AMBWENE MWASONGWE - ALIKUTA IBADA (OFFICIAL MUSIC VIDEO)
Музыка
Ambwene Mwasongwe presents the music video for "Alikuta Ibada"
Wimbo huu ni maalumu Kwa ajili ya kulikumbusha kanisa la Bwana kuwa tumefikia Hali ileile ya Mafarisayo na Masadukayo ya unafiki.....
Nakukumbusha tunapaswa kumwabudu Bwana kwa roho na kweli.....
Tuondoe na kuyaacha mambo mengi ya mwili tuliyoyaingiza kanisani, turudi kwanza msalabani Kisha tuendelee na safari....
Mungu akubariki utayeuona huu wimbo na nisaidie kuwatumia link na wengine ili ujumbe umfikie kila MKRISTO
Watch All Music Videos by Ambwene Mwasongwe: • Ambwene Mwasongwe All ...
Follow Ambwene Mwasongwe
Instagram: / ambwenemwasongwe_
Subscribe to Ambwene Mwasongwe: / @ambweneobadiamwasongwe
Digital Branding & Marketing By:
Black Ozen Entertainment Limited: / blackozenentertainment...
Alikuta Ibada - Ambwene Mwasongwe (Lyrics)
Alikuta ibada zinaendelea
Ila zina tatizo
Alikuta maombi yanafanyika
Ila yana kasoro
Alikuta mifungo inaendelea
Ila ina dosari
Akakuta sadaka zinatolewa
Ila zina makandokando mengi
Akashangaa mwili umetawala
Badala ya Roho!
Akawafundisha ibada za Rohoni
Jinsi zitakiwavyo
Muombapo msiombe sala ndefu
Ili watu wawasifu
Mtoapo msitoe kwa matangazo
Ili watu wawaone
Mfungapo msijionyeshe
Ili watu wawasifu
Ila baba yenu aliye sirini
Yeye atawajazi
Mungu ni roho
Na wote wamwabuduo
Imewapasa kumwabudu
Kwa roho na kweli
Yeye huona kile ambacho jicho haliwezi kuona
Yeye hushika kile ambacho mkono hauwezi kukishika
Yeye hutafsiri lugha ya moyo hata mdomo usiposema
(Kwake hakuna siri)
Akawakemea Viongozi wa dini
Na washika sheria
Waandishi na mafarisayo
Na masadukayo
Hawakutaka-Walikasirika
Wakaleta vitabu
Kwa mamlaka ya nani wafanya haya?
Wapate kumshitaki
Wakadhani kiroho ni shule
Ili wamfedheheshe
Akawatazama akawapima
Walikuwa weupe
Wakamletea mwanamke mzinzi
Aliyefumaniwa
Wakataka wasikie neno lake
Atakavyomuhukumu
Akainama akachora chini
Akaandika majina yao
Ardhi ikageuka "video touch"
Wote wakakimbia
Mzee wa kanisa alipojiona
Akilewa na wake za watu
Shemasi kaona aibavyo sadaka
Naye akakimbia
Wanakwaya wakaona wanavyosengenyana
Na kupiga majungu
Yesu alipoinuka
Wote wamekimbia
Akasema na mimi sikuhukumu
Nenda usitende dhambi tena!
Ole mafarisayo na masadukayo
Mwaosha vikombe kwa nje
Ila ndani ni vichafu
Mwapaka makaburi chokaa
Ndani yake ni mifupa
Mwawabebesha watu mizigo
Ninui hambebi
Ole!
Mwawatungia wengine sheria ninyi hamzifuati!
Ey!
Akalikaribia kapu la sadaka
Aone wanachotoa
Ghafla akamwona mwanamke mjane
Anatoa kichache
Akasema huyu ametoa vingi
Kuliko ninyi nyote
Maana kwa Mungu wingi sio idadi
Ni ukamilifu wa jambo
Wengi mmetoa kwa mbwembwe
Vimeonekana vingi
Ila mlivyobakisha nyumbani ni vingi
Sio kama mwanamke huyu
Akaona wanagawana chenji ibadani
Akakasirika
Wanauza vitu kama mnada hekaluni
Mahali pa ibada
Akachukua fimbo akawachapa
Akapinduapindua
Nyumba yangu itakuwa ya sala
Sio nyumba ya biashara
Uko wapi moyo wa ibada?
Uko wapi moyo wa kicho!?
Ule moyo wa kutetemeka
Tusikiapo neno la Bwana
Mambo haya Je yamo kanisani leo basi tujiulize
Akija yule mwenye kanisa
Je hatatuchapa?
Mungu ni Roho
Na wote wamwabuduo
Imewapasa kumwabudu kwa roho na kweli
Maana yeye huona kile ambacho jicho
Haliwezi kuona
Yeye hushika kile ambacho mkono
Hauwezi kukishika
Yeye hutafsiri lugha ya moyo hata mdomo usiposema
Tunatakiwa tumwabudu Bwana
Tusichonge sanamu
Tuangalie tusije kujiabudu wenyewe
Pamoja na vitu vyetu
Tukicheza ili watu watuone
Tumejiabudu wenyewe
Tukiimba ili watu watufurahie
Tumetwaa utukufu
Tukigeuka nyuma na kutafuta maoni ya watu
Tumejichuuza wenyewe
Hicho ndicho kilichomponza lusifa
Alitaka asifiwe
ooh!
#AmbweneMwasongwe #AlikutaIbada
Пікірлер: 1 600
Jaman tunapoandka jina Mungu tusianzie na herufi ndogo,anza na herufi kubwa maana ndo Mungu aliyehai,ukiandika kwa herufu ndogo c Mungu aliyehai
mungu akubaliki ambwene mwasongwe mimi wakati nime anza kusikia nyimbozako nili amuwa kuokoka kwa sasa niko bishop wakanisa inchi burundi🇧🇮
@israelmbedule3897
Жыл бұрын
Barikiwa sana
@ziadaambanjaula8900
Жыл бұрын
Du umeokoka aya ubalikiwe
@elizabethleonard1809
Жыл бұрын
Glory be to God 🙏
@cizajean-marie7223
Жыл бұрын
Wahisemwo neza ncuti y'umusaraba
@wafabian8116
Жыл бұрын
God is great hallelujah
Kaka Mungu akubariki waimbaji wa Tanzania nadhani wajifunze kwako miaka mingi upo unamtukuza Mungu lakini hauchoshi my brother Yesu akubariki Sana
Nataka like zenu kama huna kinyongo na mwenzio ( moyo mweupe)
@moseskipawua9548
Ай бұрын
😢😢😢😢😢😢😢😢😢
Naomba jina lako kamili nikutumie muchango mdogo imekuwa muda ume nibariki sana
@ambweneobadiamwasongwe
2 жыл бұрын
Mungu akubariki Sana 0767619931 au 0713619931 Ambwene Mwasongwe
Huu wimbo kila nikikaa niangalie TV lazima nianze na huu wimbo najiona kama nahubiriwa na mtume Paulo,ambwene Mungu wa mbinguni azid kukutumia uendelee kuomba kirohoo
Hi wimbo unanijenga sana
Mungu nijalie kuyafany mapenzi Yako wewe uonae moyoni mwangu😭😭😭😭
Ubarikiwe mtumishi wa munngu kwa ujumbe wa mungu kwa mataifa naamini wengi tumefunguliwa ubarikiwe sana
Amen ambwene
Amen wimbo mzuri Sana unaponya moyo
Nasikiliza huku nasisimka...asante kwa msg nzur
Sema Ambwene una madini sana.. Daaah, we endelea tu kuimba Kaka, sisi tunapona huku.. Songs straight from the throne of heaven.. Hiki kizazi kina bahati ya kuwa na mtu kama wewe.
@safindume5051
2 жыл бұрын
Kabisa
@selestinekaale7545
2 жыл бұрын
Ni kweli kaka usemalo, Aisee! Halafu Tazama Hekima za BWANA, yeye kaka Ambwene anaona kawaida tu Aisee!😃😃
@willyke2251
2 жыл бұрын
Very true
@gilbertgodfrey6376
2 жыл бұрын
Kabisa huyu mwamba namkubali kinoma maana hamuigi mtu kuimba na anaimba kwa kumaanisha
@gilbertgodfrey6376
2 жыл бұрын
Yaani waimbaji wa siku hizi naona wamebaki wamili Ambwene na mchungaji abiudi wengine wote wanarapu na wananiudhi sana maana wanatoka nnje ya maadili ya mungu
True worshipers will worship in Spirit and Truth.
Endelea kutumikia KUSUDI LA MUNGU kwa kicho. BWANA YESU anaona utumishi wako
Wimbo mzuri sana. Picha pia iko vizuri sana. Mungu aibariki huduma yako
Hizi ndizo nyimbo tunazohitaji kusikiliza. Barikiwa Ambwene
@mzurikwaorevocatus2972
2 жыл бұрын
Kwel yan
@givasmwananzumi5941
Жыл бұрын
@@mzurikwaorevocatus2972 kabisaaa hi nyimbo nzuri xn
Wimbo muzuli Sana mungu akubaliki
Halloo halloo hii imeenda safiiii oyoooo
Nzuri sana jamani eeeh baba akubariki Mungu aah😅
Namshukuru Mungu kwa kutupatia zawadi hapa Tanzania 🇹🇿 ambayo ni #Ambwene_Mwasongwe na #Boaz_Danken kiukweli nyie watu mna Mungu ninaemuabudu mimi na mnaongozwa na Roho wa kweli
@nancygilliad2883
Жыл бұрын
Wimbo huu unanibariki sana san haya ndio mambo yapo leo makanisan Mungu atusaidie kweli,ubarikiwe Ambwene
Katika watumishi wa Mungu tuliobaki nao Tz wanaoimba katika roho na kweli! Barikiwa saana Mtumishi! Unaponya saana mioyo ya wengi!
@mzurikwaorevocatus2972
2 жыл бұрын
N kwel
@jeanettekikonde987
2 жыл бұрын
Kwel kabisa nyimbo zake. Pamoja na mavazi yake inapendeza Sana ubarikiwe sana maombi ni silaa tosha
Mungu nisaidie mengi yanautesa moyo wangu, from now nimeachilia
Hapa comment za wakenya ni chache na sababu ni za kiroho,,, hongera sana mtu wa rohoni kaka🎉
Uko wapi moyo wa ibada, moyo kutetemeka aiseeeh Mungu nipe moyo wa ibada nikuabudu katika roho na kweli
@rebeccan2321
3 ай бұрын
Uko wapi wa moyo wa Ibada ,ee Mungu wangu nanyenyekea kwako nope Moyo wa Ibada nikuabudu ktk Roho na kweli.❤
Huu Wimbo ni Mawaidha, huu wimba ni mahubiri, huu wimbo ni Ibada, huu wimbo ni Misa takatifu...ubarikiwe sana Mtumishi wa Mungu...endelea kutimiza jukumu la Mungu kukuleta Duniani🙏
Ninapo sikiriza wimbo huu najifunz kitu mungu akubark ambwene mwasongwe ukyala utufighwe fihjo kangi fihjo
Nmejikuta nanena kwa lugha barikiwa mtumishi wa bwana
Amina🎉🎉❤
Hakika mwenyez MUNGU amekubarik kipaji MUNGU aendelee kukutumia
Mtumishi wimbo huu uko vizuri Sana Sana ebuwatu wausikilize ktk Roho Kuna Mambo makubwa ya kujifunza
Mtumishi wa Bwana ubarikiwe. Tumepata ujumbe toka Yohana 4:24 kwa njia ya nyimbo. Kiukweli huwa unaimba theologia, tunapona kwa nyimbo zako. juzi mwana wa Azali, leo tena ujumbe huu muhimu.Mungu atusaidie tuabudu katika roho na kweli 🙏🙏🙏
@emmasanga4279
2 жыл бұрын
Ubarikiwe sana Kaka endeleaa mbele .
@giftasifiwe
Жыл бұрын
Hii nyimbo imenikumbusha mwaaka 1984.kanisani.turivyofundishwa.
@daudicherehanis
Жыл бұрын
mungu akuzidishe katika huduma yako
Amina baba ubalikiwe San nabarkiwa San na nyimbo zako na haipit sku nimeskilza nakpenda san maana nyimbo zako nazielewa sana 🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽❤️❤️❤️❤️❤️
Huu ni zaidi wa Wimbo. Ujumbe wa Yesu Kristu.
Natamani sasa Mungu akupe neema ya kuanza kufundisha na semina, seems you have more and we need to hear more!! Una hazina kubwa moyoni mwako .. Ikimpendeza Mungu akupe namna nyingine ya kutufikishia kwa wingi. Stay blessed
Our own Ambwene,. Kanisa letu la Tanzania lina baraka sana kuwa na mtu wa aina yako,. Umebarikiwa ulikumbushe kanisa na watu wa Mungu kuhusu maisha halisi ya Rohoni kabisa kabisa,.😌
@neemakitano5894
2 жыл бұрын
Kaka Ambwenee nabarikiwa Sana nanyimbo zako. MUNGU akubariki sanaaaa sanaaaa 🙌🙌🙌🙌
Wimbo huu hunifanya ni barikiwee sanaa .... Mungu akutunzeee mtumishi
Namshukuru MUNGU kwa ajiliyako kwamaana katikati ya mabadiliko ya dunia Sayansi na tecnolojia lkn bado nakupata kakaangu unaemwimbia MUNGU ktk roho na kweli, MUNGU AKUTUNZE !
My role model Kupitia nyimbo zako kaka niliamua kumfuata Yesu "Mzee wa siku" ni ushuhuda wangu Barikiwa
@salimalimasi1326
2 жыл бұрын
Akubariki Mungu
Powerful Message! "Inatupasa kumwabudu kwa Roho na Kweli. Anaye tafsiri lugha ya Moyo" Mungu akubariki sana Ambwene Mwasongwe.
Kaka Ambwene wewe endelea hivyohivyo kumsikiliza Mungu ktk huduma yako, hubiri kupitia uimbaji, tulio wengi chanzo cha kuokoka ni kupitia uimbaji, achana nao hao wanaoifuata dunia, wewe mtumikie Mungu kikamilifu
Nyimbo niipendayo kila sku lazma niiskize Mungu akubariki sana kweny huduma
😭😭😭😭 Mungu tusaidie kurudi katika Neno na tuishi katika Roho.
Duh!!!kuna wakati Daudi akiona kile Mungu amekiweka ndani yako anafarijika sana huko mbinguni na anatabasamu akijua kapata pacha aliyebaki hapa duniani. Ninampenda Mungu kwa ajili yako Ambwene🙏🙏🙏
@maggishillah4847
2 жыл бұрын
Kabisaa yaani... It's a Powerful Song!
@juliananicodemus2746
2 жыл бұрын
Wimbo mzuri mungu akubariki sna kaka Ambwene
Touching.. ujumbe mzito saana mpaka nimeogopa
Hakika wew ni mwamna imara daaaa nyimbo nmeikuta TikTok daa nmeifata ujumbe mzito sana najivunia kua na wew tz
Huu wimbo umasema yanayotendeka kwa makanisa siku hizi Mtumishi wa mungu kakangu Ambwena kwa kweli nyimbo zako za nitia nguvu sana.. Wimbo mtaamu mno..Barikiwa sana South Africa 🇿🇦 Cape Town tunabarikiwa Ujumbe ufikia watoto wetu nchini Kenya 🇰🇪
@geitandelwa299
Жыл бұрын
Ameni tuna Mambo MENGI Ila Sio ya MUNGU
Ambwene mwasongwe is underated his music is beyond international level ...God bless you MoG ...my favorite artist
Amen sana ubunifu mkubwa mtumishi wa BWANA, zidi kubarikiwa!
Tenashara wa kizazi hiki. Yesu angekuchagua kuwa tenashara kaka,, Coz angeutazama moyo wa Utumishi ndani Yako.
Kwa nyimbo zako tunamtukuza Mungu....live long life in music!! Stay blessed.
Hii ni Injili, this is Gospel mpeni maua yake Mwasongwe
Kaka nabarikiwaga sana na nyimbo zako hakika unanigusa sana nakuelewa sana nazichambuaga mpaka napata maana Barikiwaaa
Ubarikiwe kaka AMBWENE hakika MUNGU katupa wewe zawadi watanzania
I love this man of God Bless u🇺🇬🇺🇬
Ubarikiwe na Mungu ! Nyimbo zako zimenibariki Sana! Toka DRCongo. Lubumbashi.
Uko wapi moyo wakanisa😭😭😭😭😭😭😭😭😭yeye awona tusipo biona😭😭😭😭Mungu atusamehe🙏😭😭👆
Tuponye vijana wa sasa Mtumishi na MUNGU atusaidie
Naupenda sana huu wimbo
Hongera kwa huu wimbo mzuri
Mungu wa mbinguni akubali sana mtumish wa bwana kristo akutie nguvu
Barikiwa sanàaaa
Ibada njema
😀🔥Mungu akikupa kibari sehemu frani🔥 usinyamaze🔥🙌
uko kama mrisho mpoto kwenye muundo wa mashahiri lakin wewe uko kizazi zaidi , ubarikiwe sna Big Up
Ambwene Ambwene Ambwene Mwasongwe MUNGU BABA WA MBINGUNI AKUBARIKI SANA
🥳🥳🥳🥳 Mungu azidi kukupa mafunuo Mtumishi wa Mungu kulifundisha kanisa kile Mungu anataka tuenende nacho🙏🏼🙏🏼 yaan ni ujumbe kwa kanisa na mtu mmoja mmoja anayetaka kumwona Mungu katika viwango vingine
I just love how our Tanzanian brothers and sisters make music straight from the scriptures. More love form Nairobi!
@rogathesarwatt
2 жыл бұрын
All about Lugha Adhu ya Kiswahili
@paulwachenje861
2 жыл бұрын
That's exactly what I was heading to post but you represented the likes of us well
@barakahiluka4905
2 жыл бұрын
Mungu akubaliki sana mtumishi👐
@danielnzali5609
2 жыл бұрын
Mungu akutunze mtumishi....🔥🔥
@dollnjosy3210
2 жыл бұрын
🙏🙏❤️
Akawaafundisha ibada za rohon jinc zitakiwavyo
Hii nyimbo inatosha kukuweka kwenye uwepo wa roho mtakatifu
My favorite musician be blessed ambwene mwasongwe 🙏🙏
Huyu Mtumshi anaimbia Mungu wakweli kabisa eee Mungu umuongoze asitoke kwenye mstari wako Kama wengine
Mandiko mwanzo mwisho.just how it should be.
Wawouuuuuh,unajuwa kweli ,Mungu akupanuliye mipaka.
Kuna vile hii nyimbo inatuonesha bible ni kitabu kizuri sana, kitachotufanya tukutane na watu walioshi maisha kama yetu , ILa walikuja kubadirika na kuwa watu wema sana, mungu akubariki na kukutunza sana kaka ambwene, akuweke ili kupitia wewe wengi kati yetu tumrudie mungu🤲 na kuijua kweli🙏.
Glory to God ❤❤
Asante sanaa kwa kunikumbusha Ibabda ya Moyoni Mtumishi
Jehovah aonaye Sirini braza azodi kukuweka makumbusho kwa ajili ya UTUKUFU WAKE...Ahsante nimepokea ujumbe wangu
Man of God. Kyala akutule
I just bumped into your songs,,, this one's is on another level
Mungu akuinue zaidi mtumishi wa Mungu.... Kwa kazi nzuri....
Asante kaka...kwa huu wimbo hakika una mafunzo, much love from kenya 🇰🇪
Sijashangaa kwa uzuri wa wimbo huu maana Mungu amekuinua,nyimbo zako zote ni nzuri na zina mafundisho. Mungu aendelee kukuinua.
Mungu akubariki sana Ambwene Mwasongwe. Full song from the Scriptures. My favorite Tanzanian Gospel Artist.
Mungu akubaliki nyimbo zako zinanibariki
Ee Mwenyezi Mungu tunaomba utusaidie masikio ya Rohoni tunapo hubiriwa mafundisho kama haya kwa nyimbo tusiyapuuze bali yakalete mabadiliko ndani ya mioyo yetu.Amina
I'm blessed Mungu aendelee kukutumia jinsi apendavyo yeye mtumishi🙌💅🙌
Mungu asikuachee
Ubarikiwe mtumishi...Ujumbe mzuri sana 👏
This is exactly what is happening in our churches today, wimbo huu una mafundisho ya kweli.....
Kwa neema ya Bwana hujawahi kukosea ,sifa na utukufu ni kwa Bwana nangoja official video ya UMENIPA HESHIMA 🔥🔥🔥
Mungu akujaze baraka kwa huduma hii Ambwene
Mungu Aku bariki muimbadji wa Mungu bwana
Moyo wa Ibada 🙌what a song straight from the Word of God 🙏🙏more blessings to you🙌❤
Wasaidieni wake zenu wavae kibibilia
🙏🙏🙏Abwene MUNGU akubariki sanaa
The music saasa; uwiiiiii this song 🙌🙌🙌🤭... life transforming to the church kabisa kabisa 😭🙌
What a powerful message! This is a whole sermon! Ahsante kwa Neno, more grace to you Mtumishi wa Yesu! Blessings
@mamy1605
2 жыл бұрын
Amen amen 🙏🙏🙏🙏
@munyibonface166
2 жыл бұрын
Indeed it is!
@masatuzephania4036
2 жыл бұрын
Niceee sanaa
@gloriousn6425
2 жыл бұрын
It really is 🙏🏿
@oten2731
2 жыл бұрын
@@mamy1605 q1q11
Najifunza na ninakua kiroho kupitia jumbe zitokanazo na Neno la Mungu.. Barikiwa sana mtumish wa Mungu..
Ambweneeee ndaga fijooooo utukufu kwa YESU. Naitwa Happy Mwaigwisya. Prophetess of the most high God.