ALIKIBA AMTAMBULISHA SALIM KIKEKE CROWN TV

ANAANDIKA ALIKIBA KUPITIA INSTAGRAM YAKE
My Brother salim_kikeke hii ilikuwa ndoto na maono tuliyokuwa nayo muda mrefu. Wakati unafanya maamuzi ya kurudi Nyumbani Tanzania tulipata nafasi ya kuzungumza na nikakueleza kiu yangu yakutaka kufanya kazi na wewe Gwiji, Nguli na Mtaalam wa Tasnia hii ya
Habari Afrika na Dunia.
Najua Simu zilikuwa nyingi sana lakini uliona CROWN ni sehemu sahihi sana kwako. Karibu kuwa sehemu ya
Historia tunayoenda kuiandika pamoja.
Nimekuvisha Taji na CROWN Media tunaamini Hesabu zetu za Kimkakati zimekaa Sawa. Karibu sana Nyumbani
@crownfmtz na @crowntv

Пікірлер

    Келесі