Prof. Joyce Ndalichako aungana na Ask Sospeter Ndenza kuhimiza wakristo kushiriki ibada ya CCT DAY

Prof. Joyce Ndalichako mbunge wa jimbo la Kasulu Mjini amesisitiza wakristo wote hasa wa makanisa wanachama CCT kushiriki kikamilifu katika maadhimisho ya CCT Day ambapo kilele ni Mei 26th 2024. Hayo ameyasema aliposhiriki Ibada ya maombi (mgeni rasmi) ya wanavyuo toka Mkoa wa Kigoma (USCF) ambayo yamefanyika katika Kanisa Kuu la KKKT Mjini Kasulu. Katika ibada hiyo Baba Ask Sospeter Ndenza ambaye ndiye mwenyekiti wa CCT Mkoa wa Kigoma ametoa ufafanuzi wa kila Wilaya kuadhimisha CCT Day wiki moja kabla ya Kilele ili kuwezesha Wilaya zote kushiriki ibada ya pamoja kimkoa siku ya Kilele cha Maadhimisho hayo. Zaburi 133:1

Пікірлер