Wafanyabiashara wafunga maduka wakimshtumu meneja TRA Handeni
Wafanyabiashara wa maduka ya jumla na rejareja wilayani Handeni mkoani Tanga wamefunga maduka yao kutwa nzima wakidai kutolewa lugha za vitisho na Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania wilayani hapa, wakati wanapofika ofisini kwake.
Wakizungumza kwenye mkutano na kamati ya ulinzi na usalama katika kikao kilichofanyika viwanja vya Handeni Square, wafanyabiashara hao wamesema shida kubwa wanayokutana nayo TRA, ni lugha za vitisho kutoka kwa meneja na makadirio ya kodi ambayo si rafiki kwao.
Akijibu shutuma hizo, Meneja wa TRA wilayani Handeni, Venance Ephraim amesema changamoto iliyopelekea hali hiyo ni wafanyabiashara wengi kukosa elimu ya kodi na waliowengi hawataki kutoa risiti.
Пікірлер: 8
Safi sana mkuu wa Wilaya kwa maelekezo yako mazuri maana huyo meneja akiambiwa akafanye hiyo Biashara na Mfanyabiashara akawe meneja wa TRA ukweli huyo meneja atashindwa na mfanyabiashara ataimudu vizuri hiyo kazi ya Umeneja.
Wanakosea sana kuajiri mtu ambaye hajawahi uchuuzi
Nisikilizenii watanzania TRA sio tatizo tatizo ni wawekezaji wa kihindi na kichina ndio wameharibu biashara tunashindwa kusimamia bei kwa sababu Yao wawekezaji Hadi wateja wamekuwa na kiburi kutokana na uhorela wa bei zao kibiashara
Muongo huyu meneja anaonesha amachoka kazi sasa naitwe makonda aje amnyooshe
Kiufupi meneja aondolewe hapo wilayani sababu sio rafiki na wafanya biashara sheria afate mkondo
Huyu kashapitiwa na makonda??? kama Risiti sasa maduka yote wafunge kwa Risiti mbona Aifanani hiyo mkuu wa TRA 😂😂 5:34
Mnatuwekea taarifa nusu mbona hivyo
Mchawi samia mwaka huu niko kote tunaonewa wamekopa nchi inadaiwa ndo mana wanatukandamiza mm nko manyara huku tumepigwa kod kubwa sana tena uku porin samia hafai kuwa rais