Salama Na MASOUD KIPANYA SE6 EP60 | HERI KUFA MACHO… PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460
Ойын-сауық
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Habibi Masoud Kipanya ni Ally Masoud Nyomwa ambaye ni LEGEND. Kwa mujibu wake alizaliwa huku kakunja ngumi na dhana yake ni kwamba alizaliwa ili awe bondia! Kwa anacho kifanya na ambacho amekua akikifanya tena kwa ufasaha kwa miaka nenda miaka rudi bila ya shaka ni UBONDIA. Hakuna ambaye atabisha juu ya hilo. Amekua akipigania mambo tele na kuyasemea mengi pamoja na kuchekesha na kuelimisha kupitia kalamu yake. Kwa mujibu wake yeye ni mbobevu katika taaluma ya kupuuza na kuchukulia mambo poa kwa kipindi sasa. Lakini pia anaamini yeye ni MTATA. Tukienda mbele na kurudi nyuma, hapo kwenye UTATA hakuna ambaye anaweza kumbishia, hasa kwa wale ambao kalamu yake imewanyoosha kwa kiasi kikubwa.
Mimi na yeye tulikutana kwa mara ya kwanza takriban miaka kumi na tisa iliyopita, wakati huo mimi mbichi hasa na yeye akiwa kashajielewa na chemchem yake ya kipato tayari ilikua inatoa neema. Mimi nilikua ndo kwanza naanza kazi ya kujishikiza pale Times FM kipindi hiko bado ilikua kule Kamata. Masoud alikua analichorea gazeti la Majira ambalo lilikua liko kwenye mwamvuli mmoja na Radio ambayo nami nilikua nimejishikiza baada tu ya kumaliza skuli. Urafiki wetu ulikuja naturally tu maana sote tunapenda kucheka. Kupitia Zuhura Yunus na Binti mwengine wa kuitwa Rahma ndo mimi naye tulifahamiana. Wakati huo yeye alikua na gari kwahiyo lifti za hapa na pale zilikua hazikauki. Pia tulikua tunaitumia gari yake kama sehemu ya ku chill na kuskiliza muziki kwenye parking za Times FM.
Huwezi kukaa kwenye tasnia moja kwa muda mrefu kama wewe si hodari na mwenye kujielewa. Moja ya vitu ambavyo naviusudu kutoka kwake ni uelewa wake wa mambo tele wa tele, IQ yake ni ya juu sana na jinsi ambavyo ana reason ndo huwa anamaliza kabisa, kama binadamu wakati mwengine ni bora kukubaliana kuto kukubaliana na kwakwe yeye wakati mwengine jinsi anavyo wachora baadhi ya matukio na watu huwa haviishii kuzuri lakini hiyo haikuwahi kuwa sababu ya yeye kuacha kufanya ambacho anakifanya na ambacho amekua akikifanya kwa muda sasa. Uelewa wake kwenye mambo ambayo yanaendelea, uwezo wake wa kuona mbali na kuweka sanaa yake hiyo kwenye karatasi kisha kutuachia sisi tung’amue maana yake kwa kweli ni kipaji cha kipekee ya sana. Mmoja anatakiwa akae tu mbali na ku admire akifanyacho na hiko ndo ambacho mimi nimeamua kufanya.
Nilikua nataka anielezee maana halisi ya baadhi ya michoro yake ambayo iliacha gumzo kwa muda mrefu lakini kwa sababu ambazo niliziheshimu alisema asingependa iwe hivyo, uhuru wa kuwaacha watu watafsiri wao ndo raha ya kazi yake ingawa yeye anajua hasa kwanini alichora na maana yake hasa ni nini! Kwa heshima ya sanaa ilibidi nikubali matokeo. Toka umeanza kumjua na kufuatilia kazi yake, mara ngapi ushawahi kuskia Masoud yuko matatani? Yaani kakamatwa au hajulikani alipo? Kwangu mara kadhaa lakini haikuwahi kuwa kizuizi cha yeye kuacha kufanya afanyacho, kuogopa je? Nadhani kama binadamu kuwa na uoga ni jambo la kawaida, ila unafanyaje baada ya hapo ndo tofauti yetu.
Episode hii inajumuisha karibu yote ambayo niliwahi kutaka kumuuliza, mengine nilipata majibu nlotaka na mengine yalitolewa mbavuni, kwa ki vyovyote vile nili enjoy sana mimi na wenzangu na kutoka kwetu tunatumai nawe uta enjoy kama ambayo nasi tuli enjoy na kujifunza kutoka kwa MWAMBA huyu.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Пікірлер: 102
Ukiitoa show ya ruge kwenye mkasi, hii ndo show bora ya salama, mahojiano yenye contents. Nime enjoy na kujifunza big up y'all
Hilo swali la "Tanzania yako unaiona wapi" majibu yake aiseeee, ni akili ya kiwango Cha juu Sana🙏🙏🙏🙌
Hakika nimejifunza vitu vingi na ninazidi kujifunza 🤲🙏salama 🤲🙏masoudy🤲🙏asantee kwa darasa
Masoudy ni kama muda wake ulikuwa mdogo ilifaa aendelee kutuambia mambo mengi zaidiiii ....... nimejifunza I wish maisha plus irudi tena
This is the one of the Greatest Man in the World, pengine hatukumwaga damu back in a days kipindi cha uhuru, ama pengine amani tuliyonayo inatufanya tunarelax na kujisahau but INAWEZEKANA
@cheka480
Жыл бұрын
indeed
Salama kama unahitaji kujua uwekezaji was hisa na Hati fungani niambie. Ntakusaidia elimu for free. I am your fan
@lutufyojason2598
Жыл бұрын
Kaka John .naomba uniongeza na mimi
@gracepaulo704
Жыл бұрын
Namm nahtaj weka no bro
@joshuamacha8751
Жыл бұрын
Mimi nataka kujua pia
Masoud Amezaliwa Zama Ambazo Sio Zake, Atusamehe Bure, Tukitaka Kumuelewa Tumpe Nchi.
Salama J! Kipindi chako kinaelimisha, kinajenga ujasiri, kinakuza kiimani. Nawe Mungu akuweke kama ulivyomwambia Masoud
Nilikuwa nampenda malkom tangu akiwa mdogo japo nilikuja kumuona akiwa amekuwa kuwa,nakumbuka nilikuwa ndo kabinti niliuwa sipitwi na kipindi cha wàtoto chuchuchu , kaka masood na malkom,marehem Amina chifupa na rahmani,,yaani nino, na kaka bonda yey hakuwa na mototo walikuwa wakimcheka kimatani,,aisee
Mungu akupe umri mrefu na Afya NJEMA Masoud Wetu 🙏
This guy is one of a kind my best quote "mnanunua hela mnapata wapi" kama nyie ni consumers na si producers
Kali sana hii na nilikua naisubiri hongera kwa kutuletea huyu mtu, sasa bado SALAMA NA MILLARD AYO
Watu wasikujue saana...Familiarity breeds contempt Masoud nailed that
Mtu muhimu sana kwenye taifa letu na maisha ya WaTanzania ...💯🔥
@alifocusmsham7623
Жыл бұрын
Yani intrerview imeisha wakati ndokwanza inataka kuanza
Nakupenda sana Masoud, huwa sichoki kukusiliza. MUNGU azidi kukutunza, una vitu vingi sana kwa ajili ya kuisadia jamii yetu (nchi yetu). Salama, nakupenda pia, kipindi chako kina mambo mengi sana ya muhimu kwetu. Big up you all!
Hiii show imekuwa fupi sana. "Tafuta taarifa upate maarifa"
Huwa sikuzote simalizi kiu yangu ya kumsikiliza Masoud, nimeangalia interview zake nyingi sana lakini bado nataka zaidi na zidi.
Strong heart Boss Kipanya, hiyo mentality wachache sana wanazo hasa wababa so tumejifunza mamb mengi sana hapo hasa sisi wanaume…be blessed Salama zaidi tupe watu makini sio wale channel za udaku na kutafuta umbea😂😂
Vp ile show ya maisha plus bonge moja la show itufunza mambo mengi sana kama vijana tunaihitaji tafafhali
masoud anaongea vizuri na kwa ufasaha sana
Shukran sana Kwa hichi Sister Salama,mbalikiwe sana na muishi sana
Hawa ndo watu wa kuwekwa serikalini walete elimu na mabadiliko katika jamii, siyo tuu watu watuuu
There is very thin line between love and hate🔥
God bless you masoud wewe ni genius sana aise naamn watu walio karibu na wewe kuna vitu vingi sana wanavipata kutoka kwako ,pia nikupongeze sana salamaa uko smart kwenye kazi yako #greatinterview
Plz Salama tuna muitaji tena japo 2hrs tu maana Ana vingi vya kutufunza From Kansas in USA 🤜🏿🤛🏿
@veridianacharles4511
Жыл бұрын
Niliona kama kuna mengi tunahitaji kujifunza toka kwake
Masud kipanya ni Kati ya watu wenye fikra nyingi sana katika nchi ya Tanzania na bara lake sema sisi watu weusi tumeloga na aliyetuloga kafa, watu Kama yeye uwa tunawachukulia kawaida sana …… mungu ampe maisha marefu kaka yetu kwani bado ana mambo mengi sana kutujuza toka kwenye kichwa chake, Salama sina mengi ya kusema juu yako , you one of the best interview ever live in our generation, was good talk I love it
Masoud, my faviurite presenter…since Chuchuchu ya Clouds fm, power breakfast…you are genius
Rais Anateua Watu Kushika Nyadhifa MbaliMbali Katika Serikal Na Maeneo Ya Nchi Lkn Iman Yngu Mpka Leo Bado Hajajua Ww Utashka Nafas Gani Ww Ni GENIUS
Men 🎉 Big up to Masoud I like your critical thoughts. Asante salama
What an Interview.....Absolutely Sensational!
Great interview. Thought-provoking. Masoud has a big mind.
Kuna content mmezikata na zilikuwa zinaumuhimu mno sanjari na Hilo bado show ni Kali mashaallah
This is hands down the best interview I have listened to tangu hii show ianze
Safi sana Masoud. Hapo kwenye Business Plan. Ni Ukweli Mchungu. very true.
Masoud I'm 55years, I studied mechanical engineering, based to motor vehicle, for over 30year, you inspires me big time, man you have great mind weather we want it or not but the truth stand still, Is there any chance we can meet, I would say we are some way alike, I'm a practically man ,you won't regret lay the table with me,
Duuuuhhh!! Nimejifunza kitu kikubwa saaana, hongera sana cis Salama na big up kaka Masoud, Mungu aendelee kukuweka na kile kilichopo ndani kiendelee kumea
Kipindi kizuri...shukran kwa Mtangazaji,shukran kwa mgeni Ustadh Msoud...tumenufaika na kufaidika piya kupitiya mazungumzo yenu...
Naomba umuhoji Masoud kila siku...
@joycembuya8480
Жыл бұрын
🤣
This is the best asante sana salama 🙏
NAWAKUBALI SANA.NBRO.masoud Kipanya nakukubali sana
Yaani baba Malcolm iko kama Mimi simtu wamarafiki.naninapenda saaaana kuka pekeangu kwa sababu Mimi nafkiria saaaaaaaana
Let me challenge Masoud, Dubai leo ina mafuta na utalii hela wanapata huko as Nation, Urussi ina Gas na Mafuta inapata fedha hapo, sisi tuna Gas, Madini, Utalii how we optimise these resources ziwe na tija kwa Taifa huoni kuna sehemu hatuko sawa, our Gvt needs to be Rich enough tukifika hapo itakuwa simple wao kufacilitate hizo manufacturing ma exports na kuleta Technology mpya, Serikali kama hela ya budget yake ni mpaka itafutane hatufiki, hiyo china, Marekani, Urussi, hata urabuni serikali zao zina hela nyingi sana kwakuwa ni wakali na wamesimamia ukweli kwenye resources zao!!
@abdallahmakombo3866
11 ай бұрын
Shida kuu Kwa nchi zetu ni , Elimu na ufahamu, Tumekosa elimu na ufahamu Kwa viongozi,mtu mmoja mmoja na jamii zetu, Hizo nchi uzitajazo Zina technology, knowledge, Ufahamu huo huwapa , Mawazo, ambayo huwatafuta watu sahihi Kisha hao watu huwapa mtaji / capital ambayo huleta kutatua changamoto za kidunia Kisha hupata zawadi( fedha nyingi/ THAMANI zaidi. Kwa hiyo Kuna haja kubwa ya kuwekeza kwenye wazo ( maarifa)Kisha technology ( mifumo ya uzalishaji Mali kisasa ,na ndipo tufike mbali ,HUKU TUKIJUA UJASUSI WA KIUCHUMI KIMATAIFA . Bado sana
SHIRT LAKE KALI SANA
Masoud akili nyingi sana.. very inspired
Nimependa hapo kwa rafiki
Super genius🔥
Bonge la interview 👏👏👏
Hili ni darasa huru nimechukua point za kutosha sana leo, ahsante.
Masoud amebarikiwa IQ kubwa..! Best Interview 🙏
Genius Masoud.
I love Masoud Kipanya huyu jamaa ana akili nyingi sana
Nimejifunza shukran sana kwenu
Daaaaah nimejifunza kitu kikubwa Sana thank brother 🙏
@enockcharles6750
Жыл бұрын
salama si haki hii ya mwaka jana iruduwe bwana
Makini broo❤❤
Big brains maahn🙏
hua namuelewa sana huyu jamaa. (kipanya) ni moja ya hazina , well done , please tuletee kaimu shehe wa mkoa DSM.
Big up brother Masoud na dada yetu Salama
Ruge Mutahaba, Masoud kipanya ,Massanja,Zembela, Roma mkatoli ,Nauka nafikiri Hawa jamaa Tanzania inabidi iwatumie sana!
Akili hzi za masoud Hawa ndio ilitakiwa wawepo bungeni,bahati mbaya wapo Africa.
❤ masoud, thanks Salama but please mrudishe tena tafadhali 🙏🇹🇿🇨🇭
@georgemuigai7427
Жыл бұрын
Hakika nimejifunza kitu kwa brother masoud,Mimi nataka kitabu nitakipata wapi?
Duuh bonge la interview
Ningefurahi sana Kama nitapata namba ya Kipanya, from Germany
Masoud mtu special
Nakukubali kaka
Masud nakukubali na kunakitu chakujifunza toka kwako
I have worked for 30 years I did different kind of innovation, at the meantime I'm thinking of working with sustainable agriculture based to irritation, your a philosopher,
12:10,🤣🤣🤣🤣🙌🙌🙌, magari siyo matikiti au siyooo😂😂
Salma na ston town show naomba mniruhusu nitukane ili kiongozii wetu ajee hapa kumsikiliza huyu Kaka 😢😭😭😭
On Podcast is 2 good hours, this is summarized.
only content in this mahojiano 🎉
Voice over artist
kitabu chake kinaitwaje na kinapatikana wapi
Big brother is not a show to impact an African community, nothing in there. May Allah make it easy for Kipanya to continue with MaishaPlus
Mi napenda tu slama tabasam lake
Maisha plus ingerudi Tena
Asaalaam Alleykum naomba utuletee na ezden jumanne!
Nasubiria salama na Roma mkatoliki, salama na Kala Jeremiah
Masoud kipanya atafutwe tena, bado hajakata kiu yetu kama watazamaji
Hakika, SISI WA TANZANIA NI WACHUUZI KABISA. BIDHAA ILIOTENGENEZWA NA MWINGINE HALAFU UNANUNUA ILI KUUZA KWA FAIDA
Natamani sana kama utakuwa unaleta watu wahivi wengi kuliko ambao hawana uwezo mkubwa wa kuzungumza vitu sensitive kama hawa mkifanya hivi wallah mtafika mbali hata vipindi vyenu kuwa namba 1 tanzania kuliko channel nyingi za hovyo cause hapa kuna vitu vingi vya kujifunza
Wakwanza
12:13 utemgenezaji wa magari sio kilimo cha matikiti😉😉
Why wasimpee aat uongoziii uyu jamaaaa ... mee naaminii iii Dhahabu kwa watanzaniaa aseee
Moja kati ya watu ambao wanafanya nijivunie kua Mtanzania
wa pili
Jmn mahojiano mbn mafupi
Watatu
I wish Maisha plus Ingerud tena ngoja tuendelee kuomba dua
Startup is hassling 🛺💪🏿, asante sana KP
@erickmorro8852
Жыл бұрын
eMo Bodaboda Tanzania
Usimruhusu mtu akakujua kuna siku atakutumia vibaya sana kukujua kwako