Dizasta Vina - Tattoo ya asili

Музыка

A video lyrics of Dizasta Vina perfoming Tatoo ya asili
off the album The Verteller
Stream and download Tatuu ya asili Audio
Mdundo - mdundo.com/song/2081292
Boomplay - www.boomplay.com/songs/635535...
Spotify - open.spotify.com/track/3TrnMl...
Audiomack - audiomack.com/dizastavina/son...
Apple Music - music.apple.com/us/album/tato...
Lyrics - genius.com/Dizasta-vina-tatoo...
Other contents
Audiomack - audiomack.com/dizastavina
Boom play - www.boomplay.com/artists/3288611
Mdundo - mdundo.com/a/2263
Spotify - open.spotify.com/artist/1IC2b...
Apple music - / dizasta-vina
Connect with Dizasta Vina on social medias
Instagram - / dizastavina
Twitter - / dizastavina
Facebook - / dizastavina07
sw.wikipedia.org/wiki/Dizasta...
Business: Pan.authentik@yahoo.com
Website - bio.link/dizastavina
Lyrics
Amezongwa na zimwi
Alisikia jirani akitoa hoja kwa kijiji
Sababu ya kukosa elimu ya maambukizi
Walihisi kurogwa ndio sababu ya gonjwa la Ukimwi
Huyo ni mgonjwa jamani
kama wagonjwa wengine alisema mwalimu
Mwenyekiti alimwambia kaa kimya
Sio unaropoka kama mwendawazimu
Elimu ya mwalimu ilikuwa nuru potevu
Nuru ambayo haifiki gizani
Ikawekwa idhini mezani kuuwa mizimu imechukia
Mgonjwa afukuzwe kijiji cha mbali
Akasindikizwa njiapanda
Mwisho wa kijiji mwanzo wa msitu mkubwa wa Sanza
Alitengwa kama walivyotengwa wengi
Kwa mila na desturi zilizoanza tangu enzi
Kibuyu cha maji furushi la matunda
Na makubazi yaliyoalika funza
Hakuna hodi inapofika kiama
Mama na nyika nyika na mama
Na alikuwa peke yake na ule mzigo mdogo mgongoni
Wasiwasi usoni mtoto tumboni
Alitamani matawi yaanguke yamtunze
Dhidi ya baridi ya mji uliosahaulika na Wabunge
Umauti aliuhisi
Alijitazama na hakuona tofauti na maiti
Alilia peke yake porini huku sauti yake
Ikisindikizwa na sauti za fisi
Wadudu wenye sumu nyingi walimvizia
Alikutana na visiki alipotaka njia
Mvua kubwa ilinyesha kuonyesha
Hata hali ya hewa ilimsaliti pia
Alivuka salama mpaka ng'ambo
Akajikongoja mpaka kando
Kando kwenye mti mkubwa uchungu ulimshika
Alizaliwa mtoto mdogo huku mama anakufa
Ujinga uliotamalaki kwa kijiji
Ndio ujinga uliomnyima haki ya kuishi
Alipambana mpaka ilifika tamati Pumzi
Akamwacha mwanae na zawadi ya virusi
Natoa nukuu kariri
Mtoto alifunikwa na nguo kuu kuu kwenye mwili
Alikuwa na madoa makuu mawili
Katikati ya mgongo mfano wa tatuu ya asili
Ninatokwa na mate
Alisikika kijana akitoa hoja kwa wenzake
Waliopanga foleni kwenye chumba chenye mwanga
Hafifu kila mmoja akiingoja zamu yake
Walikuwa vijana sita wenye umri wa shule
Usipojua thamani utahisi wanaivuta pumzi ya bure
Alilala msichana kati ya hawa
Kwenye matandiko machafu yalioarika chawa
Jamani huyu ni mtoto bado
Alisikika mmoja aliyeegemea ndoo ndogo kando
Walimfokea alipokataa kushiriki tukio
Wakimfananisha na Mbwa asiyevuka uzio
Walimvua msichana nguo zake za mwili
Walimpiga alipojaribu kuficha sehemu zake za siri
Alibakwa kama walivyobakwa wengi
Kwa tabia za vijana zilizoanza tangu enzi
Hawakujua kuhusu mpaka wa hamu
Halali na haramu kila mmoja alimbaka kwa zamu
Alitendewa uasi
Kwa vijana walioshindwa kulelewa na wazazi
Mfano wa mlo wa hija walimfakamia
Aliliona giza alipotaka njia
Alisema imetosha ila hakuna aliyemsikia
Maana wengine dada zao walibakwa pia
Alitakiwa awe nyumbani labda
Kalala kakumbatia Mwanasesere kitandani labda
Alilia na sauti yake haikukidhi
Kwa sababu hata mji ulisahaulika na polisi
Msimuliaji toka chini nalia juu
Nasimulia yaliyotukia huruma inaniingia
Lakini sina cha kufanya kwa sababu
Kazi yangu mi' kusimulia tu
Kuta zingeongea zingeusema huu ukatili
Wa maumivu ya juu ya mwili
Kuta zingesema alikuwa na madoa makuu mawili
Kati' ya mgongo mfano wa tatuu ya asili

Пікірлер: 280

  • @_jizy
    @_jizy11 ай бұрын

    Ali said It's not bragging if you can back it up and this one definitely cements it !! " Talk about story telling, look at my damn halo Sequel zako nyepesi, you're not ready bado " " Naweza kufanya uhisi unaexperience msosi Baada ya njaa kali, mi ni Shakespearean ghost " 😂🤝🏾 And Ringle knows how to deal the cards right

  • @alphaabdallah1406
    @alphaabdallah1406 Жыл бұрын

    Ingekuwa ni maamuzi yangu, Ningekupa Udaktari wa heshima na ungekuwa mkuu idara ya Sanaa bunifu pale Chuo Kikuu cha Dar es salaam

  • @shaibinhojr3209
    @shaibinhojr3209 Жыл бұрын

    Hiiiiiiiii ndy nyimbo yenye story za books na kupata maswali mengi San kuhusu elimu iliopo🫂 ahsant dizasta vina Kwa elimu simuliz🙏🙏

  • @pinecompilation5631
    @pinecompilation5631 Жыл бұрын

    Enyi watoto mnaosikiliza hii nyimbo mwaka Huu 2043... Dizasta Vina was a great artist hatuwahi kupata Tanzania

  • @Chimgege
    @Chimgege Жыл бұрын

    Hii ngoma imefichwaa sana wanaoamini ilo gonga like alafu tusubili review ya huu wimbo

  • @drmubarakhassan8010

    @drmubarakhassan8010

    Жыл бұрын

    NI SERA ya mwalimu NYERERE adui watatu . ujinga maradhi na umasikini. ila Vina ametumia maradhi ukimwi doa la tatu mawili kati ya mgongo ni ujinga na umasikini. paia ameihusisha na jinsi mambo hayo na ukimwi ulivyoingia tz. then utagudua anasema msimuliaji natoka chini naenda juu, verse ya pili ndio mwanzo wa story. kwa ufupi tu japo kuna mengi ya kufafanua na kujifunza.

  • @mosesharrison5233

    @mosesharrison5233

    Жыл бұрын

    ​@drmubarakhassan8010 verse ya pili ndo mwisho wa story ni yule mtoto mchanga amekua na kaishia kupitia kile kile kilichomkuta mama yake

  • @stevewanga957
    @stevewanga957 Жыл бұрын

    Hichi kichwa kiko sawa...much love frm 🇶🇦🇶🇦

  • @ghyldinhoclassic9635
    @ghyldinhoclassic96352 ай бұрын

    Mimi ni shabiki Yako mpya from Burundi 🇧🇮 +257 Bro mimi umeniacha mbali sana yani ngoma zako nimeziskia mpaka naanza tumia makamusi tu we ni Genius ❤ Respect Dizasta Vina ❤

  • @jemedalibasama5000
    @jemedalibasama5000 Жыл бұрын

    Hujawahi kuniangusha kaka 🙌🏽📌ukiona leo sauti yako haitoki vizuri basi chanzo ni Mimi huku nimeweka repeat 🧷👊🏼🙌🏽

  • @MackLaueent-tg7si
    @MackLaueent-tg7si Жыл бұрын

    Dizasta kwenye ubora wake💪

  • @abdurahmnsobo4810
    @abdurahmnsobo481011 ай бұрын

    Mwamba cna muda mrefu tangu nianze kukufatilia unajua sana japo ngoma zako nazozijua 3 Africa, Uhuru na wimbo huu ww co mtu wa kawaida ili mtu akuelewe inatakiwa acklize wimbo wako zaidi ya Mara moja ule wimbo wa Africa ulnixumbua sana kuuelewa

  • @kingrasdee445
    @kingrasdee445 Жыл бұрын

    Dizasta uko juu zaid kuwa na subra na zid kukaza nlikwelewa tang wayback man.

  • @kelvinlugono6513
    @kelvinlugono6513 Жыл бұрын

    Mimi huwa sijutii kukupa skio langu unanibless sana 🙏🏼

  • @raphaelboniventus7215
    @raphaelboniventus7215 Жыл бұрын

    Pamoja msimuliaji. Kazi nzuri💪

  • @fahadjoseph
    @fahadjoseph Жыл бұрын

    Kak unatishaaa hii ngom nilskia kat kat nikaomba ianzee upyaaa kak hii 🔥🔥🔥

  • @Shortbtz
    @Shortbtz8 ай бұрын

    Dizasta vina ni msanii ambae kila neno linalomoka unatamani kuendelea kusikia neno gan lingine linalo fata,,kiufipi jamaa niaatali sana

  • @KazeLona
    @KazeLona Жыл бұрын

    Dizasta vina nimeskiliza Zaid ya mara tano🔥🔥🔥🔥🔥

  • @jumasamir7317
    @jumasamir7317 Жыл бұрын

    anaishi kwenye anga ambayo ni miungu2 wanasettle👊

  • @badloso1049
    @badloso1049 Жыл бұрын

    Hongera sana kazi nzuri

  • @CharmingCharlz
    @CharmingCharlz8 ай бұрын

    Bro Your talent is unique kwangu mimi wewe ni musician GOAT

  • @kiduaalute603
    @kiduaalute603 Жыл бұрын

    Unaweza kusema vina katumia miaka 5 kutunga hii nyimbo kumbe kwake ni simple tu PURE TALENTS

  • @TheRealAtomeec55.
    @TheRealAtomeec55. Жыл бұрын

    Ukiachana na ufundi wa sanaa ya utunzi, ni msanii asie fuata mkumbo wa kuSwitch Genre🔥🙌 JASIRI HAIACHI ASILI.

  • @sebastianlubava1535

    @sebastianlubava1535

    Жыл бұрын

    na ndio rapa mwenye tatoo ya asil dunian

  • @TheRealAtomeec55.

    @TheRealAtomeec55.

    Жыл бұрын

    @@sebastianlubava1535 heheh😂 Maan ni ngum sana kuipata tattoo iyo kwa various artists hakika🔥🙌

  • @ibrangala7753

    @ibrangala7753

    Жыл бұрын

    Apa kenya🇰🇪 twamsikiza sana uyo mwamba

  • @detlantamarooned1809

    @detlantamarooned1809

    Жыл бұрын

    ​@@ibrangala7753tuko pamoja sana ndugu.

  • @pacojr9441
    @pacojr944111 ай бұрын

    Tatoo ya asili...vicious cycle of HIV/AIDS, dizasta umetisha sna,napendekeza gvn wakuweke ktk watunzi wa mashairi ya kufundishia ....uko level moja na chinua achebe💪🏾

  • @samwelalphonce6326
    @samwelalphonce6326 Жыл бұрын

    Ya kikubwa Sana hii mzee wangu

  • @DaudiAntony
    @DaudiAntony Жыл бұрын

    Hakika dizasta kwangu ndo mwan hip-hop was Karne ya20

  • @FadhiliSolomoni-jr6rs
    @FadhiliSolomoni-jr6rs Жыл бұрын

    Sana broooo nakubali kaka

  • @daudisinani8342
    @daudisinani8342 Жыл бұрын

    still listening na sijasikia bado... tuelewane sijasikia zaid ya dizasta

  • @abdfattah883
    @abdfattah883 Жыл бұрын

    Nakubali dizasta hukosei man

  • @princenzago5234
    @princenzago523411 ай бұрын

    Huyuuu jamaaaaa mbn mwamba sana akili ako si ya kawaida kabisa duuuuuuh

  • @therealevah7775
    @therealevah777511 ай бұрын

    Duuh noma Sanaa nataman siku Moja niweze kupita vizuri Kama wewe bro aisee unajua sanaa🔥🔥🔥

  • @barikinehemiah170
    @barikinehemiah170 Жыл бұрын

    Hii ngoma n nomaaaa🎉🎉

  • @thobiasmtakatifu3174
    @thobiasmtakatifu3174 Жыл бұрын

    Shika .maua yako kaka 🌹🌹

  • @Mbeyaconscious
    @Mbeyaconscious Жыл бұрын

    Brother Una Akili Ambayo Ni Ya Kizazi Cha 2090 Huko Ndiyo Watakuja Elewa Nini Unafanya. 🙌🏼🙌🏼🙌🏼🙌🏼

  • @enockkasunzu8937
    @enockkasunzu8937 Жыл бұрын

    Duuuuh wewe jamaa una kichwa

  • @africanasplumbing8780
    @africanasplumbing8780 Жыл бұрын

    We jamaabunaandika sana yaaani kama movie

  • @marcodavid7448
    @marcodavid7448 Жыл бұрын

    Found genius and gifted forever...hebu BASATA ifanye kitu kwak we Jamaa 🥺 you are a really meaning of pure literature... you're beyond Chomsky, ole soyenka,ngungi wa thiongo,chinue achebe and okoit p'bitek 🙌🙌

  • @usafirionline4465
    @usafirionline44658 ай бұрын

    Kudadeq 🙌 jamaa una madini sanaaaa. Hii ndo tunaita sanaa. Una utofauti mkubwa na ma rapper au wasanii wengine hakika. Huu wimbo nime u Shazam mtaani ikabidi nifatilie

  • @daudisinani8342
    @daudisinani8342 Жыл бұрын

    Embu tuamue sisi kama mashabiki tuifikishe trending za juu zaidi haya twende kazi, share as much as u can watu wanatakiwa wasikie hizi sumu zenye darasa ndani yake

  • @nicokimario3791
    @nicokimario3791 Жыл бұрын

    Unawakilisha jina💥🙌🏿

  • @selemankilango246
    @selemankilango246 Жыл бұрын

    King wa hizi kazi aka teacher big endelea ku2pa darasa wao waendelee kucheza amapiano🙌🙌🙌

  • @radothehacker4489
    @radothehacker4489 Жыл бұрын

    Wa kwanza gonga like

  • @komboally8600
    @komboally8600 Жыл бұрын

    Kk tuko pamojaaaa d vina

  • @jaymapambanojuma856
    @jaymapambanojuma856 Жыл бұрын

    Daah!kuna BinaadamU wamepewana Mungu walichostahili

  • @KingJacka_MwanaNzambe_
    @KingJacka_MwanaNzambe_11 ай бұрын

    Hahahaaaa mwamba sana,So genius Brother.Kwa tunaokuelewa "To be continued........."Bonge moja la Muvie daaah.

  • @roberthonjovu6045
    @roberthonjovu6045 Жыл бұрын

    My Idol best story teller

  • @detlantamarooned1809
    @detlantamarooned1809 Жыл бұрын

    Kuhusu huyu Dizasta Vina mimi sina la kusema tena, that's very sure,Dizasta ni wa moto kushinda Jua.

  • @cobwaafri
    @cobwaafri11 ай бұрын

    napenda sana hizi stori yani unajua na unajua tena

  • @alphoncesamwel6973
    @alphoncesamwel6973 Жыл бұрын

    Nmesubiri tattoo ya asili namba 2 itapendezaa zaidi kwa tunaokufuatilia I expect higher from Vina rymes

  • @aishaobo6186
    @aishaobo6186 Жыл бұрын

    Big love from 254 watu wangekuangalia kwa jicho la tatu

  • @emiliangasto9467
    @emiliangasto9467 Жыл бұрын

    Kaka respect kubwa kwako dah akili nyingi ndo unaweza elewa hili goma

  • @youngcee3145
    @youngcee3145 Жыл бұрын

    Kaka umekua mtu flan ivii ambaye Kila siku huchokw kisikilizwa,umenikubusha namna ya kuish 🙏🙏🙏🙏🔥🔥🔥 appreciate sanaaa

  • @youngtone4333
    @youngtone4333 Жыл бұрын

    Dah... fumbo hili embu niludia hata mara kumi

  • @amanimushi4052
    @amanimushi4052 Жыл бұрын

    Aiseee hawakukosea walio kuita VINA ✊🏾

  • @UPCOMINGWHALE
    @UPCOMINGWHALE Жыл бұрын

    nakubali sana @dizasta vina kazi nzuri

  • @Dancheba_tz
    @Dancheba_tz Жыл бұрын

    Aisee d.. noma sana

  • @allenmushema5844
    @allenmushema5844 Жыл бұрын

    huu wimbo haujaisha, kabisa yani🙌🏾🙌🏾

  • @rajabmpamwa9051
    @rajabmpamwa9051 Жыл бұрын

    Daaah mashair yako unayaficha sana lazima utulize kichwa ndo uelewe.

  • @user-rj2sz8vb6u
    @user-rj2sz8vb6u Жыл бұрын

    Umetisha bro

  • @josureabely8899
    @josureabely8899 Жыл бұрын

    *Akazindikizwa njia panda mwisho wa makazi mwanzo wa msitu mkubwa wa sanza" fasihi Kali zipo umuu hii n chakula ya ubongoo kweliiiii kaka🧠🧠

  • @user-op7wy8rk4l
    @user-op7wy8rk4l Жыл бұрын

    Kuna abalikuu kutoka kwa kitaa flani, mistari kama nimetafuna daftari. Dah bado bongo sjaiona mwana hip hop kama uyu🔬

  • @afterx3172
    @afterx3172 Жыл бұрын

    Hunaga kazi mbovu mzee

  • @seangraceswt8037
    @seangraceswt80378 ай бұрын

    Nakubali sana njia zako bro ubarikiwe

  • @azaboicomedy
    @azaboicomedy11 ай бұрын

    Who narrates better than DIZASTA, I think the answer is no one like VINA

  • @nyikaummary814
    @nyikaummary814 Жыл бұрын

    Mama na nyika nyika na mama🧏🧏

  • @chrispinhenry3362
    @chrispinhenry3362 Жыл бұрын

    Kaka unafanya mziki waheshima sana wenye mafundixho katika jamii ...naomba utengweeh 🔥🔥 mana una upeo na frikra za tofauti 🙌🙌

  • @batatatheog5256
    @batatatheog5256 Жыл бұрын

    Kama Kawa hujainiangusha. Big up dizasta. Tour Kenya please

  • @nyemomtwanga9449
    @nyemomtwanga9449 Жыл бұрын

    Dah nilijua flashback kumbe dogo alikuja kubakwa tena probably na wajombazake, maana nao dada zao waliwah kubakwa na alieendq kufia porin probably alibàkwa

  • @4x.Mafole
    @4x.Mafole Жыл бұрын

    Damn, broh. so conscious.

  • @michaelisolomon6059
    @michaelisolomon6059 Жыл бұрын

    Kaka huna dhambi nautakapokufa hakika hautaoza@vina🙏🙏🙏

  • @shepherdizotarimo8227
    @shepherdizotarimo8227 Жыл бұрын

    Ticha leo nimetoka patupu ngoja nisikilize tena

  • @mj.tv.forpeople992
    @mj.tv.forpeople992 Жыл бұрын

    Hawakujua kuhusu mpaka wa hamu

  • @scotawizzymrplanb
    @scotawizzymrplanb Жыл бұрын

    Hip hop kwenye mikono salama 🔥🔥🔥🔥

  • @hamzermahundu6371
    @hamzermahundu6371 Жыл бұрын

    Nomaa

  • @victorlutrac3667
    @victorlutrac3667 Жыл бұрын

    nakukubar mkuu ❤

  • @bennyframa4505
    @bennyframa4505 Жыл бұрын

    Afu juzi tu nilikuwa naiifikiriaa. One of the best track kwenye collection za Dizasta🙌. Ringle ametisha sanaaa kwenyehii DARK Beat. Mvua kubwa ILINYESHA, KUONESHA , hata HALI YA HEWA ILIMSALITI PIAA."

  • @inocentmpina4850
    @inocentmpina485011 ай бұрын

    Kwakua ukuta ulificha kitendo hiki basi ni siku pekee zitawaambia ukweli pindi dalili zitapowakumbusha kuwa siku walipobaka nao waliachiwa zawadi ya virusi. Only Dizasta vina can do this killing lines💯🔥🔥

  • @inocentmpina4850

    @inocentmpina4850

    9 ай бұрын

  • @musambaruku6661
    @musambaruku6661 Жыл бұрын

    Mya favorite song

  • @mataizytembo7043
    @mataizytembo7043 Жыл бұрын

    Nakubali

  • @Cabosport
    @Cabosport Жыл бұрын

    My favorite singer, I'm learning more from this guy.🇲🇿🇲🇿

  • @lutenganomwalivale754
    @lutenganomwalivale75411 ай бұрын

    20100 I'm commenting here just to inspire all of you that hip hop is lesson 🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏

  • @wamtei
    @wamtei Жыл бұрын

    D teacher🙌🙌

  • @Yuteman_Bigdon
    @Yuteman_Bigdon Жыл бұрын

    Dizasta vina kabla ujafa ushaacha chata ukutani ambayo aifutiki zaidi ya tattoo ya asiri

  • @frankaloyce6438
    @frankaloyce6438 Жыл бұрын

    Very genius Dizasta,...The best story teller, but huu wimbo umenifikirisha sana kuuelewa🤔🤔🔥🔥🔥

  • @gaddibullahtzg5635
    @gaddibullahtzg5635 Жыл бұрын

    Dizasta Vinaaaaaaa unatisha kama radiation congratulations Brother nakubali lecture zakoooooo🎉🎉🎉🎉

  • @leenashob7791
    @leenashob7791 Жыл бұрын

    Wee jamaaa noma sana bhna

  • @MashakaKilama-km5gm
    @MashakaKilama-km5gm Жыл бұрын

    Dizasta ni mwamba wa rap bongo nzima

  • @ojkolabo8737
    @ojkolabo8737 Жыл бұрын

    Haujawahi nianggusha bro 🎉🎉🎉🎉🎉wanom🎉🎉

  • @kashindemhapa2015
    @kashindemhapa2015 Жыл бұрын

    moja ya ngoma ambayo hua naisikiliza bila kuchoka "shahidi" now umekuja na kitu kipya mithili ile ya shahidi keep up bro umetisha sana vina👍👍

  • @user-so6fu3yb5z
    @user-so6fu3yb5z Жыл бұрын

    Dizasta mwenye vina vyake black Maradona we ndo king Wang wa hii game bongo

  • @mosesharrison5233
    @mosesharrison5233 Жыл бұрын

    Bro your a genius, this is art in its purest form.

  • @dizastavina

    @dizastavina

    Жыл бұрын

    Thank you so much

  • @mdudamotorc9600

    @mdudamotorc9600

    Жыл бұрын

    Cjawah kuona genius wa song like you najuta kuchelewa kujua😭😭

  • @mdudamotorc9600

    @mdudamotorc9600

    Жыл бұрын

    @@dizastavina najuta kuchelewa kukujua we ni genius Mr good song

  • @jacobmaganga3354
    @jacobmaganga3354 Жыл бұрын

    ifike mahali dizasta na nacha wapewe tuzo jaman, hawa wanoibeba maana halisi ya sanaa kwenye jamii

  • @husseinabdi3377
    @husseinabdi3377 Жыл бұрын

    Muungano wa tangnyka na zenji.nipeni likes zangu bac

  • @mosesshayo1733
    @mosesshayo173311 ай бұрын

    Promo wanapewa mafara ... Sharout brooo🙌🙌

  • @johnngitta369
    @johnngitta369 Жыл бұрын

    Ahsante Sana kwa mistari yenye fikra pevu🙌🙌🙌

  • @nyamwezkid1431
    @nyamwezkid1431 Жыл бұрын

    Alafu kuna wasuka suka nywele wanajifananisha na hii talent huyu jamaa ni genius , nakubali uwezo wako nigah.

  • @RamadhanSwalehe-dw6oh
    @RamadhanSwalehe-dw6oh Жыл бұрын

    What a genius from this man always i support u since day one

  • @user-rh8wt9nb2p
    @user-rh8wt9nb2p Жыл бұрын

    Kaka umetisha🙌

  • @Yo_tune-tb5sn
    @Yo_tune-tb5sn Жыл бұрын

    Brooh nakukubali sana vina vyako vimenyooka sana

  • @dullywamashairi121
    @dullywamashairi121 Жыл бұрын

    Ukimwi upo, ukimwi unaua

  • @Slyme12
    @Slyme12 Жыл бұрын

    💥🏝💥

  • @alfredyjoseph9832
    @alfredyjoseph9832 Жыл бұрын

    Brother anajua sana sema anamafumbo sana

Келесі