Askofu Musomba aweka wazi/Mafuta ya Upako/Kutangatanga/Uvivu wa Kiroho/Kutaka Miujiza.

Kwa Ujasiri mkubwa Askofu Stephano Musomba kwenye Mahubiri yake katika kanisa la Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu Mbezi Jimbo kuu la Dar Es Salaam, Siku ya jumatano ya Majivu, ameonyesha wazi kutokufurahishwa na hali ya waumini wakatoliki waliopata Sakramenti zote kukingiuka na kuchanganya Imani zao na zile ambazo hawana misingi nazo ikiwemo wengi wao kutaka uharaka wa Maisha kwa Kukanyaga mafuta na kutafuta Miujiza bila ya kujua yote hayo yanachangiwa na mahangaiko ya maisha ambayo mwisho wake hayana tija ya kweli katika maisha yao.
Askofu Musomba ametoa mifano kadhaa ambayo licha ya uchungu wake bado mifano hiyo inabaki kuwa dawa kwa wale wanaopenda kupata matibabu ya kweli katika Kristo.
CHUNGU KUMEZA LAKINI INATIBU.
#BreezOnlineTv​​​​​​​​​​​​​ #TubuninaKuiaminiIsnjili
Breez Online Tv
S.L.P 38655
Dar Es Salaam Tanzania
Phone No: +255 756494796
Barua pepe: izackbreez11@gmail.com
Mitandao Mingine ya Kijamii:
Facebook: breez online Tv
Facebook Link: / breez-online. .
Instagram:Breez Online Tv

Пікірлер: 68

  • @simonnjovu586
    @simonnjovu5862 жыл бұрын

    Mapadre waache uvivu wa kuwafundisha waamini. Wajibu maswali yanayowasumbua waamini na wao wenyewe. Wakristo wafundishwe na wahimizwe kusoma Neno la Mungu na kuliishi. Huwezi kuwa mkristo safi na mwaminifu kwa Mungu kwa mahubiri ya dakika 5-15 mara moja kwa juma.

  • @paulmsape163
    @paulmsape1639 ай бұрын

    Nafikiri ni ufahamu tu,wengi wetu wanapenda miujiza kuliko neno la Mungu

  • @VenerandaKundi-ph4hg
    @VenerandaKundi-ph4hg5 ай бұрын

    Nakushukuru mtumishi sema watu tupone maana mie nashangaa sana sie wakatoriki wengi tunahangaika ukimkataza anakuchukia wengi wamekufa muundelee kutuelewesha na kutuongoza kipindi hiki ni kigumu msichoke semeni

  • @milley7185
    @milley7185 Жыл бұрын

    Baadae wanalazwa na miunguuuuu......n kelele maskio kila mmoja Alalama

  • @thobiasbeda7204
    @thobiasbeda72042 жыл бұрын

    Baba huko Ni kujazwa hofu uchonganishi kusifia uchawi kumpandisha mapepo pia huko wanatoa pesa bila kupenda akili zao zimefungwa lakini kanisa liludishe maombi ya kweli yenye nguvu ili watu wapokee upako wa kweli itawasaidia wasiende hongera

  • @zablonshisia364
    @zablonshisia364 Жыл бұрын

    Wow very nice maubiri

  • @jordanjuma6709
    @jordanjuma67092 жыл бұрын

    YESU KRISTO anasema ijue kweli nayo itakuweka huru

  • @jordanjuma6709
    @jordanjuma67092 жыл бұрын

    Kwanini mnamtukuza bikira maria mmeweka na sanamu hamsini kama mnawapeleke watu motoni

  • @jordanjuma6709
    @jordanjuma67092 жыл бұрын

    Mbona hatuonagi uponyaji kanisa la katoriki mnaabudu sanamu zisizoweza kusema tuombe Tina kwa BWANA YESU

  • @jordanjuma6709
    @jordanjuma67092 жыл бұрын

    Tatizo katoriki mmejaa mapokeo tu hamfundishi NENO LA MUNGU ila mapokeo tu fundisheni BIblia

  • @samwelgaspar7361
    @samwelgaspar73612 жыл бұрын

    Amina

  • @jordanjuma6709
    @jordanjuma67092 жыл бұрын

    Mnajihesabia haki kama wale mafarisayo

  • @alisasportsTV
    @alisasportsTV2 жыл бұрын

    Yn 14:13-14 SUV "Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya" Yaani huyu askofu ni wa mchongo kabisaa hana lolote anatoa majungu akiwa madhabahuni... amesahau kuwa kanisa la Roman katoliki linaamini zaidi kwenye mapokeo kuliko neno la Mungu..ndio maana kanisa limejaa masanamu kila kona na kusahau kuomba kwa Jina la YESU!! MUNGU ATUSAIDIE SANA KATIKA NYAKATI HIZI TULIZONAZO!

  • @thobiasbeda7204
    @thobiasbeda72042 жыл бұрын

    Hongera Sana baba huo ndio ukweli siku za mwisho tuache kuhubiri dini tumhubiri Kristo uvivu wa kiroho ndio tatizo wahasham wanalala usingizi wameridhika kuhudumiwa na masista kutembelea magari makubwa Sasa wauza mafuta ,vitambaa vya upako Sasa ndala za upako na mazingaumbwe na kujazwa mapepo kumbu 13:1--12 onyo kwa wote

  • @marie-laurene.
    @marie-laurene.2 жыл бұрын

    Asante Baba!!! Mungu akulinde Mtumishi.👍🇨🇩

  • @deborahmgedzi7269
    @deborahmgedzi72692 жыл бұрын

    Mungu Mwenyezi Awabariki viongozi wanaochunga kondoo waliokabidhiwa na Baba.

  • @judithnzisa9048
    @judithnzisa90482 жыл бұрын

    Asante Baba Askofu kwa kuwakumbusha kondoo kwamba washike imani kikamilifu na kuwa na msimamo wa kiimani.Mungu akubariki..Baba

  • @jordanjuma6709
    @jordanjuma67092 жыл бұрын

    Pia imeandikwa lipo jina lipitalo majina yote ni jina la YESU KRISTO wa Nazareth sio bikira maria

  • @annamazengo975
    @annamazengo9752 жыл бұрын

    Acha majungu kwenye madhabahu hubiri neno,kinakuuma,unaharibu watu Wala huwajengi.

  • @julianadaudi8541
    @julianadaudi85412 жыл бұрын

    Asante baba kwa neno zuri .

  • @mathayomwashambwa1238
    @mathayomwashambwa12382 жыл бұрын

    ANZENI KUFANYA ISHARA ZA MITUME KAMA MATENDO 5:14-17. KIVULI CHA MITUME PETRO KILIINUA WAGONJWA, KANISA KATOLIKI WASHENI MOTO WA NGUVU ZA MUNGU ILI KUKOMESHA MAKANISA YANAYOINUKIA KTK NGUVU ZA KIROHO...SAA IMEFIKA MOTO WA KRISTO UTAWAKA MAHEKALU YATABAKIA WAZIIIIIII

  • @leonardmrope9528
    @leonardmrope95282 жыл бұрын

    Ahsante BABA

  • @raphaelnzulimwashibanda3762
    @raphaelnzulimwashibanda37622 жыл бұрын

    Amina baba mm E A G T Ila huu ni ukweli sema kweli watu wapone nami nipote hii ndo injili ya kweli

  • @restitutanjau2585
    @restitutanjau25852 жыл бұрын

    Asante sana Baba kwa Somo,nimepata kitu ktk imani yangu

  • @brownmtofole
    @brownmtofole2 жыл бұрын

    Watu wanafuata imani inayotenda kazi...

  • @frankjohn8706
    @frankjohn87062 жыл бұрын

    Watu wanatafuta kufunguliwa sio mapambo ya maneno kama ameponywa na YESU kwann amuache,

  • @jordanjuma6709
    @jordanjuma67092 жыл бұрын

    Pia mmejaa mapokeo kwa nini mnasema bikira maria atuombee wakati BWANA YESU ndiye anayetuombea kwa MUNGU upo hp

  • @chazyshadrack2558
    @chazyshadrack25582 жыл бұрын

    Amina baba .kwa neno ubariwe sana 🔥🔥

  • @sixtuscharles1788
    @sixtuscharles17882 жыл бұрын

    Ubarikiwe sana baba

  • @raphaelnzulimwashibanda3762
    @raphaelnzulimwashibanda37622 жыл бұрын

    Tupone baba tupone

  • @victorpatrickmnyika5948
    @victorpatrickmnyika59482 жыл бұрын

    Asante baba kwa mafundisho mazuri

  • @wilfredlukowo9476
    @wilfredlukowo94762 жыл бұрын

    Wakatoriki mnajichanganya sana kuyasema makanisa mengine.tukiwachambua hamuwezi simama wekeni mdahalo wa nani anafanya kazi ya MUNGU na anae fanya kazi ya wazungu

  • @prophetislael5265

    @prophetislael5265

    2 жыл бұрын

    Mungu wao nimwanamke bikija malia

  • @marrylimu6968
    @marrylimu69682 жыл бұрын

    Asante baba kwa neno nzurii Mungu atusaidie sana

  • @neemarenaida6667
    @neemarenaida66672 жыл бұрын

    Sema baba wenye masikio tusikie

  • @milley7185
    @milley7185 Жыл бұрын

    Viini macho hivyo

  • @tecklamgomberi4253
    @tecklamgomberi42532 жыл бұрын

    Amen

  • @patrickshirima3583
    @patrickshirima35832 жыл бұрын

    Ujumbe mzuri sana hongera kwa ujasiri huo

  • @lemykiyeyeu5436
    @lemykiyeyeu54362 жыл бұрын

    Songa mbele baba askofu tupone

  • @jordanjuma6709
    @jordanjuma67092 жыл бұрын

    Msimseme mtumishi wa BWANA pia msijione kama katoriki ninyi kuwa mpo sahihi sio hivyo kila mtu anavyoamini lmani ni kitu kingine usiseme wewe upo sawa

  • @jordanjuma6709

    @jordanjuma6709

    2 жыл бұрын

    Ahaa katoriki mnaabudu sanamu zisizoweza kusema toweni hayo masanamu

  • @SmilingCityMap-xb9md
    @SmilingCityMap-xb9md4 ай бұрын

    Sijaona tofauti ya makuhani wakatoliki na manabii maana wote wanatumia vifaa vya kiroho katika Ibada zao hakuna tofauti nashangaa Kwa nini wanatupiana madongo au NI mwendo wa kugombea waumini ?

  • @kasianzulu3859
    @kasianzulu38592 жыл бұрын

    Tunaambiwa kila sku ila kuelewa hua hamna lakini ni ukaid tu wakatolik wengi wanajua kabisa kuhusu kanisa letu

  • @VenerandaKundi-ph4hg
    @VenerandaKundi-ph4hg5 ай бұрын

    Hivi watu wagumu jamani mtu anaenda huku kuhangaika kwenye kukanyaga mafuta mie naenda katolic natoa zaka maombi yangu shida zangu mungu anajibu palepale siwadanganyi tusitangetange katolic mapadre wanafundisha vizuri pia kuna karismatic tuache mambo ya hovyo mathayo 24 soma sura yote

  • @ghatimakonge9383
    @ghatimakonge93832 жыл бұрын

    🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏

  • @annamazengo975
    @annamazengo9752 жыл бұрын

    Tokeni mtaani muone mateso ya watu,acha watafute uponyaji,hamna mbingu ya kupeleka mtu,hayo ni majungu Yesu hakaagi na wenye majungu.

  • @prophetislael5265

    @prophetislael5265

    2 жыл бұрын

    Wanaonesha wazi kuwa hawamuabudu Mungu kunakitu wanamuabudu hawajui kuomba hawajui kufundisha kaz kujifanya mtakatifu mtakatifu wakati niwalev

  • @joyceAdam-xn2yw

    @joyceAdam-xn2yw

    4 ай бұрын

    Wee anna una matatizo yako binafsi, mtu ambaye hana imani ndip anatangatanga, kama mwana mke malaya

  • @samwelysilungwe9767
    @samwelysilungwe97672 жыл бұрын

    Asante kwa SoMo zuri Baba sema yote tupone. Ubarikiwe sana

  • @wilfredlukowo9476
    @wilfredlukowo94762 жыл бұрын

    Uhuru wa kuabudu msitishe watu

  • @wilfredlukowo9476
    @wilfredlukowo94762 жыл бұрын

    Mnatakiwa kujibiwa na wasomi wa BIBLIA MNA MATENDO MENGI MABAYA .WIVU WA KIHUDUMA MMEKWAMA NA MAFUNDISHO YA KINYONGE WATU WANATAKA MAJIBU YA ROHO NA MAISHA YAO

  • @joyceAdam-xn2yw

    @joyceAdam-xn2yw

    4 ай бұрын

    Wewe mtakatifu, huna dhambi, tulia upashwe wewe mvivu wa kuamini

  • @warriouslendika1289
    @warriouslendika12892 жыл бұрын

    Hakuna zehebu lenye watu, Bali watu ndio hufuata zehebu analotaka kila mchungaji achunge kondoo wake usiwapotoshe Kyle ama hapa ndio sehemu sahihi

  • @paulmsape163
    @paulmsape1639 ай бұрын

    Ujumbe huu utuguse kiroho,maana tuliowengi hatusomi Biblia tunasubili kusomewa tu

  • @milley7185
    @milley7185 Жыл бұрын

    He

  • @rihannajoseph5796
    @rihannajoseph57962 жыл бұрын

    Hayo mafuta mbona ww hukuyakataa kipindi unapakwa acheni uchoyo bora mwamposa alipakwa mafuta na yy ametumwa atupake amefata maandiko ya Bible yanavyosema kama husomi biblia au padre hajafundisha huwez kujua

  • @dominickrukokelwa1284
    @dominickrukokelwa12842 жыл бұрын

    Tusome kitabu cha Baruku

  • @odhiaodhia9898
    @odhiaodhia98982 жыл бұрын

    Wanafata uponyaji maana yake nikwamba nyie mnamaneno ya uzima lakini Uzima haumo ndani yenu

  • @mwigarleysaid5406

    @mwigarleysaid5406

    2 жыл бұрын

    🙆🙆🤣🤣🤣🤣

  • @shamimushittindi1418

    @shamimushittindi1418

    2 жыл бұрын

    Uponyaji gani uponyaji utaipata ukiongeza wewe mwenyewe kiwango chako cha imani

  • @mamertkibori2450
    @mamertkibori24502 жыл бұрын

    Asante baba, kwa neno lenye afya Mungu akubariki. I 🙏🙏🙏

  • @epifaniamilinga2848
    @epifaniamilinga28482 жыл бұрын

    Wachungaji wa katoliki inawapasa kuweka semina za Mara kwa Mara kufundisha. neno.Jumapili hadi Jumapili.tena saa 2 tu.Biblia siyo kipaumbele.hapo kuna shida Sana.hasa kipindi hiki shetani Ana mbinu za kisasa.

  • @shamimushittindi1418

    @shamimushittindi1418

    2 жыл бұрын

    Kuna novena mafungo mbona yanatosha kabisa ni umalaya tu wa imani na kutokujitambua

  • @gabrielsaelie8091
    @gabrielsaelie80912 жыл бұрын

    Mwamposa aambiwe ukweli kuwa ni MPOTOSHAJI. Roma Catholic Church kemeeni hadharani hayo anayofanya Mwamposa yasiyo sahihi kulingana na neno la MUNGU. TUNAMLAANI ZUMARIDI MBONA TUNACHELEA KUMLAANI MWAMPOSA?

  • @matumizbinafsi4094

    @matumizbinafsi4094

    2 жыл бұрын

    Tuchapeni injili watu wanaomjua Kristo wapate kuongezeka

  • @godfreymwamaso2424

    @godfreymwamaso2424

    2 жыл бұрын

    Kwani Mwamposa anewafanya nini wakatolic hata siku moja sijawahi kumsikia akiwasema mapadri Wala maparoko mafundisho yake anawafundisha watu kimwili na kiroho na ameweza kuwafikia hata watu wasiyokuwa na Dini watu wa mataifa ambao kanisa katoliki limeshindwa kuwafikia tuache kuwakatisha tamaa watumishi wa Mungu kwa sababu tu wamelitikisa kanisa lenu acheni kujihesabia haki Mungu awabariki

Келесі