Jux : "Nilikaa Na Jackie Mwezi Mzima China, Akawa Hapatikani, Sikumuona Tena" | SALAMA NA JUX PT 2
Ойын-сауық
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Juma Jux ni mtanashati haswa hicho ndicho cha kwanza na suala la yeye pia kuwa muimbaji mzuri (na anayeendelea kujengeka) kunamfanya pia awe wa kipekee, anajua maana halisi ya kufanya kazi kwa bidii ili uweze kutimiza malengo ambayo wewe unakua umejiwekea. Ana aibu pia sana ila hili unaweza ukalitilia shaka kwasababu ya kazi aliyoamua kuichagua. Kwa nilivyo muelewa mimi yeye aliamua kufanya muziki kwasababu rafiki zake walikua wanafanya muziki na zaidi akiamini yeye ni Rapper kuliko hata kuwa muimbaji.
Kwa mujibu wake kwenye kundi lao hilo la shule yeye ndo alikua sio mkali na wala hakua na neno juu ya hilo, zaidi yeye alikua anataka ku fit in zaidi. Lakini leo hii yeye ndo mwenye mafaniko zaidi kwenye fani yake kuliko wale walokua ndo wakali wa kazi hizo wakati bado wako shuleni. Jux ananiambia mpaka leo wanaendelea kuwa marafiki na rafiki zake wa shule, zaidi Cyrill Kamikaze ambaye amekua kama ndugu yake. Pia anakumbuka mara ya kwanza wimbo wake ulipoenda redioni bila ya matarajio yake na wakati anaambia B12 ameupenda na angependa akutane nae anasema baridi na uwoga na aibu aliyokua anasikia ni Mungu pekee ndo anajua.
Uzuri pia Jux ana muonekano mzuri na utanashati wake umekua ukimfanya ajikusanyie mashabiki wengi haswa wanawake na ku inspire vijana wengi watake kupita kwenye nyendo zake ili nao waweze kuja kuwa kama yeye siku moja. Combination yake na Bob Maneke nayo ni kitu ambacho kimemfanya Jux aendelee kuwa pale. Wanafahamiana vizuri na kazi ambayo wamekua wakiifanya pamoja imekua ikijieleza yenyewe.
Jux anakumbuka utanashati na kujituma kwa Marehemu Baba yake ambaye kwa maelezo yake anasema alikua Baba BORA sana, kwanza hakuwahi hata siku moja kumuona Mzee wake na Mama yake wanagombana na siku zote alikua anahakikisha watoto wake wanaishi na kusoma vizuri, nadhani nia yake ilikua kutaka kuwaona watoto wake wakiwa wasomi labda na kufanya kazi za maana zaidi au kuishi maisha mazuri zaidi kuliko yeye wakati anakua. Jux ana kumbuka Mzee wake kama mtu wa kujituma sana ambaye alijichanga kumfikisha mkewe mjini baada ya kupata kazi, yeye alikua tu fundi wa magari ila baada ya mke wake kupata kazi mjini, alihakikisha anafika na mambo mengine yaende kwa uzuri kama ambavyo alikua akiyataka kwa wanawe.
Mama yake pia humuambia zaidi siku hizi za karibuni baada ya Jux kuanza kung’ara kwenye muziki na biashara zake, Mama yake anamuambia anamkumbusha mno Marehemu mume wake na anajua fika kama angekua hai basi angekua anajivunia yeye kupita kiasi. Uvaaji wake na utanashati na jinsi ambavyo anajituma hivyo vyote Juma Jux amerithi kutoka kwa Marehemu Mzee wake. Mwenyezi Mungu Aendelee Kumpumzisha kwa Amani.
Mapenzi yake ya dhati ambayo huyaonyesha kwa watu ambao amekua nao katika mahusiano nae pia kwa kiasi kikubwa amechukua kutoka kwa wazazi wake, jinsi ambavyo Baba yake alivyokua anampenda Mama yake, ni kitu ambacho Juma amekua akikikubali sana. Na yoyote ambaye anakua nae amekua akifanya analoweza ili waendelee kudumu. Mwenzetu amekua na mwalimu mzuri sana.
Kwa akili ya muziki na biashara nadhani tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa kijana huyu hodari wa ki Tanzania. Hivi karibuni brand yake ya African Boy imetia makubaliano na kampuni moja kutoka China ambayo wamekua wakimuona Juma anafanya biashara hiyo tokea akiwa mwanafunzi na kwa jinsi ambayo amekua akifanya kwa muda mrefu na brand na yeye kama mwanamuziki kuzidi kukua nadhani na wao pia waliona fursa ya kufanya nae ushirikiano ili waweze kumuwezesha zaidi ili waweze kushinda WOTE.
Yangu matumaini kama ada uta enjoy episode hii na kujifunza zaidi.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Пікірлер: 88
Jux is is the best artsit among the five favorite artsit in Tanzania...kuanzia mziki wako adi swag zako nakuelewa sana
Nilichojifunza kwenye hii interview kubwa zaidi ni kumpa mtu nafasi. Naenda mpa nafasi my wife katika maisha kama babake jux.
One of the best interview ever! Jux is the realest person ever!Very fluent! Salama Is the best host!anajua kubalance conversation na kumpa nafasi mtu na maswali ayajibu at right time! Nmejifunza vzuri kwa africanboy,cha msingi do ya thing,keeep going hyo brand ni kubwa sana! Utareach far....remember im your die hard fan to y'all,just keep it real son
@nakijamussa6312
Жыл бұрын
Muo
Salama jabir one of the best journalist in this country, please mualike diamond platnumz one day, itakuwa moja ya interview kubwa mnoooo
Interview iko ppoa .. nakubal kaz zenu Allah awajaalie mzidi kuleta watu wenye maadil na kufundisha jamii yapo kwa uchache... kila la kheri kwa yeyote aliefanikisha hiv interview
“Solution sio kutafuta Mpenzi mwengine nikutafuta Hela“
best female presenter in East n centre Africa.
Nakumbuka ngoma iliyonishawishi kumpenda Jux ni NITASUBIRI niliisikia siku moja kwenye Radio usiku ikanifanya nisipate usingiz Jux popote pale ulipo ujuwe ninakupenda sana brother ❤❤❤❤ mwenyezi mungu awe kwenye mustari wa mbele kukuwezesha kwa kila jambo unalolikusudia❤❤❤❤
@filamupictures9349
Жыл бұрын
😂😂 We jamaa nyimbo ya jux ilikufanya ukose usingizi na una komenti na makopa kopa hahaha thats so homo 😂😂
@iddikipulli510
Жыл бұрын
Hahahaha Mungu amuweke anasemaa
Humble & smart 🤓 boy 👍👌❤🇨🇭🇹🇿
Ise story imenibariki sana Mungu azidi kukusimamia kaka Jux
Jux ur smart kunasehemu nimekuelewa Sana kwenye kujielezea kuhusu biashara TUSIOGOPE 😎
One of the best interviews big up Salama and j
Always Salam am your fan when it comes to interviews 🇩🇰& ,🇹🇿❤️👍🏼
It's good seeing #jux talking his business side of him👏👏👏
One of the best interviews.
Nice interview...Mungu akuweke tushuhudie mengi sana kwako dada salama
My favorite interview show
Awww🥺thank you for this
Now i am seeing why Diamond keeps respect to Jux💥
Very inspired boy napenda saana
Very smart eloquent guy..
I love the interview
Last minutes za hii interview he talked sense. Najifunza sana jinsi ya kumuongelea mtu, hasa yule nisiyemjua kiundani... streets got a lot of shit talkings
Mm sijawahi kuona wazazi wangu wakigombana wala kuhisi wana ugomvi mpaka baba yangu anafariki ila najua lazima walikuwa wanagombana kwa siri.
🤝nimependa saaana Salama&Jux hao wazazi waJux ni mimi na mumewngu kidg nilie the way mumewng na mm tunavoishi allah atueke na watt wetu wajifunze mazuri 🙏
@lareineminah1353
Жыл бұрын
ALLAAH awalinde jamani
Wooow very good story I want to do some business Leo ume ni chanua Jax
Hongera sana dada salama...
Heshima kwako #Salama Jabir
Plz ufanye interview na Millardayo plz plz
Nimependa sana
Sim unknown 😅 Kisha ukaipiga haipatikani 😅😅😅😅
interview konk sana 💪💪💪💪
To be honest,i remember, i was Maneno aliyo yarudia sana Bwana Jux😂
Jack nimekaa nae lugalo Area J na tumesoma wote lugalo primary chini ya Mwalimu Mkuu Kabigi
6:22-23 (swali zuri kutoka kwa salama)
Allah atuhifadhi J jux
Kaligraph,J makamba,Cathy Magige,Riziwan and Izzo Business
He is honest for everything but agekuwa diamond duhh😁😁😁 uwongo ugenkuwa mwingi au sio?
Lavalava next pls
Mualike millardayo cku moja
@emmamatemu8225
Жыл бұрын
Kabisa
@filamupictures9349
Жыл бұрын
Kashawahi kumhoji Millard ayo ila zamani, nadhani kwenye mkasi
@dianerditto
Жыл бұрын
@@filamupictures9349 kuna mengi yameishapita hapo katikati kuna mengi hatujayaskia kutoka kwake kama kaoa kweli au lilikuwa tangazo hajatujibu mpk leo tuna mambo ya kujifunza mpk kafika alipo
Nakubali
Millard ayo please aje
Mdada alomvunja moyo ni jack wolper ukisikiliza kipindi cha salam na wakina fid q alisemaga maneno hayahaya anayosema jux kipindi amepewa gari na Dalla
My Favorite,#Jux!❤👌🏻😍
salama next Zuchu pls
Wolper huyu 😃 alimtesa sana dogo
Namkubali huyu jamaaa
the portions of the food samaki samaki gives to the guests on this show deserves a round of applause👏👏👏👏👏
@coleilukcole3816
Жыл бұрын
mlafi
Salama tultee mandonga mtu kazi 🤣🤣🤣🤣
😘😘
JUX🔥🔥
Jux is smart
Konde nae anatuhusu boss
“Its possible”
harmonize je
woow♥️♥️
Penda sana
alihongwa x5
Champion boy mbwana samatta lini??
Bb
Kununua madaftari 😂😂😂
Ivi kwann ma*** tu na isiwe watu wa kawaida. Salama what do you think to establish this period of to enterview some body where you got this idea? When and me?
Wolper huyo
Huyo mtu wa kwanza Wolper kapewa mpira mkali BMW X6 biashara zangu
Ni kweli ulimtongoza Mimi mars 🙄😠
JUX ANATUSHAURI TUTAFUTE PESA
@jrsaid4270
Жыл бұрын
Ee tuache uvivu
NJIA ZA KUFANIKIWA KWA KUACHA UWONGO kzread.info/dash/bejne/ZIdkyMGvdbrIdJs.html
Salama na LavaLava next
mmmmh
@lawimalanda8907
Жыл бұрын
Plz make with Aishi manula!!!
Hicho kiti lazima nije nikae
@neemamoses7011
Жыл бұрын
In Shaa Allah
@ashminaabdulla8946
Жыл бұрын
Inshaallah
4:30 🔥 6:24 18:04 19:54 23:08
China upewe three bedrooms bure? Kuna business behind unafanya
@encernstudios3745
Жыл бұрын
Kwamba china unapajua snaa au sio
@jaymshana1426
Жыл бұрын
SIKILIZA KWA UMAKINI
@irenejerome5894
Жыл бұрын
alionga hela ndo akapewa
@emmamatemu8225
Жыл бұрын
@@encernstudios3745 kama hupajui ni wewe