IFAKARA: 5311 WAPATA HUDUMA YA MATIBABU YA MACHO.

#HABARI: Wagonjwa 5311 wamefikiwa na huduma za kibingwa za matibabu ya macho katika Mji mdogo wa Ifakara, wilayani Kilombero, mkoani Morogoro, wamepatiwa matibabu bure wakiwemo wagonjwa 219 wamefanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho, 2450 wamepatiwa miwani na 3258 wamepatiwa dawa na taasisi ya mo dewji foundation .
Huduma hizo za kibingwa ambazo zilikuwa zikitolewa katika Hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Fransisko Ifakara, wilayani Kilombero kwa siku tatu baadhi ya wagonjwa wakiwemo watu wenye ulemavu wa ngozi pamoja na baadhi ya viongozi wamefurahia kupata matibabu bure.

Пікірлер