Wafanyabiashara wafunga maduka wakimshtumu meneja TRA Handeni

Wafanyabiashara wa maduka ya jumla na rejareja wilayani Handeni mkoani Tanga wamefunga maduka yao kutwa nzima wakidai kutolewa lugha za vitisho na Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania wilayani hapa, wakati wanapofika ofisini kwake.
Wakizungumza kwenye mkutano na kamati ya ulinzi na usalama katika kikao kilichofanyika viwanja vya Handeni Square, wafanyabiashara hao wamesema shida kubwa wanayokutana nayo TRA, ni lugha za vitisho kutoka kwa meneja na makadirio ya kodi ambayo si rafiki kwao.
Akijibu shutuma hizo, Meneja wa TRA wilayani Handeni, Venance Ephraim amesema changamoto iliyopelekea hali hiyo ni wafanyabiashara wengi kukosa elimu ya kodi na waliowengi hawataki kutoa risiti.

Пікірлер: 8

  • @modestwenceslaus9
    @modestwenceslaus94 ай бұрын

    Safi sana mkuu wa Wilaya kwa maelekezo yako mazuri maana huyo meneja akiambiwa akafanye hiyo Biashara na Mfanyabiashara akawe meneja wa TRA ukweli huyo meneja atashindwa na mfanyabiashara ataimudu vizuri hiyo kazi ya Umeneja.

  • @user-xt3ly1pv2e
    @user-xt3ly1pv2e4 ай бұрын

    Wanakosea sana kuajiri mtu ambaye hajawahi uchuuzi

  • @hurumalunda2490
    @hurumalunda249027 күн бұрын

    Nisikilizenii watanzania TRA sio tatizo tatizo ni wawekezaji wa kihindi na kichina ndio wameharibu biashara tunashindwa kusimamia bei kwa sababu Yao wawekezaji Hadi wateja wamekuwa na kiburi kutokana na uhorela wa bei zao kibiashara

  • @user-ef6tl6fy1g
    @user-ef6tl6fy1g4 ай бұрын

    Muongo huyu meneja anaonesha amachoka kazi sasa naitwe makonda aje amnyooshe

  • @WilsonGilbert-ut5fg
    @WilsonGilbert-ut5fg4 ай бұрын

    Kiufupi meneja aondolewe hapo wilayani sababu sio rafiki na wafanya biashara sheria afate mkondo

  • @kilogreekachananawatuwasio4054
    @kilogreekachananawatuwasio40544 ай бұрын

    Huyu kashapitiwa na makonda??? kama Risiti sasa maduka yote wafunge kwa Risiti mbona Aifanani hiyo mkuu wa TRA 😂😂 5:34

  • @bishopjohnolenaata5581
    @bishopjohnolenaata55814 ай бұрын

    Mnatuwekea taarifa nusu mbona hivyo

  • @josephfrancis9943
    @josephfrancis99434 ай бұрын

    Mchawi samia mwaka huu niko kote tunaonewa wamekopa nchi inadaiwa ndo mana wanatukandamiza mm nko manyara huku tumepigwa kod kubwa sana tena uku porin samia hafai kuwa rais