Madam Rita Afunguka Asili Yake Na Alipozaliwa "Nina Makabila Matatu" | SALAMA NA MADAM RITA PT 1
Ойын-сауық
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
SOMETHING SPECIAL
Ms Rita Sundi Paulsen Hans ni mtu muhimu kwangu na kwa mamia kama pengine si maelfu ya wenzangu hapa nyumbani Tanzania. Yeye ni Mama kwanza, Dada kwa wengine, Aunt poa sana kwa kina Malik na Jamal, Bosi ya Mboka kwa Salama na wenzie lakini kubwa kabisa ni MJASIRIAMALI, jambo ambalo amekua akilisimamia lile analo liamini kwa miaka zaidi ya 30 sasa. Rita au Madam Rita alianza kufanya kazi toka alipokua na miaka yake ya mwanzo kabisa ya 20.
Mtoto kutoka kwenye familia ya kitajiri maana Marehemu Mzee Paulsen hakua mnyonge. Baba Mjerumani na Mama Mwenye asili ya kisukuma, kirudi na mchanganyiko wa makabila mengine kadhaa ambayo atatuambia humu ndani. Amekulia kwenye mitihani mingi mara baada ya Baba yake kufariki wakati yeye ana miaka 12 tu. Kutoka kwenye mazoea ya maisha ya kishua mpaka kupata mimba akiwa na umri mdogo na hilo kumlazimisha yeye kuondoka nyumbani akiwa na umri mdogo ndo mi naamini lililomfanya awe CHUMA mpaka leo. Naamini vile wanavyosema kila mtu na njia zake. Kila kitu kinachotokea kwenye maisha yetu kina sababu yake. Yeye kufariki kwa Baba yake ndo kulipelekea kupita KOTE alipopita. Shida na mitihani wakati mwengine huja kwa baraka tele, BARAKA ambazo mpaka leo hii ambayo mimi naandika waraka huu kwa majivuno mengi juu yake. Kweli kila kitu hutokea kwa sababu ili kitu kengine kizuri zaidi kiweze kukufuata ulipo.
Mimi na yeye tulifahamiana kwaajili ya kazi, nadhani wengi wanaijua hiyo khadhithi, ila kama hufahamu mimi na yeye makutano yetu ya kwanza yalikua ya kunipa kazi ya ku host Kili Music Awards ila hiyo kazi ilikuja baada ya pinduapindua nyingi alizo zifanya pale EATV baada ya siku moja mimi kuisema vibaya moja ya video ambazo kampuni yake ya Benchmark ilizitengeneza. Ilikua mtihani haswa baada ya kuskia naitwa tena ofisini kwake? Haya jengine lipi tena? Kumbe round hii ilikua kwa Neema sana, ila Bahati mbaya hiyo kazi wala sikuipata maana na watu wa Kili nao walinikataa kwasababu huko nyuma pia niliwasemea tuzo zao ambazo ki ukweli zilikua za kiwango CHA CHINI MNO considering hela ambazo wanazo wao kama KAMPUNI, kwa kweli lile halikua linapaswa kunyamaziwa.
Basi, peleka mbele mwaka mmoja au miwili baada ya hiyo incident akaniita tena kwaajili ya kazi ya Bongo Star Search sasa, na hii nyengine skia, nilipoitwa sikujua kama yeye ananitaka mimi kama Judge, mawazo yangu yalidhani anataka MTANGAZAJI wa shindano hilo, kumbe yeye alikua na BETTER idea, kama wazungu wanavyosema, the rest is history.
Rita ameniona mimi nakua mbele ya macho yake, nami pia nimeona transformation ya maisha yake kama Mama na Dada. Mengi amepitia ya hadharani na kwas siri, ninayo yajua na nisiyo yajua, ila ambalo nina uhakika nalo ni JINSI AMBAVYO MIMI NAJIVUNIA YEYE, kwa mishale yote ALOIKWEPA na kuendelea KUSIMAMA IMARA, Rita Paulsen Hans ni SHUJAA NA NUSU.
Mengi ameyaongea humu, ambayo ningependa uyaskie MWENYEWE bila ya mimi kudokoa lolote, hakuna chumvi wala sukari ilozidishwa humu ili ‘picha ipendeze’, badala yake ni simulizi nyundo ambazo kama kawaida zitakufanya ujifunze mambo mengi na pia kuangalia baadhi ya vitu kwa jicho jengine.
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Пікірлер: 135
They’re the Definition of Independent Women ♥️
Wonderful interview. Wow madam Rita what a wonderful personality you have. Salama u r an amazing interviewer. Well done
Jesca Leo Kabadilisha Nguo Kumbe Ana Kijitako Cha Bunduki 🤣🤣
My favorite show with my favorite Host...I love you Da Salama since then❤️😍
Icon...🔥 One among my favourite people...♥️ Thank you Ecejay!
Madam is a whole different person. Her personality is 🔥
Salama you're one of the best presenters in Africa.👏👏👏. That's why I like your interviews. 🔥🔥🔥✔️🇰🇪👊
Tusisahau kutuma Tip kupitia Mpesa aisee, kazi nzuri wanafanya😁
She’s a strong woman ! Started from the beginning, she has a beautiful soul ! 😭♥️
I appreciate. Sana madam kwa unachokifanya mungu azid kukulinda
Ki ukwe ukweli huyo Mama nanpenda sana sana*Allah ampe umri mrefu
A pure administrator! All the best 👍 madam
Wanaume Mungu anatuona!! Yaani uende kumchukua mtoto wa watu ili umuendeleze Shule kwa sababu ni mdogo na alishapewa mimba akiwa na umri mdogo! Then badala ya kumuendeleza shule unamtia mimba nyingine!! Je! Huu ni ukatili au sio ukatili? Pole sana Madam Rita kwa safari hiyo ya maisha uliyopitia!!!
@maryamtan682
3 ай бұрын
Wanasema akili ku mkichwa😂😂😂😂
@roseruhuta3325
3 ай бұрын
Mada Rita ❤
I love the fact she didn’t want to use the words “it was an accident” and changed it to “it wasn’t planned “🙏💯
Hongera sana Salama kwa hii platform ya mahojiano. Shukran kwa haya mahojiano na da Rita. Endelea na kazi bora!
God akulinde madam Ritha umeongea nimemuelewa Sanaa Sanaa endelea kubariki vijana wetu
Nakubari sana hizi Interview 👏👏✌️
Madam Ritha wewe ni mtu na nusu nakubali kazi yako. Keep it up
hii ni exclusive yaani ..........big up salama...!
Kazi nzuri 👊🏿
She is a strong woman !
Mada masha allah jamn nakupenda jamn sirias toka zamani sema nafasi nakosa kpzzzzzz jaman nakupenda eee nko mkoa eee
Kuna mambo mengi sikuwahi kuyasikia kwenye interview yoyote aliyowahi kufanya Ritha,ila leo nimepata majibu ya maswali yote niliyokuwa nikijiuliza. Umepitia mengi, lakini hukuwahi kukata tamaa pamoja na mapito yote.You are a super women🎉
Kupungua kwa uzuri inategemea na hali ya maisha ya kila siku ila nampenda sana huyu dada ana huruma sana mpenda watu mchapa kazi j say big up madam🎉
@DEBORAHMASANJA-yz3go
2 ай бұрын
Hi Madam Rita nakupenda sana
Your story put me on point to look you in a very special manner. But all in all pole Sana kwa yote uliyopitia to where you're today.
We call them over thinker they have smart mind, focoused, open minded and always think positive
Mupitie na kwangu wapenzi..sapoti kusapotiana❤
Good interview
Madam Rita pls naomba niwe rafiki yako ! ❤nitapata mengi kwako
Madame ritha mnyamwezi sanaaa🤪❤️
Nzurii
Nami ni mmojawapo wa watu wanaotaka kukaa peke yangu muda mwingi.
@josephlorri431
3 ай бұрын
Mtoto mzuri wewe, kwa nini ukae mwenyewe muda mrefu? Toa nafasi, nipo
@user-oi1qy8uj6r
3 ай бұрын
Even me dear
@wennybarny168
3 ай бұрын
Mimi ni super loner hadi watu hawanielewi na wanahisi nataka kujiua
Mwaka 2023 Nakuja Bss Natamani Sanaa
Wanawake kweli kama maua,yanachanua na baadaye kufunga. True with time we decay,urembo wake wote mzuri sana umepungua sanaaa,daah wkt ni ukuta
@FiollaIsaya
2 ай бұрын
Huyu madamu mara mbili siku tofauti nili msalimia shikamoo alikaa kimya nilijisikia vibaya sana afu nilikua shabiki yake sana
Yani nakipenda kipindi hichi San Kwanza mazingira yake uwandaaji wake Yani nimzuri sana
Iron lady very difficult to understand her, genueas and confident this type of lady there are very few in this planet.
Salama mnoma
Mek up ya Leo mbaya sana madam
@masturaabdul1007
2 жыл бұрын
😃😃😃😃😃sanaaaa. Mbaya mbaya mbayayaayyaa
@wennybarny168
3 ай бұрын
Hiyi make inaitwa "nude" na ndo fashion ya wakati huu
Kizungu jamani warundi hatuerewi
🔥🔥
Ki King'eng'e kimezidi banaaaa
Wa kwanza leo
@abdulraufmohammedsalum6806
2 жыл бұрын
Wa kwanz mm tulia
Salama...... you ar so good and fit on presenting a sessions with..... to me you ar not boaring in all of ur ukorofi questions....
Salama twawapenda s punguzen kiizungu
Thats me loneeeer🙏
Sauti za jamaa wanaopiga picha zinasikika. Mnaweza lifanyia kazi hilo pia.
Huyu mama wange mpa ile nafasi ya Stive nyerere kaleta vipaji vingi sana tena wakali.
@saumusalimuhassan2499
2 жыл бұрын
True my dear 👍
@catenzeki678
2 жыл бұрын
Nakubaliana na ww 100 kwa 100
@ngoshachaula172
2 жыл бұрын
Chapesa sikubaliani naww ni tapeli
@Chapesatv
2 жыл бұрын
@@ngoshachaula172 sawa ila uliwahi kusoma mikataba yao au kujuwa makubaliano yao maana watanzania mara nyingi kusoma mikataba tunauvivu nako sana. Kwahio sote ukweli hatuujuwi tusimuhukumu.
@vj8313
2 жыл бұрын
Kabisa
WHERE IS JESICA ????????? WE WANT HER BACK
My favorite 😘
Pole Madam ila sitaki kuwa mnafiki alokupamba kakuharibu kama hujatambuliswa nisingekujuwa😃 Madam achana na mpambaji huyoo
@salomewandya7257
2 жыл бұрын
Kabisaaa
Ila kiukweli hii ni moja ya interview ngumu sana ambayo salama amewahi kufanya Imagine anam interview boss wake na rafiki yake.
@wennybarny168
3 ай бұрын
Alishawahi kumhoji kwenye kipindi chake cha zamani yeye Salama kinaitwa MKASI. Hii anamhoji ni mara ya pili.
@wennybarny168
3 ай бұрын
Salama alishawahi kumhoji huyu bosss wake kwenye kipindi chake cha MKASI kabla ya hiki
Am a loner too..na ni kitu kizuri sana...unafanya hata maamuzi kwa iuyafikiria wewe kama wewe. Madam Ritha ni mtu poa sana. Nakumbuka the day I met her akanisifia mpaka nikajisikia raha sana👌😘😘
@aloyceshaban1348
Жыл бұрын
Mmmmh
Kumbe wewe n mtu wa rwanda dada yetu kalibu nyumbani🇷🇼
@ngoshachaula172
2 жыл бұрын
Uoni komweee hilo
salama jitahidi kuwaambia wapunguze kingereza siunajua wa tz tuna hiyo shida😅
Dada salama.. mimi binafsi naona uongozi ndani yako.. hebu pita kidogo huko alafu kuna watu watakushukuru kwa maamuzi utakayochukua
Dada ongea kiswahili bila kuchanganya kiingereza wengine hatuelewi😢😢
@yustersimon5104
3 ай бұрын
Hata hicho kiswahili kajifunza mwaya
Tupo wengi tunapenda sana kua pekee yangu nilijua ni ugonjwa
@beatricekitara5808
Жыл бұрын
Iyo ni shida sio kawaida
Kingereza kingi madam vp ? Kumbuka kuna ambao hawajasoma wanatizama kipindi hata hiyo english yako hawaijui so speak national language banaa, all in all uko good jasiri muonyesha njia 🔥
@rommelmauma8081
2 жыл бұрын
Hakuna ubaya endapo mahojiano yatakuwa kwa Kiswahili au Kiingereza; kuchanganya lugha hizo mbili kunaharibu mazingira ya maudhui ya mahojiano. Chuchumilieni kuongea Kiswahili!!
Apewe heshima yake huyu mama
Omg
jesca leo vipi?
Nimependa mama
Yani madam rita story yako kwakweli inaendana Na yangu kabisa
Madam pole ulipitia
@halimalachpat1927
2 ай бұрын
Hivi mi nauliza ni nani aliwahi kuwa mtoto?nadhanni jibu ni wote usichana,umama,na uzee?je hali si inaenda kubadilika? Mangapi yamemtokea madam?linganisha jani bichi na njano uzri wake .maisha ni safari ndefu.
Be specific Sasa kitambulisho cha NiDa umejaza hayo makabila ya baba zako 3 Siku zote tunafuata ukoo wa baba Aliyeweka mimba kwa mama yako Halafu wewe unajulikana kama hata shule umepia Huko ni kujikaa Ritha
Madam nakupenda but kuhus age umetudanganya
Mimi Nina makabila 9 yani sieleweki😂😂😂😂😂kila kits nipo tofauti
I lv madam Rita but she looks very difficult ☺
Hapo kwenye sura zake mbili nimeziona hiyo sura yake ya kazi unaweza usiamini kama ni the same person 😂😂
@khadijahali4837
Жыл бұрын
🤣🤣
MAJIZI GROUP 😅😅😅
Who is madam Rita ?
***Napajua Umurushaka,Nkwenda,Kaisho,Murongo Kona kumi na mbili,****
Alikua anaupenda tu huo mchezo
Me hivyo viti mlivyo kalia , hata sijavielewa kabisaa.. Khaa🤗 ukihojiwa na mtu anaekujua ngumu kuficha ukweli Asante Salama
Kama Mimi nimezaa14 nikateseka
Kumbe hata kama u unahela mambo ni magumu tu😅
Aisee Mbona Heleni Za Madame Kama Ni Mzigo 🤣🤣 Au Basi Itakuwa Kakata Nyororo Ya Mbwaaa
@catenzeki678
2 жыл бұрын
😂😂😂😂😂😂
@mwajumalubunga1534
2 жыл бұрын
🤣🤣🤣🤣🤣🙆♀️🙆♀️
@petermanala6138
3 ай бұрын
😂😂😂😂😂dar sawa bwana
@wennybarny168
3 ай бұрын
Jamani watu wanapenda kuongea vibaya
Hivi ukisema kua hupend mtu muongo mnafiki sjh nn na nn hiv inakuaje kwa upande wako wewe mwenyew hivyo vtu u didn't get au manake uongo kuuepuka Ni Mara chache Sana same tu unafiki jmn tusiwe waongo katka ilo🤣🤣🤣
Where is the camera interviewer is looking away..we see legs n shoes can u be serious
The Accent is boring.... juzi tuu the accent was well booom it has changed
Heshma Kwa mama Samia kurudisha wajawazito shulen
Inawezekana akawa ni mhaya wapenda English.
@KhadijaMiteya-hh8xl
2 ай бұрын
Amesha kwambia msukuma na mjerumani ujasoma comment?
Madam Ritha mimi pia sio mnafki, nikuombe tu umfukuze kazi huyo makeup artist wako aliekufanya hvo uson kwenye interview hii
@abdulraufmohammedsalum6806
2 жыл бұрын
😆😆😆😆
@masturaabdul1007
2 жыл бұрын
😃😃😃😃😃😯😃😃 kweli age imeenda ila makeup mbaya sanaa
@salomewandya7257
2 жыл бұрын
Hahaha kweli aiseee🤣
@tuliadamson3422
2 жыл бұрын
🤣🤣🤣
@mwajumalubunga1534
2 жыл бұрын
🤣🤣🤣🤣✌
Jamani hiyo ni fashion ya make inaitwa "nude" Naona watu hawajailelewa ila iko namna hiyo Wakati prince Harry anaoa mjukuu wa Queen Elizabeth, mtoto wa prince Charles (ambaye sasa ndo king wa uingereza) watu walisema bi arusi hajatumia makeup kabisa, kumbe alitumia makeup ya milioni 30 za kitanzania. Ni make ya nude ambayo rangi zake ziko kimya. Rangi hazi-shout.
Mm binafsi nakubali hiki kipindi lkn kwauchunguz wangu nimebauni wanaongea kingereza Sasa kuliko kiswahili ndio hua siku mbaya ya kipindi
@magorymara5515
3 ай бұрын
Ni lugha ya pili Tanzania kama hujui moja lazima utajua moja huko ndo ukweli