Salama Na KALITO Ep 41 | THE ORIGINATOR Part 2
Ойын-сауық
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #0762797291
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Carlos Bastos aka Kalito ni moja kati ya wale binadamu ambao hawahitaji ‘kutambulishwa’ na hiyo si kwa sababu ya muonekano wake hata kidogo zaidi ni personality yake, anaongea, anachekesha, anajielewa, anajua nini cha kusema na wapi pa kusema pia. Katika watu ambao namshukuru Mungu kwa kuwafanya wawe rafiki zangu Kalito ni mmoja wapo.
Jinsi ambavyo alifika Tanzania inaweza ikakufanya ujue pia yeye ni mtu wa aina gani haswa, kutoka mwenyewe familia ambayo mtoto wa kiume ni pekee, na pengine alikua na uhakika wa kupata kila anachotaka lakini aliamua kupaki begi na kuchanja mbuga kuja hapa Tanzania. Kusema za ukweli story yake ya maisha ni ya kuamsha sana. Imagine wewe leo unatoka ulikotoka ukaenda zako pa kwenda, ukajimix kwa kuhudumia watu kwa kuwapa burudani na chakula mpaka akapata upenyo wa kufanya yake. Ni wangapi kati yetu wanaweza kufanya hivyo? Najua wengi wetu hatukuzaliwa hapa Dar es Salaam ila tumekuja tukalikita na mpaka sasa Alhamdulillah mambo yanaenda. Ila si wengi wanaweza kusema hivyo. Tunajua huchukua jasho machozi na pengine damu kufikia malengo.
So binafsi haswa nimejifunza au najifunza nini kutoka kwa rafiki yangu huyu kila siku? Cha kwanza ni kuwa MKWELI. Kama unayo unayo, kama unaweza kufanya/kufika utafanya hivyo, kama unaweza kutoa unatoa na kama huwezi UNASEMA. Naamini ndani ya moyo wangu, hiyo ni moja ya silaha kubwa sana kama unataka kufanikiwa, kama unataka MAENDELEO. Cha pili pia ambacho bado kinakaa kwenye UKWELI ni UAMINIFU. Ukikopa pesa RUDISHA maana hii itakupa nafasi ya kuweza kurudi na kukopa tena kama mambo yako yatakua bado sio sukari, sasa imagine hujarudisha na ukapata shida nyengine je utaweza kurudi kukopa tena? Vipi kama alokukopesha nae kashawaambia ma don wenzake kwamba wewe huwa hulipi? Utasogea kweli?... Mwisho wa siku DAWA YA DENI ni KULIPA tu.
Jengine KUBWA zaidi ni kutokua na SIRI nyiiiingi. Mambo ambayo yatakufanya uwe unaweka vitu vingi ndani, ambavyo hauwezi kusema labda kwasababu ya aibu au pengine hauko huru kuviongea nalo ni TATIZO. Ni kweli sote tuna SIRI zetu, ila zikizidi ndo zinaleta msongo wa mawazo. So kuwa muangalifu na kipi unasema na kipi unaweka. Kujijazia mavitu moyoni ki afya si mpango hata kidogo.
Kalito yuko HURU, anaskiliza watu na kujifunza kila siku pia kama mimi na wewe tu, pia ana shida zake ambazo kwa kiasi kikubwa ameweza kuzifanya zisiwe chanzo cha yeye kutokua na furaha au kumpa unyonge. Pengine unaweza kusema ni kwa sababu ana hela au biashara inayomuingizia kipato kila siku ndo maana ni rahisi kwake kucheka kwa yote, ila Amini nikikuambia hata yeye huwa ana kutana na mitihani mikubwa tu, lakini kwasababu yuko POSITIVE muda wote unakuta anamalizana na shida zake kwa roho safi tu. Anakubali pale anapokua kashindwa na kujifunza na anafurahia pia challenges ambazo binafsi anazishinda kwa uzuri tu. Yeye pia ni rafiki nambari MOJA wa wafanyakazi wake karibia WOTE wa Samaki Samaki na sasa Kuku Kuku wa kuwajua mmoja mmoja kwa majina yao. Mpaka mafundi wake wote hao ni familia yake.
Wangu tumekuletea Kalito kwenye meza ili uone mambo kwa utofauti haswa. Ujifunze kutoka kwa watu ambao unawaangalia kila siku na ambao pengine unadhani mambo yao ni SUKARI kila siku iendayo kwa Mungu. Yangu matumaini utaokota mawili matatu humu. Maana ukiachana na biashara pia alizungumza maisha yake. Alivyoumwa, watoto wake na jinsi alivyofika Tanzania na nchi yetu hii na watu wake. Alituambia pia kuhusu mapenzi yake na Bahari na mahusiano yake na watoto wake na Mama yao ambaye hayuko nae tena sasa. Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Пікірлер: 69
Nimejifunza usijudge m2 kwa muonekano aliyokuwa nao pengne kwa muonekano aliyokuwa nao sio mzur lkn ndani yake Kuna mengi mazur ya kujifunza kupitia kwake💪#kalito
the Guy is originator for sure, has a lot to give as lessons. thanks Salama keep good work alive
@alphamenson3784
3 жыл бұрын
Definitely bro
31:35 unaweza kuwa na sifa zote za kuwa mtanzania ila process ya kuwa mtanzania inahitaji uvumilivu mno. I am wishing you all the best Kalito. Wewe ni Mtanzania tayari kwa moyo tu.
Huyu jamaa kanifundisha kitu kikubwa sana..... appearance yake ni tofaut na roho yake.......... Asante bint jabir
Ukifanya ubaya utalipwa ubaya ukifanya uzuri utalipwa uzuri
Kati ya interview kali au nzur hii ni best kwangu 💥💥💥nairudia mara kibao kuitazama big up Kalito &salama
Mbona salama leo anadeka akiongea na jamaa
i like this guy...very genuine
Mlete tena huyu ana madini sana and I really like salamas’joke 😀
A genius and an icon for sure
Carlos anaongea kama Zlatan Ibrahimovic aisee
Nimejua the difference kufumaniwa vs kukamatwa japo mwanaume hafumaniwi, anakutwa
Boos wangu nampenda san
Safi sana Salama tuletee watu wenye madini kama hawa 💪
Great Interview... That brother is wise in being humane. Hongera Salama kwa 40s, Jah aendelee kuprovide tuishi na mainterview makali zaidi ya haya
Hapo kwènýè kugonganisha magar 😂😂😂😂
Je umeagiza GARI 🚘🚗nje ya nchi na unahitaji huduma ya clearance ya gari lako( Clearing & Forwarding ) kwa uharaka na BEI NAFUU ila unawaza Clearing Agent ⚓️🚢gani atalitimiza Hilo? Basi ondoa shaka na karibu nikuhudumie. Tazama baadhi ya bei zangu za kutoa magari bandarini 🚢Dar Es Salaam (Local) aina ya *TOYOTA* km ifuatavyo.. Kama aina ya gari uliyoagiza haipo kwenye orodha usisite kuniuliza📞Pia wateja wa mizigo ya AIRPORT 🛫/ CONTAINER & MAGARI🚗 yanayokwenda nje ya nchi ( TRANST ) mnakaribishwa..... ------------------ Kwa wateja waishio Dar Es Salaam utafikishiwa gari lako mpaka ulipo BURE na kwa wateja wa mkoani utalipia gharama ya Dereva kutokana na umbali uliopo kutokea Dar Es Salaam kama ukihitaji kusafirishiwa, Asante 1: IST old - 850,000/= 2: HARRIER New-1,000,000/= 3: HARRIER Old-950,000/= 4: RAV 4 - 950,000/= 5: RAUM - 850,000/= 6: SPACIO - 850,000/= 7: PASSO - 800,000/= 8: VITZ - 800,000/= 9: PREMIO - 850,000/= 10: ALTEZA - 850,000/= 11: SUBARU - 850,000/= 12: CARINA - 850,000/= ---------------------------------------- Gharama hizi zinahusisha malipo ya 1: Port Charges 2: Shipping Line 3: Walfage 4: Agent Fee 5: Plate no ---------------------------------------- ☎️DM/Piga/Text 0653953900 / 0742996876 ☎️Whatsapp +255 653953900 📧 Email: charlessabikazi@gmail.com 📢Marketing by @cairo_promotions 🏢Company: Mofaz movers 📍Location: PSSSF Tower, Samora Avenue Dar es salaam, Tanzania *NB: Triangle & Fire Extinguisher 🧯 BURE *NB: KUAGIZIWA GARI NI BURE 🙏 *NB: KUAGIZIWA BIDHAA CHINA 🇨🇳 NI BURE🙏
Nimependa , napenda unavyotuletea watu tofauti Salama. Jah bless
Be in peace with your self Thanks Kalito😊....social media na unafiki yaani umenigusaaa...people are so fake😞
Dude is GENIUS 🙌🏻
Ahsante sana salama na carlos hongera sana carlos kwa kazi nzuri na ahsante pia kwa kuchagua kuwekeza tanzania nimejifunza mengi kwako hongera sana carlos
Asante sana Salama this so uplifting interview hii imengia top three zangu baada ya "Lordi" na Speshoz!
Penda sana salama
nime enjoy na kujifunza vitu kwa hii interview asante sana salama na kalito
Inner peace is evrything !!!!
The guy is very smart
Bado kuna watu wema duniani ✌️✌️
Wooow nice interview
Salama hako kakicheko 9:50 😃😃...nami nimejikuta nafurahi with no reason
Mlete Ally Choki mzee wa farasi
He looks like Giroud
Ana roho nzuri na tabia nzuri. Wa spain wanafwata dini sana.
Nimeipenda
Kalito 😍😍
Nzuri
Tunaomba mrudishe carlos pls anamambo mengi ya kufundisha jamiiii
i liked the interview, very calm and professional
salama mjitahidi kuongeza sauti ya video plz
Asante tena
visuri, mwanso n.k mspanish halisi! hahaa regardless hongera kwa kiswahili!
Salama jamani....unamchanganya na kiswahili hahahahaha jamaa hana kumbukumbu
Eeeeh salama leo umetuletea balaa...nmejua yule wa apocalypto
Great
Nimependa sana tuendelee Na unafikii😂😂
haiandikwi Kalito inaandikwa Carlito!
Genius sana... Nimejifunz sana kitu apa
Shule bila ada👌🏻👌🏻
Kuiba mademu🤣🤣🤣🤣
Umetisha salama leo
Kumbe kuna kufumaniwa na kukamatwa haha
Great i like that
Love you Salama more love 🥰🥰🥰💋💋
Wakwanza ☺
Very honest
Tuletee fred vunjabei
Mabruki kipindi kizuri
dah eti ongeza bando😁😁😁
I’m inspired everything happens in yo life for a reason never loser hope🙏❤️
Bravo bora kujichunga mwenye
✌👊👍
Una kucha za plastic, unajisifia nini?
Munguwang Huumt mbonayukoiv? Anatish
The interview is nice🔥
@bonneytv9441
3 жыл бұрын
can i have your number❤️
Kikaratas karatas ñďò unadaiwa 😂😂😂
💥💥💥💥💥💥👍
Asantee kwa swali la jicho nilitamani sana kujua...nakupenda salama
Mlete Ally Choki mzee wa farasi