Salama Na MASOUD KIPANYA SE6 EP60 | HERI KUFA MACHO… PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460
Ойын-сауық
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Habibi Masoud Kipanya ni Ally Masoud Nyomwa ambaye ni LEGEND. Kwa mujibu wake alizaliwa huku kakunja ngumi na dhana yake ni kwamba alizaliwa ili awe bondia! Kwa anacho kifanya na ambacho amekua akikifanya tena kwa ufasaha kwa miaka nenda miaka rudi bila ya shaka ni UBONDIA. Hakuna ambaye atabisha juu ya hilo. Amekua akipigania mambo tele na kuyasemea mengi pamoja na kuchekesha na kuelimisha kupitia kalamu yake. Kwa mujibu wake yeye ni mbobevu katika taaluma ya kupuuza na kuchukulia mambo poa kwa kipindi sasa. Lakini pia anaamini yeye ni MTATA. Tukienda mbele na kurudi nyuma, hapo kwenye UTATA hakuna ambaye anaweza kumbishia, hasa kwa wale ambao kalamu yake imewanyoosha kwa kiasi kikubwa.
Mimi na yeye tulikutana kwa mara ya kwanza takriban miaka kumi na tisa iliyopita, wakati huo mimi mbichi hasa na yeye akiwa kashajielewa na chemchem yake ya kipato tayari ilikua inatoa neema. Mimi nilikua ndo kwanza naanza kazi ya kujishikiza pale Times FM kipindi hiko bado ilikua kule Kamata. Masoud alikua analichorea gazeti la Majira ambalo lilikua liko kwenye mwamvuli mmoja na Radio ambayo nami nilikua nimejishikiza baada tu ya kumaliza skuli. Urafiki wetu ulikuja naturally tu maana sote tunapenda kucheka. Kupitia Zuhura Yunus na Binti mwengine wa kuitwa Rahma ndo mimi naye tulifahamiana. Wakati huo yeye alikua na gari kwahiyo lifti za hapa na pale zilikua hazikauki. Pia tulikua tunaitumia gari yake kama sehemu ya ku chill na kuskiliza muziki kwenye parking za Times FM.
Huwezi kukaa kwenye tasnia moja kwa muda mrefu kama wewe si hodari na mwenye kujielewa. Moja ya vitu ambavyo naviusudu kutoka kwake ni uelewa wake wa mambo tele wa tele, IQ yake ni ya juu sana na jinsi ambavyo ana reason ndo huwa anamaliza kabisa, kama binadamu wakati mwengine ni bora kukubaliana kuto kukubaliana na kwakwe yeye wakati mwengine jinsi anavyo wachora baadhi ya matukio na watu huwa haviishii kuzuri lakini hiyo haikuwahi kuwa sababu ya yeye kuacha kufanya ambacho anakifanya na ambacho amekua akikifanya kwa muda sasa. Uelewa wake kwenye mambo ambayo yanaendelea, uwezo wake wa kuona mbali na kuweka sanaa yake hiyo kwenye karatasi kisha kutuachia sisi tung’amue maana yake kwa kweli ni kipaji cha kipekee ya sana. Mmoja anatakiwa akae tu mbali na ku admire akifanyacho na hiko ndo ambacho mimi nimeamua kufanya.
Nilikua nataka anielezee maana halisi ya baadhi ya michoro yake ambayo iliacha gumzo kwa muda mrefu lakini kwa sababu ambazo niliziheshimu alisema asingependa iwe hivyo, uhuru wa kuwaacha watu watafsiri wao ndo raha ya kazi yake ingawa yeye anajua hasa kwanini alichora na maana yake hasa ni nini! Kwa heshima ya sanaa ilibidi nikubali matokeo. Toka umeanza kumjua na kufuatilia kazi yake, mara ngapi ushawahi kuskia Masoud yuko matatani? Yaani kakamatwa au hajulikani alipo? Kwangu mara kadhaa lakini haikuwahi kuwa kizuizi cha yeye kuacha kufanya afanyacho, kuogopa je? Nadhani kama binadamu kuwa na uoga ni jambo la kawaida, ila unafanyaje baada ya hapo ndo tofauti yetu.
Episode hii inajumuisha karibu yote ambayo niliwahi kutaka kumuuliza, mengine nilipata majibu nlotaka na mengine yalitolewa mbavuni, kwa ki vyovyote vile nili enjoy sana mimi na wenzangu na kutoka kwetu tunatumai nawe uta enjoy kama ambayo nasi tuli enjoy na kujifunza kutoka kwa MWAMBA huyu.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Пікірлер: 95
Masoud aliwahi kunifundisha kuchora cartoon ilikua ni semina ya wikimbili kwa watoto wa shule ya msingi wenye vipaji vya uchoraji yalikua ni maswala ya usalama barabarani shule ya msingi Naura Arusha Central namshukuru sana nilipata basics nzuri juu ya comic na sasa nafanya Graphics web development na 3d graphics making big up to him.
Masoud ni Kijana wa Sasa anayeishi mifumo ya Zamani, Birthday, Anniversary SIO ISHUUU... Safi sana 👊🏽👊🏽👊🏽
From a Kenyan based in the states: Masoud has that rare quality of exuding wisdom without much affectation, a wisdom that is edifying & actually locally derived. Apwe Heshima Yake! The same can be states of Salama: a wise woman indeed without being off putting & hyperbolic.
I wonder why hizi doctorate za heshima hapewi Dr Kipanya
@carolineoyugi7771
Жыл бұрын
Sa ajanunua atapewa vipi na umesikia watu wananunua😂😂😂
@ashurajengela3926
Жыл бұрын
Yani yuko very genius
@prudencemushi6948
Жыл бұрын
Nadhan busara ilitumika wakaona apewe Babu Tale kwanza
@DoctorPesandegeMgangaTibAsili
Жыл бұрын
Tatizo mbahili mno huyu jamaa 😅
We ❤ you masoud kwaajili ya Allah Asante Salama kwa kumleta kipenzi chetu ❤🙏🇹🇿🇨🇭
Nakukubali sana Masoud, sijawahi kukereka kwenye interview yako yoyote ile, bro Nakupenda sana 😘 *Masoud Kipanya*
Salama unajua ya jufanya mahojiano mazito yawe kama 'kupiga stori' Big up sana
Sichoki kumuangalia Kipanya toka mkasi hadi Yah Stonetown bonge moja la kolabo Masoud na Salama
Huyu jamaa anahitaji heshima yake 👍
Salama uu mwanamke jasiri na mwerevu sana Big up
Wewe ni mtu poa sana masudi
Ahaaaa😀😀😀😀😀 salama bhana
Ushauri mzuri sana
Masoud Kipanya ni akili kubwa sana wallah
Pride of Africa Masoud kipanya
salama nimependa sana,maswali yako,na jinsi masoud kipanya anavyo jibu,maswali yako,natamani sana kujua jinsi ya kununua hisa
@joviangeofrey7212
Жыл бұрын
Nafikir ni vyema utafute taarifa za makampuni mbalimbali. Kuna muda wanatangaza hiza
Masoud is a very smart man aisee. Salama sasa tuletee Podcast.
Asante Kaka Mosoud kuna jambo nimejifunza kupitia maelezo ya Malcom. Barikiwa sana kwa hili.
Incredible interview.
Mzee wa vipanya 🎉
Nimependa sana brother Masoud,nimepata kitu❤️🔥
🔥🔥🔥
Superb interview, never thought KP atakuwa down to earth like this.
Duh Allah amsameh huyo mtu unafurahiya maradhi ya mwenzio kweli
Genius
Kp 🗽
Logic sister salama 👊🏻
nimeipenda hii, #siyo issue
Mwamba Kabsa, Mtu Makin Jamaa Ambaye Sijawah kuchoka Kumsikiliza Na Kujifunza Kutoka Kwake KP
@emmamatemu8225
Жыл бұрын
Umeandikaje hujaeleweka
@abdulhamis9825
Жыл бұрын
@@emmamatemu8225 typing error
Kumbe wengine hawapeleki michango SHUBAMIT..😀😀
Haya bhana kwa hiyo mmeamua kurudi nyuma miaka,2022 😁
Kiukweli nimejifunza ktu...elimu nzuri sana
✌️✌️
Nilikuwa Naisubiliaa Kwa Muda Hii Interview 🏃🏃
I was waiting for this interview so badly.
@rehemaothman2475
Жыл бұрын
❤❤❤❤Nimejiona
Masoud arudishe ile #MaishaPlus
Kipanya Kama kipanya
Nimecheka sana kwakweli
Hio ya makochi jamani hata mie nilishachanaa😅😅😅😅 daah!! Nilichezea zakufa mtu😅😅😅
Yaan story ya malcom hua lazima nlie pole sana masud😢😢😢
Hilo cheko la Salama
nimesubir sana hii yani
Jamani tujifunze kupitia interview za ece jay not always tunataka kuona makosa t,ila we need to be strong bhna as broo kp did to handle Malcolm's issues
Sister Salama Leo umecheka sana Jamani :), Huu sio 2022 ni 2023.
@godblessmwacha5201
Жыл бұрын
ni ya muda kweli.. usidhani ni wamekosea. ivi vipindi vingi vya salama ni vya muda.
Masudi anamuonekano wa umwakyembe flani ivi
2022 😀
et huu mwaka gani salama
Leo ndo umeamua kuiachia si ndio😅😅😅 haya bwana master mind salama
Hakuna mzee asiyejua siku za kuzaliwa watoto wake huyo mzee mjanja sana namkubali sana big up masoud. Huyu jamaa ni mind reader 😂😂😂😂😂
@nsanyarasheeed8693
Жыл бұрын
Kubali ukakae watoto 8 utakumbuka siku zao za kuzaliwa kuna sis unakumbuka siku ya kuzaliwa imepita
kumbe ni ya mwaka 2022? Dah
Masoud ni mwamba hasa ila nashangaa kwanini kwenye teuzi zinazofanywa wanamsahau, Ana kitu huyu 😂😂😂😂
Jaman kuna benk flan ilitaka kuanzishwa nikanunua hisa. Huu mwaka wa kumi sijapewa gawio. Inauma jmn
Nlijua dr harison 😅
Akili mingi mno mwamba hasa
Kumbe ya kitambo salama 22 tena
Mwamba wamda marefu like kwake👊
Tuna hitaji elimu kwenye hisa
13:30 😂 16:10 😂 19:52 22:40 kaka imara sana
Kipanya
huyu #Mzee Hanaga shidah.
Salama ivi nikifikia level gani ya kimaisha naweza fanyiwa Interview na wewe
Apo kweny family dah nmechKaaa saNaa Brooo kipaNya! Birthday na hio namba yao Dah! But ....
Tunatak interview yak salama
@famymbirore2756
Жыл бұрын
Yan apatikane mtu wa kumuhoji vizuri kama yeye anavyowahoji wengine
Watu wawili wenye IQ kubwa wamekutana.
😂😂😂😂 Masoudy kama Masoudy
@philomenamushi5606
Жыл бұрын
Shubaamiti😝hapo ndo kashatukana
Salma ume una ma swali 😮
Miaka imeridi nyuma mwaka 2022😂😂😂😂
@nzumbimasanja
Жыл бұрын
Wanarekodi kisha wanapandisha muda wowote. Hii ni ya zamani
Making sana,jamaa alinifany nipend kuchor
OPENING YA KIBABE KABISA
@leonarddamian
Жыл бұрын
Sana
17:00 hizi interview nyingine zilifanyika mwaka jana nini.
@brightvatta284
Жыл бұрын
Yawezekana naona pia mtangazaji kasema 2022
🤔😂salama hii ni 2022😓🤔realy😳👀😳hii ni 2023 tafadhali✋🏿
@highmanjerry9640
Жыл бұрын
Kipindi kilisha recodiwa mzee kama ww ni mfatiliaji kwa tv ungesha jua,humu kwa youtube huwa wanaweka baada ya kuonekana kwa tv kwhyo walio kosa show kwa tv basi utakutana nayo huku
@charlesolomi9514
Жыл бұрын
Interview yooteee umeona hilo kosa tu
Interview was badly .salama anakuuliza swali .but swali halijibu anatoa maelezo mengi sana nje ya swali.
@piuslwinga6233
Жыл бұрын
Utakuwa unachuki zako tu
I know you was want to act like genius. But wasn't what happens like you was wish .try to listen question carefully before answering questions
@frankkajoba8372
19 күн бұрын
Tatizo kujifanya "much know" kiingereza gani hicho sasa wewe chizi? Hujui chochote kipindi kama hiki hakikufai kasikilize singeli ndio saizi yako.
""anivesari""???🤣🤣🤣🤣🤣@masoudkipanya🙌🙌🙌🙌