Adam Mchomvu: "Ofa Zinakuja, Wanakopi Kile Tunafanya, Tushapigwa Mawe Sana |SALAMA NA ADAM MCHOMVU 2
Ойын-сауық
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Adam Mchomvu ni jina kubwa kati ya majina makubwa ya watangazaji mahiri ambao nchi yetu imeshawahi kuona. Toka kuanzishwa kwa Radio za FM hapa nyumbani ambayo ilikua miaka ya kati kati ya 90 mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2000, hapo pia ndo kilipoanza kuzalishwa kizazi cha watangazaji na ma DJ mahiri ambao pia kwa kiasi kikubwa waliweza kulisukuma soko la vipaji mbali mbali vya muziki na filamu kufikia hapa vilipo leo hii. Kazi nzuri iliyotukuka ambayo pia imejaa jasho machozi na damu ilipitiwa. Mpaka leo hii ukiona watu wana launch album zao au filamu zao ujue kuna kazi nzuri ya kujenga misingi ilifanywa na walioianza kazi hii miaka hiyo ya nyuma.
Kwa uelewa wangu Adam ni Generation ya tatu ya wimbo hilo la watangazaji, ukiachana na kina Charles Hilary, Abubakar Liongo na Marehemu Misanya Bingi au Mike Mhagama, kizazi kilichofuata baada ya hapo ni hiki chetu, cha kiza Dozen na Fetty na Anna Peter na kina Adam Mchomvu. Generation sasa ya Bongo Flava na Bongo movie. Kizazi hiki ndo ambacho umahiri wa Adam ulianza kuonekana, XXL bila ya yeye kwa asilimia 100 utalisikia pengo lake, aina ya matamshi na kusema mambo kwa jinsi yalivyo ndo kumemjengea huo upekee. Ila pia ukaribu wake na wasanii wa Bongo flava pia umesaidia kumpatia story za ndani kabisa pamoja na kujua maendeleo ya kazi zao na struggle zao.
Pengine ukaribu huo ndio ulimfanya na yeye atake kuwa mwana muziki?
Sote tunajua kama mziki una mambo yake mengi sana, pengine wewe unaweza ukadhani unauweza na ni rahisi sana kuufanya lakini nadhani ukimuangalia Adam na kumfuatilia kwa kiasi kikubwa unaweza kujua ugumu wa zoezi zima maana kwa mtu kama Adam ambaye yuko jikoni kabisa ameshindwa kufanya muziki kama kazi yake nyengine au kama ambavyo yeye angetaka iwe muziki ndo maisha yake, si tahisi kama ambavyo unadhania. Kwa miaka ambayo nimekua nilifanya kazi kama mtangazaji wa Radio nimeona watangazaji wengi nao wakitaka kujikita kwenye muziki, ambao wamefanikiwa ni wanawake zaidi kuliko wanaume. Adam ameniambia kwenye maongezi yetu haya kwamba wakati mwengine anaona kama watu wanahisi hayuko seriou pengine, pia ameniambia kuhusu utajiri wa nyimbo alizonazo kwenye hifadhi yake. Hii pia imenionyesha jinsi tunavyokua tunafanya kazi ambayo wewe una hakika nayo ni nzuri sana ila kwa watu upokeaji wake unakua sio kama ambavyo wewe umetegemea.
Mi naamini kuna siku tutamuelewa tu maana kwa kumskiliza tu utaelewa utashi wake na jinsi ambavyo anaangalia vitu na uelewaji wake. Kwa wengi Adam ni HODARI na ambaye ameweza kufanya kazi kwa muda mrefu na kuwa muaminifu pia kwa muajiri wake, kama unakumbuka hapo katikati kulikua na wimbi la wafanyakazi wa Radio kupata ofa kubwa za kuhamia Radio nyengine, na nna uhakika mwingi na yeye ofa hizo alizipata, tena nyingi ila aliamua kuendelea kubaki palepale alipokua. Tunaambiwa loyalty haiuzwi wala huwezi kumfundisha mtu, ni aidha unakua nayo au hauna.
Humu mimi na yeye tulizungumzia mwanzo wake, fahamu zake za vitu na maamuzi yake ya kutaka kufanya kazi ambayo anafanya leo. Jinsi ambavyo wazazi au mzazi wake alilipikea hilo. Pia nilitaka kujua mazingira ambayo amekulia, humu amenielezea utukutu wake na jinsi ambavyo alikua na uwezo wa kumdanganya Mama yake ilimradi aishi kwenye aina ya maisha ambayo alikua ameichagua. Na jinsi pia ambavyo aliweza kujichomoa kutoka kwenye dunia hiyo ambayo ilikua imejaa kupotea kama asingekua makini.
Yangu matumaini kuna kadhaa ya kujifunza na yatakua na faida kwako na kwa uwapedao.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Пікірлер: 141
Namkubali sana mchomvu nisaidie nataka niwe dj
My favourite presenter of all the time
Adam namwonanmbali, Sana appreciate kwake bruda from home land
Vibe la Adam jamn me cjawahi lizoea miaka oooote namuona mpya kila cku
Moja ya interview kali nilizokuwa nazisubiri 🙌🙌🔥🔥
Am happy cz umemkumbuka mtto wako Adamu bila kuanza kula
Mchovu Akili sana Kama yangu 🧡😀salama keep going 🔥👑
Kali sana hii nilikua naisubiri asante kwa kutuletea SALAMA na MCHOMVU, sasa nasubiri SALAMA na MILLARD AYO, SALAMA na B DOZEN, SALAMA na MWIJAKU, SALAMA na DIVA THE BAWS, SALAMA NA GEAH HABIB, SALAMA na SHAFIH DAUDA na SALAMA na MASOUD KIPANYA ,
@dianerditto
Жыл бұрын
Mwijaku mtoe kwenye hio list
@allyjuma8120
Жыл бұрын
Adam anajua sana,hyu jamaa nambar 1 tz kw watngzaji wakiume
Adam yupo vizur, thanx Salama
Mtangazaji wangu bora wa muda wote
Energy ya hii interview ni hatari saaana🙌🏿
Napenda sana interview za huyu jamaa.
Jamaa nimekutana nae tukabadili namba lakini uwe strictly sana ukiwa nae usiwe mjanja mjanja nakubali ana akili sana Adam mchomvu
This guy is a whole vibe 🔥 🔥 🔥
You doin a good job salama... Mchomvu is always a vibe 🤟🏽
Salama Leo umetisha sana huyu jamaa ni noma mchomvu walimu mmekutana ktk interview wote wakali mjawai kuharibu wote wawili
Namkubali bro mchomvu
Adam unanipa Raha sana
Next Dozen, Millard ,Sky.Jonijo...
11:33 🔥 17:42 human talking 19:11 😆 funny guy
Una enjoy interview Adam noma
#AsoHiliAnaLile njmeipenda hii nilikua najua only in -ve way, Adam kaniongezea +ve pia, so imekua Hakuna mwema aso na ubaya, nahakuna mbaya aso na jema, kila mwenye nguvu anaudhaifu wake, na kila dhaifu ana ambalo ananguvu nalo, usiabudu wala kudharau mtu.
Nakukubali sana mzeee
Mirad ayo next
Flo mbovu,Yani huna saut yakufanya nikusikilize ukifloo by Geoffrey Mbele
Brandy ya Kitaa... I do appreciate the guy@ Adam mchomvu
AD PLUS BEST PRESENTER EAST AND CENTRAL AFRICA
Oyaaaa nathaminika ama😀😀😀😀 Nmekumbuka maneno ya mbasha ghafla. Shkamoo Broo Adam😊
Adam ni mwana Sana na yupo humble Sana na yupogo to hapo
I like aunt salama napenda san kipindi chako kina2elimisha sana sis vijana
Best of the best presenter Tz,AD +
The Classic presenter AD + nakubali😘
Is my Boy Alright Out there? 🙌🏾 Dadies Duties….
Adam si ndio aliyempiga mwenzie mtama si ilikuwa kwenye majukwaa ya wanasiasa
Salama nakuelewa na Adam pia mtu mbadi
Hot story Big up Sallama na Adam
Eyoo mchomvu #chuga represent
Ndoto yangu pia imetimia🙏
Nimecheka Sana Nampenda Sana huyu kaka.
Namkubaali mbayaaa
Bongo fleva bado inakuhitaji sana AD..mpk mda huu bado hawakuelew...
Adam anaakili nyingi sana
Noma sana hii naisubir na salama na fatma hassan (dj fetty)
Mchomvu is always on fire 🔥🔥🔥
Great 👍 show. The vibe is great..!
He is real may god keep him up…
Asante sana sister salama
Nice interview
RIP JPM.. you’ll always be remembered 😢
One of the best
Appreciate dada mkubwa
Salama Na B dozen
Super star wa nabii
aiseee the best interview everr
Kali Sanaa hiiii
Yaani mi napendaga mchomvu anavosema komba mwiko Fm😂😂😂
Yoo such a nice interview .....
Jamaa awali chakula
Adam ur so charming
He is very funny 😂
Adam aka Jack chan...zee la mitama
Sidhani kama ninaflow mbaya kushinda sugu😄😃😃😃😃@ad+
Nice and fun interview
Adam we noma sana umetema checheza moto interview ya maanakinoma noma
KIUKWEL MCHOMVU NAMKUBALI MBAYA
Next Luffa🔥
Jamaa anajua
Good one
Great interview, keep up the good work. please correct the video description *wimbi Sio wimbo
Makn san brother smart
😂😂😂😂😂😂 Utuletee milard Ayo
tunahitaji pia interview ya salama na zuchu
Good salaam
Namkubari sana uyu mwamba Mkrisilam mwenzangu natmani siku nikutane nae tupige story za kutoosha
🔥🔥🔥🔥
Mtafute na unju sasa
Namfaham sana kwajina THE INK
Bm kama bm.....#mchomvu..!!
Huo ni uongo huo niuongo bhana mchomvu ashawahi kuwa MC katka chama mapinduzi ndio siku aliyompiga mtama mbashs
@aliganzel6512
Жыл бұрын
Alikuwa pale as Mic controller wa event na sio part ya campaign haina tofauti kati ya alichofanya Adam na alichofanya Haji Manara
that man yuko na slang nzur
Bro unajua sanaa
👍👍
Interview nzur san...
Nice interview as always 👌 👍 👏 🙌 😊
Salama unajua sana
Chiii nice interview
🔥🔥🔥🔥🔥
Adam mchomvu (Tall wa Ajabu)
Mkali
Nondo za kutosha (Content)
Namkubali sana mwamba .adam big up
AD PLUS
Yaan adamu leo anamuhoji yeye salama
Really good!
Mchomvu hachoshi kumsikiliza
Yote kwa yote Salama mi sijapenda hivyo viti kwakweli!
Adamu umedondosha kitu cha ganja hapo chini cheupe man 😁😁😁
mchomvu🔥🔥🔥
Ila huyu Mchomvu...😂🙌😂
Umetuongopea hapo kwenye media yenu kujihusisha na siasa. Clouds ni ccm tupu