MKOA WA KIGOMA UTAKUWA MWANZO WA RELI KATIKA SEKTA YA MIUNDOMBINU

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya miundombinu ya barabara katika Mkoa wa Kigoma ili kuufanya Mkoa huo kuwa mwanzo wa reli na sio mwisho wa reli katika Sekta ya Miundombinu.
Bashungwa ameeleza hayo leo Julai 08, 2024 mbele ya wananchi wa eneo la Kazuramimba katika ziara ya Makamu wa Rais, Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango ya ukaguzi wa utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya Malagarasi - Ilunde - Uvinza Mkoani Kigoma.
#wizarayaujenzi

Пікірлер: 1

  • @mansooralaisri5200
    @mansooralaisri520013 күн бұрын

    Hizo kilomita 51 toka enzi za Kikwete mpaka Sasa Hazijatekelezwa. Bila kumpata makamu wa Raisi kutoka kigoma, ingekuwa mpaka Kiama.

Келесі