RAIS MWINYI: WANASIASA WASHINDANE KATIKA KULETA HUDUMA BORA ZA KIJAMII KWA WANANCHI

Ойын-сауық

PEMBA: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewataka wanasiasa kushindana kwa kuwaletea wananchi huduma bora za kijamii na kimaendeleo, badala ya kuleta hoja za uvunjifu wa amani. Akizungumza wakati wa makabidhiano na ufunguzi wa nyumba za Wafanyakazi wa Hospitali ya Abdullah Mzee, Mkoa wa Kusini Pemba tarehe 01 Julai 2024, Rais Mwinyi alisisitiza umuhimu wa kulinda na kudumisha amani nchini, hususani katika kipindi cha uchaguzi mkuu ujao.
Rais Mwinyi alieleza mafanikio ya serikali yake katika sekta ya afya, ikiwemo ujenzi wa hospitali katika kila wilaya na kuboresha huduma za kijamii. Aliahidi kuendelea kuboresha vituo vya afya na kujenga hospitali kubwa ya rufaa ya kimataifa ya Binguni. Aidha, aliishukuru Serikali ya China kwa msaada wake katika sekta ya afya, hususani kwa kufanikisha mradi wa nyumba za Wafanyakazi wa Hospitali ya Abdullah Mzee wenye gharama za shilingi bilioni 16.5 za kitanzania.
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: / spotileo-176. .
HabariLeo: / habarileo
DailyNews: / dailynewstz
INSTAGRAM;
HabariLeo: habarileo_tz?ig...
SpotiLeo: spotileo?igshid...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: HabariLeo?s=09

Пікірлер

    Келесі