AWESO AMUWEKA KIKAANGONI MENEJA DAWASA, AMUHOJI 'WANANCHI WANAKOSA MAJI, MNAPOKEA MISHAHARA'
Waziri wa Maji Mhe Jumaa Aweso leo tar. 04 Julai 2024 amefika Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar Es Salaam kutembelea na kukagua Mradi Mkubwa wa Maji katika Miundombinu ya Tenki la Maji lita mil.15.
Waziri Aweso anaendelea na ziara ya kikazi mkoa wa Dar Es Salaam.
Waziri Aweso amemtaka Meneja wa DAWASA Kigamboni kufanya kazi kwa bidii na kuboresha utendaji kazi wake na kuahidi kufanya mabadiliko makubwa wilaya ya Kigamboni kwani halizishwi na utendaji kazi wa eneo hilo.
Katika hatua nyingine Mhe Aweso amekutana na Watumishi wa mkoa wa DAWASA - Kigamboni ambapo amewasisitiza watumishi kufanya kazi kwa bidii na kudumisha umoja ili kuleta maendeleo katika mkoa wa Dar es Salaam.
Пікірлер: 14
Asante sana waziri wa maji,hao watu huwa wananyimwa maji makusudi fukuza wote weka wapya
Nafikiri Aweso anafahamu undani WA tatizo NDANI ya dawasa . Mambo ya msingi kama maji hayana siasa . Kila siku watu wanalalamika ukipiga simu unaambiwa pressure ndogo 😂😂
Njooo na katoro kuna madudu maji ni ya shida
Hawa mawaziri wamekua wasanii sanaa
Mh waziri nakukubari Sana pings spna hao
Yani dawasa imeozaaaaa
Tundwi Songani badooooo
Fukuza hao wanafanya kazi kwa mazoea wapo vijana wanahitaji kaz na wasomi
Juma awesu tia kamba hawa
Yani kuna vituko kwa vituko JAMANI
Kuna kitu kinatakiwa kifanywe
Nani kamaga Pombe yangu!😂
Sikuizi mpaka wana siasa wanatafuta content 😂
@philemonmagesa5548
12 күн бұрын
Ww ulitakaje?