Sativa kupatiwa matibabu Dar, ndege yapata dharura
Wakati wowote kuanzia sasa Edgar Mwakabela maarufu Sativa anayedaiwa kutoweka Juni 23 na kupatikana mkoani Katavi, atawasili Dar es Salaam kwa ajili ya kupata huduma za matibabu.
Sativa alitakiwa kuwasili Dar es Salaam leo saa tisa alasiri kwa ndege maalumu ya kukodi, lakini kutokana na dharura iliyojitokeza, amelazimika kusafirishwa kwa gari la wagonjwa akitokea mkoani Dodoma kuletwa jijini hapa.
Sativa mkazi wa Mbezi wilayani Ubungo alipatikana Alhamisi Juni 27, 2024 katika pori la Hifadhi ya Taifa ya Katavi akiwa na majeraha mwilini, akiomba msaada wa kupelekwa hospitalini.
Akizungumza na wanahabari leo Jumamosi, Juni 29, 2024 katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, mratibu wa matibabu na safari ya Sativa, Martin Masese maarufu ‘MMM’ alisema Mwakabela anaendelea vema na hali yake inazidi kuimarika, ndiyo maana madaktari wametoa ruhusa asafirishwe.
Masese amesema Sativa alikuwa asafiri na Shirika la Ndege la Tanzania, tangu Juni 28 kutoka Katavi kupitia Tabora hadi Dar es Salaam, lakini kwa bahati mbaya usafiri huo ulishajaa.
Kutokana na hali hiyo, Masese amesema walishauriana na ndugu wa Sativa na madaktari na kuazimia mgonjwa huyo aletwe Dar es Salaam na gari la wagonjwa badala ya kusubiria ndege iliyopangwa kufika Dodoma usiku.
Пікірлер: 32
Mnajua kutufunga kamba kumbe Kwa Gari angeweza kufika vp mkae kusubili ndege?
Mungu aliyemlinda uhai wake usipotee ndo Mungu atamponya Ameen
Kwanini msichukue V8
@exprodigitaltechtv5571
4 күн бұрын
Sas V8 ndo ambulance?
Na mchunge kutoa taarifa kamil na ikiwezekana mpeleken hata Kenya hapo watamvzia kumalizia
Danadana Mpira wenye chenga nyingi
Poleni sana
Huyo rpc ni WA serekali hii mnayoishbulia Kila siku au??
Poleni saana
Mpelekeni Kenya, wasije wakammalizia
Hivi hawa watekaji ni dini gani? Mbona hawana huruma? Pole sana,
mbona umbali wa dom-dar ni mdogo kuliko umbali wa katavi-dom, c mngemleta dar kwa gari tu
SASA Dodoma mgeendaoja Kwa moja mpka dar
Chukua visa ninda nje ya nchi utanishukuru badae
Nyie akili ndogo sana 😢
Unaongea sana bila vtendo , katavi to Dar usafl upo na Kuna mabas mazur sana, ninyi mnasubili ndege , are you serious ,acheni uzembe
Mnakaa kungoja ndege wakati kuna luxury bus mngechukua hata private ila yote kwa yote apewe ulinzi hata ikiwezakana apelekwe nje ya nchi sina iman na serekali yetu imebeba watekaji kukilinda chama tu😭😭
Kwa hiyo uma wasipojua alike ndio usalama wake, au wasiojulikana ndio hawatakiwi kujua,
Tanzania ni Nchi ya Amani saaana ila kwa wanao funga midomo, watekaji hawakuwa na lengo la kumuua yaelekea lengo ni kufikisha ujumbe au walivyoona media zimeanza kurusha wakaona Isiwe tabu , hizi taarifa siku hizi zinafika Dunia nzima na ndio mambo yanayo ichafulia Nchi , kwenye ripoti ya haki za Binam kwa Tz sio nzuri saana , huwa wanatahadharisha saana watu wao wakija kufanya utalii
@nzitogondwe9976
3 күн бұрын
Rais wenu sio
Watekaji hinaonyesha bado watu hawatak kuua ndo maana kila mbombo yanagoma lisu na huyu vinagoma mama samia saidia hawa watu mama wanakutis ubaya
Ingekua mbunge maeezezo yotehayo yangekuepo
@msakadoobongeladada-uh3sk
Күн бұрын
hapana
Askali wanalinda nn eneo la tukio?