“TUFIE KWENYE HUU MRADI ,KAZI IFANYIKE USIKU NA MCHANA” AWESO

Фильм және анимация

JARIBIO la pili katika mradi wa Maji wa Same - Mwanga - Korogwe la kusukuma maji kutoka eneo la matibabu ya maji yaani Treatment Unit limefanyika na kushuhudiwa na Watendaji wa Wizara ya Maji wakiongozwa na Waziri wake Jumaa Aweso pamoja na katibu Mkuu wa wizara hiyo Mwajuma Waziri.
Huenda hii ikawa ni dallili njema kwa Watendaji wa Wizara ya Maji ya kukamilisha ahadi yam aji kufika kwa wananchi wa maeneo ya Same ,Mwanga na Korogwe ifikapo Mwezi Juni ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rai Dkt Samia Suluhu Hassan kupitia kwa Makamu wa Rais SDkt Philp Isdor Mpango .

Пікірлер

    Келесі