KCMC wafunguka wanavyohangaika kumtafuta muuguzi aliyetoweka

Muuguzi wa afya katika Hospitali ya KCMC, Lenga Masunga Ng'hajabu anadaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha baada ya kutoonekana kazini kwa siku 5 huku simu zake za mkononi zikiwa hazipatikani.
Ng'hajabu ambaye ni Muuguzi katika idara ya masikio, pua na koo katika hospitali hiyo, anadaiwa kutoonekana kazini tangu Julai 4, mwaka huu ambapo mpaka sasa hajulikani alipo.
Mwananchi digital leo ilifika katika hospitali hiyo na kuongea na Ofisa Uhusiano wa hospitali hiyo, Gabriel Chisseo akizungumzia juu ya tukio hilo afisa uhusiano wa hospitali hiyo amesema muuguzi huyo ametoweka tangu tarehe 3 mwezi julai mwaka huu na mpaka sasa hakuna taarifa inayotia matumaini huku simu zake zikiwa hazipatikani.
Mwananchi Digital haikushia hapo ilienda kutembelea makazi yake anapoishi na kuongea na mwenye nyumba, Robert Mwakalinga ambae Ng'ahabu alikuwa anaishi kama mpangaji amesema mara ya mwisho kumuona ni siku ya jumanne na hakutoka lakini asubuhi alikuta mlango upo wazi hali ambayo haikua ya kawaida.

Пікірлер: 13

  • @Lanihsarumu
    @Lanihsarumu4 күн бұрын

    Mungu mlindinde arudi salama

  • @salomekense525
    @salomekense52513 күн бұрын

    Mungu wetu ni mwema atamrudisha Sama.

  • @ruqaiamohammed345
    @ruqaiamohammed34512 күн бұрын

    Uko wap kaka mungu akuweke huko uliko salama 😢

  • @user-xo4gl3we1t
    @user-xo4gl3we1t12 күн бұрын

    jamani Mungu tunaomba ufanye muujiza kaka yetu awe mzima. Mahali alipo arudi

  • @dismasmariananga4776
    @dismasmariananga477612 күн бұрын

    Mungu mulinde Usk na mchana arudi salama na awe na afya njema

  • @VeronicaMacha-pl3xt
    @VeronicaMacha-pl3xt12 күн бұрын

    Kwani huyo mwanamke aliyekuwa anaishi naye yuko wapi wakati huu?

  • @VeronicaMacha-pl3xt
    @VeronicaMacha-pl3xt12 күн бұрын

    Mungu akulinde huko uliko mja wake

  • @user-xk7vy4gb6g
    @user-xk7vy4gb6g12 күн бұрын

    Atafutwe huyo mchumbaake. Mungu amlinde huko aliko

  • @mtzhalisi2232
    @mtzhalisi223212 күн бұрын

    Mungu afanye wepesi

  • @nsiamasawe4578
    @nsiamasawe457812 күн бұрын

    Ee Mungu tunaomba umtunze mahali alipo.

  • @nsiamasawe4578
    @nsiamasawe457812 күн бұрын

    Huyo msichana wake atafutwe

  • @ibrahimkasim922
    @ibrahimkasim92212 күн бұрын

    Duuh😢

  • @DativaMbowe
    @DativaMbowe10 күн бұрын

    Abananishwe uyo mchumba ake,

Келесі