Adam Mchomvu: "Ofa Zinakuja, Wanakopi Kile Tunafanya, Tushapigwa Mawe Sana |SALAMA NA ADAM MCHOMVU 2

Ойын-сауық

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Adam Mchomvu ni jina kubwa kati ya majina makubwa ya watangazaji mahiri ambao nchi yetu imeshawahi kuona. Toka kuanzishwa kwa Radio za FM hapa nyumbani ambayo ilikua miaka ya kati kati ya 90 mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2000, hapo pia ndo kilipoanza kuzalishwa kizazi cha watangazaji na ma DJ mahiri ambao pia kwa kiasi kikubwa waliweza kulisukuma soko la vipaji mbali mbali vya muziki na filamu kufikia hapa vilipo leo hii. Kazi nzuri iliyotukuka ambayo pia imejaa jasho machozi na damu ilipitiwa. Mpaka leo hii ukiona watu wana launch album zao au filamu zao ujue kuna kazi nzuri ya kujenga misingi ilifanywa na walioianza kazi hii miaka hiyo ya nyuma.
Kwa uelewa wangu Adam ni Generation ya tatu ya wimbo hilo la watangazaji, ukiachana na kina Charles Hilary, Abubakar Liongo na Marehemu Misanya Bingi au Mike Mhagama, kizazi kilichofuata baada ya hapo ni hiki chetu, cha kiza Dozen na Fetty na Anna Peter na kina Adam Mchomvu. Generation sasa ya Bongo Flava na Bongo movie. Kizazi hiki ndo ambacho umahiri wa Adam ulianza kuonekana, XXL bila ya yeye kwa asilimia 100 utalisikia pengo lake, aina ya matamshi na kusema mambo kwa jinsi yalivyo ndo kumemjengea huo upekee. Ila pia ukaribu wake na wasanii wa Bongo flava pia umesaidia kumpatia story za ndani kabisa pamoja na kujua maendeleo ya kazi zao na struggle zao.
Pengine ukaribu huo ndio ulimfanya na yeye atake kuwa mwana muziki?
Sote tunajua kama mziki una mambo yake mengi sana, pengine wewe unaweza ukadhani unauweza na ni rahisi sana kuufanya lakini nadhani ukimuangalia Adam na kumfuatilia kwa kiasi kikubwa unaweza kujua ugumu wa zoezi zima maana kwa mtu kama Adam ambaye yuko jikoni kabisa ameshindwa kufanya muziki kama kazi yake nyengine au kama ambavyo yeye angetaka iwe muziki ndo maisha yake, si tahisi kama ambavyo unadhania. Kwa miaka ambayo nimekua nilifanya kazi kama mtangazaji wa Radio nimeona watangazaji wengi nao wakitaka kujikita kwenye muziki, ambao wamefanikiwa ni wanawake zaidi kuliko wanaume. Adam ameniambia kwenye maongezi yetu haya kwamba wakati mwengine anaona kama watu wanahisi hayuko seriou pengine, pia ameniambia kuhusu utajiri wa nyimbo alizonazo kwenye hifadhi yake. Hii pia imenionyesha jinsi tunavyokua tunafanya kazi ambayo wewe una hakika nayo ni nzuri sana ila kwa watu upokeaji wake unakua sio kama ambavyo wewe umetegemea.
Mi naamini kuna siku tutamuelewa tu maana kwa kumskiliza tu utaelewa utashi wake na jinsi ambavyo anaangalia vitu na uelewaji wake. Kwa wengi Adam ni HODARI na ambaye ameweza kufanya kazi kwa muda mrefu na kuwa muaminifu pia kwa muajiri wake, kama unakumbuka hapo katikati kulikua na wimbi la wafanyakazi wa Radio kupata ofa kubwa za kuhamia Radio nyengine, na nna uhakika mwingi na yeye ofa hizo alizipata, tena nyingi ila aliamua kuendelea kubaki palepale alipokua. Tunaambiwa loyalty haiuzwi wala huwezi kumfundisha mtu, ni aidha unakua nayo au hauna.
Humu mimi na yeye tulizungumzia mwanzo wake, fahamu zake za vitu na maamuzi yake ya kutaka kufanya kazi ambayo anafanya leo. Jinsi ambavyo wazazi au mzazi wake alilipikea hilo. Pia nilitaka kujua mazingira ambayo amekulia, humu amenielezea utukutu wake na jinsi ambavyo alikua na uwezo wa kumdanganya Mama yake ilimradi aishi kwenye aina ya maisha ambayo alikua ameichagua. Na jinsi pia ambavyo aliweza kujichomoa kutoka kwenye dunia hiyo ambayo ilikua imejaa kupotea kama asingekua makini.
Yangu matumaini kuna kadhaa ya kujifunza na yatakua na faida kwako na kwa uwapedao.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Пікірлер: 141

  • @ChidwadarChidwadar
    @ChidwadarChidwadar3 ай бұрын

    Namkubali sana mchomvu nisaidie nataka niwe dj

  • @kulwakisoma1019
    @kulwakisoma1019 Жыл бұрын

    My favourite presenter of all the time

  • @mr.futurefrozie2558
    @mr.futurefrozie25586 ай бұрын

    Adam namwonanmbali, Sana appreciate kwake bruda from home land

  • @dianerditto
    @dianerditto Жыл бұрын

    Vibe la Adam jamn me cjawahi lizoea miaka oooote namuona mpya kila cku

  • @majojo9166
    @majojo9166 Жыл бұрын

    Moja ya interview kali nilizokuwa nazisubiri 🙌🙌🔥🔥

  • @emmanuelmchomvu2676
    @emmanuelmchomvu2676 Жыл бұрын

    Am happy cz umemkumbuka mtto wako Adamu bila kuanza kula

  • @nicolenabintu2509
    @nicolenabintu2509 Жыл бұрын

    Mchovu Akili sana Kama yangu 🧡😀salama keep going 🔥👑

  • @mrfashion1687
    @mrfashion1687 Жыл бұрын

    Kali sana hii nilikua naisubiri asante kwa kutuletea SALAMA na MCHOMVU, sasa nasubiri SALAMA na MILLARD AYO, SALAMA na B DOZEN, SALAMA na MWIJAKU, SALAMA na DIVA THE BAWS, SALAMA NA GEAH HABIB, SALAMA na SHAFIH DAUDA na SALAMA na MASOUD KIPANYA ,

  • @dianerditto

    @dianerditto

    Жыл бұрын

    Mwijaku mtoe kwenye hio list

  • @allyjuma8120

    @allyjuma8120

    Жыл бұрын

    Adam anajua sana,hyu jamaa nambar 1 tz kw watngzaji wakiume

  • @mariamusaulo4429
    @mariamusaulo4429 Жыл бұрын

    Adam yupo vizur, thanx Salama

  • @finiaskalist747
    @finiaskalist747 Жыл бұрын

    Mtangazaji wangu bora wa muda wote

  • @derickdepota101
    @derickdepota101 Жыл бұрын

    Energy ya hii interview ni hatari saaana🙌🏿

  • @emmanuelnzaligo6262
    @emmanuelnzaligo6262 Жыл бұрын

    Napenda sana interview za huyu jamaa.

  • @madownloadionlinetv759
    @madownloadionlinetv759 Жыл бұрын

    Jamaa nimekutana nae tukabadili namba lakini uwe strictly sana ukiwa nae usiwe mjanja mjanja nakubali ana akili sana Adam mchomvu

  • @asenathogallo2154
    @asenathogallo2154 Жыл бұрын

    This guy is a whole vibe 🔥 🔥 🔥

  • @kibwanakhamisi5604
    @kibwanakhamisi5604 Жыл бұрын

    You doin a good job salama... Mchomvu is always a vibe 🤟🏽

  • @mbenamdudu7856
    @mbenamdudu7856 Жыл бұрын

    Salama Leo umetisha sana huyu jamaa ni noma mchomvu walimu mmekutana ktk interview wote wakali mjawai kuharibu wote wawili

  • @hoseayesaya4751
    @hoseayesaya4751 Жыл бұрын

    Namkubali bro mchomvu

  • @irakozeaudrey8643
    @irakozeaudrey8643 Жыл бұрын

    Adam unanipa Raha sana

  • @nellymatalanga5033
    @nellymatalanga5033 Жыл бұрын

    Next Dozen, Millard ,Sky.Jonijo...

  • @richardcastromzena5136
    @richardcastromzena5136 Жыл бұрын

    11:33 🔥 17:42 human talking 19:11 😆 funny guy

  • @smartmussadozen3535
    @smartmussadozen3535 Жыл бұрын

    Una enjoy interview Adam noma

  • @Jefa_Adili
    @Jefa_Adili Жыл бұрын

    #AsoHiliAnaLile njmeipenda hii nilikua najua only in -ve way, Adam kaniongezea +ve pia, so imekua Hakuna mwema aso na ubaya, nahakuna mbaya aso na jema, kila mwenye nguvu anaudhaifu wake, na kila dhaifu ana ambalo ananguvu nalo, usiabudu wala kudharau mtu.

  • @AfricanGiant-te9et
    @AfricanGiant-te9et Жыл бұрын

    Nakukubali sana mzeee

  • @marwajuma7493
    @marwajuma7493 Жыл бұрын

    Mirad ayo next

  • @secondyoana-uv4wn
    @secondyoana-uv4wn Жыл бұрын

    Flo mbovu,Yani huna saut yakufanya nikusikilize ukifloo by Geoffrey Mbele

  • @nathanaeljimmy5393
    @nathanaeljimmy5393 Жыл бұрын

    Brandy ya Kitaa... I do appreciate the guy@ Adam mchomvu

  • @jacksonbahemu8172
    @jacksonbahemu8172 Жыл бұрын

    AD PLUS BEST PRESENTER EAST AND CENTRAL AFRICA

  • @tanzaniamycountry9308
    @tanzaniamycountry9308 Жыл бұрын

    Oyaaaa nathaminika ama😀😀😀😀 Nmekumbuka maneno ya mbasha ghafla. Shkamoo Broo Adam😊

  • @barakakusa7606
    @barakakusa7606 Жыл бұрын

    Adam ni mwana Sana na yupo humble Sana na yupogo to hapo

  • @edgardevis8152
    @edgardevis8152 Жыл бұрын

    I like aunt salama napenda san kipindi chako kina2elimisha sana sis vijana

  • @benedictmacoy4798
    @benedictmacoy4798 Жыл бұрын

    Best of the best presenter Tz,AD +

  • @robinsonjames9711
    @robinsonjames9711 Жыл бұрын

    The Classic presenter AD + nakubali😘

  • @karimhemed9261
    @karimhemed9261 Жыл бұрын

    Is my Boy Alright Out there? 🙌🏾 Dadies Duties….

  • @immaabukuku7180
    @immaabukuku7180 Жыл бұрын

    Adam si ndio aliyempiga mwenzie mtama si ilikuwa kwenye majukwaa ya wanasiasa

  • @mbenamdudu7856
    @mbenamdudu7856 Жыл бұрын

    Salama nakuelewa na Adam pia mtu mbadi

  • @casablancastudioarusha775
    @casablancastudioarusha775 Жыл бұрын

    Hot story Big up Sallama na Adam

  • @adolfmathew9698
    @adolfmathew9698 Жыл бұрын

    Eyoo mchomvu #chuga represent

  • @adamore854
    @adamore854 Жыл бұрын

    Ndoto yangu pia imetimia🙏

  • @rahabumasebo8084
    @rahabumasebo8084 Жыл бұрын

    Nimecheka Sana Nampenda Sana huyu kaka.

  • @kennedjohn5785
    @kennedjohn5785 Жыл бұрын

    Namkubaali mbayaaa

  • @baliatuhamis9696
    @baliatuhamis9696 Жыл бұрын

    Bongo fleva bado inakuhitaji sana AD..mpk mda huu bado hawakuelew...

  • @rizikiones5687
    @rizikiones5687 Жыл бұрын

    Adam anaakili nyingi sana

  • @mohammedmwarizo3700
    @mohammedmwarizo3700 Жыл бұрын

    Noma sana hii naisubir na salama na fatma hassan (dj fetty)

  • @AlfredCarol_tz
    @AlfredCarol_tz Жыл бұрын

    Mchomvu is always on fire 🔥🔥🔥

  • @joeljoshua1940
    @joeljoshua1940 Жыл бұрын

    Great 👍 show. The vibe is great..!

  • @majatv1088
    @majatv1088 Жыл бұрын

    He is real may god keep him up…

  • @sarahkitindi3420
    @sarahkitindi3420 Жыл бұрын

    Asante sana sister salama

  • @ngambikomsu64
    @ngambikomsu64 Жыл бұрын

    Nice interview

  • @wilsonchishomi1083
    @wilsonchishomi1083 Жыл бұрын

    RIP JPM.. you’ll always be remembered 😢

  • @damiankimaro9665
    @damiankimaro9665 Жыл бұрын

    One of the best

  • @renatusmpete3527
    @renatusmpete3527 Жыл бұрын

    Appreciate dada mkubwa

  • @ubaoni57
    @ubaoni57 Жыл бұрын

    Salama Na B dozen

  • @johariramadhan5236
    @johariramadhan5236 Жыл бұрын

    Super star wa nabii

  • @carenmsafiri8498
    @carenmsafiri8498 Жыл бұрын

    aiseee the best interview everr

  • @BBrown_vevo
    @BBrown_vevo Жыл бұрын

    Kali Sanaa hiiii

  • @gibsonkabusola6923
    @gibsonkabusola6923 Жыл бұрын

    Yaani mi napendaga mchomvu anavosema komba mwiko Fm😂😂😂

  • @enrico955
    @enrico955 Жыл бұрын

    Yoo such a nice interview .....

  • @justnjustn6168
    @justnjustn6168 Жыл бұрын

    Jamaa awali chakula

  • @marksulle6120
    @marksulle6120 Жыл бұрын

    Adam ur so charming

  • @chiticollemans
    @chiticollemans Жыл бұрын

    He is very funny 😂

  • @raimajimoto1122
    @raimajimoto1122 Жыл бұрын

    Adam aka Jack chan...zee la mitama

  • @khamseysagrado7547
    @khamseysagrado7547 Жыл бұрын

    Sidhani kama ninaflow mbaya kushinda sugu😄😃😃😃😃@ad+

  • @nyamarasapeter4302
    @nyamarasapeter4302 Жыл бұрын

    Nice and fun interview

  • @gibsonbitende
    @gibsonbitende Жыл бұрын

    Adam we noma sana umetema checheza moto interview ya maanakinoma noma

  • @shukurumswagala5256
    @shukurumswagala5256 Жыл бұрын

    KIUKWEL MCHOMVU NAMKUBALI MBAYA

  • @laflame3450
    @laflame3450 Жыл бұрын

    Next Luffa🔥

  • @martinechangwa2046
    @martinechangwa2046 Жыл бұрын

    Jamaa anajua

  • @adrianboniventure5509
    @adrianboniventure5509 Жыл бұрын

    Good one

  • @princenyerere4048
    @princenyerere4048 Жыл бұрын

    Great interview, keep up the good work. please correct the video description *wimbi Sio wimbo

  • @user-ev3vb8hp2y
    @user-ev3vb8hp2y5 ай бұрын

    Makn san brother smart

  • @susannesusie3217
    @susannesusie3217 Жыл бұрын

    😂😂😂😂😂😂 Utuletee milard Ayo

  • @michaelkipara8205
    @michaelkipara8205 Жыл бұрын

    tunahitaji pia interview ya salama na zuchu

  • @dilipdab3714
    @dilipdab37144 ай бұрын

    Good salaam

  • @salimtiba4614
    @salimtiba4614 Жыл бұрын

    Namkubari sana uyu mwamba Mkrisilam mwenzangu natmani siku nikutane nae tupige story za kutoosha

  • @sabanajr6455
    @sabanajr6455 Жыл бұрын

    🔥🔥🔥🔥

  • @hudsonhenry1849
    @hudsonhenry1849 Жыл бұрын

    Mtafute na unju sasa

  • @allynizam7138
    @allynizam713810 ай бұрын

    Namfaham sana kwajina THE INK

  • @danielagustino3130
    @danielagustino3130 Жыл бұрын

    Bm kama bm.....#mchomvu..!!

  • @fadhilhussein8845
    @fadhilhussein8845 Жыл бұрын

    Huo ni uongo huo niuongo bhana mchomvu ashawahi kuwa MC katka chama mapinduzi ndio siku aliyompiga mtama mbashs

  • @aliganzel6512

    @aliganzel6512

    Жыл бұрын

    Alikuwa pale as Mic controller wa event na sio part ya campaign haina tofauti kati ya alichofanya Adam na alichofanya Haji Manara

  • @brianrichard9022
    @brianrichard9022 Жыл бұрын

    that man yuko na slang nzur

  • @smashowupdates2377
    @smashowupdates2377 Жыл бұрын

    Bro unajua sanaa

  • @chefr3020
    @chefr3020 Жыл бұрын

    👍👍

  • @waziriseif5384
    @waziriseif5384 Жыл бұрын

    Interview nzur san...

  • @ibrahimkibira9943
    @ibrahimkibira9943 Жыл бұрын

    Nice interview as always 👌 👍 👏 🙌 😊

  • @LumolaSteven
    @LumolaSteven Жыл бұрын

    Salama unajua sana

  • @sumay8817
    @sumay8817 Жыл бұрын

    Chiii nice interview

  • @humphreydastan1032
    @humphreydastan1032 Жыл бұрын

    🔥🔥🔥🔥🔥

  • @fraitmgala5966
    @fraitmgala5966 Жыл бұрын

    Adam mchomvu (Tall wa Ajabu)

  • @ericgardner7509
    @ericgardner7509 Жыл бұрын

    Mkali

  • @hassanikipusa8328
    @hassanikipusa8328 Жыл бұрын

    Nondo za kutosha (Content)

  • @mussamoshi3205
    @mussamoshi3205 Жыл бұрын

    Namkubali sana mwamba .adam big up

  • @denislazaro818
    @denislazaro818 Жыл бұрын

    AD PLUS

  • @johariramadhan5236
    @johariramadhan5236 Жыл бұрын

    Yaan adamu leo anamuhoji yeye salama

  • @amiriyusuph2950
    @amiriyusuph2950 Жыл бұрын

    Really good!

  • @chafumirro5617
    @chafumirro5617 Жыл бұрын

    Mchomvu hachoshi kumsikiliza

  • @omarmahewa928
    @omarmahewa928 Жыл бұрын

    Yote kwa yote Salama mi sijapenda hivyo viti kwakweli!

  • @iandavid4878
    @iandavid4878 Жыл бұрын

    Adamu umedondosha kitu cha ganja hapo chini cheupe man 😁😁😁

  • @BANJO_MOULDING_DECORATION
    @BANJO_MOULDING_DECORATION Жыл бұрын

    mchomvu🔥🔥🔥

  • @maryshirima1234
    @maryshirima1234 Жыл бұрын

    Ila huyu Mchomvu...😂🙌😂

  • @1000Brain
    @1000Brain Жыл бұрын

    Umetuongopea hapo kwenye media yenu kujihusisha na siasa. Clouds ni ccm tupu

Келесі