AWESO AMUWEKA KIKAANGONI MENEJA DAWASA, AMUHOJI 'WANANCHI WANAKOSA MAJI, MNAPOKEA MISHAHARA'

Waziri wa Maji Mhe Jumaa Aweso leo tar. 04 Julai 2024 amefika Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar Es Salaam kutembelea na kukagua Mradi Mkubwa wa Maji katika Miundombinu ya Tenki la Maji lita mil.15.
Waziri Aweso anaendelea na ziara ya kikazi mkoa wa Dar Es Salaam.
Waziri Aweso amemtaka Meneja wa DAWASA Kigamboni kufanya kazi kwa bidii na kuboresha utendaji kazi wake na kuahidi kufanya mabadiliko makubwa wilaya ya Kigamboni kwani halizishwi na utendaji kazi wa eneo hilo.
Katika hatua nyingine Mhe Aweso amekutana na Watumishi wa mkoa wa DAWASA - Kigamboni ambapo amewasisitiza watumishi kufanya kazi kwa bidii na kudumisha umoja ili kuleta maendeleo katika mkoa wa Dar es Salaam.

Пікірлер: 14

  • @AgnessKabamanywa-sd2dw
    @AgnessKabamanywa-sd2dw13 күн бұрын

    Asante sana waziri wa maji,hao watu huwa wananyimwa maji makusudi fukuza wote weka wapya

  • @NdovuDentalClinic_
    @NdovuDentalClinic_13 күн бұрын

    Nafikiri Aweso anafahamu undani WA tatizo NDANI ya dawasa . Mambo ya msingi kama maji hayana siasa . Kila siku watu wanalalamika ukipiga simu unaambiwa pressure ndogo 😂😂

  • @peterfujokalogi7821
    @peterfujokalogi782113 күн бұрын

    Njooo na katoro kuna madudu maji ni ya shida

  • @harithrashid5314
    @harithrashid531413 күн бұрын

    Hawa mawaziri wamekua wasanii sanaa

  • @francismadirisha3511
    @francismadirisha351113 күн бұрын

    Mh waziri nakukubari Sana pings spna hao

  • @edithtarimo5872
    @edithtarimo587212 күн бұрын

    Yani dawasa imeozaaaaa

  • @zully756
    @zully75613 күн бұрын

    Tundwi Songani badooooo

  • @hawaelymaricca7602
    @hawaelymaricca760213 күн бұрын

    Fukuza hao wanafanya kazi kwa mazoea wapo vijana wanahitaji kaz na wasomi

  • @Kim19onlinetv
    @Kim19onlinetv13 күн бұрын

    Juma awesu tia kamba hawa

  • @ayoubmtumishi50
    @ayoubmtumishi509 күн бұрын

    Yani kuna vituko kwa vituko JAMANI

  • @nujakaluhende9428
    @nujakaluhende942813 күн бұрын

    Kuna kitu kinatakiwa kifanywe

  • @dhireshrajput548
    @dhireshrajput54813 күн бұрын

    Nani kamaga Pombe yangu!😂

  • @drewsondeniss709
    @drewsondeniss70912 күн бұрын

    Sikuizi mpaka wana siasa wanatafuta content 😂

  • @philemonmagesa5548

    @philemonmagesa5548

    12 күн бұрын

    Ww ulitakaje?