Aziz KI amtumia salamu ‘Fei Toto’ kuelekea msimu ujao | Mavunde afunguka

Mchezaji wa Yanga yenye maskani yake mitaa ya Jangwani jijini Dar es Salaam Stephane Aziz KI amesema kuwa miongoni mwa vitu anavyofurahia ni kushuhudia michezo ya ndondo hapa Tanzania, kwa sababu vipaji vingi vinapatikana kwenye timu na ligi za mitaani.
Aziz KI amesema kuwa imani yake ni kuona Shirikisho la Soka Tanzania linaweza kupita chini na kuyatumia mashindano ya Ndondo kupata wachezaji wengi watakaoisaidia timu ya taifa ya Tanzania.
Mbali na hilo nyota huyo amempa salamu nyota wa zamani wa timu hiyo Feisal Salum 'Fei Toto' kuwa ajiandae vyema na msimu ujao kwani amefurahishwa na ushindani wa msimu huu.
Ameyasema hayo leo Juni 15, 2024 akiwa ameongozana na Djigui Diarra walipomtembelea Waziri wa Madini na Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde ambaye pia ni mfadhili wa mashindano ya Ujirani Mwema Ndondo Cup mkoani humo ili kuangalia maendeleo ya michezo jimboni kwake.

Пікірлер

    Келесі