Dizasta Vina - Tattoo ya asili
Музыка
A video lyrics of Dizasta Vina perfoming Tatoo ya asili
off the album The Verteller
Stream and download Tatuu ya asili Audio
Mdundo - mdundo.com/song/2081292
Boomplay - www.boomplay.com/songs/635535...
Spotify - open.spotify.com/track/3TrnMl...
Audiomack - audiomack.com/dizastavina/son...
Apple Music - music.apple.com/us/album/tato...
Lyrics - genius.com/Dizasta-vina-tatoo...
Other contents
Audiomack - audiomack.com/dizastavina
Boom play - www.boomplay.com/artists/3288611
Mdundo - mdundo.com/a/2263
Spotify - open.spotify.com/artist/1IC2b...
Apple music - / dizasta-vina
Connect with Dizasta Vina on social medias
Instagram - / dizastavina
Twitter - / dizastavina
Facebook - / dizastavina07
sw.wikipedia.org/wiki/Dizasta...
Business: Pan.authentik@yahoo.com
Website - bio.link/dizastavina
Lyrics
Amezongwa na zimwi
Alisikia jirani akitoa hoja kwa kijiji
Sababu ya kukosa elimu ya maambukizi
Walihisi kurogwa ndio sababu ya gonjwa la Ukimwi
Huyo ni mgonjwa jamani
kama wagonjwa wengine alisema mwalimu
Mwenyekiti alimwambia kaa kimya
Sio unaropoka kama mwendawazimu
Elimu ya mwalimu ilikuwa nuru potevu
Nuru ambayo haifiki gizani
Ikawekwa idhini mezani kuuwa mizimu imechukia
Mgonjwa afukuzwe kijiji cha mbali
Akasindikizwa njiapanda
Mwisho wa kijiji mwanzo wa msitu mkubwa wa Sanza
Alitengwa kama walivyotengwa wengi
Kwa mila na desturi zilizoanza tangu enzi
Kibuyu cha maji furushi la matunda
Na makubazi yaliyoalika funza
Hakuna hodi inapofika kiama
Mama na nyika nyika na mama
Na alikuwa peke yake na ule mzigo mdogo mgongoni
Wasiwasi usoni mtoto tumboni
Alitamani matawi yaanguke yamtunze
Dhidi ya baridi ya mji uliosahaulika na Wabunge
Umauti aliuhisi
Alijitazama na hakuona tofauti na maiti
Alilia peke yake porini huku sauti yake
Ikisindikizwa na sauti za fisi
Wadudu wenye sumu nyingi walimvizia
Alikutana na visiki alipotaka njia
Mvua kubwa ilinyesha kuonyesha
Hata hali ya hewa ilimsaliti pia
Alivuka salama mpaka ng'ambo
Akajikongoja mpaka kando
Kando kwenye mti mkubwa uchungu ulimshika
Alizaliwa mtoto mdogo huku mama anakufa
Ujinga uliotamalaki kwa kijiji
Ndio ujinga uliomnyima haki ya kuishi
Alipambana mpaka ilifika tamati Pumzi
Akamwacha mwanae na zawadi ya virusi
Natoa nukuu kariri
Mtoto alifunikwa na nguo kuu kuu kwenye mwili
Alikuwa na madoa makuu mawili
Katikati ya mgongo mfano wa tatuu ya asili
Ninatokwa na mate
Alisikika kijana akitoa hoja kwa wenzake
Waliopanga foleni kwenye chumba chenye mwanga
Hafifu kila mmoja akiingoja zamu yake
Walikuwa vijana sita wenye umri wa shule
Usipojua thamani utahisi wanaivuta pumzi ya bure
Alilala msichana kati ya hawa
Kwenye matandiko machafu yalioarika chawa
Jamani huyu ni mtoto bado
Alisikika mmoja aliyeegemea ndoo ndogo kando
Walimfokea alipokataa kushiriki tukio
Wakimfananisha na Mbwa asiyevuka uzio
Walimvua msichana nguo zake za mwili
Walimpiga alipojaribu kuficha sehemu zake za siri
Alibakwa kama walivyobakwa wengi
Kwa tabia za vijana zilizoanza tangu enzi
Hawakujua kuhusu mpaka wa hamu
Halali na haramu kila mmoja alimbaka kwa zamu
Alitendewa uasi
Kwa vijana walioshindwa kulelewa na wazazi
Mfano wa mlo wa hija walimfakamia
Aliliona giza alipotaka njia
Alisema imetosha ila hakuna aliyemsikia
Maana wengine dada zao walibakwa pia
Alitakiwa awe nyumbani labda
Kalala kakumbatia Mwanasesere kitandani labda
Alilia na sauti yake haikukidhi
Kwa sababu hata mji ulisahaulika na polisi
Msimuliaji toka chini nalia juu
Nasimulia yaliyotukia huruma inaniingia
Lakini sina cha kufanya kwa sababu
Kazi yangu mi' kusimulia tu
Kuta zingeongea zingeusema huu ukatili
Wa maumivu ya juu ya mwili
Kuta zingesema alikuwa na madoa makuu mawili
Kati' ya mgongo mfano wa tatuu ya asili
Пікірлер: 280
Ali said It's not bragging if you can back it up and this one definitely cements it !! " Talk about story telling, look at my damn halo Sequel zako nyepesi, you're not ready bado " " Naweza kufanya uhisi unaexperience msosi Baada ya njaa kali, mi ni Shakespearean ghost " 😂🤝🏾 And Ringle knows how to deal the cards right
Ingekuwa ni maamuzi yangu, Ningekupa Udaktari wa heshima na ungekuwa mkuu idara ya Sanaa bunifu pale Chuo Kikuu cha Dar es salaam
Hiiiiiiiii ndy nyimbo yenye story za books na kupata maswali mengi San kuhusu elimu iliopo🫂 ahsant dizasta vina Kwa elimu simuliz🙏🙏
Enyi watoto mnaosikiliza hii nyimbo mwaka Huu 2043... Dizasta Vina was a great artist hatuwahi kupata Tanzania
Hii ngoma imefichwaa sana wanaoamini ilo gonga like alafu tusubili review ya huu wimbo
@drmubarakhassan8010
Жыл бұрын
NI SERA ya mwalimu NYERERE adui watatu . ujinga maradhi na umasikini. ila Vina ametumia maradhi ukimwi doa la tatu mawili kati ya mgongo ni ujinga na umasikini. paia ameihusisha na jinsi mambo hayo na ukimwi ulivyoingia tz. then utagudua anasema msimuliaji natoka chini naenda juu, verse ya pili ndio mwanzo wa story. kwa ufupi tu japo kuna mengi ya kufafanua na kujifunza.
@mosesharrison5233
Жыл бұрын
@drmubarakhassan8010 verse ya pili ndo mwisho wa story ni yule mtoto mchanga amekua na kaishia kupitia kile kile kilichomkuta mama yake
Hichi kichwa kiko sawa...much love frm 🇶🇦🇶🇦
Mimi ni shabiki Yako mpya from Burundi 🇧🇮 +257 Bro mimi umeniacha mbali sana yani ngoma zako nimeziskia mpaka naanza tumia makamusi tu we ni Genius ❤ Respect Dizasta Vina ❤
Hujawahi kuniangusha kaka 🙌🏽📌ukiona leo sauti yako haitoki vizuri basi chanzo ni Mimi huku nimeweka repeat 🧷👊🏼🙌🏽
Dizasta kwenye ubora wake💪
Mwamba cna muda mrefu tangu nianze kukufatilia unajua sana japo ngoma zako nazozijua 3 Africa, Uhuru na wimbo huu ww co mtu wa kawaida ili mtu akuelewe inatakiwa acklize wimbo wako zaidi ya Mara moja ule wimbo wa Africa ulnixumbua sana kuuelewa
Dizasta uko juu zaid kuwa na subra na zid kukaza nlikwelewa tang wayback man.
Mimi huwa sijutii kukupa skio langu unanibless sana 🙏🏼
Pamoja msimuliaji. Kazi nzuri💪
Kak unatishaaa hii ngom nilskia kat kat nikaomba ianzee upyaaa kak hii 🔥🔥🔥
Dizasta vina ni msanii ambae kila neno linalomoka unatamani kuendelea kusikia neno gan lingine linalo fata,,kiufipi jamaa niaatali sana
Dizasta vina nimeskiliza Zaid ya mara tano🔥🔥🔥🔥🔥
anaishi kwenye anga ambayo ni miungu2 wanasettle👊
Hongera sana kazi nzuri
Bro Your talent is unique kwangu mimi wewe ni musician GOAT
Unaweza kusema vina katumia miaka 5 kutunga hii nyimbo kumbe kwake ni simple tu PURE TALENTS
Ukiachana na ufundi wa sanaa ya utunzi, ni msanii asie fuata mkumbo wa kuSwitch Genre🔥🙌 JASIRI HAIACHI ASILI.
@sebastianlubava1535
Жыл бұрын
na ndio rapa mwenye tatoo ya asil dunian
@TheRealAtomeec55.
Жыл бұрын
@@sebastianlubava1535 heheh😂 Maan ni ngum sana kuipata tattoo iyo kwa various artists hakika🔥🙌
@ibrangala7753
Жыл бұрын
Apa kenya🇰🇪 twamsikiza sana uyo mwamba
@detlantamarooned1809
Жыл бұрын
@@ibrangala7753tuko pamoja sana ndugu.
Tatoo ya asili...vicious cycle of HIV/AIDS, dizasta umetisha sna,napendekeza gvn wakuweke ktk watunzi wa mashairi ya kufundishia ....uko level moja na chinua achebe💪🏾
Ya kikubwa Sana hii mzee wangu
Hakika dizasta kwangu ndo mwan hip-hop was Karne ya20
Sana broooo nakubali kaka
still listening na sijasikia bado... tuelewane sijasikia zaid ya dizasta
Nakubali dizasta hukosei man
Huyuuu jamaaaaa mbn mwamba sana akili ako si ya kawaida kabisa duuuuuuh
Duuh noma Sanaa nataman siku Moja niweze kupita vizuri Kama wewe bro aisee unajua sanaa🔥🔥🔥
Hii ngoma n nomaaaa🎉🎉
Shika .maua yako kaka 🌹🌹
Brother Una Akili Ambayo Ni Ya Kizazi Cha 2090 Huko Ndiyo Watakuja Elewa Nini Unafanya. 🙌🏼🙌🏼🙌🏼🙌🏼
Duuuuh wewe jamaa una kichwa
We jamaabunaandika sana yaaani kama movie
Found genius and gifted forever...hebu BASATA ifanye kitu kwak we Jamaa 🥺 you are a really meaning of pure literature... you're beyond Chomsky, ole soyenka,ngungi wa thiongo,chinue achebe and okoit p'bitek 🙌🙌
Kudadeq 🙌 jamaa una madini sanaaaa. Hii ndo tunaita sanaa. Una utofauti mkubwa na ma rapper au wasanii wengine hakika. Huu wimbo nime u Shazam mtaani ikabidi nifatilie
Embu tuamue sisi kama mashabiki tuifikishe trending za juu zaidi haya twende kazi, share as much as u can watu wanatakiwa wasikie hizi sumu zenye darasa ndani yake
Unawakilisha jina💥🙌🏿
King wa hizi kazi aka teacher big endelea ku2pa darasa wao waendelee kucheza amapiano🙌🙌🙌
Wa kwanza gonga like
Kk tuko pamojaaaa d vina
Daah!kuna BinaadamU wamepewana Mungu walichostahili
Hahahaaaa mwamba sana,So genius Brother.Kwa tunaokuelewa "To be continued........."Bonge moja la Muvie daaah.
My Idol best story teller
Kuhusu huyu Dizasta Vina mimi sina la kusema tena, that's very sure,Dizasta ni wa moto kushinda Jua.
napenda sana hizi stori yani unajua na unajua tena
Nmesubiri tattoo ya asili namba 2 itapendezaa zaidi kwa tunaokufuatilia I expect higher from Vina rymes
Big love from 254 watu wangekuangalia kwa jicho la tatu
Kaka respect kubwa kwako dah akili nyingi ndo unaweza elewa hili goma
Kaka umekua mtu flan ivii ambaye Kila siku huchokw kisikilizwa,umenikubusha namna ya kuish 🙏🙏🙏🙏🔥🔥🔥 appreciate sanaaa
Dah... fumbo hili embu niludia hata mara kumi
Aiseee hawakukosea walio kuita VINA ✊🏾
nakubali sana @dizasta vina kazi nzuri
Aisee d.. noma sana
huu wimbo haujaisha, kabisa yani🙌🏾🙌🏾
Daaah mashair yako unayaficha sana lazima utulize kichwa ndo uelewe.
Umetisha bro
*Akazindikizwa njia panda mwisho wa makazi mwanzo wa msitu mkubwa wa sanza" fasihi Kali zipo umuu hii n chakula ya ubongoo kweliiiii kaka🧠🧠
Kuna abalikuu kutoka kwa kitaa flani, mistari kama nimetafuna daftari. Dah bado bongo sjaiona mwana hip hop kama uyu🔬
Hunaga kazi mbovu mzee
Nakubali sana njia zako bro ubarikiwe
Who narrates better than DIZASTA, I think the answer is no one like VINA
Mama na nyika nyika na mama🧏🧏
Kaka unafanya mziki waheshima sana wenye mafundixho katika jamii ...naomba utengweeh 🔥🔥 mana una upeo na frikra za tofauti 🙌🙌
Kama Kawa hujainiangusha. Big up dizasta. Tour Kenya please
Dah nilijua flashback kumbe dogo alikuja kubakwa tena probably na wajombazake, maana nao dada zao waliwah kubakwa na alieendq kufia porin probably alibàkwa
Damn, broh. so conscious.
Kaka huna dhambi nautakapokufa hakika hautaoza@vina🙏🙏🙏
Ticha leo nimetoka patupu ngoja nisikilize tena
Hawakujua kuhusu mpaka wa hamu
Hip hop kwenye mikono salama 🔥🔥🔥🔥
Nomaa
nakukubar mkuu ❤
Afu juzi tu nilikuwa naiifikiriaa. One of the best track kwenye collection za Dizasta🙌. Ringle ametisha sanaaa kwenyehii DARK Beat. Mvua kubwa ILINYESHA, KUONESHA , hata HALI YA HEWA ILIMSALITI PIAA."
Kwakua ukuta ulificha kitendo hiki basi ni siku pekee zitawaambia ukweli pindi dalili zitapowakumbusha kuwa siku walipobaka nao waliachiwa zawadi ya virusi. Only Dizasta vina can do this killing lines💯🔥🔥
@inocentmpina4850
9 ай бұрын
❤
Mya favorite song
Nakubali
My favorite singer, I'm learning more from this guy.🇲🇿🇲🇿
20100 I'm commenting here just to inspire all of you that hip hop is lesson 🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏
D teacher🙌🙌
Dizasta vina kabla ujafa ushaacha chata ukutani ambayo aifutiki zaidi ya tattoo ya asiri
Very genius Dizasta,...The best story teller, but huu wimbo umenifikirisha sana kuuelewa🤔🤔🔥🔥🔥
Dizasta Vinaaaaaaa unatisha kama radiation congratulations Brother nakubali lecture zakoooooo🎉🎉🎉🎉
Wee jamaaa noma sana bhna
Dizasta ni mwamba wa rap bongo nzima
Haujawahi nianggusha bro 🎉🎉🎉🎉🎉wanom🎉🎉
moja ya ngoma ambayo hua naisikiliza bila kuchoka "shahidi" now umekuja na kitu kipya mithili ile ya shahidi keep up bro umetisha sana vina👍👍
Dizasta mwenye vina vyake black Maradona we ndo king Wang wa hii game bongo
Bro your a genius, this is art in its purest form.
@dizastavina
Жыл бұрын
Thank you so much
@mdudamotorc9600
Жыл бұрын
Cjawah kuona genius wa song like you najuta kuchelewa kujua😭😭
@mdudamotorc9600
Жыл бұрын
@@dizastavina najuta kuchelewa kukujua we ni genius Mr good song
ifike mahali dizasta na nacha wapewe tuzo jaman, hawa wanoibeba maana halisi ya sanaa kwenye jamii
Muungano wa tangnyka na zenji.nipeni likes zangu bac
Promo wanapewa mafara ... Sharout brooo🙌🙌
Ahsante Sana kwa mistari yenye fikra pevu🙌🙌🙌
Alafu kuna wasuka suka nywele wanajifananisha na hii talent huyu jamaa ni genius , nakubali uwezo wako nigah.
What a genius from this man always i support u since day one
Kaka umetisha🙌
Brooh nakukubali sana vina vyako vimenyooka sana
Ukimwi upo, ukimwi unaua
💥🏝💥
Brother anajua sana sema anamafumbo sana