AMBWENE MWASONGWE - ALIKUTA IBADA (OFFICIAL MUSIC VIDEO)

Музыка

Ambwene Mwasongwe presents the music video for "Alikuta Ibada"
Wimbo huu ni maalumu Kwa ajili ya kulikumbusha kanisa la Bwana kuwa tumefikia Hali ileile ya Mafarisayo na Masadukayo ya unafiki.....
Nakukumbusha tunapaswa kumwabudu Bwana kwa roho na kweli.....
Tuondoe na kuyaacha mambo mengi ya mwili tuliyoyaingiza kanisani, turudi kwanza msalabani Kisha tuendelee na safari....
Mungu akubariki utayeuona huu wimbo na nisaidie kuwatumia link na wengine ili ujumbe umfikie kila MKRISTO
Watch All Music Videos by Ambwene Mwasongwe: • Ambwene Mwasongwe All ...
Follow Ambwene Mwasongwe
Instagram: / ambwenemwasongwe_
Subscribe to Ambwene Mwasongwe: / @ambweneobadiamwasongwe
Digital Branding & Marketing By:
Black Ozen Entertainment Limited: / blackozenentertainment...
Alikuta Ibada - Ambwene Mwasongwe (Lyrics)
Alikuta ibada zinaendelea
Ila zina tatizo
Alikuta maombi yanafanyika
Ila yana kasoro
Alikuta mifungo inaendelea
Ila ina dosari
Akakuta sadaka zinatolewa
Ila zina makandokando mengi
Akashangaa mwili umetawala
Badala ya Roho!
Akawafundisha ibada za Rohoni
Jinsi zitakiwavyo
Muombapo msiombe sala ndefu
Ili watu wawasifu
Mtoapo msitoe kwa matangazo
Ili watu wawaone
Mfungapo msijionyeshe
Ili watu wawasifu
Ila baba yenu aliye sirini
Yeye atawajazi
Mungu ni roho
Na wote wamwabuduo
Imewapasa kumwabudu
Kwa roho na kweli
Yeye huona kile ambacho jicho haliwezi kuona
Yeye hushika kile ambacho mkono hauwezi kukishika
Yeye hutafsiri lugha ya moyo hata mdomo usiposema
(Kwake hakuna siri)
Akawakemea Viongozi wa dini
Na washika sheria
Waandishi na mafarisayo
Na masadukayo
Hawakutaka-Walikasirika
Wakaleta vitabu
Kwa mamlaka ya nani wafanya haya?
Wapate kumshitaki
Wakadhani kiroho ni shule
Ili wamfedheheshe
Akawatazama akawapima
Walikuwa weupe
Wakamletea mwanamke mzinzi
Aliyefumaniwa
Wakataka wasikie neno lake
Atakavyomuhukumu
Akainama akachora chini
Akaandika majina yao
Ardhi ikageuka "video touch"
Wote wakakimbia
Mzee wa kanisa alipojiona
Akilewa na wake za watu
Shemasi kaona aibavyo sadaka
Naye akakimbia
Wanakwaya wakaona wanavyosengenyana
Na kupiga majungu
Yesu alipoinuka
Wote wamekimbia
Akasema na mimi sikuhukumu
Nenda usitende dhambi tena!
Ole mafarisayo na masadukayo
Mwaosha vikombe kwa nje
Ila ndani ni vichafu
Mwapaka makaburi chokaa
Ndani yake ni mifupa
Mwawabebesha watu mizigo
Ninui hambebi
Ole!
Mwawatungia wengine sheria ninyi hamzifuati!
Ey!
Akalikaribia kapu la sadaka
Aone wanachotoa
Ghafla akamwona mwanamke mjane
Anatoa kichache
Akasema huyu ametoa vingi
Kuliko ninyi nyote
Maana kwa Mungu wingi sio idadi
Ni ukamilifu wa jambo
Wengi mmetoa kwa mbwembwe
Vimeonekana vingi
Ila mlivyobakisha nyumbani ni vingi
Sio kama mwanamke huyu
Akaona wanagawana chenji ibadani
Akakasirika
Wanauza vitu kama mnada hekaluni
Mahali pa ibada
Akachukua fimbo akawachapa
Akapinduapindua
Nyumba yangu itakuwa ya sala
Sio nyumba ya biashara
Uko wapi moyo wa ibada?
Uko wapi moyo wa kicho!?
Ule moyo wa kutetemeka
Tusikiapo neno la Bwana
Mambo haya Je yamo kanisani leo basi tujiulize
Akija yule mwenye kanisa
Je hatatuchapa?
Mungu ni Roho
Na wote wamwabuduo
Imewapasa kumwabudu kwa roho na kweli
Maana yeye huona kile ambacho jicho
Haliwezi kuona
Yeye hushika kile ambacho mkono
Hauwezi kukishika
Yeye hutafsiri lugha ya moyo hata mdomo usiposema
Tunatakiwa tumwabudu Bwana
Tusichonge sanamu
Tuangalie tusije kujiabudu wenyewe
Pamoja na vitu vyetu
Tukicheza ili watu watuone
Tumejiabudu wenyewe
Tukiimba ili watu watufurahie
Tumetwaa utukufu
Tukigeuka nyuma na kutafuta maoni ya watu
Tumejichuuza wenyewe
Hicho ndicho kilichomponza lusifa
Alitaka asifiwe
ooh!
#AmbweneMwasongwe #AlikutaIbada

Пікірлер: 1 600

  • @nakilingwembele9504
    @nakilingwembele95049 ай бұрын

    Jaman tunapoandka jina Mungu tusianzie na herufi ndogo,anza na herufi kubwa maana ndo Mungu aliyehai,ukiandika kwa herufu ndogo c Mungu aliyehai

  • @pasteurelizabethruzoviyo3978
    @pasteurelizabethruzoviyo39782 жыл бұрын

    mungu akubaliki ambwene mwasongwe mimi wakati nime anza kusikia nyimbozako nili amuwa kuokoka kwa sasa niko bishop wakanisa inchi burundi🇧🇮

  • @israelmbedule3897

    @israelmbedule3897

    Жыл бұрын

    Barikiwa sana

  • @ziadaambanjaula8900

    @ziadaambanjaula8900

    Жыл бұрын

    Du umeokoka aya ubalikiwe

  • @elizabethleonard1809

    @elizabethleonard1809

    Жыл бұрын

    Glory be to God 🙏

  • @cizajean-marie7223

    @cizajean-marie7223

    Жыл бұрын

    Wahisemwo neza ncuti y'umusaraba

  • @wafabian8116

    @wafabian8116

    Жыл бұрын

    God is great hallelujah

  • @japhetmichael7608
    @japhetmichael76082 жыл бұрын

    Kaka Mungu akubariki waimbaji wa Tanzania nadhani wajifunze kwako miaka mingi upo unamtukuza Mungu lakini hauchoshi my brother Yesu akubariki Sana

  • @johnmgaya2280
    @johnmgaya2280 Жыл бұрын

    Nataka like zenu kama huna kinyongo na mwenzio ( moyo mweupe)

  • @moseskipawua9548

    @moseskipawua9548

    Ай бұрын

    😢😢😢😢😢😢😢😢😢

  • @citovunjabeilimitedcompany4455
    @citovunjabeilimitedcompany44552 жыл бұрын

    Naomba jina lako kamili nikutumie muchango mdogo imekuwa muda ume nibariki sana

  • @ambweneobadiamwasongwe

    @ambweneobadiamwasongwe

    2 жыл бұрын

    Mungu akubariki Sana 0767619931 au 0713619931 Ambwene Mwasongwe

  • @SupajrChagaa
    @SupajrChagaa3 ай бұрын

    Huu wimbo kila nikikaa niangalie TV lazima nianze na huu wimbo najiona kama nahubiriwa na mtume Paulo,ambwene Mungu wa mbinguni azid kukutumia uendelee kuomba kirohoo

  • @VastineKahindo
    @VastineKahindoАй бұрын

    Hi wimbo unanijenga sana

  • @user-cr4eu4zc6u
    @user-cr4eu4zc6u2 ай бұрын

    Mungu nijalie kuyafany mapenzi Yako wewe uonae moyoni mwangu😭😭😭😭

  • @JanethMgeni-cr4wl
    @JanethMgeni-cr4wl2 ай бұрын

    Ubarikiwe mtumishi wa munngu kwa ujumbe wa mungu kwa mataifa naamini wengi tumefunguliwa ubarikiwe sana

  • @REHEMAMGENI
    @REHEMAMGENI2 ай бұрын

    Amen ambwene

  • @lazarozebedayo4948
    @lazarozebedayo49482 ай бұрын

    Amen wimbo mzuri Sana unaponya moyo

  • @nasramtuluma3949
    @nasramtuluma3949 Жыл бұрын

    Nasikiliza huku nasisimka...asante kwa msg nzur

  • @rtlusungu
    @rtlusungu2 жыл бұрын

    Sema Ambwene una madini sana.. Daaah, we endelea tu kuimba Kaka, sisi tunapona huku.. Songs straight from the throne of heaven.. Hiki kizazi kina bahati ya kuwa na mtu kama wewe.

  • @safindume5051

    @safindume5051

    2 жыл бұрын

    Kabisa

  • @selestinekaale7545

    @selestinekaale7545

    2 жыл бұрын

    Ni kweli kaka usemalo, Aisee! Halafu Tazama Hekima za BWANA, yeye kaka Ambwene anaona kawaida tu Aisee!😃😃

  • @willyke2251

    @willyke2251

    2 жыл бұрын

    Very true

  • @gilbertgodfrey6376

    @gilbertgodfrey6376

    2 жыл бұрын

    Kabisa huyu mwamba namkubali kinoma maana hamuigi mtu kuimba na anaimba kwa kumaanisha

  • @gilbertgodfrey6376

    @gilbertgodfrey6376

    2 жыл бұрын

    Yaani waimbaji wa siku hizi naona wamebaki wamili Ambwene na mchungaji abiudi wengine wote wanarapu na wananiudhi sana maana wanatoka nnje ya maadili ya mungu

  • @Ijusthavequestions
    @Ijusthavequestions Жыл бұрын

    True worshipers will worship in Spirit and Truth.

  • @user-fv9tu2pe8s
    @user-fv9tu2pe8s4 ай бұрын

    Endelea kutumikia KUSUDI LA MUNGU kwa kicho. BWANA YESU anaona utumishi wako

  • @martinchambai5460
    @martinchambai5460 Жыл бұрын

    Wimbo mzuri sana. Picha pia iko vizuri sana. Mungu aibariki huduma yako

  • @lucywilson5875
    @lucywilson58752 жыл бұрын

    Hizi ndizo nyimbo tunazohitaji kusikiliza. Barikiwa Ambwene

  • @mzurikwaorevocatus2972

    @mzurikwaorevocatus2972

    2 жыл бұрын

    Kwel yan

  • @givasmwananzumi5941

    @givasmwananzumi5941

    Жыл бұрын

    @@mzurikwaorevocatus2972 kabisaaa hi nyimbo nzuri xn

  • @letisiabaritazari7606
    @letisiabaritazari7606Ай бұрын

    Wimbo muzuli Sana mungu akubaliki

  • @SamsonEzekiel-or9xc
    @SamsonEzekiel-or9xc2 ай бұрын

    Halloo halloo hii imeenda safiiii oyoooo

  • @katarinasimon8647
    @katarinasimon86473 ай бұрын

    Nzuri sana jamani eeeh baba akubariki Mungu aah😅

  • @jamesbavo
    @jamesbavo2 жыл бұрын

    Namshukuru Mungu kwa kutupatia zawadi hapa Tanzania 🇹🇿 ambayo ni #Ambwene_Mwasongwe na #Boaz_Danken kiukweli nyie watu mna Mungu ninaemuabudu mimi na mnaongozwa na Roho wa kweli

  • @nancygilliad2883

    @nancygilliad2883

    Жыл бұрын

    Wimbo huu unanibariki sana san haya ndio mambo yapo leo makanisan Mungu atusaidie kweli,ubarikiwe Ambwene

  • @magrethmkongwee8512
    @magrethmkongwee85122 жыл бұрын

    Katika watumishi wa Mungu tuliobaki nao Tz wanaoimba katika roho na kweli! Barikiwa saana Mtumishi! Unaponya saana mioyo ya wengi!

  • @mzurikwaorevocatus2972

    @mzurikwaorevocatus2972

    2 жыл бұрын

    N kwel

  • @jeanettekikonde987

    @jeanettekikonde987

    2 жыл бұрын

    Kwel kabisa nyimbo zake. Pamoja na mavazi yake inapendeza Sana ubarikiwe sana maombi ni silaa tosha

  • @AnnaMasangula-h5e
    @AnnaMasangula-h5eАй бұрын

    Mungu nisaidie mengi yanautesa moyo wangu, from now nimeachilia

  • @Gwa-Kayaga
    @Gwa-KayagaАй бұрын

    Hapa comment za wakenya ni chache na sababu ni za kiroho,,, hongera sana mtu wa rohoni kaka🎉

  • @nellykobadi8142
    @nellykobadi8142 Жыл бұрын

    Uko wapi moyo wa ibada, moyo kutetemeka aiseeeh Mungu nipe moyo wa ibada nikuabudu katika roho na kweli

  • @rebeccan2321

    @rebeccan2321

    3 ай бұрын

    Uko wapi wa moyo wa Ibada ,ee Mungu wangu nanyenyekea kwako nope Moyo wa Ibada nikuabudu ktk Roho na kweli.❤

  • @Bryson883
    @Bryson8839 ай бұрын

    Huu Wimbo ni Mawaidha, huu wimba ni mahubiri, huu wimbo ni Ibada, huu wimbo ni Misa takatifu...ubarikiwe sana Mtumishi wa Mungu...endelea kutimiza jukumu la Mungu kukuleta Duniani🙏

  • @franksentiyongo8803
    @franksentiyongo8803 Жыл бұрын

    Ninapo sikiriza wimbo huu najifunz kitu mungu akubark ambwene mwasongwe ukyala utufighwe fihjo kangi fihjo

  • @brendakinenekejo8464
    @brendakinenekejo8464 Жыл бұрын

    Nmejikuta nanena kwa lugha barikiwa mtumishi wa bwana

  • @ZaiElias
    @ZaiElias2 ай бұрын

    Amina🎉🎉❤

  • @mariampatrick3479
    @mariampatrick34792 жыл бұрын

    Hakika mwenyez MUNGU amekubarik kipaji MUNGU aendelee kukutumia

  • @evansimsagaatkog1953
    @evansimsagaatkog19532 жыл бұрын

    Mtumishi wimbo huu uko vizuri Sana Sana ebuwatu wausikilize ktk Roho Kuna Mambo makubwa ya kujifunza

  • @eliufoosimonchuri4160
    @eliufoosimonchuri41602 жыл бұрын

    Mtumishi wa Bwana ubarikiwe. Tumepata ujumbe toka Yohana 4:24 kwa njia ya nyimbo. Kiukweli huwa unaimba theologia, tunapona kwa nyimbo zako. juzi mwana wa Azali, leo tena ujumbe huu muhimu.Mungu atusaidie tuabudu katika roho na kweli 🙏🙏🙏

  • @emmasanga4279

    @emmasanga4279

    2 жыл бұрын

    Ubarikiwe sana Kaka endeleaa mbele .

  • @giftasifiwe

    @giftasifiwe

    Жыл бұрын

    Hii nyimbo imenikumbusha mwaaka 1984.kanisani.turivyofundishwa.

  • @daudicherehanis

    @daudicherehanis

    Жыл бұрын

    mungu akuzidishe katika huduma yako

  • @mackrinaerenesto6402
    @mackrinaerenesto6402 Жыл бұрын

    Amina baba ubalikiwe San nabarkiwa San na nyimbo zako na haipit sku nimeskilza nakpenda san maana nyimbo zako nazielewa sana 🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽❤️❤️❤️❤️❤️

  • @robertwaichigo2553
    @robertwaichigo25532 жыл бұрын

    Huu ni zaidi wa Wimbo. Ujumbe wa Yesu Kristu.

  • @faithikenda
    @faithikenda2 жыл бұрын

    Natamani sasa Mungu akupe neema ya kuanza kufundisha na semina, seems you have more and we need to hear more!! Una hazina kubwa moyoni mwako .. Ikimpendeza Mungu akupe namna nyingine ya kutufikishia kwa wingi. Stay blessed

  • @joellumala3206
    @joellumala32062 жыл бұрын

    Our own Ambwene,. Kanisa letu la Tanzania lina baraka sana kuwa na mtu wa aina yako,. Umebarikiwa ulikumbushe kanisa na watu wa Mungu kuhusu maisha halisi ya Rohoni kabisa kabisa,.😌

  • @neemakitano5894

    @neemakitano5894

    2 жыл бұрын

    Kaka Ambwenee nabarikiwa Sana nanyimbo zako. MUNGU akubariki sanaaaa sanaaaa 🙌🙌🙌🙌

  • @rosadinahjoseph9137
    @rosadinahjoseph9137 Жыл бұрын

    Wimbo huu hunifanya ni barikiwee sanaa .... Mungu akutunzeee mtumishi

  • @christinamwangoc4779
    @christinamwangoc47792 жыл бұрын

    Namshukuru MUNGU kwa ajiliyako kwamaana katikati ya mabadiliko ya dunia Sayansi na tecnolojia lkn bado nakupata kakaangu unaemwimbia MUNGU ktk roho na kweli, MUNGU AKUTUNZE !

  • @pris_jimsband
    @pris_jimsband2 жыл бұрын

    My role model Kupitia nyimbo zako kaka niliamua kumfuata Yesu "Mzee wa siku" ni ushuhuda wangu Barikiwa

  • @salimalimasi1326

    @salimalimasi1326

    2 жыл бұрын

    Akubariki Mungu

  • @morrismuriithi6741
    @morrismuriithi67412 жыл бұрын

    Powerful Message! "Inatupasa kumwabudu kwa Roho na Kweli. Anaye tafsiri lugha ya Moyo" Mungu akubariki sana Ambwene Mwasongwe.

  • @jannethjohn747
    @jannethjohn747 Жыл бұрын

    Kaka Ambwene wewe endelea hivyohivyo kumsikiliza Mungu ktk huduma yako, hubiri kupitia uimbaji, tulio wengi chanzo cha kuokoka ni kupitia uimbaji, achana nao hao wanaoifuata dunia, wewe mtumikie Mungu kikamilifu

  • @sarahnyamwendo2118
    @sarahnyamwendo2118 Жыл бұрын

    Nyimbo niipendayo kila sku lazma niiskize Mungu akubariki sana kweny huduma

  • @milkajm4762
    @milkajm47622 жыл бұрын

    😭😭😭😭 Mungu tusaidie kurudi katika Neno na tuishi katika Roho.

  • @ebenezerdayan3797
    @ebenezerdayan37972 жыл бұрын

    Duh!!!kuna wakati Daudi akiona kile Mungu amekiweka ndani yako anafarijika sana huko mbinguni na anatabasamu akijua kapata pacha aliyebaki hapa duniani. Ninampenda Mungu kwa ajili yako Ambwene🙏🙏🙏

  • @maggishillah4847

    @maggishillah4847

    2 жыл бұрын

    Kabisaa yaani... It's a Powerful Song!

  • @juliananicodemus2746

    @juliananicodemus2746

    2 жыл бұрын

    Wimbo mzuri mungu akubariki sna kaka Ambwene

  • @habarikiswahili
    @habarikiswahili Жыл бұрын

    Touching.. ujumbe mzito saana mpaka nimeogopa

  • @vedastomtasha
    @vedastomtasha2 жыл бұрын

    Hakika wew ni mwamna imara daaaa nyimbo nmeikuta TikTok daa nmeifata ujumbe mzito sana najivunia kua na wew tz

  • @josephinemwambe3385
    @josephinemwambe3385 Жыл бұрын

    Huu wimbo umasema yanayotendeka kwa makanisa siku hizi Mtumishi wa mungu kakangu Ambwena kwa kweli nyimbo zako za nitia nguvu sana.. Wimbo mtaamu mno..Barikiwa sana South Africa 🇿🇦 Cape Town tunabarikiwa Ujumbe ufikia watoto wetu nchini Kenya 🇰🇪

  • @geitandelwa299

    @geitandelwa299

    Жыл бұрын

    Ameni tuna Mambo MENGI Ila Sio ya MUNGU

  • @vickynduku4753
    @vickynduku47532 жыл бұрын

    Ambwene mwasongwe is underated his music is beyond international level ...God bless you MoG ...my favorite artist

  • @kelvinkijo7500
    @kelvinkijo75002 жыл бұрын

    Amen sana ubunifu mkubwa mtumishi wa BWANA, zidi kubarikiwa!

  • @farajaemanuel1992
    @farajaemanuel19922 жыл бұрын

    Tenashara wa kizazi hiki. Yesu angekuchagua kuwa tenashara kaka,, Coz angeutazama moyo wa Utumishi ndani Yako.

  • @pardonmwalyego9947
    @pardonmwalyego99472 жыл бұрын

    Kwa nyimbo zako tunamtukuza Mungu....live long life in music!! Stay blessed.

  • @damasmayanja2930
    @damasmayanja2930 Жыл бұрын

    Hii ni Injili, this is Gospel mpeni maua yake Mwasongwe

  • @mamacaren1519
    @mamacaren1519 Жыл бұрын

    Kaka nabarikiwaga sana na nyimbo zako hakika unanigusa sana nakuelewa sana nazichambuaga mpaka napata maana Barikiwaaa

  • @isayasementi2646
    @isayasementi2646 Жыл бұрын

    Ubarikiwe kaka AMBWENE hakika MUNGU katupa wewe zawadi watanzania

  • @patranabwire4012
    @patranabwire40122 жыл бұрын

    I love this man of God Bless u🇺🇬🇺🇬

  • @michelmwamba5630
    @michelmwamba56302 жыл бұрын

    Ubarikiwe na Mungu ! Nyimbo zako zimenibariki Sana! Toka DRCongo. Lubumbashi.

  • @ReineDorDiamant
    @ReineDorDiamant2 жыл бұрын

    Uko wapi moyo wakanisa😭😭😭😭😭😭😭😭😭yeye awona tusipo biona😭😭😭😭Mungu atusamehe🙏😭😭👆

  • @damianmwombeki5879
    @damianmwombeki58792 жыл бұрын

    Tuponye vijana wa sasa Mtumishi na MUNGU atusaidie

  • @hyasintapastory4398
    @hyasintapastory4398 Жыл бұрын

    Naupenda sana huu wimbo

  • @b.jmwalupii7684
    @b.jmwalupii7684 Жыл бұрын

    Hongera kwa huu wimbo mzuri

  • @michaelmwanda1673
    @michaelmwanda16732 жыл бұрын

    Mungu wa mbinguni akubali sana mtumish wa bwana kristo akutie nguvu

  • @masterke536
    @masterke536 Жыл бұрын

    Barikiwa sanàaaa

  • @Jenipha-so9rk
    @Jenipha-so9rk3 ай бұрын

    Ibada njema

  • @LuganoMwandoto-pf8zg
    @LuganoMwandoto-pf8zg9 ай бұрын

    😀🔥Mungu akikupa kibari sehemu frani🔥 usinyamaze🔥🙌

  • @mamakoku5123
    @mamakoku5123 Жыл бұрын

    uko kama mrisho mpoto kwenye muundo wa mashahiri lakin wewe uko kizazi zaidi , ubarikiwe sna Big Up

  • @argentinachottah5962
    @argentinachottah5962 Жыл бұрын

    Ambwene Ambwene Ambwene Mwasongwe MUNGU BABA WA MBINGUNI AKUBARIKI SANA

  • @neemashirima1617
    @neemashirima16172 жыл бұрын

    🥳🥳🥳🥳 Mungu azidi kukupa mafunuo Mtumishi wa Mungu kulifundisha kanisa kile Mungu anataka tuenende nacho🙏🏼🙏🏼 yaan ni ujumbe kwa kanisa na mtu mmoja mmoja anayetaka kumwona Mungu katika viwango vingine

  • @TheKapungala
    @TheKapungala2 жыл бұрын

    I just love how our Tanzanian brothers and sisters make music straight from the scriptures. More love form Nairobi!

  • @rogathesarwatt

    @rogathesarwatt

    2 жыл бұрын

    All about Lugha Adhu ya Kiswahili

  • @paulwachenje861

    @paulwachenje861

    2 жыл бұрын

    That's exactly what I was heading to post but you represented the likes of us well

  • @barakahiluka4905

    @barakahiluka4905

    2 жыл бұрын

    Mungu akubaliki sana mtumishi👐

  • @danielnzali5609

    @danielnzali5609

    2 жыл бұрын

    Mungu akutunze mtumishi....🔥🔥

  • @dollnjosy3210

    @dollnjosy3210

    2 жыл бұрын

    🙏🙏❤️

  • @neemasanga5998
    @neemasanga5998 Жыл бұрын

    Akawaafundisha ibada za rohon jinc zitakiwavyo

  • @montteyfloki3953
    @montteyfloki39532 жыл бұрын

    Hii nyimbo inatosha kukuweka kwenye uwepo wa roho mtakatifu

  • @rebecasamwel6185
    @rebecasamwel61852 жыл бұрын

    My favorite musician be blessed ambwene mwasongwe 🙏🙏

  • @Jehovarohiband
    @Jehovarohiband Жыл бұрын

    Huyu Mtumshi anaimbia Mungu wakweli kabisa eee Mungu umuongoze asitoke kwenye mstari wako Kama wengine

  • @yulemwinjilisti
    @yulemwinjilisti Жыл бұрын

    Mandiko mwanzo mwisho.just how it should be.

  • @soniamuvyeyi
    @soniamuvyeyi2 жыл бұрын

    Wawouuuuuh,unajuwa kweli ,Mungu akupanuliye mipaka.

  • @daynesnyoni2715
    @daynesnyoni27152 жыл бұрын

    Kuna vile hii nyimbo inatuonesha bible ni kitabu kizuri sana, kitachotufanya tukutane na watu walioshi maisha kama yetu , ILa walikuja kubadirika na kuwa watu wema sana, mungu akubariki na kukutunza sana kaka ambwene, akuweke ili kupitia wewe wengi kati yetu tumrudie mungu🤲 na kuijua kweli🙏.

  • @user-tk2lw3wu2u
    @user-tk2lw3wu2u3 ай бұрын

    Glory to God ❤❤

  • @ezekielenock4650
    @ezekielenock4650 Жыл бұрын

    Asante sanaa kwa kunikumbusha Ibabda ya Moyoni Mtumishi

  • @beatricemwasunda5027
    @beatricemwasunda50272 жыл бұрын

    Jehovah aonaye Sirini braza azodi kukuweka makumbusho kwa ajili ya UTUKUFU WAKE...Ahsante nimepokea ujumbe wangu

  • @mussafredy5165
    @mussafredy51652 жыл бұрын

    Man of God. Kyala akutule

  • @canciasnyabiondo7434
    @canciasnyabiondo74344 ай бұрын

    I just bumped into your songs,,, this one's is on another level

  • @evansbaraka3255
    @evansbaraka32552 жыл бұрын

    Mungu akuinue zaidi mtumishi wa Mungu.... Kwa kazi nzuri....

  • @merymalachy1707
    @merymalachy17072 жыл бұрын

    Asante kaka...kwa huu wimbo hakika una mafunzo, much love from kenya 🇰🇪

  • @sebastianmwantuge5597
    @sebastianmwantuge5597 Жыл бұрын

    Sijashangaa kwa uzuri wa wimbo huu maana Mungu amekuinua,nyimbo zako zote ni nzuri na zina mafundisho. Mungu aendelee kukuinua.

  • @emanueldarema1751
    @emanueldarema17512 жыл бұрын

    Mungu akubariki sana Ambwene Mwasongwe. Full song from the Scriptures. My favorite Tanzanian Gospel Artist.

  • @vumiliajumanne8217
    @vumiliajumanne8217 Жыл бұрын

    Mungu akubaliki nyimbo zako zinanibariki

  • @ozanasylvester3663
    @ozanasylvester36632 жыл бұрын

    Ee Mwenyezi Mungu tunaomba utusaidie masikio ya Rohoni tunapo hubiriwa mafundisho kama haya kwa nyimbo tusiyapuuze bali yakalete mabadiliko ndani ya mioyo yetu.Amina

  • @glorymusa4869
    @glorymusa48692 жыл бұрын

    I'm blessed Mungu aendelee kukutumia jinsi apendavyo yeye mtumishi🙌💅🙌

  • @anoldkapinga758
    @anoldkapinga758Ай бұрын

    Mungu asikuachee

  • @victormaganga4590
    @victormaganga4590 Жыл бұрын

    Ubarikiwe mtumishi...Ujumbe mzuri sana 👏

  • @kamotajunior1681
    @kamotajunior16812 жыл бұрын

    This is exactly what is happening in our churches today, wimbo huu una mafundisho ya kweli.....

  • @pascazianhigula1900
    @pascazianhigula19002 жыл бұрын

    Kwa neema ya Bwana hujawahi kukosea ,sifa na utukufu ni kwa Bwana nangoja official video ya UMENIPA HESHIMA 🔥🔥🔥

  • @veronicazengo6201
    @veronicazengo6201 Жыл бұрын

    Mungu akujaze baraka kwa huduma hii Ambwene

  • @guershombenoit7156
    @guershombenoit71562 жыл бұрын

    Mungu Aku bariki muimbadji wa Mungu bwana

  • @furaharukoel7298
    @furaharukoel72982 жыл бұрын

    Moyo wa Ibada 🙌what a song straight from the Word of God 🙏🙏more blessings to you🙌❤

  • @leticiamakoye4871
    @leticiamakoye48715 күн бұрын

    Wasaidieni wake zenu wavae kibibilia

  • @tanzaniaonlinetv8821
    @tanzaniaonlinetv88212 жыл бұрын

    🙏🙏🙏Abwene MUNGU akubariki sanaa

  • @florentinafabian3537
    @florentinafabian35372 жыл бұрын

    The music saasa; uwiiiiii this song 🙌🙌🙌🤭... life transforming to the church kabisa kabisa 😭🙌

  • @nsiandumindossi
    @nsiandumindossi2 жыл бұрын

    What a powerful message! This is a whole sermon! Ahsante kwa Neno, more grace to you Mtumishi wa Yesu! Blessings

  • @mamy1605

    @mamy1605

    2 жыл бұрын

    Amen amen 🙏🙏🙏🙏

  • @munyibonface166

    @munyibonface166

    2 жыл бұрын

    Indeed it is!

  • @masatuzephania4036

    @masatuzephania4036

    2 жыл бұрын

    Niceee sanaa

  • @gloriousn6425

    @gloriousn6425

    2 жыл бұрын

    It really is 🙏🏿

  • @oten2731

    @oten2731

    2 жыл бұрын

    @@mamy1605 q1q11

  • @amonramothy6790
    @amonramothy67902 жыл бұрын

    Najifunza na ninakua kiroho kupitia jumbe zitokanazo na Neno la Mungu.. Barikiwa sana mtumish wa Mungu..

  • @esthermwaigwisya1775
    @esthermwaigwisya17752 жыл бұрын

    Ambweneeee ndaga fijooooo utukufu kwa YESU. Naitwa Happy Mwaigwisya. Prophetess of the most high God.

Келесі