"SIKUTAKI" MAKONDA AMTIMUA MENEJA WA RUWASA, AGUNDUA UBADHILIFU NA UONGO
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda amemtaka Meneja wa Mamlaka ya Maji sa fi na Usafi wa mazingira (Ruwasa) Wilaya ya Longido, Ramadhan Musiba kuwasiliana na bosi wake (Katibu Mkuu Wizara ya Maji) ili amuachishe kazi kwa kumdanganya mbele ya wananchi na kushindwa kufuatilia miradi ya maji anayotakiwa kuisimamia.
Hatua hiyo imefikiwa leo Mei 23, 2024 baada ya Makonda kufanya ziara ya kukagua Zahanati ya Leremeta iliyopo wilayani Longido na kugundua changamoto ya maji katika eneo hilo.
Akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa, Mwenyekiti wa Kijiji cha Leremeta Supuk Melita, amesema wamekuwa na changamoto zaidi ya miezi saba na wamekuwa wakitoa taarifa hiyo lakini hakuna kilichofanyiwa kazi.
Meneja huyo alipoulizwa na Makonda, amesema taarifa ya kutopatikana maji eneo hilo aliipata kwa wiki mbili zilizopita.
Baada ya taarifa hiyo, Makonda ameng’aka: "Mwenyekiti anasema amekwambia zaidi ya miezi mitatu alafu wewe unasema umepewa taarifa kwa wiki mbili, kwa umri wako unaona ni vizuri kudanganya? Mtafute katibu mkuu mwambie Makonda kasema sifai, hanitaki."
Пікірлер: 27
waaaaah,,, MAKONDA Ni Kiboko,,,be blessed 🙏🙏
Makonda you are the one
Jembe hilo huyu ndiyo mwanaume .
Vijana wapo mkuu
Makonda longido walichakachia sana sana
wanateuana wenyewe kwa wenyewe... wanatenguana wenyewe kwa wenyewe... kinachobakia ni sifa kwa viongozi, hasara kwa mali ya umma na shida kwa wananchi...
@jabirkasunzu6841
Ай бұрын
Tatizo wateuliwa wenyewe wanakengeuka, lawama kwa Rais.
😂😂😂daah huyu ndo MAKONDA sasa🙌🏼🙌🏼🙌🏼
@denisyohana8104
Ай бұрын
magufuli kafufuka,makonda yuko poa sana
Haya Mzee kalee wajukuu Sasa.. KAZI waachie vijana.. 😂😂
Kizee kibishi,😮😮
Huyu mzee namjua.huwaga hajui kusimamia kazi,mbishina ni muongo hivyohivyo
Anatakiwa astaafu!
Jamani mimi ngoja niendelee kuwa mjasiriamali maana ukiwa mzee kubali kufanya kazi zako binafsi
Makonda Jimbo la Ubungo linakungoja wanainchi tunakutaka.ulituombea Hospitali uliotuombea haijakamilika
Alishachoka huyo Mzee hakuna kitu aondoke tu
Kwanza huyu mzee anaonekana alidaganya umri mm nafikiri alitakiwa awe amestaafu Shida ndo hiyo huyo ni babu
Huu ndio mlima wa moto .
Dah we makonda unanikosha na kaz zako
Kaz km hizi zisingekuwa za uteuzi ....wasome watume cv wachujwe.......tafuteni korean movie ya son of concubine mjifunze.
@user-en5sg8bs4p
Ай бұрын
Ko pamoja nakuteuliwa unaisi anaelimu ya kitoto au unamzidi Mbona ww hujateuliwa acha kukalili maneno ya wanasiasa uyo ni injinia ni cv ndo zimefanya ateuliwe nenda naww wakuteuwe
Makonda siku ukimtumbuwa na yule mzee mkurugenzi wa arusha nitafurahi mnoooo.. nipo kanda ya ziwa ila kazi yako naikubali mjomba..
Namuona mlithi wa JPM kapatkana
@paulmaganga9700
Ай бұрын
Kabisa
Makonda.ubunge.huoooo 2025
@denisyohana8104
Ай бұрын
no ,uraisi
@denisyohana8104
Ай бұрын
sema ,mama angejua angepumzika tumpe nchi hii makonda