Salama Na MASOUD KIPANYA SE6 EP60 | HERI KUFA MACHO… PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Ойын-сауық

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Habibi Masoud Kipanya ni Ally Masoud Nyomwa ambaye ni LEGEND. Kwa mujibu wake alizaliwa huku kakunja ngumi na dhana yake ni kwamba alizaliwa ili awe bondia! Kwa anacho kifanya na ambacho amekua akikifanya tena kwa ufasaha kwa miaka nenda miaka rudi bila ya shaka ni UBONDIA. Hakuna ambaye atabisha juu ya hilo. Amekua akipigania mambo tele na kuyasemea mengi pamoja na kuchekesha na kuelimisha kupitia kalamu yake. Kwa mujibu wake yeye ni mbobevu katika taaluma ya kupuuza na kuchukulia mambo poa kwa kipindi sasa. Lakini pia anaamini yeye ni MTATA. Tukienda mbele na kurudi nyuma, hapo kwenye UTATA hakuna ambaye anaweza kumbishia, hasa kwa wale ambao kalamu yake imewanyoosha kwa kiasi kikubwa.
Mimi na yeye tulikutana kwa mara ya kwanza takriban miaka kumi na tisa iliyopita, wakati huo mimi mbichi hasa na yeye akiwa kashajielewa na chemchem yake ya kipato tayari ilikua inatoa neema. Mimi nilikua ndo kwanza naanza kazi ya kujishikiza pale Times FM kipindi hiko bado ilikua kule Kamata. Masoud alikua analichorea gazeti la Majira ambalo lilikua liko kwenye mwamvuli mmoja na Radio ambayo nami nilikua nimejishikiza baada tu ya kumaliza skuli. Urafiki wetu ulikuja naturally tu maana sote tunapenda kucheka. Kupitia Zuhura Yunus na Binti mwengine wa kuitwa Rahma ndo mimi naye tulifahamiana. Wakati huo yeye alikua na gari kwahiyo lifti za hapa na pale zilikua hazikauki. Pia tulikua tunaitumia gari yake kama sehemu ya ku chill na kuskiliza muziki kwenye parking za Times FM.
Huwezi kukaa kwenye tasnia moja kwa muda mrefu kama wewe si hodari na mwenye kujielewa. Moja ya vitu ambavyo naviusudu kutoka kwake ni uelewa wake wa mambo tele wa tele, IQ yake ni ya juu sana na jinsi ambavyo ana reason ndo huwa anamaliza kabisa, kama binadamu wakati mwengine ni bora kukubaliana kuto kukubaliana na kwakwe yeye wakati mwengine jinsi anavyo wachora baadhi ya matukio na watu huwa haviishii kuzuri lakini hiyo haikuwahi kuwa sababu ya yeye kuacha kufanya ambacho anakifanya na ambacho amekua akikifanya kwa muda sasa. Uelewa wake kwenye mambo ambayo yanaendelea, uwezo wake wa kuona mbali na kuweka sanaa yake hiyo kwenye karatasi kisha kutuachia sisi tung’amue maana yake kwa kweli ni kipaji cha kipekee ya sana. Mmoja anatakiwa akae tu mbali na ku admire akifanyacho na hiko ndo ambacho mimi nimeamua kufanya.
Nilikua nataka anielezee maana halisi ya baadhi ya michoro yake ambayo iliacha gumzo kwa muda mrefu lakini kwa sababu ambazo niliziheshimu alisema asingependa iwe hivyo, uhuru wa kuwaacha watu watafsiri wao ndo raha ya kazi yake ingawa yeye anajua hasa kwanini alichora na maana yake hasa ni nini! Kwa heshima ya sanaa ilibidi nikubali matokeo. Toka umeanza kumjua na kufuatilia kazi yake, mara ngapi ushawahi kuskia Masoud yuko matatani? Yaani kakamatwa au hajulikani alipo? Kwangu mara kadhaa lakini haikuwahi kuwa kizuizi cha yeye kuacha kufanya afanyacho, kuogopa je? Nadhani kama binadamu kuwa na uoga ni jambo la kawaida, ila unafanyaje baada ya hapo ndo tofauti yetu.
Episode hii inajumuisha karibu yote ambayo niliwahi kutaka kumuuliza, mengine nilipata majibu nlotaka na mengine yalitolewa mbavuni, kwa ki vyovyote vile nili enjoy sana mimi na wenzangu na kutoka kwetu tunatumai nawe uta enjoy kama ambayo nasi tuli enjoy na kujifunza kutoka kwa MWAMBA huyu.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Пікірлер: 95

  • @GivenTobago
    @GivenTobago Жыл бұрын

    Masoud aliwahi kunifundisha kuchora cartoon ilikua ni semina ya wikimbili kwa watoto wa shule ya msingi wenye vipaji vya uchoraji yalikua ni maswala ya usalama barabarani shule ya msingi Naura Arusha Central namshukuru sana nilipata basics nzuri juu ya comic na sasa nafanya Graphics web development na 3d graphics making big up to him.

  • @leylamohamed9939
    @leylamohamed9939 Жыл бұрын

    Masoud ni Kijana wa Sasa anayeishi mifumo ya Zamani, Birthday, Anniversary SIO ISHUUU... Safi sana 👊🏽👊🏽👊🏽

  • @echolude
    @echolude Жыл бұрын

    From a Kenyan based in the states: Masoud has that rare quality of exuding wisdom without much affectation, a wisdom that is edifying & actually locally derived. Apwe Heshima Yake! The same can be states of Salama: a wise woman indeed without being off putting & hyperbolic.

  • @frankissaya2578
    @frankissaya2578 Жыл бұрын

    I wonder why hizi doctorate za heshima hapewi Dr Kipanya

  • @carolineoyugi7771

    @carolineoyugi7771

    Жыл бұрын

    Sa ajanunua atapewa vipi na umesikia watu wananunua😂😂😂

  • @ashurajengela3926

    @ashurajengela3926

    Жыл бұрын

    Yani yuko very genius

  • @prudencemushi6948

    @prudencemushi6948

    Жыл бұрын

    Nadhan busara ilitumika wakaona apewe Babu Tale kwanza

  • @DoctorPesandegeMgangaTibAsili

    @DoctorPesandegeMgangaTibAsili

    Жыл бұрын

    Tatizo mbahili mno huyu jamaa 😅

  • @aminanamoyo83
    @aminanamoyo83 Жыл бұрын

    We ❤ you masoud kwaajili ya Allah Asante Salama kwa kumleta kipenzi chetu ❤🙏🇹🇿🇨🇭

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan2499 Жыл бұрын

    Nakukubali sana Masoud, sijawahi kukereka kwenye interview yako yoyote ile, bro Nakupenda sana 😘 *Masoud Kipanya*

  • @onlyacappellaallowed1743
    @onlyacappellaallowed1743 Жыл бұрын

    Salama unajua ya jufanya mahojiano mazito yawe kama 'kupiga stori' Big up sana

  • @abdallahmdangadachi7030
    @abdallahmdangadachi7030 Жыл бұрын

    Sichoki kumuangalia Kipanya toka mkasi hadi Yah Stonetown bonge moja la kolabo Masoud na Salama

  • @agostineminde6025
    @agostineminde6025 Жыл бұрын

    Huyu jamaa anahitaji heshima yake 👍

  • @joycembuya8480
    @joycembuya8480 Жыл бұрын

    Salama uu mwanamke jasiri na mwerevu sana Big up

  • @stanleymanimo769
    @stanleymanimo769 Жыл бұрын

    Wewe ni mtu poa sana masudi

  • @tanzaniamycountry9308
    @tanzaniamycountry9308 Жыл бұрын

    Ahaaaa😀😀😀😀😀 salama bhana

  • @claratemba44
    @claratemba44 Жыл бұрын

    Ushauri mzuri sana

  • @Marjeby
    @Marjeby Жыл бұрын

    Masoud Kipanya ni akili kubwa sana wallah

  • @mohdapper
    @mohdapper Жыл бұрын

    Pride of Africa Masoud kipanya

  • @philemonpeter8973
    @philemonpeter8973 Жыл бұрын

    salama nimependa sana,maswali yako,na jinsi masoud kipanya anavyo jibu,maswali yako,natamani sana kujua jinsi ya kununua hisa

  • @joviangeofrey7212

    @joviangeofrey7212

    Жыл бұрын

    Nafikir ni vyema utafute taarifa za makampuni mbalimbali. Kuna muda wanatangaza hiza

  • @sossyforreal814
    @sossyforreal814 Жыл бұрын

    Masoud is a very smart man aisee. Salama sasa tuletee Podcast.

  • @epiphaniaallute2726
    @epiphaniaallute2726 Жыл бұрын

    Asante Kaka Mosoud kuna jambo nimejifunza kupitia maelezo ya Malcom. Barikiwa sana kwa hili.

  • @Stevematongo
    @Stevematongo Жыл бұрын

    Incredible interview.

  • @abuujuhayfa4321
    @abuujuhayfa4321 Жыл бұрын

    Mzee wa vipanya 🎉

  • @Calky__-un5qd
    @Calky__-un5qd Жыл бұрын

    Nimependa sana brother Masoud,nimepata kitu❤️🔥

  • @nurdinkarata7985
    @nurdinkarata7985 Жыл бұрын

    🔥🔥🔥

  • @VictorChrispinSamson
    @VictorChrispinSamson Жыл бұрын

    Superb interview, never thought KP atakuwa down to earth like this.

  • @fatmaahamadabass8080
    @fatmaahamadabass8080 Жыл бұрын

    Duh Allah amsameh huyo mtu unafurahiya maradhi ya mwenzio kweli

  • @bumbuli4170
    @bumbuli4170 Жыл бұрын

    Genius

  • @emilyrenatus9374
    @emilyrenatus9374 Жыл бұрын

    Kp 🗽

  • @nurdinkarata7985
    @nurdinkarata7985 Жыл бұрын

    Logic sister salama 👊🏻

  • @franciskassanga7999
    @franciskassanga7999 Жыл бұрын

    nimeipenda hii, #siyo issue

  • @abdulhamis9825
    @abdulhamis9825 Жыл бұрын

    Mwamba Kabsa, Mtu Makin Jamaa Ambaye Sijawah kuchoka Kumsikiliza Na Kujifunza Kutoka Kwake KP

  • @emmamatemu8225

    @emmamatemu8225

    Жыл бұрын

    Umeandikaje hujaeleweka

  • @abdulhamis9825

    @abdulhamis9825

    Жыл бұрын

    @@emmamatemu8225 typing error

  • @nepiasmwasanga1309
    @nepiasmwasanga1309 Жыл бұрын

    Kumbe wengine hawapeleki michango SHUBAMIT..😀😀

  • @msafirimiracle6613
    @msafirimiracle6613 Жыл бұрын

    Haya bhana kwa hiyo mmeamua kurudi nyuma miaka,2022 😁

  • @queenmaa30
    @queenmaa30 Жыл бұрын

    Kiukweli nimejifunza ktu...elimu nzuri sana

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 Жыл бұрын

    ✌️✌️

  • @albogastmselejr4583
    @albogastmselejr4583 Жыл бұрын

    Nilikuwa Naisubiliaa Kwa Muda Hii Interview 🏃🏃

  • @jacklineabella7634
    @jacklineabella7634 Жыл бұрын

    I was waiting for this interview so badly.

  • @rehemaothman2475

    @rehemaothman2475

    Жыл бұрын

    ❤❤❤❤Nimejiona

  • @salviusbasil5334
    @salviusbasil5334 Жыл бұрын

    Masoud arudishe ile #MaishaPlus

  • @ramadhanimtetu3656
    @ramadhanimtetu365613 күн бұрын

    Kipanya Kama kipanya

  • @florageofrey9486
    @florageofrey9486 Жыл бұрын

    Nimecheka sana kwakweli

  • @amytullah2175
    @amytullah2175 Жыл бұрын

    Hio ya makochi jamani hata mie nilishachanaa😅😅😅😅 daah!! Nilichezea zakufa mtu😅😅😅

  • @mwajabujumanne9025
    @mwajabujumanne9025 Жыл бұрын

    Yaan story ya malcom hua lazima nlie pole sana masud😢😢😢

  • @NGUFUSALOMI
    @NGUFUSALOMI Жыл бұрын

    Hilo cheko la Salama

  • @enockcharles6750
    @enockcharles6750 Жыл бұрын

    nimesubir sana hii yani

  • @JanethKomba-tv7jy
    @JanethKomba-tv7jy Жыл бұрын

    Jamani tujifunze kupitia interview za ece jay not always tunataka kuona makosa t,ila we need to be strong bhna as broo kp did to handle Malcolm's issues

  • @SeekerMaulid
    @SeekerMaulid Жыл бұрын

    Sister Salama Leo umecheka sana Jamani :), Huu sio 2022 ni 2023.

  • @godblessmwacha5201

    @godblessmwacha5201

    Жыл бұрын

    ni ya muda kweli.. usidhani ni wamekosea. ivi vipindi vingi vya salama ni vya muda.

  • @barakawiseman5073
    @barakawiseman5073 Жыл бұрын

    Masudi anamuonekano wa umwakyembe flani ivi

  • @mohamednaaman188
    @mohamednaaman188 Жыл бұрын

    2022 😀

  • @issakitundu617
    @issakitundu617 Жыл бұрын

    et huu mwaka gani salama

  • @abdulhakimmwango9370
    @abdulhakimmwango9370 Жыл бұрын

    Leo ndo umeamua kuiachia si ndio😅😅😅 haya bwana master mind salama

  • @allybobsaith
    @allybobsaith Жыл бұрын

    Hakuna mzee asiyejua siku za kuzaliwa watoto wake huyo mzee mjanja sana namkubali sana big up masoud. Huyu jamaa ni mind reader 😂😂😂😂😂

  • @nsanyarasheeed8693

    @nsanyarasheeed8693

    Жыл бұрын

    Kubali ukakae watoto 8 utakumbuka siku zao za kuzaliwa kuna sis unakumbuka siku ya kuzaliwa imepita

  • @godblessmwacha5201
    @godblessmwacha5201 Жыл бұрын

    kumbe ni ya mwaka 2022? Dah

  • @barakakusa7606
    @barakakusa7606 Жыл бұрын

    Masoud ni mwamba hasa ila nashangaa kwanini kwenye teuzi zinazofanywa wanamsahau, Ana kitu huyu 😂😂😂😂

  • @joviangeofrey7212
    @joviangeofrey7212 Жыл бұрын

    Jaman kuna benk flan ilitaka kuanzishwa nikanunua hisa. Huu mwaka wa kumi sijapewa gawio. Inauma jmn

  • @hustlaztv2352
    @hustlaztv2352 Жыл бұрын

    Nlijua dr harison 😅

  • @sangomamourice3539
    @sangomamourice3539 Жыл бұрын

    Akili mingi mno mwamba hasa

  • @leilaassey1726
    @leilaassey1726 Жыл бұрын

    Kumbe ya kitambo salama 22 tena

  • @romes-tz7323
    @romes-tz7323 Жыл бұрын

    Mwamba wamda marefu like kwake👊

  • @Jaycollection
    @Jaycollection Жыл бұрын

    Tuna hitaji elimu kwenye hisa

  • @richardcastromzena5136
    @richardcastromzena5136 Жыл бұрын

    13:30 😂 16:10 😂 19:52 22:40 kaka imara sana

  • @hamyrhai9957
    @hamyrhai9957 Жыл бұрын

    Kipanya

  • @nicodemusmajani9698
    @nicodemusmajani9698 Жыл бұрын

    huyu #Mzee Hanaga shidah.

  • @dansondannytv8111
    @dansondannytv811111 ай бұрын

    Salama ivi nikifikia level gani ya kimaisha naweza fanyiwa Interview na wewe

  • @mactongathe179
    @mactongathe179 Жыл бұрын

    Apo kweny family dah nmechKaaa saNaa Brooo kipaNya! Birthday na hio namba yao Dah! But ....

  • @dengahmediatz1230
    @dengahmediatz1230 Жыл бұрын

    Tunatak interview yak salama

  • @famymbirore2756

    @famymbirore2756

    Жыл бұрын

    Yan apatikane mtu wa kumuhoji vizuri kama yeye anavyowahoji wengine

  • @mr.theoswahiliteacher.
    @mr.theoswahiliteacher. Жыл бұрын

    Watu wawili wenye IQ kubwa wamekutana.

  • @abdulnaseermrisho4342
    @abdulnaseermrisho4342 Жыл бұрын

    😂😂😂😂 Masoudy kama Masoudy

  • @philomenamushi5606

    @philomenamushi5606

    Жыл бұрын

    Shubaamiti😝hapo ndo kashatukana

  • @Yusufu940
    @Yusufu940 Жыл бұрын

    Salma ume una ma swali 😮

  • @peterkichochi7510
    @peterkichochi7510 Жыл бұрын

    Miaka imeridi nyuma mwaka 2022😂😂😂😂

  • @nzumbimasanja

    @nzumbimasanja

    Жыл бұрын

    Wanarekodi kisha wanapandisha muda wowote. Hii ni ya zamani

  • @godfreymiho4927
    @godfreymiho4927 Жыл бұрын

    Making sana,jamaa alinifany nipend kuchor

  • @Hashdough
    @Hashdough Жыл бұрын

    OPENING YA KIBABE KABISA

  • @leonarddamian

    @leonarddamian

    Жыл бұрын

    Sana

  • @joesimba
    @joesimba Жыл бұрын

    17:00 hizi interview nyingine zilifanyika mwaka jana nini.

  • @brightvatta284

    @brightvatta284

    Жыл бұрын

    Yawezekana naona pia mtangazaji kasema 2022

  • @philomenamushi5606
    @philomenamushi5606 Жыл бұрын

    🤔😂salama hii ni 2022😓🤔realy😳👀😳hii ni 2023 tafadhali✋🏿

  • @highmanjerry9640

    @highmanjerry9640

    Жыл бұрын

    Kipindi kilisha recodiwa mzee kama ww ni mfatiliaji kwa tv ungesha jua,humu kwa youtube huwa wanaweka baada ya kuonekana kwa tv kwhyo walio kosa show kwa tv basi utakutana nayo huku

  • @charlesolomi9514

    @charlesolomi9514

    Жыл бұрын

    Interview yooteee umeona hilo kosa tu

  • @godsonmunisi7229
    @godsonmunisi7229 Жыл бұрын

    Interview was badly .salama anakuuliza swali .but swali halijibu anatoa maelezo mengi sana nje ya swali.

  • @piuslwinga6233

    @piuslwinga6233

    Жыл бұрын

    Utakuwa unachuki zako tu

  • @godsonmunisi7229
    @godsonmunisi7229 Жыл бұрын

    I know you was want to act like genius. But wasn't what happens like you was wish .try to listen question carefully before answering questions

  • @frankkajoba8372

    @frankkajoba8372

    19 күн бұрын

    Tatizo kujifanya "much know" kiingereza gani hicho sasa wewe chizi? Hujui chochote kipindi kama hiki hakikufai kasikilize singeli ndio saizi yako.

  • @blandinamyinga9489
    @blandinamyinga9489 Жыл бұрын

    ""anivesari""???🤣🤣🤣🤣🤣@masoudkipanya🙌🙌🙌🙌

Келесі