachaga tunalilia hela tu mekuuu

  • @evelinemsaki2057

    @evelinemsaki2057

    2 жыл бұрын

    Sasa huo ni ujinga mnakufa na majanga moyoni

  • @sabraridhwan2858
    @sabraridhwan28582 жыл бұрын

    Sasa salama kila kipindi unavaa nguo nyeusi hauna nguo nyengine

  • @evelinemsaki2057

    @evelinemsaki2057

    2 жыл бұрын

    Wewe salama analipua mavazi hatar huyo ni tajiri na msomi ety usimchukulie was kawaida tajiri huyo

  • @ismaildavid6970
    @ismaildavid69702 жыл бұрын

    BROO YOU LIKE ME SORRY BROO.

  • @emmamatemu8225
    @emmamatemu82252 жыл бұрын

    Dred na rasta Tofauti ni lugha au ni aina?

  • @khadijahali4837

    @khadijahali4837

    Жыл бұрын

    Dredi ni zauzi na rasta hz km nywele

  • @emmamatemu8225

    @emmamatemu8225

    Жыл бұрын

    @@khadijahali4837 na zile wanazosuka akina dada zinaitwaje

  • @khadijahali4837

    @khadijahali4837

    Жыл бұрын

    @@emmamatemu8225 zote ndo hz hz

  • @nwntz
    @nwntz Жыл бұрын

    WachGue moja nigg

Келесі