NI HATARI!!! KASEKENYA ATIMBA MLIMA BUSUNZU // BARABARA YAKATIKA, AAGIZA HAYA KWA MKANDARASI

Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya amemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Kigoma kwa kushirikiana na Mkandarasi STECOL kuhakikisha wanaweka alama za tahadhari na kukagua mara kwa mara eneo la Mlima Busunzu sehemu ilipotokea changamoto ya kuharibika kwa kipande cha barabara chenye urefu wa takriban mita 100, wakati wakisubiri utatuzi wa kudumu kwenye eneo hilo.
Kasekenya ameelekeza hayo wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya Kabingo- Kasulu- Manyovu (Km 260), sehemu ya Mvugwe - Nduta (Km 59.35) na kueleza kuwa mkandarasi bado yupo eneo la mradi na kwa sasa anasubiri timu ya wataalamu inayofanya utafiti kuhusu kupata ufumbuzi wa tatizo hilo ili kuendelea na ujenzi katika kipande hicho.

Пікірлер: 1

  • @SelijusiMalambo-rh6sf
    @SelijusiMalambo-rh6sfАй бұрын

    Wachimbe wamwage mawe

Келесі