STORY YANGU S1:E1| DOLLY RESTIE

Hii ni story ya kusisimua ya Dolly Restie mtu aliyevunja matarajio yote ili kuunda hatima yake ya mafanikio.
Akizaliwa Dodoma, Dolly aliamua kuwa njia yake ya mafanikio ipo Dar es Salaam. Alipofika Dar, kazi yake ya kwanza ilikuwa ni mhudumu wa bar (barmaid), kazi aliyofanya kwa changamoto nyingi kutokana na kuwa mwanamke. Alikumbana na wanaume wengi waliomtaka kimahusiano wakiahidi kumpa maisha bora.
Dolly aliamua kuacha kazi ya uhudumu wa bar na kuingia kwenye tasnia ya ulimbwende maarufu kama Video Vixen. Alipata bahati ya kushiriki kwenye video kadhaa za wasanii wakubwa kama Barnaba, Marioo, G nako lakini umaarufu wake uliongezeka alipofanya kazi na Rayvanny. Wengi walimfananisha na Fahyma, mke wa Rayvanny.
Dolly anasema ingawa kazi ya Video Vixen inadharauliwa na wengi kwa kudhani haina maadili, anaamini ni kazi itakayomfikisha kwenye mafanikio anayoyatamani. Kwa Dolly, kitu cha msingi ni nidhamu na heshima katika kazi yake.

Пікірлер: 5

  • @MasaweRafaeli
    @MasaweRafaeliАй бұрын

    NOMA SANA

  • @Sally-hamisi
    @Sally-hamisiАй бұрын

    ❤❤

  • @NuruOmary-nc2xh
    @NuruOmary-nc2xhКүн бұрын

    Dolly 😂😂

  • @Citymedia25
    @Citymedia25Ай бұрын

    Chica❤

  • @AminaAbdallah-yj8ns
    @AminaAbdallah-yj8nsАй бұрын

    Nakupenda dolly ❤❤