MAJALIWA ATOA MAELEKEZO UJENZI SHULE YA WASICHANA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Iramba wilayani Mufindi ambayo inatarajiwa kugharimu sh. bilioni 1.78 hadi kukamilika kwake.
Gharama za ujenzi wa shule hiyo zinahusisha jengo la utawala moja, madarasa nane, ofisi nne, maabara tatu, chumba cha TEHAMA kimoja, nyumba za walimu tani za 2-in-1, bwalo la chakula moja na mabweni manne.
Akizungumza baada ya kufanya ukaguzi wa shule hiyo iliyopo katika kijiji cha Iramba, kata ya Itandula, wilayani Mufindi, mkoani Iringa, leo mchana (Jumapili, Julai 07, 2024), Waziri Mkuu amewapongeza madiwani kwa wazo lao la kutenga fedha na kujenga mradi huo.
Waziri Mkuu ambaye yuko mkoani Iringa kwa ziara ya kikazi ya siku nne, ameitaka Halmashauri hiyo iendelee kubaini vyanzo vitakavyoongeza fedha ili waweze kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo. “Moja kati ya mapungufu ya baadhi ya Halmashauri ni kutotumia fedha za ndani kujenga miradi inayoonekana, ujenzi wa shule hii ni mfano wa kuigwa na Halmashauri zote, ongezeni kasi ya mkamilishe mradi huu kwa wakati.”
Pia amewataka watumie vizuri fedha iliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo ili miundombinu yote itakayojengwa iendane na fedha iliyotolewa. “Fanyeni mapitio ya fedha mliyopanga kutumia kwa ajili ya kujenga nyumba za walimu, shilingi milioni 100 ni nyingi kwa nyumba moja.”
Pia ameagiza madawati yote ambayo hayana eneo la kuweka daftari kwa ajili ya wanafunzi yaondolewe na kurudishwa kwa fundi kwa sababu hayakidhi viwango vya madawati ya shule za msingi na sekondari.
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: / spotileo-176. .
HabariLeo: / habarileo
DailyNews: / dailynewstz
INSTAGRAM;
HabariLeo: habarileo_tz?ig...
SpotiLeo: spotileo?igshid...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: HabariLeo?s=09

Пікірлер

    Келесі