WAMEYAKANYANGA | WAZIRI MKUU AINGILIA KATI MAUAJI YA MTOTO ASIIMWE, ATOA MAELEKEZO MAZITO
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameielekeza Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, mara upelelezi utakapokamilika, kuwafikisha mahakamani mara moja watuhumiwa wote waliohusika na mauaji ya mtoto Asiimwe Novath aliyekuwa na umri wa miaka miwili na nusu mkoani Kagera, ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaofikiria kufanya vitendo kama hivyo.
Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo bungeni jijini Dodoma leo asubuhi alipokuwa akiwasilisha tamko la Serikali kuhusu ulinzi wa mtoto ambapo amewataka wananchi kuachana na imani potofu au mizaha inayolenga kuaminisha kuwa viungo vya watu wenye Ualbino vinaweza kuwaletea utajiri.
Пікірлер: 7
Nawaombeni sanaa serekeli Sheria ifuate mkondo wake ikiwapendeza wapigwe risasi hadharanii...ili iwefundisho kwa wenyetabia kama hii ..kunyonga kwa siir haitofundishaa sana....twaomba Sheria ifuate mkondo wake....
Shida watu sasa wanafiria pesa zaidi kuliko mwenyezi mungu.
Mungu awape nguvu jeshi la polisi
Mh raisi bola ulivyo chukua atua ya kutatsfuta aki ya uyo bint ashmwe 🙏
Wapewe Adhabu kali sana ikiwemo ya kukatwa kiungo kimoja kimoja hadi kufa, hili litakuwa fundisho na kwa wengine wenye Tabia kama hii:
Agizo limewafika
Mbona nguvu hiyobya kuwapata watuhumiwa haikutumika kumtafuta mtoto? Nina imani nguvu na jitihada za kumtafuta zingefanyika kwa nguvu hiyo basi mtoto angepatikana na kuokolewa akiwa hai. Jeshi la polisi lijitafakari.......