"RAIS SAMIA YUKO TAYARI KWA KATIBA MPYA LAKINI NASHANGAZWA NA WASAIDIZI WAKE" - WAKILI KIBAMBA

NA ALBERT G. SENGO/MWANZA
Mjadala kuhusu madai ya katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umepata msukumo mpya baada ya viongozi wa asasi za kiraia, wanafunzi kutoka vyuo vikuu na wanaharakati kuungana na wadau wa sekta mbalimbali jijini Mwanza kupaza sauti.
Mada kuu iliyowasilishwa katika mdahalo huo wa wazi wa siku moja ulofanyika jijini Mwanza ulikuwa ulikuwa umeegemea kwenye kichwa cha habari cha Mjadala wa Wazi Mchakato wa Upatikanaji wa Katiba Mpya.
Kutoka Jukwaa la Katiba Wakili Deus Kibamba anasema Rais Samia Suluhu Hassan katika matukio mbalimbali amewahi kutamka waziwazi kwamba yuko tayari kwa mabadiliko ya Katiba lakini wakili Kibamba anashindwa kuwaelewa wasaidizi wake.
Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA) Ananelia Nkya amezungumza namna jukwaa lake lilivyo jipanga tayari kwa mchakato huo saa yoyote.

Пікірлер

    Келесі