UJENZI WA GATI BANDARI ZA KIBIRIZI NA UJIJI KUKAMILIKA OKTOBA, "FURSA" MAZINGIRA MAZURI KIBIASHARA..

#viral #news #tanzania Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa amesema hayo wakati akikagua maendeleo ya miradi hiyo na kuwataka wakandarasi wanaojenga bandari hizo kuongeza kasi ili zikamilike ifikapo mwezi Oktoba mwaka huu.
Akizungumza na wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari za Ziwa Tanganyika Prof. Mbarawa amesema uwekezaji unaokusudiwa kufanywa katika bandari nchini unatarajiwa kuongeza mapato, ajira na kukuza ufanisi wa utendaji.

Пікірлер