REA KUMWAGA NOTI, MIKOPO UJENZI VITUO VYA MAFUTA

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini imeanzisha mpango wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondosha madhara yatokanayo na njia zisizo salama. Madhara hayo ni pamoja na:
a) Gharama kubwa za upatikanaji wa bidhaa hizo maeneo ya vijijini tofauti na bei elekezi;
b) Gharama kubwa za usafiri hasa maeneo ya vijijini;
c) Kuadimika kwa bidhaa hizo maeneo ya vijijini;
d) Uuzaji na uhifadhi wa bidhaa za mafuta usio safi na salama (mapipa na madumu ya plastiki ndani ya nyumba);
e) Milipuko ya moto ambayo inaweza kugharimu maisha ya wananchi na hivyo kupunguza nguvu kazi ya Taifa;
f) Uharibifu wa mazingira unaotokana na bidhaa hizo kumwagika maeneo mbalimbali kwa sababu ya uhifadhi usiofaa;
g) Kuikosesha Serikali mapato ambayo wauzaji wa mafuta (petroli na dizeli) hawalipi kodi na tozo mbalimbali; na
h) Kuathiri afya kutokana na kuvuta hewa isiyo safi na salama kwa sababu ya kuhifadhi bidhaa hizo ndani ya nyumba.
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: / spotileo-176. .
HabariLeo: / habarileo
DailyNews: / dailynewstz
INSTAGRAM;
HabariLeo: habarileo_tz?ig...
SpotiLeo: spotileo?igshid...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: HabariLeo?s=09

Пікірлер

    Келесі