MAKONDA: "Endeleeni Kunitukana, ila Ukiitwa Kimbia Usisubiri Nikufate"

MAKONDA: "Endeleeni Kunitukana, ila Ukiitwa Kimbia Usisubiri Nikufate"
NI wiki ya kitimtim! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kutoa wito kwa wanawake waliotelekezewa watoto na wanaume kufika ofisini kwake, Ilala jijini Dar kwa ajili kupatiwa msaada wa kisheria.
Awali, zoezi hilo lililotarajiwa kudumu kwa takriban siku 5 mfululizo, lilianza kuchukua nafasi Jumatatu iliyopita ambapo mamia ya wanawake walijitokeza na kuifanya ofisi ya mkuu wa mkoa kufurika, hadi kufikia hatua ya kuzuia kwa muda safari za magari katika njia ambazo zinakutana katika ofisi hiyo.
Wanawake wasiopungua 480 walijitokeza ambapo kwa mujibu wa Makonda, 47 kati yao waliwataja waheshimiwa wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huku 14 wakiwa ni viongozi wa dini.
Akizungumza na wanahabari mara baada ya wanawake wengi kujitokeza na kusikilizwa na wanasheria mbalimbali pamoja na watu wa dawati la jinsia, Makonda alitoa wito kwa wanaume ambao wametajwa na wanawake wao waliowatelekeza, wajitokeze wenyewe ili kusikiliza kesi zao. Makonda alienda mbali zaidi kwa kuwataka wanaume ambao nao wametelekezewa watoto au wenye malalamiko mbalimbali dhidi ya wanawake, nao wafike ofisini kwake kwa ajili ya kusaidiwa.
WANAUME NAO WAJITOKEZA
Mara baada ya Makonda kutoa wito huo, Jumanne iliyopita wanaume walijitokeza katika ofisi yake na kutoa malalamiko mbalimbali.
Kuna ambao walidai kukimbiwa na wanawake wao kutokana na kuugua kwa muda mrefu, kuna wengine walilalamikia wake zao kugeuza nyumba kuwa danguro. Kama hiyo haitoshi, kuna mpiga picha maarufu wa Ilala jijini Dar, Vedasto Mdesa ambaye alisema amefika ofisini hapo ili kueleza jinsi alivyokimbiwa na mkewe.
“Mimi na mke wangu tulibahatika kuzaa watoto watatu, wawili wakiwa mapacha, mke wangu niliyezaa naye tulikutana hapa mjini akisoma Chuo Cha Kampala University na tulikuwa tunapendana lakini familia yake ndiyo haikukubali mimi kumuoa mwanamke huyo.
“Nimekuwa nikipata shida sana ya kukutana na mzazi mwenzangu kutokana na uchumi wangu kuwa mdogo kwani mimi ni mpigapicha tu eneo la Buguruni, nimekuwa nikipata vikwazo vingi kutokana na familia yangu kuwa ya kimaskini na mke wangu kutoka katika familia ya kitajiri, kiukweli mke wangu yeye anatoka familia ya kitajiri na ndugu zake wengine wanaishi Urusi na ndiyo hasa wanaosababisha mimi nisiishi na huyo mwanamke lakini bado nampenda na yeye ananipenda, cha msingi namuomba Makonda anisaidie niweze kurudishiwa familia yangu,” alisema paparazi huyo.
WATU WAKESHA
Kuonesha kwamba tatizo hilo ni kubwa, usiku wa kuamkia Jumatano, wapo akinamama ambao walidaiwa kukesha katika ofisi ya Makonda ili kuweza kuwahi foleni asubuhi na mapema.
lnstal GlobalPublishersApp Android: bit.ly/2AAQe1d iOS: apple.co/2Assf4M Subscribe / uwazi FACEBOOK: / globalpublis. .
TWITTER: / globalhabari Visit globalpublishers.co.tz/, Subscribe / uwazi1
kupata video nyingine za aina hii, subscribe kwenye chanell yetu kwa kubofya… / uwazi1 / uwazi1 / uwazi1 WEBSITE: globalpublishers.co.tz/ FACEBOOK: / globalpublis. . TWITTER: / globalhabari INSTAGRAM: / globalpubli .

Пікірлер: 74

  • @hamidajuma7804
    @hamidajuma78046 жыл бұрын

    Baba umewanyosha Wanaume wanaotelekeza watoto. Mwenyezi Mungu akubariki sana tena sana Makonda Makonda Baba Mwenyezi Mungu Akulipe

  • @emanuelngusa8161
    @emanuelngusa81616 жыл бұрын

    hongera sana mkuu wamkoa kwa jitihada zako, mh. makonda

  • @joasalfred4503
    @joasalfred45036 жыл бұрын

    Daaaaa.......wewe ni kiongozi wa namna ya pekee,piga kazi mkuu na Mungu akutetee akupe uzima tele na hekma na nguvu za kuendelea kuchapa kazi.

  • @dorahmathias5476
    @dorahmathias54766 жыл бұрын

    Asante makonda piga kaz baba Mungu atakuwezesha

  • @navoneiwamgonja9010
    @navoneiwamgonja90106 жыл бұрын

    Mungu akubariki ufanikishe ndoto zako

  • @AliM-di8dz
    @AliM-di8dz6 жыл бұрын

    Yaani wewe unafanya vitu vimekuzidi umri Wako, mungu awe nawe milele nakupenda sana

  • @leilainnocent6532
    @leilainnocent65326 жыл бұрын

    Barikiwa sana Makonda.

  • @dr.erickjmazyala8905
    @dr.erickjmazyala89056 жыл бұрын

    Makonda Mungu akujarie mafunuo zaidi! Mpaka vidume tuwe makini kutekeleza majukumu yetu!

  • @blandinamwarabu5025
    @blandinamwarabu50256 жыл бұрын

    We Makonda fanya kazi tu kwani wanaume wamezidi kutelekeza watoto watakaokuwa wanalalamika hajafikwa

  • @mamyabdalah885
    @mamyabdalah8856 жыл бұрын

    Asante sana mkuu mungu akubariki sana

  • @angelakundi1059
    @angelakundi10596 жыл бұрын

    Mungu akubariki kwa hili.

  • @henrykulwa6659
    @henrykulwa66596 жыл бұрын

    Asante makonda

  • @fortunatamfinanga287
    @fortunatamfinanga2876 жыл бұрын

    Kaziii nzuriiiiiiii

  • @hamidajuma7804
    @hamidajuma78046 жыл бұрын

    Anaekubeza hana hakili hata kidogo. Mwenyezi Mungu akuzidishie. wewe ni Jembe Kabisa. Rais magufuli Hajakosea kukuchagua. Tena wewe Umeletwa Mwenyezi Mungu Aje kutetea wanyonge. Abalikiwe Rais magufuli kukuchagua uwe mkuu wa mkoa wetu. wewe nijembe tuu.

  • @dinakidai4118
    @dinakidai41186 жыл бұрын

    yaaani Mungu akutunzeer

  • @mamyabdalah885
    @mamyabdalah8856 жыл бұрын

    Yani nakupenda makonda mpaka naumwa mungu akubariki sana

  • @victorsolomon2140
    @victorsolomon21406 жыл бұрын

    Big up sana makonda.

  • @wilsonkaseha2034
    @wilsonkaseha20346 жыл бұрын

    Yes dude! Piga kazi bruh!

  • @zainabualtz1455
    @zainabualtz14556 жыл бұрын

    😃😃😃😃😃 wambiee haoo Mungu akulinde kaka ata yesu alitukanwa sembuse ww

  • @masungakasanda3575
    @masungakasanda35756 жыл бұрын

    kwa kweli makonda chapa kazi maana kwenye jambo zuriii vipangimizi haziishi

  • @leilainnocent6532
    @leilainnocent65326 жыл бұрын

    Hata Yesu alitukanwa usiwaangalie hao wadhaifu.

  • @abuuhafsah9630
    @abuuhafsah96306 жыл бұрын

    makonda kweli were nice fundi....

  • @stevenmsaaada.msaada.389
    @stevenmsaaada.msaada.3896 жыл бұрын

    Uyu jamaa mungu amzidishie sana.

  • @AliM-di8dz
    @AliM-di8dz6 жыл бұрын

    Wewe ni mti Wa matunda mengi na nimatamu mno , mawe lazima utapigwa , vumilia mungu yupamoja sanaudikate tamaa.

  • @ednagagur7522

    @ednagagur7522

    6 жыл бұрын

    Ali M1966 àà8

  • @matobholwamanonu5919
    @matobholwamanonu59196 жыл бұрын

    Hivi wale walikuwa wanampinga makonda itakuwa wanamichepuka sana....

  • @samusonibalazingiza3689
    @samusonibalazingiza36896 жыл бұрын

    Yangu macho

  • @MarsUk-cg1gq
    @MarsUk-cg1gq6 жыл бұрын

    Vumilia na yote wanayo kukashifu kiukweli haifai KWA binadam kwani wao walio zaa na wakawatupa mahodari Sana mungu anaweza kuwanyanya na wakawa hawana hao watoto washenzi Sana tumewachoka kabisa

  • @nzumbimatondo4780
    @nzumbimatondo47806 жыл бұрын

    wanaokumeza kwa jambo hili ni wale wazinzi

  • @marwaiboroshaisombe6304
    @marwaiboroshaisombe63046 жыл бұрын

    mungu akuongezee ujasili wazidi kuuliza unautoa hwezi kktotoresha wanawake Kama vifaranga alaf klea hataki

  • @danielbugwema6969

    @danielbugwema6969

    6 жыл бұрын

    Hata nakuja nimetelekezwa Mkuu maana hata mama zetu wametufanya tuonekani mayatima

  • @user-oh8bn3vg2w
    @user-oh8bn3vg2w6 жыл бұрын

    Hongera sana kaka nipo oman ningeungana naww maana nimetelekezewa mtoto pia nimefurahi sana kwakulitambua Hilo jukumu Mungu ibariki Tanzania

  • @shamsaismail7707

    @shamsaismail7707

    6 жыл бұрын

    سلمى سيف Mungu akubariki Makonda na akuzidishie Afya njema Akulinde na kila baya (IN-SHAA-ALLAH )

  • @wazirihongo3761

    @wazirihongo3761

    6 жыл бұрын

    سلمى سيف ي سلمي تقوآله

  • @japhetsamwelmangala8224

    @japhetsamwelmangala8224

    6 жыл бұрын

    fanya kazi kaka usitazame sura za watu

  • @dianahamischi3417

    @dianahamischi3417

    6 жыл бұрын

    سلمى سيفnambie dada uko oman sehem gan

  • @ibrahimwerejuma4816
    @ibrahimwerejuma48166 жыл бұрын

    Watanzania mimi ni mkenya lakini nawaomba baada ya rais Magufuli kumaliza muhula wake naomba uchaguzi ujao muidhinishe huyu makonda awe rais wa tanzania.

  • @emanuelmlowe6854
    @emanuelmlowe68546 жыл бұрын

    Viongozi wanatakiwa kuwa kama makonda mbunifu sana, wabuni mbinu mbali mbali kutatua matatizo ya wananchi

  • @samsonmwaipwisi313

    @samsonmwaipwisi313

    6 жыл бұрын

    Emanuel Mlowe Hakuna kiongozi hapo

  • @tedisangaa8886
    @tedisangaa88866 жыл бұрын

    Watu wanakazana kuwa wanaume wanatelekeza watoto nao Dada zetu wamezidi kuvuvua

  • @saidsaid9463
    @saidsaid94636 жыл бұрын

    Hapo sawa watajielewa

  • @saidsaid9463

    @saidsaid9463

    6 жыл бұрын

    Augustine Mhangazo hivyohvyo mh pongezi kwako

  • @mayungakidoyayi9566

    @mayungakidoyayi9566

    6 жыл бұрын

    Wewe ni jembe piga kazi usigeuke nyuma utakua jiwe songa mbele

  • @emanuelmlowe6854
    @emanuelmlowe68546 жыл бұрын

    Wazinzi wanachukia makonda.

  • @geoffrieymollel2178
    @geoffrieymollel21786 жыл бұрын

    Makonda sio karma anabuni mambo haha, la hasha duniani kote Kuna sheria ya haki ya mtoto kulelewa na baba na mama awe hawara mchepuko au wa ndoa. Huko Ktk nchi zingine inaitwa " child support" tena kwa taarifa ni kwamba, kama baba unafanya kazi serikali inakata mkwanja huko huko , wewe unapewa taarifa tu. Good job Makonda , chapa kazi .

  • @MarsUk-cg1gq
    @MarsUk-cg1gq6 жыл бұрын

    Makonda furahi tuu usijali tupo na wewe Kaka moendwa tunakupenda Sana na utalipwa na mungu unayo huzuni Ila unafuraha Sana moyoni mwako

  • @stevenjackson1582
    @stevenjackson15826 жыл бұрын

    Mr makonda endelea kushika msimamo huo kwa ustawi WA taifa letu akina mama wakiwa na furaha nchi yetu itakuwa na amani akina mama wakiwa na hasira hakuna amani ya kweli.

  • @kallahassan4896
    @kallahassan48966 жыл бұрын

    huyu jamaa kweli nikiongozi

  • @emanuelmlowe6854
    @emanuelmlowe68546 жыл бұрын

    Wabunge wanapoenda kwe bye vikao wengi WAP huchukua wanafunzi Na makahaba Kyle dodoma

  • @denismgashe5989
    @denismgashe59896 жыл бұрын

    Balkiwa baba umetenda jambo jema na mama zetu nao wapumue

  • @merymrema420
    @merymrema4206 жыл бұрын

    MUNGU akuwezeshe makonda

  • @AdamSaffi211
    @AdamSaffi211 Жыл бұрын

    We miss you! What did he do to be dumped like that.

  • @emanuelmlowe6854
    @emanuelmlowe68546 жыл бұрын

    Vikao Viki anza machangudoa nao huhamia Dodoma, nao niwabunge? Au ndowahudum wao?

  • @wahazaben7964
    @wahazaben79646 жыл бұрын

    Kweli itaishi milele ukiamua kutenda haki tenda haki katika mambo yote what about rule of law

  • @zulfamnzava6735
    @zulfamnzava67356 жыл бұрын

    Tuko pamoja MKUU hata Mimi nimetelekezwa na baba ila namuachia mungu

  • @hassanrwitita2503
    @hassanrwitita25036 жыл бұрын

    Lakini uzae angalau kamoja kwani unatoa mapovu lakini unaongea kibata kama bata fulani usimtaje sna mungu kwani we mwenyewe u ndumilakuwili

  • @utukufueliya5279
    @utukufueliya52796 жыл бұрын

    ni aibu kwa wabunge wa ccm kuungana na lowasa

  • @MarsUk-cg1gq
    @MarsUk-cg1gq6 жыл бұрын

    Wanajidai kuficha Moto wakati moshi unaonekana wapuuzi achana nao

  • @emanuelmlowe6854
    @emanuelmlowe68546 жыл бұрын

    Michepuko cy ishu

  • @catherinekanyangali4940
    @catherinekanyangali49406 жыл бұрын

    wacha waongee huwezi kumzuia binadamu mwenye kinywa

  • @abuuhafsah9630
    @abuuhafsah96306 жыл бұрын

    makonda shkamoo

  • @abuuhafsah9630

    @abuuhafsah9630

    6 жыл бұрын

    nimekuelewa mzee baba... umetisha ndugu yangu

  • @ceciliajimmy5652
    @ceciliajimmy56526 жыл бұрын

    Kanuni na taratibu zifuatwe.

  • @philipongenzatv
    @philipongenzatv6 жыл бұрын

    Toka inch iundwe hakuna mkuu was mkoa aliyefanya ivoo

  • @youngdonnyhalf-life9175
    @youngdonnyhalf-life91756 жыл бұрын

    fanya kazi kiongozi those are normal challenges

  • @Manfilly

    @Manfilly

    6 жыл бұрын

    Young Donny Half-Life True

  • @salmadashlaquimanelaquiman4427
    @salmadashlaquimanelaquiman44276 жыл бұрын

    Piga kaz kka

  • @mamyabdalah885
    @mamyabdalah8856 жыл бұрын

    Wanao mbeza huyu makonda ni wajinga tuu huwezi mtukana kiongozi kama huyu anae tetea wanyonge wajinga tuu piga kazi baba

  • @jeftajosiah40
    @jeftajosiah406 жыл бұрын

    Penda Sana makona we nikomesha wajinga

  • @kuchiafricancinema
    @kuchiafricancinema6 жыл бұрын

    Shoga huyu anawatesa wanawake mbulula

  • @isackandrew8620

    @isackandrew8620

    6 жыл бұрын

    Saddy Junior Unamjuaje kama c na ww shoga achakutukana mtu anaesimamia majukumu yake

  • @laymapeace4538
    @laymapeace45386 жыл бұрын

    boya tu wewe makonda karekebishe kwanza familia yako

  • @jamyjandro8901

    @jamyjandro8901

    6 жыл бұрын

    Mwazan Gomaa boya mwenywe ndo nyie mnao telekeza watoto bwege weeeee kubali tu yaisheeeee nini kupingaa ukwelii

Келесі