Asimulia alivyoiba pete ya ndoa ya mama yake kununua dawa za kulevya

“Nikiwa nasoma shule ya msingi, nilipata rafiki kumbe alikuwa msafirishaji wa dawa za kulevya, kwa sababu nilikuwa na tamaa ya fedha, alinipa chaneli kwamba na mimi nikijiunga naye kusafirisha, nitakuwa napata fedha. Ilifika mahali nikatakiwa niwe nameza dawa hizo na kuzisafirisha.”
Hiyo ni kauli ya Abdallah Naseeb (28), mkazi wa Nyegezi jijini Mwanza, shujaa wa kupinga matumizi ya dawa za kulevya anayefanya kazi ya utoaji wa elimu kwa waraibu wa hizo jijini humo.
Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano, Abdallah anasema baada ya kuanza kutumika kuzisafirisha dawa hizo mwaka 2007, alijikuta akishawishika kuanza kutumia dawa aina ya Heroine, jambo lililomfanya asitishe masomo akiwa kidato cha tatu mwaka 2013.

Пікірлер