SERIKALI YASITISHA ZOEZI LA UKAGUZI WA RISITI KARIAKOO

SERIKALI imesitisha zoezi la ukaguzi wa risiti za Kielekroniki (EFD) na ritani za kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), iliyokuwa ikifanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania kupitia mkoa wa kikodi wa Kariakoo, Jijini Dar es Salaam, wakati ukiandaliwa utaratibu mzuri wa utekelezaji wa suala hilo katika Soko Kuu la Kimataifa la Kariakoo.
Hayo yamesemwa kwa niaba ya Serikali, jijini Dodoma, na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, wakati akitoa maazimio ya kikao kati ya Viongozi wa Wafanyabiashara Tanzania, Viongozi wa Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kariakoo na Taasisi zinazosimamia masuala ya wafanyabiashara, kikao ambacho kiliitishwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na kuhudhuriwa pia na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.

Пікірлер: 10

  • @ndukulusudikucho_
    @ndukulusudikucho_5 күн бұрын

    Safi saana Serikali yetu sikivu

  • @abdull_hafidh
    @abdull_hafidh7 күн бұрын

    Serekali msipoangalia mkaona wananchi ni wapuuzi kwa kutuongezea kodi kila mkiamka kuna siku watachoka

  • @usafiaps318
    @usafiaps3183 күн бұрын

    Mh.Waheshimuni Kwa Kiwango Kikubwa Wafanyabiashara Hawa Wazawa. Hawa Waiteni Mara Kwa Mara Sasikilizeni Sio Kwa Madharau.

  • @hassanmsangi1155
    @hassanmsangi11559 күн бұрын

    Nan kamtuma kwanza chalamila k/koo

  • @mudhihirissa274
    @mudhihirissa2746 күн бұрын

    Chalamila hatumtaki mkoa wa Dar es salam

  • @hassankongolilo8408
    @hassankongolilo84089 күн бұрын

    kuna kijusi kinatutishia uku ata busara halina

  • @obbybenitho5803
    @obbybenitho58033 күн бұрын

    Mshamba tu chalamila

  • @CheerfulCakeSlice-po2ht
    @CheerfulCakeSlice-po2ht7 күн бұрын

    Yaani kamata kamata itarudi tena!!!

  • @user-rg2py2yz4x
    @user-rg2py2yz4xКүн бұрын

    Bando..

  • @makelemohuya2723
    @makelemohuya27237 күн бұрын

    Chalamila hasa busara na hekima anakurupuka hovyo hovyo tu kama mganga wakienyeji

Келесі