NGUVU IONGEZEKE KUDHIBITI WANYAMAPORI WANAOVAMIA MAKAZI YA WATU

Serikali imeombwa kuongeza nguvu katika kampeni za kudhibiti wanyamapori wanaolazimika kuvamia makazi ya watu tatzo ambalo licha ya kuchangiwa zaidi na mabadiliko ya tabianchi, linaendelea kuongeza umasikini na makali ya maisha kwa baadhi ya wananchi hasa walioko pembezoni.
Ombi hilo limetolewa na Kamshna Msaidizi wa Uhifadhi, Privatusi Kasisi alipokuwa akizungumzia baadhi ya changamoto zinazoendelea kujitokeza katika kampeni za kuwadhibiti wanyama hao ikiwemo ya mazingira magumu katika maeneo yaliyokithiri kwa migogoro.

Пікірлер