"HAKUNA KUPEWA MRADI MWINGINE..!", BASHUNGWA AWAONDOA WATAALAMU WOTE WA BARABARA YA KIBAONI - MLELE
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameagiza kuondolewa kwa wataalam wote wanaosimamia ujenzi wa Barabara ya Kibaoni - Sitalike, sehemu ya kwanza ya Kibaoni - Mlele (km 50) kwa kiwango cha lami kutokana na ujenzi wa mradi huo kusuasua na utekelezaji wake kuwa nyuma kwa asilimia 23.71.
Ameagiza kuondolewa kwa Wataalam wote wa Mhandisi Mshauri wa Mradi Kampuni ya Crown Tech, Msimamizi wa Mradi kutoka Makao makuu ya TANROADS, Eng. Ramadhan Myanzi pamoja na Msimamizi wa Mradi Mkoa wa Katavi, Eng. Albert Laizer.
Bashungwa ametoa agizo hilo Aprili 08, 2024 mkoani Katavi wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Kibaoni, Mkoani Katavi mara baada ya kukagua mradi huo ambao kwa sasa umefikia asilimia 14.7 na kutoridhishwa na kasi ya usimamizi na utekelezaji wa mradi huo.
Пікірлер: 16
Yeah!🇹🇿kwa staili hii Tanzania itaendelea.safi sana waziri.
Hongera sana sana waziri
Bashungwa upo juu sana hongera sanaa.. Big up
Kaka bashungwa nakubari njoo nadodo uwanja wandege msalato tunanyanyasika
Mzee mwenyewe ni mpole sana hafai
Namna hii nimependa utendaji wako waziri.
Piga kazi Jembe
Duh! Safi mkuu watu hawaamini kwamba Mambo hamebadilika wataelewa tu !
Hao Chico mkuu Hana maajabu hapo wameshakuwa waswahili
Mheshimiwa Bashunga pls Tunakuomba sana Pamoja na Kwamba unapambana huko Mikoani naomba nikuulize pale Muhimbili zile Barabara ya kuingia Muhimbili Dar Mjini kuna Chamoto gani? Maana pale wagonjwa wazazi wanaletwa na Ambulance 🚑 wako hoi yale Mashimo waziri mkuu alitoa maagizo , Makam wa Rais alitoa Maagizo tataizo liko wapi? Matengenezo
Tatizo ni makampuni ya usimamizi ndio changamoto.
Mijitu nimijizi mpaka basi alafu wananchi wana pelekeshwa kwa vitu vidogo tu yani
Kipande Cha SGR MAKOTOPORA ISAKA KAKA KIMELALA UJE UJIONEE
Mhe una sema local contractor Babaishazi umpe hawa Bado Utaona Mambo Zaidi. Uli nyima sisi Mpwapwa Gulwe umpe Hawa. We are not interested now wasting time of local contractor.
Hawa watu hawa wanatakiwa wafungwe jela sasa mlisomea upuuzi gani huko shule bora hata wapewe watu darasa la saba yaan watu ni wajinga mtu huwez kusimamia mambo na eti umepoteza ada zako kusomea kitu hiko kweli mimi najiamini kwa kule kusimamia msumamo wangu wa kwamba vyeti hainifanyi nimpe mtu kazi
Barabara ya pangani tanga inamiaka.15 haimaliziki sioni.watu.wakihoji.chochote.wala mawaziri ambao niwakazi.wa tanga wamekaa kimya sijui wanamatatizogani