Sizonje - Mrisho Mpoto ft Banana Zorro (Official Video)

Музыка

Nyimbo Mpya ya Mwaka 2016, Sizonje.
[Kibwagizo - Banana Zorro]
Sizonje hii ndio nyumba yetu
Milango ipo wanapita madirishani
Sizonje ndio nyumba yetu
Milango ipo wanapita madirishani
Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
[Bridge - Banana Zorro]
Tulikaa barazani, tukasikia kelele
Kelele toka ndani, mtu anaruka dirishani
Sizonje, karibu nyumbani kwetu
Uone maajabu ya nyumba yetu
[Verse 1 - Mrisho Mpoto]
Karibu sana Sizonje, hii ndo nyumba yetu,
Tulipoficha mundu za kupondea wezi,
Kwani, makaburi yaliofukuliwa lazima yazikwe upya?
Nyumba hii Sizonje ina vyumba vinne,
Vitatu havifunguki, kimoja hakina mlango,
Japo kuwa kina watu ndani, na hawaongei kiswahili,
Wenyeji wanalala sebleni na walishazoea,
Sizonje kule tulipotoka panaitwa jikoni,
Huna haja ya kwenda kule, kumejaa mafundi wa kupika
Sasa hivi wanakupikia wewe ili ule ulale
Ukiamka muongee nini hasa ujio na dhima ya safari yako
Wanashangaa mbona ghafla
Samahani sana mgeni
Wapishi wameniomba kwamba
Nikuulize tena kwa kukuomba kwamba
Eti unapenda vya mafuta au vya nazi?
Wanataka kukuonyesha madoido katika mapishi yao Sizonje
Sizonje chumba hiki naomba usiingie
Ukimaliza nitakwambia kwanini
Kuna sauti inajirudia mara kwa mara
Na hapa mlangoni kulikuwa na picha mbili kubwa
Moja picha, nyingine mchoro wa picha wa kwanza
Ninachokumbuka iliwahi kuandikwa
“USIYEMTAKA KAJA”
Hatukuwahi kuelewa maana yake
Labda kwa sababu ya ujio wako unaweza kutusaidia
[Chorus - Banana Zorro]
Sizonje hii ndio nyumba yetu
Milango ipo wanapita madirishani
Sizonje hii ndio nyumba yetu
Milango ipo wanapita madirishani
Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
[Verse 2 - Mrisho Mpoto]
Najua, wimbo mbaya haufai kubembelezea mtoto
Na kamwe mtoto hawezi kuungua
Kwa kiazi kilichokuwa kwenye kiganja cha mama yake mzazi
Njoo huku uone Sizonje
Si unajua, harufu ya uzazi haiishi mpaka mtoto akue?
Sawa, Sizonje, huu hapa ni ua
Lile pale ni shimo la taka
Na kile pale ni choo
Kinachotutisha na kutuogopesha zaidi
Wanaoishi humu ndani hawajawahi kutupa taka
Wala kwenda chooni
Kama ukiwa makini
Kwa nje utasikia sauti za makundi ya watu
Wengi ni vijana, wana bahasha za khaki mikononi
“KAMA HAMTUPI TAKA SHIMO HILI MLICHIMBA LA NINI?”
Lakini pia kwenye sauti zao, Sizonje
Kuna watoto, wazee na kina mama
Ukiunganisha sauti zao ndio unapata hizo kelele
Ninavyosikia, ila sina uhakika
Waliambiwa kihistoria nyumba hii ni ya kwao
Na wana haki ya kutupa taka na kutumia choo hiki
Sasa, njoo nikuonyeshe huku uchochoroni
Uone maajabu mengine ya nyumba hii
Sizonje, ukiona tembo anaringa
Ujue mvua zinakaribia
[Chorus - Banana Zorro]
Sizonje hii ndio nyumba yetu
Milango ipo wanapita madirishani
Sizonje ndio nyumba yetu
Milango ipo wanapita madirishani
Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu

Пікірлер: 407

  • @kombakomba7922
    @kombakomba79223 жыл бұрын

    Nyumba ni nchi,kwa nje inatafsirika na kuonekana ni maskini ila ndani ina utajiri mkubwaa,ila inaibiwa na manyemera wanaopita njia za panya kuiba rasilimali zetu, pia undugunization kwenye ajira ni tatizo,afya za kina mama na watoto,uchumi,rushwa na uwajibikaji ila sizonje ushafika umekomesha hayo yote. Hongera sana sana Mrisho na hongera kwa Sizonje.

  • @Richplumbing11

    @Richplumbing11

    2 жыл бұрын

    Leo ndio nimeielewa atari sana uyu jamaa

  • @tengezashemisea1787

    @tengezashemisea1787

    2 жыл бұрын

    Hongera mrisho, ila bado mwendo hujaumaliza endelea kuwa kumbusha wenye dhamana , hakika bado tunakuhitaji.

  • @alvinmuthui

    @alvinmuthui

    2 жыл бұрын

    Elenzea zaidi tafadhali

  • @user-rd7jt1vi5x

    @user-rd7jt1vi5x

    2 жыл бұрын

    duuuuuuh kumbe ndo nimejua leo hii maana ya wimbo huu

  • @bonfacemark9048

    @bonfacemark9048

    Жыл бұрын

    Asante kwa tafsiri yako ndugu from 🇰🇪 🙏

  • @upendorealestateagentintan190
    @upendorealestateagentintan1906 ай бұрын

    Mjomba Tanzania imekumiss sana. Tunaamini bado unatupenda yapo mengi tunahitaji utusemee hasa ktk wakati huu.

  • @stephanokigosi656
    @stephanokigosi6562 жыл бұрын

    huu wimbo ulikuwa special to MAGUFULI..Rest in paradise our icon 🕯🕯😭😭

  • @mariammalendeja370
    @mariammalendeja37011 ай бұрын

    nyimbo hii ulimuimbia maghufuli nae akaskia sauti yako akawaadhibu wadhalimu hadi wakaanza kupitia mlangoni r.i.p maghufuli tutakukumbuka milele

  • @jimmyfredmwanswaswa4562
    @jimmyfredmwanswaswa45622 жыл бұрын

    Tutolee nyimbo nyingine nzuri kama hii Mrisho! Asante kwa kutufundisha Kiswahili na utunzi! Mashairi Yako natamani watoto wetu wayasome shuleni!

  • @jodasonudavis1131
    @jodasonudavis11317 жыл бұрын

    MLANGO UPO WANAPITA MADIRISHANI.... ..kwamba Kuna utaratibu wa kufikia jambo fulani Ila watu hutumia njia za mkato(rushwa) kupata jambo hilo.....SHIMO HALITUPWI TAKA WALA HAWAENDI CHOO... maana yake Kuna mfumo wa watu kustaafu Lakini Kuna watu hawaachii nyazifa na pia kuna kazi fulani hivi zimekuwa za koo fulani wanarithishana kutoka kwa baba then mtoto hatimae mjukuu mfano(benki kuu) na hivyo kusababisha vilio vya vijana wengi wasomi kuzunguka na bahasha kwa kutafuta ajira na ajira hamna.......This is the best literature song I ever meet. Good work for this guy

  • @martinnsuhuje4391

    @martinnsuhuje4391

    7 жыл бұрын

    Asante kwa kufafanua kidogo nadhan umesoma kiswahili vzr

  • @jodasonudavis1131

    @jodasonudavis1131

    7 жыл бұрын

    Sikuachwa nyuma sana katika fasihi

  • @davidomemu471

    @davidomemu471

    7 жыл бұрын

    Nakubaliana nawe Jodasonu kabisa, the best oral lit, of modern time, big up MPOTO.

  • @khadijambuta4360

    @khadijambuta4360

    7 жыл бұрын

    Jodasonu Davis yani huko benk kuu ndio ucseme watu wapitishana tu msemo wao hpa kaz tu

  • @doreenmalesi6039

    @doreenmalesi6039

    6 жыл бұрын

    Asante kwa kunifafanulia

  • @kenneth.m.siwale9699
    @kenneth.m.siwale96995 жыл бұрын

    Pamoja na hayo mjomba Mpoto,leo hii nikiwa natokea kwenye kilele cha sherehe ya kilele cha miaka mia moja ya vita kuu ya Dunia ya kwanza! Mjomba Mpoto nimelazimika kutumia au kuiba jumbe zako hizi kwa mapenzi na ujumbe sahihi kwa wakati mwafaka hasa hapa kwetu Zambia!

  • @kenneth.m.siwale9699
    @kenneth.m.siwale96995 жыл бұрын

    Mjomba Mpoto utaniwia radhi kwakweki mjomba uliwahi kuniliza enzi za awamu ya nne ya Mzee wetu Dr. wa Ukweli wa Msoga, niliwahi kulia na kucheza sana pala LUGOBA!ulikuwa wimbo Adela,na Sasa hivi SIZONJE huu si tu ni wimbo ni FASIHI KALI!!!!. Wewe kweli ni aina ya akina Shaban Robart

  • @phillies846
    @phillies8468 жыл бұрын

    Mrisho mwalimu wako wa kiswahili alikuwa anapata shida saana kwa kukosolewa na wewe 🙏🏽 amen

  • @merryn4891

    @merryn4891

    6 жыл бұрын

    😀😀😀😀

  • @ssur5797

    @ssur5797

    5 жыл бұрын

    Nampnda mpka bac huyu kaka mola ampe umri mrefu wenye kheri ishllh

  • @catenzeki678

    @catenzeki678

    5 жыл бұрын

    @S Sur AMINA

  • @user-zl1im3og6r
    @user-zl1im3og6r4 ай бұрын

    Ila mpoto I nyimbo nimekuja kuelewa leo trh 5-3-2024😂😂😂

  • @Gbril45

    @Gbril45

    4 ай бұрын

    Inamaanishi nini kwani? Mimi bado naangaika

  • @msafirisalehe563
    @msafirisalehe5637 жыл бұрын

    Kama umesoma sana vitabu vya Hayati Shabani Robert,hakika hutokuwa na kazi kubwa ya kumuelewa Mpoto.

  • @nyabisemaro2095
    @nyabisemaro20956 жыл бұрын

    Mrisho Unajitahidi sanaaaa kusema kweli nazipenda nyimbo zakooo hasa Sizonje,kitendawili,nikipata nauli,Waiteee nk

  • @eusebiusjmikongoti6625
    @eusebiusjmikongoti66257 жыл бұрын

    Nakukukubali sana mtaalamu Mjomba, kazi zako huwa zina nipa shida kuzielewa lakini huwa nakuelewa taratibu. Ninahisi hakuna kazi niliyowahi kukuelewa kwa 100% maana kila nikirudia kusikia wimbo fulani huwa naongeza kitu fulani kutoka humo! Wewe ni Shaaban Robert wa pili kwakweli, yapasa nawe uandike kitabu cha KUSADIKIKA kama mzee Shaaban, sijui utakiita SIZONJE....., au NYUMBA YETU!

  • @allyhussein516
    @allyhussein5165 жыл бұрын

    Bila akili ya ziada kwa mrisho mpoto hutoki na kitu njooni tuungane jaman gonga like hapa kama umeikubali hii

  • @thedoctor8301
    @thedoctor83018 жыл бұрын

    SIKU ZOTE MWENYE HEKIMA HANUKI MDOMO NA MWENYE AKILI HASEMI NDANI YA MAJI.... HESHIMA KWAKO MR MPOTO NATAMANI NIJIFUNZE ZAIDI TOKA KWAKO.

  • @IrineKimaro
    @IrineKimaroАй бұрын

    Mjomba tumemiss mashairi yako, come back legend

  • @fatmafetty4117
    @fatmafetty41174 жыл бұрын

    Sizonje naipenda mnoo sichoki kuiangalia wallah love u bro mrisho ❤️❤️❤️❤️❤️ kazi nzur sanaaaa👌👌👌👌👌👌

  • @fatmafetty4117

    @fatmafetty4117

    4 жыл бұрын

    @@rashidikufinyu444 pouwa

  • @davidomemu471
    @davidomemu4717 жыл бұрын

    Mjomba, kwa kweli nyumba za Africa mashariki zina mambo na maajabu, zaidi hapa Kenya.

  • @rosenamilia4140
    @rosenamilia41402 жыл бұрын

    Sizonje ni jina la HAYATI JOHN POMBE MAGUFULI,alilopewa na Ndugu yetu msanii Mrisho Mpoto.Nyumba ktk wimbo huu ni IKULU YA RAIS MAGOGONI Dar es Salaam.

  • @mwangacharles8474
    @mwangacharles84748 жыл бұрын

    Kaka hongera sana kaka, nimeielewa sana nyimbo hiii, hasa choo kipo lakini hakitumikiiii. Unatisha kaka.

  • @abukiczan6600
    @abukiczan66007 жыл бұрын

    Mwenye akili ndogo hawezi elewa nyimbo zako but wewe ni zaidi ya msaniu hapa afrika na natamani siku nikukumbatie kwa furaha. U are the best mjomba

  • @kihanda2554
    @kihanda25548 жыл бұрын

    Long live Mrisho mpoto. Nimekuelewa vzr mnooo. Mfumbie mtoto mkubwa ang'amue

  • @rumbikamachumu3292
    @rumbikamachumu32928 жыл бұрын

    one of the best video and nice message to Tanzanian. kazi nzuri Mjomba endelea kuelimisha ,kufundisha na kukosoa jamii

  • @barackolgeno1076
    @barackolgeno10768 жыл бұрын

    this guy is marvellous... your Tanzanian fan from Australia

  • @samwelmkondo10

    @samwelmkondo10

    6 жыл бұрын

    We are together

  • @solangeramadhani4038
    @solangeramadhani403811 ай бұрын

    Duuuh miaka nenda miaka rudi leo ssa ndonimeelewa maan ya huu winbo

  • @eliatalented7592
    @eliatalented75924 жыл бұрын

    Who else is still here in 2019

  • @zulferabour607
    @zulferabour6074 жыл бұрын

    Wakati leo nasom kiswahil ....mwalim wanv kantolea mfano wa mwanafasihi anaetumja lugh y fasihi kufikish ujumb ktm jamii....ndipo akntajia huu wimbo ....hap nmeelewa kwann mrisho umeamua kutmia lugha hii....hongera sana

  • @anitaphilip2070
    @anitaphilip20708 жыл бұрын

    upenda Wangu nimependa kilakitu wanao sema sinzuri wajaribu nawao tuona zao zitakuaje

  • @nelsonkimutai5526
    @nelsonkimutai55264 жыл бұрын

    I love the patriotism in this guys music,

  • @hermanngaiza9327
    @hermanngaiza93278 жыл бұрын

    Kiukweli wimbo umetulia una ujumbe wa maana sana.ukionesha kwamba tuwe na nguvu na kupambana ahsante brother Mpoto

  • @mhonamisaomar7011
    @mhonamisaomar70118 жыл бұрын

    ukiisikiliza mankini itailewa 2..hongera. mjomba coz umenifanya ninitulie xanaa kukusikiliza Na kufafanua..wakuache jomba..nakusikiliza. mwana Kenya nikiwa saudia nimetua mankini..

  • @muddysimba887
    @muddysimba8874 жыл бұрын

    Yuliopo hapa 2020 tupia like

  • @isackyakobo7829
    @isackyakobo78294 жыл бұрын

    Asante sizonje, Kwa sasa wenye nyumba tunalala vyumban piah, Magufuli Oyeeee! Bahasha za kaki tu ndo bado ila karbu tena 2020, ulitatue na hlo! Kwa sasa hawapt madrishan tena,

  • @richardjuma7708

    @richardjuma7708

    4 жыл бұрын

    Hatari sana

  • @nyabisemaro2095
    @nyabisemaro20956 жыл бұрын

    Wana fasihi tupo tunakuewaga sanaaaa Asante MWL wanguu wa kiswahili MWL MACHUMU, MWL Alexander na PRISCA Bila nyie mm nisingejuaaa ujumbe wa mpoto Mbarikiwe sanaaa

  • @dorcasgitari8278
    @dorcasgitari82787 жыл бұрын

    Nimeingia nami nimeyaona maaaajabu ya nyumba yenu I say...great poetical pieces. Wengi waaalewa maaana ila kwa vile ina wachoma basi wanajifanya kutoelewa I say. He heeeeee.

  • @xxlnairobitv9503
    @xxlnairobitv95038 жыл бұрын

    Can't get enough of this song. Good Job. From Nairobi Kenya.

  • @neykapoor5871
    @neykapoor58712 жыл бұрын

    Artist is more beautiful because one thing can bring different meaning and understanding as what it is in this song of. Sizonje salute mrisho mpoto

  • @abdulhalim5950
    @abdulhalim59508 жыл бұрын

    nyimbo kamuimbia MAGUFULI kama anamgahamisha kua nchi ya Tanzania ina maajabu mfano vijana wamesoma ila hakuna ajira. aliposema. " watu huja na bahasha za kaki na kuhoji kama hamtupi taka shimoni. Pia kamfahamisha kua wahalifu waliokuwemo nchini hawaadhibiwi. mfano akiposema- " watu wa nyumba hii hawaendi chooni wala jalalani kutupa taka shimoni

  • @husseinhassainlugeje6042

    @husseinhassainlugeje6042

    6 жыл бұрын

    Asante

  • @eliyadigasson6679

    @eliyadigasson6679

    4 жыл бұрын

    Vr good

  • @silassambia876
    @silassambia8764 жыл бұрын

    My all time Tanzanian Artist..love from🇰🇪

  • @ezekielbituro7969
    @ezekielbituro79698 жыл бұрын

    nimeilewa asee...mashairi yanaeleweka kiasi! HII NDO TANZANIA

  • @ernestshaha1932
    @ernestshaha19324 жыл бұрын

    Huu wimbo nimeusikiza Mara 7 sai Mjomba juu wimbo unamafundisho saana

  • @user-ge3vd3it8f
    @user-ge3vd3it8f Жыл бұрын

    Dah!!na mkubali sana mrisho miaka 7 imepita nasikia wimbo huu ila leo ndo mmeelewa sahihi ya wimbo huu

  • @Nairobipicturesstudios
    @Nairobipicturesstudios2 жыл бұрын

    Alaaah! Mrisho wanidekua kwa mishororo na ushairi wako kila tungo lanijenga ajabu. mie nasoma sana fan wako mpya hapa toka Kenya.

  • @mabudaissere2295

    @mabudaissere2295

    4 ай бұрын

    Ana kiazi cha moto mdomoni ataimbaje sasa

  • @johannesshornest4916
    @johannesshornest49168 жыл бұрын

    we unayesema amealibu au angemuonesha sizonje auna uelewa kumbuka wimbo uu ni fumbo akikuonyesha sizonje utaelewa yeye mpoto anatupa mtiani tumjue sizonje ni nani kua mwelewa sio unakulupuka kuongea tu au unadhani mpoto ni sawa na wale wa mpenzi nakupenda

  • @bitaetenge3989

    @bitaetenge3989

    7 жыл бұрын

    Johanness Hornest Mbona hote mnabaki jujuhu majela yamejengwa lakini wafisadi wakubwa ambao wangefaha watupwe na kuozea huko kama kinyesi kinavyo hozea chohoni awatupwi huko. Wasomi wanaho maliza awapewi kazi wanashinda waki zunguka mahogisini lakini awapati milango. Sizonje niserekali na nyumba ni inchi. Sio Tanzania tu Africa yote.

  • @spinxoentertainment6168
    @spinxoentertainment61683 жыл бұрын

    From the collabo with harmonize then I like mrisho the kind of creativity is on another level

  • @JosephatJuma-dj5tq
    @JosephatJuma-dj5tqАй бұрын

    Mjomba hapa Kenya unapendwa kakangu

  • @leonardcharles3169
    @leonardcharles31698 жыл бұрын

    video ni nzuri, tuendelee kumpigia kura tuzo ya kola! wonderful video,

  • @sirialemmy37

    @sirialemmy37

    8 жыл бұрын

    Yes Leonard!

  • @bwakilamychanel5951
    @bwakilamychanel59515 жыл бұрын

    sizonje hii ndiyo nyumba yetu ingia uyaone hapa anaizungumzia tz yetu jinsi watu wanavyopenda rushwa na kurisishana madaraka na wakat kila mtu ana haki

  • @salumkanju1732
    @salumkanju17327 жыл бұрын

    daah kwa sisi tuliosoma arts aisee mzee mpoto unatisha baba angu.....nakutamani san katik matumizi ya lugha na hasa lugha ya picha kikubwa zaidi ni hiyo nyumba yaudongo lakin ndani noouma!! bila shaka watanzania waliotazama video hii wamejifunza kitu, binafsi sanaa yako sio tu kiburudisho kwangu maana najifunza mengi san na ni miongoni mwa mhimili wa utamaduni wa nchi yetu! unaimba kwa kusoma upepo unavyovuma ila ulituomba nauli ili uwende kwa mjomba na je sizonje ni naniiiiiii?

  • @williammwajeka3347
    @williammwajeka33478 жыл бұрын

    "Najua, wimbo mbaya haufai kumbelezea mtoto, Na kamwe mtt hawez kuungua kwa kiaz kilichokua kweny kiganja cha mama yake mzazi, Njoo huk uone sizonje Siunajua, harufu ya uzaz haiish mpk mtt akue? Haa haa haa daahh mpoto unaandk xn, hongr xn kwa uandsh Mzur, nazkubal xn nyimbo zko ✋✋✋✋

  • @jameskamau9026
    @jameskamau90267 жыл бұрын

    mrisho mpoto kwa hakika nyimo zako za burudisha hasa katika matumizi la lugha yetu teule kiswahili

  • @abbouramsey154
    @abbouramsey1548 жыл бұрын

    Apo Godfather au nenene? bonge la kichupa straight to Urban top Ten

  • @FredySokolo
    @FredySokolo2 ай бұрын

    Kiongozzzz unajua sana ,sasa sijajua umesoma kiswahili sana au mimi ndio btplms

  • @wilhardjohn8287
    @wilhardjohn82878 жыл бұрын

    huyu hanscana ni director anayejielew pengine kuliko wote kwa sasa young but a real inspiration in music industry

  • @ezrambilinyi6788
    @ezrambilinyi67883 жыл бұрын

    Mhhh ngoja niseme ukweli tuuu. Ni miaka 3 now nasikiliza nyimbo za huyu jamaaa cjawai elewa anae elewa anielekezeee

  • @Catherinemichael1995

    @Catherinemichael1995

    2 жыл бұрын

    Amemaanisha kuwa nchi inaonekana masikin wakati ndani yake inautajir tena amemaanisha sheria ipo lkn watu wanatumia njia ya mkato ameelezea mambo mengi

  • @kedmondkepha7707
    @kedmondkepha77075 жыл бұрын

    Daaaaaaah mjomba ulisomea wapi kiswahili chako maana hayo mashairi yako hakuna anaeyaweza duuu big up sana mziki wako ni wa kibantu zaid

  • @immaculatecheroprono9670
    @immaculatecheroprono96702 жыл бұрын

    I cannot get enough of your poetry articulations in your songs.

  • @masirian06
    @masirian062 жыл бұрын

    nazipenda kazi zenu safi sana wanaTanzania... mwatufunza maadili mema ya upendo sis kama wakenya lakini wote tu waafrika na hivyo nafurahia kazi zetu,, hongera sana

  • @jovituskamugisha
    @jovituskamugisha8 жыл бұрын

    Maudhui, mashairi, rekodi,... Nimeipenda. Ahsante sana Baba Mrisho Mpoto.

  • @mwitaadah3649
    @mwitaadah36493 жыл бұрын

    Mjomba umetulia Sana. Tupe mashairi baba🔥

  • @augustinomkongwa5444
    @augustinomkongwa54444 жыл бұрын

    Usiyemtaka kaja, sizonje huyu huenda akawa ni JPM aka Jembe aka Chuma cha Pua, siyo lazima niwe sahihi kumtambua Sizonje kwenye ghani hii ya Mrisho

  • @kwekanoahbehappyintanzania5201
    @kwekanoahbehappyintanzania52017 жыл бұрын

    Never give up my best brother well done kesho ikifika waeleze kuwa kiswahili si maskini wa misamiati nakuomba ukumbuke sana kutueleza

  • @hamidmpenja2489
    @hamidmpenja24897 жыл бұрын

    ishara ya muafrika ni kioo kimulikacho na kirudishacho taswira ya uafrika na tukajivunia kama waafrica,I salute brazza,napendaga sana mashairi yako!!!

  • @sonnymjeshi

    @sonnymjeshi

    7 жыл бұрын

    adams boytz

  • @christopherkipeke7547
    @christopherkipeke75478 жыл бұрын

    Mlisho kwangu hata usipoimba, kitendo cha kukuona nahisi nguli na gwiji la sanaa anajambo analitoa

  • @cunada712
    @cunada7124 жыл бұрын

    Mwanafasihi bora niliyemshuhudia maishani mwangu kwa sasa sijaona kama huyu🙌🙌

  • @vintankirikuu1103

    @vintankirikuu1103

    Жыл бұрын

    Mwngne madebe lidai just find Tanzanian artist

  • @saknamtaki8168
    @saknamtaki81687 жыл бұрын

    Nyimbo nzuli kweli uko posh kak kimziki nakupa respect

  • @johnambrose7223
    @johnambrose72235 ай бұрын

    Siku hizi mrisho mpoto haimbi tena

  • @lightnessmruma9740
    @lightnessmruma97408 жыл бұрын

    nmeelewa kidogo,anamkaribisha maguful ikulu(nchi yetu)....asiye mtaka kaja hahaha I like this ....japo mafumbo n mnge

  • @mwalimmaroaibrah8051
    @mwalimmaroaibrah80517 жыл бұрын

    Dah! Kwakweli mashairi yamesimama sana. Hongera Mrisho kwa mashairi haya

  • @boazmosses8204
    @boazmosses82047 жыл бұрын

    kwamba kwa nje inaonekana kkukuu lakn ndani imejaa vitu vya thamani😂😂😂😂tz hyo

  • @shankyse2576
    @shankyse25767 жыл бұрын

    Mimi shabiki wako mkuu..... Nairobi/ Kenya

  • @Franko-zd6hc
    @Franko-zd6hc3 жыл бұрын

    Huu ni usanii wa hali ya juu.Utumiaji wa kejeli ilikupeana ujumbe flani.

  • @paulomroki1979
    @paulomroki19793 жыл бұрын

    2021 am still listening!! Mungu akubariki sana

  • @daudimkwela
    @daudimkwela8 жыл бұрын

    Nice video, Good Music, Production ipo poa sana. Tungo tata kama kawaida yako mzee, KORA 2016 yako.

  • @rashidhassankadege1455
    @rashidhassankadege14554 жыл бұрын

    Yaani nyumba yetu kwa nje ni mbaya sana nayakizamani mno ila ukiingia ndani ndo utajua uzuri wake najinsi ilivonakshiwa kwa mapambo ya gharama na ustaarabu uliotukuka

  • @ramadhanboi6485

    @ramadhanboi6485

    4 жыл бұрын

    Imemaaanisha mbuga za wajama na dhahabu tulizonazo na maziwa

  • @ramadhanboi6485

    @ramadhanboi6485

    4 жыл бұрын

    Imemaaanisha mbuga za wajama na dhahabu tulizonazo na maziwa

  • @paulmwambire5474
    @paulmwambire54745 жыл бұрын

    Nimezaliwa Tanzania lkn sielewi kabisa

  • @hadijapazia8255
    @hadijapazia82554 жыл бұрын

    Naikubali xn hii ngoma🔥🔥🔥🔥👌🏻👌🏻👌🏻👌🏻

  • @robymushi
    @robymushi8 жыл бұрын

    Dah.., another classic traditional song with alot od proverbs that i dnt understand but I LOVE THE SONG. Hongera Mjomba. Keep doing watchu doing Sir

  • @catherynmathias8318

    @catherynmathias8318

    8 жыл бұрын

    kihistoria tunajua tz ni nchi yetu lkn mbona hatutumii/ hatufaidiki kwa rasilimal zlizopo (kihistoria nyumba ni ya kwetu ila mbona hamtumii chuo na jalala..... milango ipo mingi lkn y wapite madirishan....?!

  • @enockjohn332
    @enockjohn3328 жыл бұрын

    mtoto hawezi kubembelezwa kwa wimbo mbaya,na mtoto aungui na kiazi kilchopo kwenye kiganja cha mama yake,nimekusoma mjomba

  • @ibrahimzuberi1029
    @ibrahimzuberi10298 жыл бұрын

    yan nimeskiliza zaid ya 10 tym sijaeleza zaid ya bahasha za kaki2...daaah shkaaaaamooooo burazaaaaa

  • @edwinpepela1205
    @edwinpepela12056 жыл бұрын

    Shairi,malumbano.african setting, traditional and meaning,economical failure.Kiasi hakiwezi mchoma mwana kikiwa kikanjani Cha mama.pili mtoto hajakuwa Hadi harufu Cha babake kiishe.Hehe if you not an African don't try to pea in that setting.You will meet with stonishment.always remember that.

  • @winstonkwoba1994
    @winstonkwoba19944 жыл бұрын

    madhumuni nimeyapata

  • @NabakiZanzibar
    @NabakiZanzibar8 жыл бұрын

    Natamani sana kuona hii video on MTV, Trace, ect. coz idea na shots zimetulia sana. Nashukuru sana kwa mashaili (Poetry) #MrishoMpoto kazi nzuri sana. Mungu akubariki, iposiku wataelewa tu.! @ThomGypsy #ThomGypsy

  • @planbmauwezo4853
    @planbmauwezo485311 ай бұрын

    DAH W MZEE MWENYZ MUNGU AKUPE UMRI MREFU SAN

  • @Jackson-pj3mw
    @Jackson-pj3mw Жыл бұрын

    Nyimbo ngumu sana kuielewa inahitaji utulivu wa kutosha

  • @estherurio6155
    @estherurio6155 Жыл бұрын

    Mmmh!!! nyimbo ngumu hii😭😭😭

  • @lewisnyagah7332
    @lewisnyagah73323 жыл бұрын

    Utunzi ulobobea yakini mwafaka hasa.. imeweza #Timeless

  • @jeneralAthanoel
    @jeneralAthanoel8 жыл бұрын

    Mjombaaa, Banana kazi nzuri sana, ni pekeee

  • @emmanuelpeter7371
    @emmanuelpeter73718 жыл бұрын

    Kaka mungu akujalie utufunze mengi kwakupitia nyimbo zako maan nakuelewa pale unapo tohoa maneno yalio sirin

  • @aliali189

    @aliali189

    8 жыл бұрын

    napenda sana nyimbo za mlisho video kali sana

  • @nicksonrichard9411
    @nicksonrichard94118 жыл бұрын

    nyimbo nzuri ya kiafrica zaidi

  • @sirialemmy37

    @sirialemmy37

    8 жыл бұрын

    hehehe ya kiafrika zaidi, hehehe, l wish if this man's philosophy is well understood

  • @emmanuelpeter7371
    @emmanuelpeter73718 жыл бұрын

    na kinachonifuraisha sana kwako ni pale unapotohoa neno ;linanifikirisha kutafuta maan yake nn yaan hua unaniparaha sana na ninatumia akili kujua unamaan gani yuu ya usemi wako kuanzia mjomba hadi leo zizonjee daaah kweli hii ndo nyumba yetu ina milango lakin watu wanapitia madirishan tena ulinimaliza pale ulipo sema wagen wanalala chumban wenyej seblen daaah hii ndio nyumba yetu ni kweli kaka endelea kutohoaa

  • @sirialemmy37

    @sirialemmy37

    8 жыл бұрын

    Emanuel Peterrrrrr kumbe wa2 wamo wa kuitafsi mafalsafa magumu? sikujua bwana. Amazing my country man!

  • @wazirikonzo7529
    @wazirikonzo75298 жыл бұрын

    nakukubari sana mpoto aka MJOMBA mngu akubariki endelea kuwambia wana sizonje

  • @amosnguvumali7869
    @amosnguvumali78698 жыл бұрын

    hahaha kwel mtoto hawez kuungua kwa kiaz kilichopo kwenye kiganja cha mama yake ahsante sana

  • @PapaTheKingMKenya
    @PapaTheKingMKenya9 ай бұрын

    Unloving memory to magufuli

  • @iamjimba9775
    @iamjimba97758 жыл бұрын

    duuh! maishairiii nondo sana

  • @sirialemmy37

    @sirialemmy37

    8 жыл бұрын

    hehehe yes yes mr

  • @aminagoliama8668
    @aminagoliama86688 жыл бұрын

    Weng ni vijan na wanabahasha za kaki mikonon daaaaah nimeelewa sana nakupend sasa mpot ii ndo nyumb yetu TZ ingia uyaone Kile ni choo wanaoish hawajawai kukitumia mean hospital zipo ila wanaenda nje hahahahahahaha 😍💞💕😘💜👏👏👏

  • @ibrahimjuma8577
    @ibrahimjuma85778 жыл бұрын

    hongera Mjomba mi huwa nakuelewa sanaa nice song babaa

  • @sirialemmy37
    @sirialemmy378 жыл бұрын

    Am not SURE, kama this UNCLE is well understood. This philosophy is more sophisticated & highly ironical in nature, it invites minds 2 think & lower in noise making--

  • @sirialemmy37

    @sirialemmy37

    8 жыл бұрын

    +Burhoney wa Mponda thank u very much 4 ur beautiful analysis and paraphrasing these solidified philosophy of the man. Yeah! it's fewer among u who can come up with that understanding bcoz someone like Diamond has made pipo more stupider & sexy thinkers & leave the state alone 2 raped by sordid avarice who admire wield that will drive titles in their homes. Class stratification of Karl Marx

  • @jimmyjizzy1076

    @jimmyjizzy1076

    5 жыл бұрын

    U BETTER UNDERSTAND THE LYRICS BRO ITS A NICE SONG WHAT HE TRY TO SPEAK IS ALL ABOUT CORRUPTION AND MISUSE OF POWER AMONG GOVERNMENT OFFICIALS IN SHOT

  • @adcutey9112

    @adcutey9112

    4 жыл бұрын

    @@jimmyjizzy1076 CORRECTTTTLY ANSWERED

  • @tiaschris7070
    @tiaschris70707 жыл бұрын

    aisehhh hii nyimbo ni hatari, xijui km ntakuja kuisikia nyimbo km hii tena

  • @barick
    @barick7 жыл бұрын

    Huyo mzee anavyo Lia na mimi nimelia mmh!sizonje

Келесі