MAJALIWA ATUMBUA IRINGA, MIL. 433 KUMSAKA MSTAAFU

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema hajaridhishwa na ujenzi wa shule ya sekondari ya wasichana ya mkoa wa Iringa na kuagiza Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo, Emmanuel Sigachuma asimamishwe kazi mara moja.
Pia ameagiza Afisa Elimu ngazi ya Sekondari ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Nelson Milanzi apewe onyo kwa kushindwa kusimamia matumizi ya fedha za ujenzi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Lugalo iliyoko kata ya Mbigili, wilayani Kilolo.
Pia ameagiza Mkurugenzi Mtendaji Mstaafu, Lain Ephraim Kamendu aitwe ili ahojiwe pamoja na wenzakekuhusu matumizi mabaya ya fedha hizo. Yeye alistaafu Aprili, mwaka huu na ujanzi ulianza yangu Agosti, 2023.
Amefikia uamuzi huo leo (Jumatatu, Julai 8, 2024) baada ya kukagua ujenzi wa sekondari hiyo na kukuta kasoro nyingi kwenye madawati, vyumba vya maabara na bwalo la wanafunzi ilhali walishapewa sh. bilioni tatu za kukamilisha majengo yote ya shule hiyo.
Kasoro kubwa zilizobainika ni ukosefu wa nyavu za kuzuia mbu kwenye baadhi ya madirisha wakati mkandarasi ameshalipwa fedha yote, viti na meza za wanafunzi kupasuka wakati havijaanza kutumika. Viti hivyo vilikabidhiwa tangu Desemba, 2023 na muda wa matazamio ulikuwa ni miezi sita lakini mkandarasi keshalipwa fedha zote.
Katika ukaguzi wa bwalo, Waziri Mkuu alielezwa na Mhandisi Sagachuma kwamba bwalo hilo lilitengewa sh. milioni 774 na wamekwishatumia sh. milioni 341 hadi kufikia hatua ya linta ambayo alidai ni sawa na asilimia 40 ya ujenzi wake.
Alipoulizwa fedha zilizobakia ziko wapi, Mhandisi huyo alijibu kwamba hazipo. Afisa Elimu Sekondari naye hakuweza kueleza ziko wapi au kama kuna vifaa vilivyokwishanunuliwa vimewekwa wapi.
Imendaliwa na Zaituni Mkwama
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: / spotileo-176. .
HabariLeo: / habarileo
DailyNews: / dailynewstz
INSTAGRAM;
HabariLeo: habarileo_tz?ig...
SpotiLeo: spotileo?igshid...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: HabariLeo?s=09

Пікірлер